Uchumi wa kati tulifikaje? Bora kuwa na nidhamu ya uoga kuliko kutokuwa na nidhamu kabisa

Elitwege

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
5,154
10,809
Mwaka 2019 bank ya dunia ilitangaza Tanzania kuingia uchumi wa kati miaka mitano mapema zaidi kinyume na ilivyokuwa imetabiriwa kwamba itachukua miaka kumi.

Je, kuwahi huku kuingia uchumi wa kati ilikuwa ni matunda ya nidhamu ya uoga? Kama nidhamu ya uoga ina matunda kiasi hiki kwa nini tuiogope sasa?

Kwa watoto wadogo na wasiojua mambo wanadhani hayati Magufuli alianza kuwa mkali alipokuwa rais wa nchi tu wakati ukweli ni kwamba Magufuli alikuwa mkali na mfuatiliaji tangu akiwa naibu waziri, waziri na baadae rais wa nchi.

Katikati ya mafisadi wakubwa wa awamu za Mkapa na Kikwete lakini walimwogopa Magufuli aliwashughulikia kila wizara aliyopelekwa, swali la kujiuliza aliwezaje?

Hata baada ya kuwa rais na kufariki dunia mpaka leo mwaka umeisha si Chadema, ACT Wazalendo wala CCM waliokuja na ushahidi usiotia shaka juu ya ufisadi wake licha ya kwamba waliahidi pindi tu atakapotoka madarakani basi watakuja na mikataba ya ufisadi na rushwa kubwakubwa zilizosainiwa na yeye.

Mwezi March 2022 umetimia mwaka mzima tangu atutoke duniani lakini mahasimu wake ikiwemo, Lisu, Lema, Nape ,Makamba, Kigogo bado hawajawaletea watanzania ufisadi wa Magufuli.

Kinyume chake wanaendeleza mafanikio na miradi ya awamu ya tano kwa kasi kubwa, walipinga kila kitu lakini sasa wanatumia kila kitu walichokipinga!

Walioahidi kuifunika legacy kumbe hawana uwezo kuifunika hata kidole chake tu!

Muda utawaumbua zaidi.
 
Mwaka 2019 bank ya dunia ilitangaza Tanzania kuingia uchumi wa kati miaka mitano mapema zaidi kinyume na ilivyokuwa imetabiriwa kwamba itachukua miaka kumi....
Tulifika kwa kuwa na uongozi hodari na imara wa mwamba JPM, ambao:
• Ulipinga rushwa
• Ulipambana na mafisadi
• Ulishughulikia wauza madawa ya kulevya
• Ulipambana na majangili
• Uliwa-empower Watanzania wanyonge kama machinga, bodaboda, mama ntilie, n.k.
• Uliimarisha, kurekebisha na kuboresha miundombinu ya maji, afya, elimu na usafiri
• Uliimarisha taasisi na kubuni na kufufua mashirika ya umma kama Air Tanzania
• Ulianzisha na kukamilisha miradi mikubwa ya kimkakati
• Ulifanya independent decisions bila kukopi kila kitu kutoka kwa mabeberu
• Ulidumisha uzalendo, uwajibikaji na uchapakazi.

Kwanini tusingefikia lengo kabla ya wakati?
 
Kikwete alichukua nchi kwa Mkapa ikiwa na GDP per Capital ya 500 USD, akaipandisha hadi 980 USD ndani ya miaka 10,
Kipindi Cha Magufuli miaka 5 ya Magufuli GDP per Capita ilipanda kwa 40 USD hadi 1020 USD ambayo ndio uchumi wa Kati

Kwa hiyo hii hili la uchumi wa Kati sio kitu kikubwa Sana kwani hata angeingia Rais mwingine angeipeleka tu, sababu ilikuwa imebaki tu kidogo

Ila wafuasi wa Magufuli kwa kuwa wengi shule hakuna, yanashangiliaaa bila hata kujua maana na historia yake
 
Historical Trend of Tanzania Shillings vs USD

1995 - 1 USD = 500 TZS
1996 - 1 USD = 580 TZS
1997 - 1 USD = 665 TZS
1998 - 1 USD = 720 TZS
1999 - 1 USD = 800 TZS
2000 - 1 USD = 820 TZS
2001 - 1 USD = 880 TZS
2002 - 1 USD = 900 TZS
2003 - 1 USD = 900 TZS
2004 - 1 USD = 910 TZS
2005 - 1 USD = 1050 TZS
2006 - 1 USD = 1100 TZS
2007 - 1 USD = 1150 TZS
2008 - 1 USD = 1200 TZS
2009 - 1 USD = 1250 TZS
2010 - 1 USD = 1260 TZS
2011 - 1 USD = 1300 TZS
2012 - 1 USD =1450 TZS
2013 - 1 USD =1620 TZS
2014 - 1USD = 1650 TZS
2015 - 1USD = 2210TZS
2016 - 1 USD = 2200TZS
2019 - 1 USD = 2300TZS
2020 - 1 USD = 2290 TZS
2021 - 1 USD = 2290 TZS

Utulivu wa Shillingi yetu ktk hio miaka mi5 ulitusaidia sana kufikia hio hatua.
 
Kikwete alichukua nchi kwa Mkapa ikiwa na GDP per Capital ya 500 USD, akaipandisha hadi 980 USD ndani ya miaka 10,
Kipindi Cha Magufuli miaka 5 ya Magufuli GDP per Capita ilipanda kwa 40 USD hadi 1020 USD ambayo ndio uchumi wa Kati

Kwa hiyo hii hili la uchumi wa Kati sio kitu kikubwa Sana kwani hata angeingia Rais mwingine angeipeleka tu, sababu ilikuwa imebaki tu kidogo

Ila wafuasi wa Magufuli kwa kuwa wengi shule hakuna, yanashangiliaaa bila hata kujua maana na historia yake
Uchumi wa kati huku wananchi wapo hoi, maanake hapa MO per capital income yake kwa mwaka ni 1020 USD, teteteete
 
Historical Trend of Tanzania Shillings vs USD

1995 - 1 USD = 500 TZS
1996 - 1 USD = 580 TZS
1997 - 1 USD = 665 TZS
1998 - 1 USD = 720 TZS
1999 - 1 USD = 800 TZS
2000 - 1 USD = 820 TZS
2001 - 1 USD = 880 TZS
2002 - 1 USD = 900 TZS
2003 - 1 USD = 900 TZS
2004 - 1 USD = 910 TZS
2005 - 1 USD = 1050 TZS
2006 - 1 USD = 1100 TZS
2007 - 1 USD = 1150 TZS
2008 - 1 USD = 1200 TZS
2009 - 1 USD = 1250 TZS
2010 - 1 USD = 1260 TZS
2011 - 1 USD = 1300 TZS
2012 - 1 USD =1450 TZS
2013 - 1 USD =1620 TZS
2014 - 1USD = 1650 TZS
2015 - 1USD = 2210TZS
2016 - 1 USD = 2200TZS
2019 - 1 USD = 2300TZS
2020 - 1 USD = 2290 TZS
2021 - 1 USD = 2290 TZS

Utulivu wa Shillingi yetu ktk hio miaka mi5 ulitusaidia sana kufikia hio hatua.
Elimu duni ya uchumi
 
Yaani utoke kuwa nchi masikioni Hadi kuwa uchumi wa Kati kwa miaka mitatu!!!?...hiyo mipango ya uchumi wa Kati iliwekwa kipindi Cha mkapa,imefanyiwa kazi kwa miaka 20,huyo jpm wako kakuta gari linaserereka tu
Uchumi wa kati huku walihodhi pesa mingi ni watu wachache inagawanywa kwa kila mtu ni formula ya hovyo sn mkuu
 
Mwaka 2019 bank ya dunia ilitangaza Tanzania kuingia uchumi wa kati miaka mitano mapema zaidi kinyume na ilivyokuwa imetabiriwa kwamba itachukua miaka kumi.
Mkuu Elitwege mbona kuna mmoja umemtaja mara mbili kwa majina tofauti.....Kigogo!,¿?
 
Ni PUNGUANI tu anayeweza kumdhihaki JPM.
JPM aliacha Mfuko wa mbolea ukiuzwa kwa sh. 45,000/- au 50,000/- lakini sasa mfuko ule ule unauzwa kwa sh.120,000/- hadi 150,000/-
Lakini si mbolea tu, bali hata vitu vingine vimepanda bei kwa zaidi ya 95%.
Ikumbukwe kwamba, kupanda kwa bei za vitu hakuwaathiri hata kidogo wenye mamlaka na waitifaki wao.
Hao wote wanatumia Bajeti za serikali, ndiyo maana hali hii kwao si chochote wala si lolote.

JPM alikuwa ni mzalendo wa kweli na aliumia sana kuona Watanzania wanaumizwa kwa mambo ya kijinga kijinga kama haya, ndiyo maana alijitoa sadaka kwa ajili yetu.
RIP, BABA YETU MPENDWA, JPM.
 
Mwaka 2019 bank ya dunia ilitangaza Tanzania kuingia uchumi wa kati miaka mitano mapema zaidi kinyume na ilivyokuwa imetabiriwa kwamba itachukua miaka kumi.

Je, kuwahi huku kuingia uchumi wa kati ilikuwa ni matunda ya nidhamu ya uoga? Kama nidhamu ya uoga ina matunda kiasi hiki kwa nini tuiogope sasa?

Kwa watoto wadogo na wasiojua mambo wanadhani hayati Magufuli alianza kuwa mkali alipokuwa rais wa nchi tu wakati ukweli ni kwamba Magufuli alikuwa mkali na mfuatiliaji tangu akiwa naibu waziri, waziri na baadae rais wa nchi.

Katikati ya mafisadi wakubwa wa awamu za Mkapa na Kikwete lakini walimwogopa Magufuli aliwashughulikia kila wizara aliyopelekwa, swali la kujiuliza aliwezaje?

Hata baada ya kuwa rais na kufariki dunia mpaka leo mwaka umeisha si Chadema, ACT Wazalendo wala CCM waliokuja na ushahidi usiotia shaka juu ya ufisadi wake licha ya kwamba waliahidi pindi tu atakapotoka madarakani basi watakuja na mikataba ya ufisadi na rushwa kubwakubwa zilizosainiwa na yeye.

Mwezi March 2022 umetimia mwaka mzima tangu atutoke duniani lakini mahasimu wake ikiwemo, Lisu, Lema, Nape ,Makamba, Kigogo bado hawajawaletea watanzania ufisadi wa Magufuli.

Kinyume chake wanaendeleza mafanikio na miradi ya awamu ya tano kwa kasi kubwa, walipinga kila kitu lakini sasa wanatumia kila kitu walichokipinga!

Walioahidi kuifunika legacy kumbe hawana uwezo kuifunika hata kidole chake tu!

Muda utawaumbua zaidi.

Muda umuumbue nani? Kati ya Mwendazake na Samia nani anaumbuka?

Do you know kwamba saizi pesa sio tatizo tena Serikalini?

Legacy itafutwa Mzee wewe elewa hili,we are not struggling again as it used to be.
 
Back
Top Bottom