Uchumi wa Magufuli: Sekta Binafsi ina-Suffer. Yalianza Maduka, Yakafuata Mashirika, Sasa ni Zamu ya Media Ina-suffer

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,463
113,515
Wanabodi

Kasi ya kukua kwa uchumi wa Tanzania ya Magufuli, ambayo umekuwa ukikua kwa asilimia zaidi ya asilimia 7% kwa mwaka, ukuaji huu is not reflected kwa Watanzania wa hali ya chini ambao ndio walio wengi, tunaelezwa uchumi unakuwa, na ripoti ya juzi juzi ya UNDP inaeleza kiwango cha umasikini kinapungua Ripoti: Kiwango cha umasikini kinapungua kwa kasi - JamiiForums lakini hali za maisha kwa walio wengi, zinazidi kuwa ngumu siku hadi siku, uchumi wa taifa unakuwa, huku uchumi wa watu individual na sekta binafsi ukizidi kuporomoka ambapo sekta binafsi ambayo ndio inategemewa kuwa the drivers we uchumi wa nchi ikiwemo Tanzania ya viwanda, ndio mhanga mkuu wa mdororo wa uchumi na ndiye anaye suffer the most.

Kwa upande wa maendeleo, ni kweli nchi yetu inapiga hatua kubwa za maendeleo, majengo, miundombinu, mabarabara, flyovers, viwanda, midege mikubwa, SGR, Stigler Gorge etc, lakini haya yote ni maendeleo ya vitu na sio maendeleo ya watu.

Je, Maendeleo ya Kweli ni Maendeleo ya Watu au Vitu?-
Wachumi Tusaidieni, Magufuli Analisaidia Taifa au Ataliangamiza?. - JamiiForums


Japo Beggars Can Not Be Choosers, Tuache Siasa Kwenye Uchumi. We Have to Choose Or. .. - JamiiForums

Tena msije kusema kuwa tulinyamaza, Sisi jf tumesema sana, tumeuliza sana humu

Tuache Siasa ktk Uchumi: Wachumi tuelimisheni Dhambi ya Fixed Deposit na Faida ya Fedha Kukaa tu BoT - JamiiForums

Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa kiuchumi? - JamiiForums

Jarida la The Economist ladai uchumi wa Tanzania unaporomoka, lahamasisha Rais Magufuli adhibitiwe kwa vikwazo kiuchumi - JamiiForums

Kupata Maendeleo ya Kweli, Tanzania Inahitaji Systems Not Dramas, Ze Comedy na One Man Shows!. - JamiiForums

Maendeleo ya kweli TZ Yataletwa na Elimu na Ukweli. Tusidanganye, Tusidanganywe, Tusidanganyike! - JamiiForums

Kwa sasa naona kama sisi sekta binafsi tuna suffer. Ku suffer huko kulianzia kufungwa kwa maduka makubwa ya bidhaa na supermarkets. Zilianza super markets za Shoprite, zikaja Uchumi, piteni maeneo ya Shoppers Plaza mshuhudie frames tupu wenyewe wamefungasha. Hata mtaa wa Samora lile jengo jipya la NHC mtaa wa Samora, lilikuwa full, sasa kuna mapengo.
Kuzorota uchumi: Stone Block wafungasha virago! - JamiiForums

Yakafuata baadhi ya mashirika na makampuni kufilisika hivyo kupunguza wafanyakazi,Uchumi wa Magufuli: Precision Air Yapumulia Machine. Yapunguza Wafanyakazi 136! - JamiiForums

Yakaja mabenki, kabla ya Magufuli, ukiingia benki kubwa zote, NMB, CRDB na NBC, unakutana foleni ndefu za wateja. Sasa kuna branches unaingia unakwenda straight to counter, anangoja wateja, IMF: Nearly half of Tanzania's banks vulnerable to financial shocks - JamiiForums

na sasa ni maduka ya fedha.

Wakati yote haya yakitokea, sisi media hatukuyaangazia vya kutosha kwa kudhani hayatuhusu!.

Sasa kibano hicho cha hali ngumu ya uchumi, kimeigusa sekta ya Media ambapo media kubwa kabisa nchini zimeanza kutikisika.

Kwenye media ilianza Star TV, kati ya wafanyakazi 500, ililazimika kupunguza wafanyakazi 100, mwaka 2016 wakabaki 400, mwaka jana wakapunguza 200 wakabaki 200, sijui mwaka huu, lakini kipindi chake most popular cha Jicho letu ndani ya habari, kinachoendeshwa na Mkongwe Dotto Bulendu, hakipo hewani!
Star Tv na Redio Free kupunguza wafanyakazi - JamiiForums

Hapa ninapo zungumza, najua kituo cha Television cha Channel Ten kinapumulia mashine. Kusipofanyika juhudi za ziada kukinusuru, Channel Ten itafuata mkondo wa Radio Uhuru na magazeti ya Chama ya Uhuru Mzalendo.

Leo kumepatikana taarifa ya wafanyakazi wa gazeti kubwa la the Guardian, hawajalipwa mishahara kwa miezi 3, hivyo kitakachofuata ni kupunguza wafanyakazi.Mti wa Xmas wazua simanzi kwa wafanyakazi wa The Guardian Limited - JamiiForums

Japo familia ya the Citizen Mwananchi, bado hawajatangaza kulia njaa, lakini kama hii ndio hali halisi ya uchumi wa Tanzania ya Magufuli, then hata Citizens, litakuwa halina jinsi, lazima nalo soon litatangaza kupunguza wafanyakazi.

Mimi mwenyewe na kale kajikampuni kangu ka PPR, ambapo tulibamba sana tenda za serikali, mwanzo tulikuwa na wafanyakazi 20, tukipangisha jengo la NHC pale Mtaa wa Mkwepu kwa kodi ya pango kwa mwezi, ya zaidi ya mshahara wa DC, sasa hakuna tena tenders za serikali, serikali inatangaza moja kwa moja na TBC, mwaka huu pia tenda zangu za kutangaza Maonyesho ya Saba Saba na Nane Nane zimefutwa, hivyo tumepunguza wafanyakazi 15!, tumebaki 5!. Na Mtaa wa Mkwepu hapakaliki hivyo tumehama, tumehamia jengo la Posta House kwenye kajichumba.

Wito kwa waandishi wenzangu, walioajiriwa kwenye media industry, kwa hali hii ya uchumi wa Tanzania ya Magufuli, usitegemee ajira pekee na usisubiri kupunguzwa kazi, bali sasa kwa sisi wanaume tufuge kuku na njiwa, na Kwa waandishi wa kike ni mambo ya ndoo na kidumu.

Kwa sisi wanaume, kuku ni kazi ya kujiajiri) na njiwa (kazi ya kuajiriwa), ili njiwa akiruka, ubaki na kuku.

Kwa waandishi wa kike, kwenye kazi ya kuteka maji, teka maji kwenye ndoo (kazi ya kudumu) na kidumu (kujiajiri), ili maji ya kwenye ndoo yakimwagika, angalau unabaki na kidumu.

Kiukweli kabisa Media tuna hali ngumu!.
Mungu saidia.
Mungu Ibariki Tanzania,
Mungu Mbariki rais Magufuli aweze kufanikiwa kukuza uchumi wa nchi yetu na kuifanya, Tanzania ya Viwanda kufanikiwa, Tanzania ya uchumi wa gesi, Tanzania ya uchumi wa kati, tukielekea kuwa nchi ya ahadi kwa mabomba nchi mzima yatatoa maziwa na asali
Jumatano Njema.
Paskali
 
Mkuu sio masihara nilimtembelea mzee wangu kazini kwake akaniambia december huu mwezi ndio anafungay ofisi yake mpaka nikamuonea huruma na kumpa mawazo mbadala.


Kuna maduka nimeyatembelea dah watu wanafunga na wafanyabiashara haswa wa kati na wa kawaida wapo kwenye wakati mgumu sana kila mmoja analalamika

Kwahili mheshimiwa na wasaidizi wake wajitathmini

Kama wewe ni kula kulala au umeajiriwa serikalini huwezi kuelewa haya yanayoendelea mitaani
 
Business restructuring, kulikuwa na hela chafu zisizokuwa na tija mtaani- hizi zimepotea na madhara yake pengine ndiyo haya. Kufungwa kwa biashara zipo sababu nyingi maana hata kipindi kile unachodhani hali ilikuwa salama pia biashara zilikuwa zinafungwa na biashara mpya zinafunguliwa.
 
Poleni sana wadau wa media. Lakini Pasco si unajua kuwa hata kama si rasmi, ninyi (media) ni mhimili wenye nguvu kubwa sana na ndo mnaendelea kumwimbia mkuu wa magogoni nyimbo za sifa kila uchao!!!

Ifike mahali mbadilike muache kusifu sifu tu kila wakati. Siku hizi hakuna TV au radio inayoweza kukosoa uongozi wa awamu hii hata kwa mafumbo sababu serikali inaongozwa na malaika ambao kwa asili hawana mawaa, yani ni watakatifu (infallible).

Mtalalamika sana mpaka mtakapochoka kuvumilia na kuishinda dhambi ya woga.

Nyie endeleeni tu kumuombea wa magogoni; ila mimi nawaombea ninyi mbadilike!

MUNGU ibariki Tanzania na wadau wote wa media!
 
Tatizo la Media za hapa kwetu ni kumpaiza anaewafanya waishi kama mashetani na kutowapa kipaumbele wale wanaowatetea.

Mfano,wapinzani wakiita waandishi, baadhi ya media hazionekani na zinazoonekana zinatoa coverage ndogo huku Jiwe wanampa coverage kubwa kwa headlines za kumnadi.

Ukweli ni kwamba,hivi sasa wamiliki wa vyombo vya habari,waandishi, wafanyakazi, wakulima, wafanyabiashara, wamiliki wa mitandao,blogs,moderators, wavuvi,wanasiasa,n.k, tunakiwa tuunganishe nguvu kupambana na huyu adui yetu(our common enemy-Jiwe) kila mtu kwa nafasi yake before it is too late.

Wenzetu wanaojifanya wako neutral, wenzetu wanaoona na kupuuza ukweli wa mambo, wanaojifanya wako fair,pamoja na wale wanaosubiri yawakute,ndio wanaoampa nguvu mbaya wetu bwana Jiwe kuendelea kutuangamiza.
 
Rais akishindwa ni jukumu la wananchi wa nchi ile kumuondoa madarakani kwa lazima. Magufuli alishashindwa kitambooo..Mimi nilimuona ni Rais wa ajabu sana mwanzoni tu mwa mwaka 2016 na nikamchukulia kama nyoka anayeninyemelea. Niliamua na sasa nimesepa. Huyo mtu siyo kabisa....Sijui kwanini haelewi? Mtu huwezi kuongoza nchi lakini bado king'ang'anizi. Ondoka! Mimi ni mmoja wa wanaoamini kuwa muuaji wa Tanzania kwa sasa ni Rais John Pombe Magufuli.
 
Back
Top Bottom