Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,468
- 113,583
Wanabodi
Kasi ya kukua kwa uchumi wa Tanzania ya Magufuli, ambayo umekuwa ukikua kwa asilimia zaidi ya asilimia 7% kwa mwaka, ukuaji huu is not reflected kwa Watanzania wa hali ya chini ambao ndio walio wengi, tunaelezwa uchumi unakuwa, na ripoti ya juzi juzi ya UNDP inaeleza kiwango cha umasikini kinapungua Ripoti: Kiwango cha umasikini kinapungua kwa kasi - JamiiForums lakini hali za maisha kwa walio wengi, zinazidi kuwa ngumu siku hadi siku, uchumi wa taifa unakuwa, huku uchumi wa watu individual na sekta binafsi ukizidi kuporomoka ambapo sekta binafsi ambayo ndio inategemewa kuwa the drivers we uchumi wa nchi ikiwemo Tanzania ya viwanda, ndio mhanga mkuu wa mdororo wa uchumi na ndiye anaye suffer the most.
Kwa upande wa maendeleo, ni kweli nchi yetu inapiga hatua kubwa za maendeleo, majengo, miundombinu, mabarabara, flyovers, viwanda, midege mikubwa, SGR, Stigler Gorge etc, lakini haya yote ni maendeleo ya vitu na sio maendeleo ya watu.
Je, Maendeleo ya Kweli ni Maendeleo ya Watu au Vitu?-
Wachumi Tusaidieni, Magufuli Analisaidia Taifa au Ataliangamiza?. - JamiiForums
Japo Beggars Can Not Be Choosers, Tuache Siasa Kwenye Uchumi. We Have to Choose Or. .. - JamiiForums
Tena msije kusema kuwa tulinyamaza, Sisi jf tumesema sana, tumeuliza sana humu
Tuache Siasa ktk Uchumi: Wachumi tuelimisheni Dhambi ya Fixed Deposit na Faida ya Fedha Kukaa tu BoT - JamiiForums
Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa kiuchumi? - JamiiForums
Jarida la The Economist ladai uchumi wa Tanzania unaporomoka, lahamasisha Rais Magufuli adhibitiwe kwa vikwazo kiuchumi - JamiiForums
Kupata Maendeleo ya Kweli, Tanzania Inahitaji Systems Not Dramas, Ze Comedy na One Man Shows!. - JamiiForums
Maendeleo ya kweli TZ Yataletwa na Elimu na Ukweli. Tusidanganye, Tusidanganywe, Tusidanganyike! - JamiiForums
Kwa sasa naona kama sisi sekta binafsi tuna suffer. Ku suffer huko kulianzia kufungwa kwa maduka makubwa ya bidhaa na supermarkets. Zilianza super markets za Shoprite, zikaja Uchumi, piteni maeneo ya Shoppers Plaza mshuhudie frames tupu wenyewe wamefungasha. Hata mtaa wa Samora lile jengo jipya la NHC mtaa wa Samora, lilikuwa full, sasa kuna mapengo.
Kuzorota uchumi: Stone Block wafungasha virago! - JamiiForums
Yakafuata baadhi ya mashirika na makampuni kufilisika hivyo kupunguza wafanyakazi,Uchumi wa Magufuli: Precision Air Yapumulia Machine. Yapunguza Wafanyakazi 136! - JamiiForums
Yakaja mabenki, kabla ya Magufuli, ukiingia benki kubwa zote, NMB, CRDB na NBC, unakutana foleni ndefu za wateja. Sasa kuna branches unaingia unakwenda straight to counter, anangoja wateja, IMF: Nearly half of Tanzania's banks vulnerable to financial shocks - JamiiForums
na sasa ni maduka ya fedha.
Wakati yote haya yakitokea, sisi media hatukuyaangazia vya kutosha kwa kudhani hayatuhusu!.
Sasa kibano hicho cha hali ngumu ya uchumi, kimeigusa sekta ya Media ambapo media kubwa kabisa nchini zimeanza kutikisika.
Kwenye media ilianza Star TV, kati ya wafanyakazi 500, ililazimika kupunguza wafanyakazi 100, mwaka 2016 wakabaki 400, mwaka jana wakapunguza 200 wakabaki 200, sijui mwaka huu, lakini kipindi chake most popular cha Jicho letu ndani ya habari, kinachoendeshwa na Mkongwe Dotto Bulendu, hakipo hewani!
Star Tv na Redio Free kupunguza wafanyakazi - JamiiForums
Hapa ninapo zungumza, najua kituo cha Television cha Channel Ten kinapumulia mashine. Kusipofanyika juhudi za ziada kukinusuru, Channel Ten itafuata mkondo wa Radio Uhuru na magazeti ya Chama ya Uhuru Mzalendo.
Leo kumepatikana taarifa ya wafanyakazi wa gazeti kubwa la the Guardian, hawajalipwa mishahara kwa miezi 3, hivyo kitakachofuata ni kupunguza wafanyakazi.Mti wa Xmas wazua simanzi kwa wafanyakazi wa The Guardian Limited - JamiiForums
Japo familia ya the Citizen Mwananchi, bado hawajatangaza kulia njaa, lakini kama hii ndio hali halisi ya uchumi wa Tanzania ya Magufuli, then hata Citizens, litakuwa halina jinsi, lazima nalo soon litatangaza kupunguza wafanyakazi.
Mimi mwenyewe na kale kajikampuni kangu ka PPR, ambapo tulibamba sana tenda za serikali, mwanzo tulikuwa na wafanyakazi 20, tukipangisha jengo la NHC pale Mtaa wa Mkwepu kwa kodi ya pango kwa mwezi, ya zaidi ya mshahara wa DC, sasa hakuna tena tenders za serikali, serikali inatangaza moja kwa moja na TBC, mwaka huu pia tenda zangu za kutangaza Maonyesho ya Saba Saba na Nane Nane zimefutwa, hivyo tumepunguza wafanyakazi 15!, tumebaki 5!. Na Mtaa wa Mkwepu hapakaliki hivyo tumehama, tumehamia jengo la Posta House kwenye kajichumba.
Wito kwa waandishi wenzangu, walioajiriwa kwenye media industry, kwa hali hii ya uchumi wa Tanzania ya Magufuli, usitegemee ajira pekee na usisubiri kupunguzwa kazi, bali sasa kwa sisi wanaume tufuge kuku na njiwa, na Kwa waandishi wa kike ni mambo ya ndoo na kidumu.
Kwa sisi wanaume, kuku ni kazi ya kujiajiri) na njiwa (kazi ya kuajiriwa), ili njiwa akiruka, ubaki na kuku.
Kwa waandishi wa kike, kwenye kazi ya kuteka maji, teka maji kwenye ndoo (kazi ya kudumu) na kidumu (kujiajiri), ili maji ya kwenye ndoo yakimwagika, angalau unabaki na kidumu.
Kiukweli kabisa Media tuna hali ngumu!.
Mungu saidia.
Mungu Ibariki Tanzania,
Mungu Mbariki rais Magufuli aweze kufanikiwa kukuza uchumi wa nchi yetu na kuifanya, Tanzania ya Viwanda kufanikiwa, Tanzania ya uchumi wa gesi, Tanzania ya uchumi wa kati, tukielekea kuwa nchi ya ahadi kwa mabomba nchi mzima yatatoa maziwa na asali
Jumatano Njema.
Paskali
Kasi ya kukua kwa uchumi wa Tanzania ya Magufuli, ambayo umekuwa ukikua kwa asilimia zaidi ya asilimia 7% kwa mwaka, ukuaji huu is not reflected kwa Watanzania wa hali ya chini ambao ndio walio wengi, tunaelezwa uchumi unakuwa, na ripoti ya juzi juzi ya UNDP inaeleza kiwango cha umasikini kinapungua Ripoti: Kiwango cha umasikini kinapungua kwa kasi - JamiiForums lakini hali za maisha kwa walio wengi, zinazidi kuwa ngumu siku hadi siku, uchumi wa taifa unakuwa, huku uchumi wa watu individual na sekta binafsi ukizidi kuporomoka ambapo sekta binafsi ambayo ndio inategemewa kuwa the drivers we uchumi wa nchi ikiwemo Tanzania ya viwanda, ndio mhanga mkuu wa mdororo wa uchumi na ndiye anaye suffer the most.
Kwa upande wa maendeleo, ni kweli nchi yetu inapiga hatua kubwa za maendeleo, majengo, miundombinu, mabarabara, flyovers, viwanda, midege mikubwa, SGR, Stigler Gorge etc, lakini haya yote ni maendeleo ya vitu na sio maendeleo ya watu.
Je, Maendeleo ya Kweli ni Maendeleo ya Watu au Vitu?-
Wachumi Tusaidieni, Magufuli Analisaidia Taifa au Ataliangamiza?. - JamiiForums
Japo Beggars Can Not Be Choosers, Tuache Siasa Kwenye Uchumi. We Have to Choose Or. .. - JamiiForums
Tena msije kusema kuwa tulinyamaza, Sisi jf tumesema sana, tumeuliza sana humu
Tuache Siasa ktk Uchumi: Wachumi tuelimisheni Dhambi ya Fixed Deposit na Faida ya Fedha Kukaa tu BoT - JamiiForums
Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa kiuchumi? - JamiiForums
Jarida la The Economist ladai uchumi wa Tanzania unaporomoka, lahamasisha Rais Magufuli adhibitiwe kwa vikwazo kiuchumi - JamiiForums
Kupata Maendeleo ya Kweli, Tanzania Inahitaji Systems Not Dramas, Ze Comedy na One Man Shows!. - JamiiForums
Maendeleo ya kweli TZ Yataletwa na Elimu na Ukweli. Tusidanganye, Tusidanganywe, Tusidanganyike! - JamiiForums
Kwa sasa naona kama sisi sekta binafsi tuna suffer. Ku suffer huko kulianzia kufungwa kwa maduka makubwa ya bidhaa na supermarkets. Zilianza super markets za Shoprite, zikaja Uchumi, piteni maeneo ya Shoppers Plaza mshuhudie frames tupu wenyewe wamefungasha. Hata mtaa wa Samora lile jengo jipya la NHC mtaa wa Samora, lilikuwa full, sasa kuna mapengo.
Kuzorota uchumi: Stone Block wafungasha virago! - JamiiForums
Yakafuata baadhi ya mashirika na makampuni kufilisika hivyo kupunguza wafanyakazi,Uchumi wa Magufuli: Precision Air Yapumulia Machine. Yapunguza Wafanyakazi 136! - JamiiForums
Yakaja mabenki, kabla ya Magufuli, ukiingia benki kubwa zote, NMB, CRDB na NBC, unakutana foleni ndefu za wateja. Sasa kuna branches unaingia unakwenda straight to counter, anangoja wateja, IMF: Nearly half of Tanzania's banks vulnerable to financial shocks - JamiiForums
na sasa ni maduka ya fedha.
Wakati yote haya yakitokea, sisi media hatukuyaangazia vya kutosha kwa kudhani hayatuhusu!.
Sasa kibano hicho cha hali ngumu ya uchumi, kimeigusa sekta ya Media ambapo media kubwa kabisa nchini zimeanza kutikisika.
Kwenye media ilianza Star TV, kati ya wafanyakazi 500, ililazimika kupunguza wafanyakazi 100, mwaka 2016 wakabaki 400, mwaka jana wakapunguza 200 wakabaki 200, sijui mwaka huu, lakini kipindi chake most popular cha Jicho letu ndani ya habari, kinachoendeshwa na Mkongwe Dotto Bulendu, hakipo hewani!
Star Tv na Redio Free kupunguza wafanyakazi - JamiiForums
Hapa ninapo zungumza, najua kituo cha Television cha Channel Ten kinapumulia mashine. Kusipofanyika juhudi za ziada kukinusuru, Channel Ten itafuata mkondo wa Radio Uhuru na magazeti ya Chama ya Uhuru Mzalendo.
Leo kumepatikana taarifa ya wafanyakazi wa gazeti kubwa la the Guardian, hawajalipwa mishahara kwa miezi 3, hivyo kitakachofuata ni kupunguza wafanyakazi.Mti wa Xmas wazua simanzi kwa wafanyakazi wa The Guardian Limited - JamiiForums
Japo familia ya the Citizen Mwananchi, bado hawajatangaza kulia njaa, lakini kama hii ndio hali halisi ya uchumi wa Tanzania ya Magufuli, then hata Citizens, litakuwa halina jinsi, lazima nalo soon litatangaza kupunguza wafanyakazi.
Mimi mwenyewe na kale kajikampuni kangu ka PPR, ambapo tulibamba sana tenda za serikali, mwanzo tulikuwa na wafanyakazi 20, tukipangisha jengo la NHC pale Mtaa wa Mkwepu kwa kodi ya pango kwa mwezi, ya zaidi ya mshahara wa DC, sasa hakuna tena tenders za serikali, serikali inatangaza moja kwa moja na TBC, mwaka huu pia tenda zangu za kutangaza Maonyesho ya Saba Saba na Nane Nane zimefutwa, hivyo tumepunguza wafanyakazi 15!, tumebaki 5!. Na Mtaa wa Mkwepu hapakaliki hivyo tumehama, tumehamia jengo la Posta House kwenye kajichumba.
Wito kwa waandishi wenzangu, walioajiriwa kwenye media industry, kwa hali hii ya uchumi wa Tanzania ya Magufuli, usitegemee ajira pekee na usisubiri kupunguzwa kazi, bali sasa kwa sisi wanaume tufuge kuku na njiwa, na Kwa waandishi wa kike ni mambo ya ndoo na kidumu.
Kwa sisi wanaume, kuku ni kazi ya kujiajiri) na njiwa (kazi ya kuajiriwa), ili njiwa akiruka, ubaki na kuku.
Kwa waandishi wa kike, kwenye kazi ya kuteka maji, teka maji kwenye ndoo (kazi ya kudumu) na kidumu (kujiajiri), ili maji ya kwenye ndoo yakimwagika, angalau unabaki na kidumu.
Kiukweli kabisa Media tuna hali ngumu!.
Mungu saidia.
Mungu Ibariki Tanzania,
Mungu Mbariki rais Magufuli aweze kufanikiwa kukuza uchumi wa nchi yetu na kuifanya, Tanzania ya Viwanda kufanikiwa, Tanzania ya uchumi wa gesi, Tanzania ya uchumi wa kati, tukielekea kuwa nchi ya ahadi kwa mabomba nchi mzima yatatoa maziwa na asali
Jumatano Njema.
Paskali