Uchumi wa Magufuli: Sekta Binafsi ina-Suffer. Yalianza Maduka, Yakafuata Mashirika, Sasa ni Zamu ya Media Ina-suffer

Wataalamu walisema mkuu aliingia na "shock therapy" kunyoosha nchi na waliokuwa wakilia kuumizwa kiuchumi ni wapiga dili. Sasa inawezekana kwenye media kuna wapiga dili wengi na sasa ni zamu yao nao kunyooshwa. Hivyo ndugu Pascali tuendelee kumuombea mkuu akamilishe zoezi la kuinyoosha nchi kwani yajayo yanafurahisha.
 
Poleni sana wadau wa media. Lakini Pasco si unajua kuwa hata kama si rasmi, ninyi (media) ni mhimili wenye nguvu kubwa sana na ndo mnaendelea kumwimbia mkuu wa magogoni nyimbo za sifa kila uchao!!!

Ifike mahali mbadilike muache kusifu sifu tu kila wakati. Siku hizi hakuna TV au radio inayoweza kukosoa uongozi wa awamu hii hata kwa mafumbo sababu serikali inaongozwa na malaika ambao kwa asili hawana mawaa, yani ni watakatifu (infallible).

Mtalalamika sana mpaka mtakapochoka kuvumilia na kuishinda dhambi ya woga.

Nyie endeleeni tu kumuombea wa magogoni; ila mimi nawaombea ninyi mbadilike!

MUNGU ibariki Tanzania na wadau wote wa media!
Na bado kucha kuchwa kwa Musiba, Bashite mara waziri nani. Ina maana msipoenda hamli? Waachieni TBC, musiba tv, na ndugu zao wote nyie fanya yenu.
 
SRG ndio nini?
Shusha verified tecnical data kutoka TRC ku substaintiate masaa yako 20
Mkuu usiwe mvivu kutafuta taarifa, IF U ARE TO BE GOOD IN DISCUSSION S.......

Utamalizia maelezo...

Tanzanian president launches construction of new phase of standard gauge railway - Xinhua | English.news.cn
Screenshot_20181207-135241.jpeg
Screenshot_20181207-135222.jpeg
 
Nadharia yako haiendani na hili swali. Hapa kuna corruption na kule kuna specialization. Vitu viwili tofauti. NB: Ufahamu: mimi sipingi kampuni binafsi kufanya kazi na serikali. Napinga kampuni zilizoundwa kijanja janja ili ku-tape fedha za serikali kwa kazi ambazo hazina umuhimu
Ili tusibishane hebu fafanua, kampuni kama ya Mayalla ilikua ina corrupt nini and how? Kampuni kama Benchmark production na yenyewe ilikua ina corrupt nini and how!? Sioni tofauti ya hiki wanacho lalamikia kina Mayalla na suala la ununuzi wa Korosho kule kusini, lengo linaweza kua zuri na matokeo ya sasa au mwaka hu yakawa mazuri but matokeo ya mbeleni yakawa mabaya, ukitazama mfumo tunao kwenda nao sasa hivi ni kama tunafata mfumo wa UJAMAA na kujitegemea, mfumo ambao ulishindwa vibaya Enzi za Nyerere na of course umeshindwa everywhere in the world. Time is the best teacher, let us wait brother.
Hizo kampuni unazo ziita kua ni zakitapeli ndio zilikua walau zina AJIRI baadhi ya wahitimu, by now serikali haiajiri na bado imezuia channels za pesa halali kwenye sekta binafsi (jambo ambalo linaweza kua zuri kwa upande mmoja) na sekta binafsi is either zinapunguza wafanyakazi au kufungwa kabisa, matokeo yake tunaongeza WAZURULAJI mitani and hence possibility ya kuongezeka VIBAKA mtaani ni kubwa!
 
Sasa mtu kama wewe Mayalla ilibidi umwambie ukweli kiongozi na wala usisifie tu, hata kama una maslahi yako binafsi. Nchi inakwenda kubaya.
Mkuu Sijali, natumaini umenielewa na kwa bahati nzuri sana, sina maslahi yangu binafsi yoyote.
P
 
Leo kumepatikana habari njema kwa Baba la Baba ametumbukiza mkono Channel Ten na kuinusuru sasa rasmi Channel Ten iko chini ya serikali kwa mgongo wa CCM, maana tusemezane la ukweli, CCM kama CCM haiwezi.

Hongera Channel Ten kupata bail out. Sasa bado Star TV.
P
 
Kijana wa Mayalla haya uliyoyatabiria kwa channel 10 leo yamepata dawa! sasa swali ni je tasnia ya habari nyote sasa mkafugie njiwa huko na mtumie vidumu kuchota maji huko?
Bado kuna kazi na sasa Exim zamu yao imefika afatae nani?
 
Wanabodi
Kasi ya kukua kwa uchumi wa Tanzania ya Magufuli, ambayo umekuwa ukikua kwa asilimia zaidi ya asilimia 7% kwa mwaka, ukuaji huu is not reflected kwa Watanzania wa hali ya chini ambao ndio walio wengi, tunaelezwa uchumi unakuwa, na ripoti ya juzi juzi ya UNDP inaeleza kiwango cha umasikini kinapungua Ripoti: Kiwango cha umasikini kinapungua kwa kasi - JamiiForums lakini hali za maisha kwa walio wengi, zinazidi kuwa ngumu siku hadi siku, uchumi wa taifa unakuwa, huku uchumi wa watu individual na sekta binafsi ukizidi kuporomoka ambapo sekta binafsi ambayo ndio inategemewa kuwa the drivers we uchumi wa nchi ikiwemo Tanzania ya viwanda, ndio mhanga mkuu wa mdororo wa uchumi na ndiye anaye suffer the most.

Kwa upande wa maendeleo, ni kweli nchi yetu inapiga hatua kubwa za maendeleo, majengo, miundombinu, mabarabara, flyovers, viwanda, midege mikubwa, SGR, Stigler Gorge etc, lakini haya yote ni maendeleo ya vitu na sio maendeleo ya watu.

Je, Maendeleo ya Kweli ni Maendeleo ya Watu au Vitu?-

Wachumi Tusaidieni, Magufuli Analisaidia Taifa au Ataliangamiza?. - JamiiForums

Tena msije kusema kuwa tulinyamaza, Sisi jf tumesema sana, tumeuliza sana humu

Tuache Siasa ktk Uchumi: Wachumi tuelimisheni Dhambi ya Fixed Deposit na Faida ya Fedha Kukaa tu BoT - JamiiForums

Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa kiuchumi? - JamiiForums

Jarida la The Economist ladai uchumi wa Tanzania unaporomoka, lahamasisha Rais Magufuli adhibitiwe kwa vikwazo kiuchumi - JamiiForums

Kupata Maendeleo ya Kweli, Tanzania Inahitaji Systems Not Dramas, Ze Comedy na One Man Shows!. - JamiiForums

Maendeleo ya kweli TZ Yataletwa na Elimu na Ukweli. Tusidanganye, Tusidanganywe, Tusidanganyike! - JamiiForums

Kwa sasa naona kama sisi sekta binafsi tuna suffer. Ku suffer huko kulianzia kufungwa kwa maduka makubwa ya bidhaa na supermarkets. Zilianza super markets za Shoprite, zikaja Uchumi, piteni maeneo ya Shoppers Plaza mshuhudie frames tupu wenyewe wamefungasha. Hata mtaa wa Samora lile jengo jipya la NHC mtaa wa Samora, lilikuwa full, sasa kuna mapengo.
Kuzorota uchumi: Stone Block wafungasha virago! - JamiiForums

Yakafuata baadhi ya mashirika na makampuni kufilisika hivyo kupunguza wafanyakazi,Uchumi wa Magufuli: Precision Air Yapumulia Machine. Yapunguza Wafanyakazi 136! - JamiiForums

Yakaja mabenki, kabla ya Magufuli, ukiingia benki kubwa zote, NMB, CRDB na NBC, unakutana foleni ndefu za wateja. Sasa kuna branches unaingia unakwenda straight to counter, anangoja wateja, IMF: Nearly half of Tanzania's banks vulnerable to financial shocks - JamiiForums

na sasa ni maduka ya fedha.

Wakati yote haya yakitokea, sisi media hatukuyaangazia vya kutosha kwa kudhani hayatuhusu!.

Sasa kibano hicho cha hali ngumu ya uchumi, kimeigusa sekta ya Media ambapo media kubwa kabisa nchini zimeanza kutikisika.

Kwenye media ilianza Star TV, kati ya wafanyakazi 500, ililazimika kupunguza wafanyakazi 100, mwaka 2016 wakabaki 400, mwaka jana wakapunguza 200 wakabaki 200, sijui mwaka huu, lakini kipindi chake most popular cha Jicho letu ndani ya habari, kinachoendeshwa na Mkongwe Dotto Bulendu, hakipo hewani!
Star Tv na Redio Free kupunguza wafanyakazi - JamiiForums

Hapa ninapo zungumza, najua kituo cha Television cha Channel Ten kinapumulia mashine. Kusipofanyika juhudi za ziada kukinusuru, Channel Ten itafuata mkondo wa Radio Uhuru na magazeti ya Chama ya Uhuru Mzalendo.

Leo kumepatikana taarifa ya wafanyakazi wa gazeti kubwa la the Guardian, hawajalipwa mishahara kwa miezi 3, hivyo kitakachofuata ni kupunguza wafanyakazi.Mti wa Xmas wazua simanzi kwa wafanyakazi wa The Guardian Limited - JamiiForums

Japo familia ya the Citizen Mwananchi, bado hawajatangaza kulia njaa, lakini kama hii ndio hali halisi ya uchumi wa Tanzania ya Magufuli, then hata Citizens, litakuwa halina jinsi, lazima nalo soon litatangaza kupunguza wafanyakazi.

Mimi mwenyewe na kale kajikampuni kangu ka PPR, ambapo tulibamba sana tenda za serikali, mwanzo tulikuwa na wafanyakazi 20, tukipangisha jengo la NHC pale Mtaa wa Mkwepu kwa kodi ya pango kwa mwezi, ya zaidi ya mshahara wa DC, sasa hakuna tena tenders za serikali, serikali inatangaza moja kwa moja na TBC, mwaka huu pia tenda zangu za kutangaza Maonyesho ya Saba Saba na Nane Nane zimefutwa, hivyo tumepunguza wafanyakazi 15!, tumebaki 5!. Na Mtaa wa Mkwepu hapakaliki hivyo tumehama, tumehamia jengo la Posta House kwenye kajichumba.

Wito kwa waandishi wenzangu, walioajiriwa kwenye media industry, kwa hali hii ya uchumi wa Tanzania ya Magufuli, usitegemee ajira pekee na usisubiri kupunguzwa kazi, bali sasa kwa sisi wanaume tufuge kuku na njiwa, na Kwa waandishi wa kike ni mambo ya ndoo na kidumu.

Kwa sisi wanaume, kuku ni kazi ya kujiajiri) na njiwa (kazi ya kuajiriwa), ili njiwa akiruka, ubaki na kuku.

Kwa waandishi wa kike, kwenye kazi ya kuteka maji, teka maji kwenye ndoo (kazi ya kudumu) na kidumu (kujiajiri), ili maji ya kwenye ndoo yakimwagika, angalau unabaki na kidumu.

Kiukweli kabisa Media tuna hali ngumu!.
Mungu saidia.
Mungu Ibariki Tanzania,
Mungu Mbariki rais Magufuli aweze kukuza uchumi wa nchi yetu kwa Tanzania ya viwanda kifanikiwa, tuwe nchi ya uchumi wa kati, tukielekea kuwa nchi ya ahadi kwa mabomba nchi mzima yatatoa maziwa na asali
Jumatano Njema.
Paskali
Mayala mimi naandika kitabu kinacho husu ujasiliamali namna ya kuanzisha na kuendeleza biashara najua watu wengi wameandika vitabu vya aina hiyo nitachangia kidogo kutoka Kwenye kitabu changu kuna topic inaitwa ''An Entrepreneur and his enviroment '' Mjasilamali na mambo yanayo mzunguka.hili huanzia kwenye Familia hadi Kimataifa ina husu mambo ambayo yanaweza athiri biashara mfano: ukifungua tu biashara unakuta TRA hao wakitoka tu watu wa Liseni hao wakitoka wa osha n.k Serikali ni chanzo kikuu kutokana na sera zake. Serikali ina majukumu matatu muhuhimu The Government has three roles 1. Regulatory role 2. Supporting role .3.Participating role Majukumu ya serikali kwa sekta binafsi ni matatu 1.Kusimamia mfano TRA 2.Kushiriki katika mipango ya kukuza biashara 3.kushiriki moja kwa moja mfano ujenzi wa ukuta wa melelani
Tatizo ninaloliona mimi nikwamba Serikali imejisahau kushiriki kwenye mipango ya kukuza biashara ''supporting role'' Serikali kuwa mkopaji mkubwa kwenye mabenki ya ndani ni tatizo na kuto lipa Madeni ya ndani kwa wakati nitatizo kubwa pia Lengo la ''topic'' ya an entrepreneur and his environment
(mjasiamali na mambo yanayo mzunguka) ni kuweza kujua nini lakufanya kuweza kukabiliana na yanayo kuzunguka kuweza kufanikwa kwenye biashara zetu. Swali fikirishi je unaweza kukabiliana na serikali km maridhiano hakuna ?
 
Leo kumepatikana habari njema kwa Baba la Baba ametumbukiza mkono Channel Ten na kuinusuru sasa rasmi Channel Ten iko chini ya serikali kwa mgongo wa CCM, maana tusemezane la ukweli, CCM kama CCM haiwezi.

Hongera Channel Ten kupata bail out. Sasa bado Star TV.
P
KUNA kampuni moja ya tours, kubwa sana nayo ni ya ccm, nitawajuza na makampunin mengine 39 makubwa ya ccm, hii nchi ioneni tu kama ilivyo
 
KUNA kampuni moja ya tours, kubwa sana nayo ni ya ccm, nitawajuza na makampunin mengine 39 makubwa ya ccm, hii nchi ioneni tu kama ilivyo
Lazima ni ile iliyoko Arusha. ILe inayoongoza kwa kuwapunja wafanyakazi na kule Kilimanjaro inaongoza kwa vifo vya porters
 
Wanabodi
Kasi ya kukua kwa uchumi wa Tanzania ya Magufuli, ambayo umekuwa ukikua kwa asilimia zaidi ya asilimia 7% kwa mwaka, ukuaji huu is not reflected kwa Watanzania wa hali ya chini ambao ndio walio wengi, tunaelezwa uchumi unakuwa, na ripoti ya juzi juzi ya UNDP inaeleza kiwango cha umasikini kinapungua Ripoti: Kiwango cha umasikini kinapungua kwa kasi - JamiiForums lakini hali za maisha kwa walio wengi, zinazidi kuwa ngumu siku hadi siku, uchumi wa taifa unakuwa, huku uchumi wa watu individual na sekta binafsi ukizidi kuporomoka ambapo sekta binafsi ambayo ndio inategemewa kuwa the drivers we uchumi wa nchi ikiwemo Tanzania ya viwanda, ndio mhanga mkuu wa mdororo wa uchumi na ndiye anaye suffer the most.

Kwa upande wa maendeleo, ni kweli nchi yetu inapiga hatua kubwa za maendeleo, majengo, miundombinu, mabarabara, flyovers, viwanda, midege mikubwa, SGR, Stigler Gorge etc, lakini haya yote ni maendeleo ya vitu na sio maendeleo ya watu.

Je, Maendeleo ya Kweli ni Maendeleo ya Watu au Vitu?-

Wachumi Tusaidieni, Magufuli Analisaidia Taifa au Ataliangamiza?. - JamiiForums

Tena msije kusema kuwa tulinyamaza, Sisi jf tumesema sana, tumeuliza sana humu

Tuache Siasa ktk Uchumi: Wachumi tuelimisheni Dhambi ya Fixed Deposit na Faida ya Fedha Kukaa tu BoT - JamiiForums

Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa kiuchumi? - JamiiForums

Jarida la The Economist ladai uchumi wa Tanzania unaporomoka, lahamasisha Rais Magufuli adhibitiwe kwa vikwazo kiuchumi - JamiiForums

Kupata Maendeleo ya Kweli, Tanzania Inahitaji Systems Not Dramas, Ze Comedy na One Man Shows!. - JamiiForums

Maendeleo ya kweli TZ Yataletwa na Elimu na Ukweli. Tusidanganye, Tusidanganywe, Tusidanganyike! - JamiiForums

Kwa sasa naona kama sisi sekta binafsi tuna suffer. Ku suffer huko kulianzia kufungwa kwa maduka makubwa ya bidhaa na supermarkets. Zilianza super markets za Shoprite, zikaja Uchumi, piteni maeneo ya Shoppers Plaza mshuhudie frames tupu wenyewe wamefungasha. Hata mtaa wa Samora lile jengo jipya la NHC mtaa wa Samora, lilikuwa full, sasa kuna mapengo.
Kuzorota uchumi: Stone Block wafungasha virago! - JamiiForums

Yakafuata baadhi ya mashirika na makampuni kufilisika hivyo kupunguza wafanyakazi,Uchumi wa Magufuli: Precision Air Yapumulia Machine. Yapunguza Wafanyakazi 136! - JamiiForums

Yakaja mabenki, kabla ya Magufuli, ukiingia benki kubwa zote, NMB, CRDB na NBC, unakutana foleni ndefu za wateja. Sasa kuna branches unaingia unakwenda straight to counter, anangoja wateja, IMF: Nearly half of Tanzania's banks vulnerable to financial shocks - JamiiForums

na sasa ni maduka ya fedha.

Wakati yote haya yakitokea, sisi media hatukuyaangazia vya kutosha kwa kudhani hayatuhusu!.

Sasa kibano hicho cha hali ngumu ya uchumi, kimeigusa sekta ya Media ambapo media kubwa kabisa nchini zimeanza kutikisika.

Kwenye media ilianza Star TV, kati ya wafanyakazi 500, ililazimika kupunguza wafanyakazi 100, mwaka 2016 wakabaki 400, mwaka jana wakapunguza 200 wakabaki 200, sijui mwaka huu, lakini kipindi chake most popular cha Jicho letu ndani ya habari, kinachoendeshwa na Mkongwe Dotto Bulendu, hakipo hewani!
Star Tv na Redio Free kupunguza wafanyakazi - JamiiForums

Hapa ninapo zungumza, najua kituo cha Television cha Channel Ten kinapumulia mashine. Kusipofanyika juhudi za ziada kukinusuru, Channel Ten itafuata mkondo wa Radio Uhuru na magazeti ya Chama ya Uhuru Mzalendo.

Leo kumepatikana taarifa ya wafanyakazi wa gazeti kubwa la the Guardian, hawajalipwa mishahara kwa miezi 3, hivyo kitakachofuata ni kupunguza wafanyakazi.Mti wa Xmas wazua simanzi kwa wafanyakazi wa The Guardian Limited - JamiiForums

Japo familia ya the Citizen Mwananchi, bado hawajatangaza kulia njaa, lakini kama hii ndio hali halisi ya uchumi wa Tanzania ya Magufuli, then hata Citizens, litakuwa halina jinsi, lazima nalo soon litatangaza kupunguza wafanyakazi.

Mimi mwenyewe na kale kajikampuni kangu ka PPR, ambapo tulibamba sana tenda za serikali, mwanzo tulikuwa na wafanyakazi 20, tukipangisha jengo la NHC pale Mtaa wa Mkwepu kwa kodi ya pango kwa mwezi, ya zaidi ya mshahara wa DC, sasa hakuna tena tenders za serikali, serikali inatangaza moja kwa moja na TBC, mwaka huu pia tenda zangu za kutangaza Maonyesho ya Saba Saba na Nane Nane zimefutwa, hivyo tumepunguza wafanyakazi 15!, tumebaki 5!. Na Mtaa wa Mkwepu hapakaliki hivyo tumehama, tumehamia jengo la Posta House kwenye kajichumba.

Wito kwa waandishi wenzangu, walioajiriwa kwenye media industry, kwa hali hii ya uchumi wa Tanzania ya Magufuli, usitegemee ajira pekee na usisubiri kupunguzwa kazi, bali sasa kwa sisi wanaume tufuge kuku na njiwa, na Kwa waandishi wa kike ni mambo ya ndoo na kidumu.

Kwa sisi wanaume, kuku ni kazi ya kujiajiri) na njiwa (kazi ya kuajiriwa), ili njiwa akiruka, ubaki na kuku.

Kwa waandishi wa kike, kwenye kazi ya kuteka maji, teka maji kwenye ndoo (kazi ya kudumu) na kidumu (kujiajiri), ili maji ya kwenye ndoo yakimwagika, angalau unabaki na kidumu.

Kiukweli kabisa Media tuna hali ngumu!.
Mungu saidia.
Mungu Ibariki Tanzania,
Mungu Mbariki rais Magufuli aweze kukuza uchumi wa nchi yetu kwa Tanzania ya viwanda kifanikiwa, tuwe nchi ya uchumi wa kati, tukielekea kuwa nchi ya ahadi kwa mabomba nchi mzima yatatoa maziwa na asali
Jumatano Njema.
Paskali
Paskali umenena vyema! Kwetu sekta ya uchapishaji (publishing) ndio balaa, kampuni zimeshindwa kulipa mishahara, pango na kodi ya serikali kisa hakuna zabuni ya vitabu bora vya shule toka serikalini, ilihali watoto na walimu wana hali mbaya ya ukosefu wa vitabu. Ndg tuombe mungu si mchezo, tumuombee pia mh rais mungu amuwezeshe aangalie na huku kwenye elimu. Asiwaamini kwa kuwasikiliza watendaji wa wizara, atumie vyombo vyake kuchunguza ukweli kuokoa taifa la kesho kielimu, vitabu bora shuleni hakunaaaaa!
 
209 Reactions
Reply
Back
Top Bottom