Uchumba unapogeuzwa pango la ngono........!!!!!!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,393
Mpaka miaka ya hivi karibuni mambo ya uchumba yalikuwa hayawezi kufanyika bila ya kuwepo wazazi na familia. Mitoko mingi na kualikana ilifanyika majumbani wakiwapo wanafamilia wote. Kujitokeza kwa usafiri na ugunduzi wa magari kumesaidia sana kuharibu utaratibu mzuri wa mitoko ya kimapenzi na uchumba kwa ujumla.

Magari si tu kwamba yamesababisha mitoko isifanyike majumbani, lakini pia yamesababisha ifanyike bila kuwashirikisha wazazi. Gari siku hizi limebadilishwa kuwa kitanda kinachotembea chakufanyia ngono wakati wa mitoko.Vijana wadogo sio kwa hapa nchini tu bali hata huko katika nchi za magharibi na ulaya wamejinyakulia uhuru mkubwa mno kutoka kwa wazazi wao, na kuzipondoponda chini mila na desturi ambazo ziliweka misingi imara katika kulinda maadili ya uchumba kwa vijana.

Lakini pia Teknolojia mpya na matumizi yake mabaya nayo imechangia kwa kiasi kikubwa kusambaratisha mila na desturi zetu zilizokuwa zikilinda maadili yetu. Simu na mitandao ya mawasilano, ni moja ya mabadiliko yaliyotufikisha hapa.

Imani na misingi ya kidini zilianza kupata mashambulizi makali toka kwa wasomi na wanafalsafa wa karne na karne. Charles Darwin na wafuasi wake walianza mashambulizi dhidi ya imani ya Mungu na mamlaka yake. Na hii ilipelekea wanatheolojia wa Ulaya kuanza kulegeza kamba kwa mambo muhimu ya kidini.Kupuuzwa kwa mila na desturi na maadili ya kidini kumechangia sana kuharibu tabia za vijana ikiwa ni pamoja na mambo ya urafiki, uchumba hadi ndoa.

Ni baada ya vita ya kwanza ya Dunia ndipo saikolojia na Sosholojia vilileta njia ya Kisayansi iliyoheshimika zaidi, nakuanzia hapo mamilioni ya watu walianza kuamini mafundisho ya akina Sigmund Freud, Margaret Mead na Alfred Charles Kinsey.
 
Magari si tu kwamba yamesababisha mitoko isifanyike majumbani, lakini pia yamesababisha ifanyike bila kuwashirikisha wazazi. Gari siku hizi limebadilishwa kuwa kitanda kinachotembea chakufanyia ngono wakati wa mitoko.Vijana wadogo sio kwa hapa nchini tu bali hata huko katika nchi za magharibi na ulaya wamejinyakulia uhuru mkubwa mno kutoka kwa wazazi wao, na kuzipondoponda chini mila na desturi ambazo ziliweka misingi imara katika kulinda maadili ya uchumba kwa vijana.

Lakini pia Teknolojia mpya na matumizi yake mabaya nayo imechangia kwa kiasi kikubwa kusambaratisha mila na desturi zetu zilizokuwa zikilinda maadili yetu. Simu na mitandao ya mawasilano, ni moja ya mabadiliko yaliyotufikisha hapa.

Zamani wakati sisi tulikuwa tunakesha kuwavizia watoto wa kike vichochoroni, lakini vijana wa siku hizi wamerahisishiwa sana, mitandao ya simu na hii ya Intenet imepelekea swala la kutongozana kuwa rahisi. Usafiri nao, kama ulivyosema ni sana na Vitanda vinavyotembea...............mara nyingi vijana hufanyia ngono kwenye magari ya wazazi wao. mzazi anapoombwa gari na mwanae kwa ajili ya kwendea Disco, basi ajue litatumika kwa shughuli nyingine, yaani kufanyia ngono.

Maadili ya kumpata mwenza yamewekwa kisasa zaidi, zile taratibu za kuchunguza familia atokako mke au mume, kwa ajili ya kujiridhisha kama binti anaolewa katika familia sahihi, au mume anaoa katika familia sahihi, hazipo na badala yake watu tunachukuana tu, na ndio maana ndoa hazidumu, watoto hawana adabu, kutoka nje ya ndoa kusiko na simile, na kila aina ya uchafu, ili mradi fujo tu...............
 
Ni sahihi kabisa kila kitu kimeathiriwa na utandawazi si masuala ya mahusiano pekee. Enzi za zamani ilikuwa mpaka siku ya harusi ndiyo wanandoa wanado lakini siku hizi mpaka bibi harusi aidha atoe mimba au afunge akiwa mjazito lakini hili si kwa wote wajameni. Hilo tu ni kiashiria tosha kuwa mambo yamebadilika sana na hata ukienda katika mambo mengine ya kijamii maadili yameshuka vibaya mno.
 
Ni sahihi kabisa kila kitu kimeathiriwa na utandawazi si masuala ya mahusiano pekee. Enzi za zamani ilikuwa mpaka siku ya harusi ndiyo wanandoa wanado lakini siku hizi mpaka bibi harusi aidha atoe mimba au afunge akiwa mjazito lakini hili si kwa wote wajameni. Hilo tu ni kiashiria tosha kuwa mambo yamebadilika sana na hata ukienda katika mambo mengine ya kijamii maadili yameshuka vibaya mno.

Umenikumbusha zile ndoa za KISARAWANDA................
 
Magari si tu kwamba yamesababisha mitoko isifanyike majumbani, lakini pia yamesababisha ifanyike bila kuwashirikisha wazazi. Gari siku hizi limebadilishwa kuwa kitanda kinachotembea chakufanyia ngono wakati wa mitoko.Vijana wadogo sio kwa hapa nchini tu bali hata huko katika nchi za magharibi na ulaya wamejinyakulia uhuru mkubwa mno kutoka kwa wazazi wao, na kuzipondoponda chini mila na desturi ambazo ziliweka misingi imara katika kulinda maadili ya uchumba kwa vijana.


Hii ni Kweli kabisa mtambuzi manake kuna kipindi wakati naishi pale mabibo hostel, kulikuwa na gari katika angalia yangu vizuri nikaanza kushangaa gari (lilikuwa tinted hivyo huoni ndani) linanesanesa yaani juu chini, juu chini mwanzo mwisho na baada ya kama nusu saa akatoka dada na pande la mtu "libaba" na kama haitoshi hapo wakakumbatiana na kula denda. Nikahisi tu hawa watu walikuwa wana.........
 
Hii ni Kweli kabisa mtambuzi manake kuna kipindi wakati naishi pale mabibo hostel, kulikuwa na gari katika angalia yangu vizuri nikaanza kushangaa gari (lilikuwa tinted hivyo huoni ndani) linanesanesa yaani juu chini, juu chini mwanzo mwisho na baada ya kama nusu saa akatoka dada na pande la mtu "libaba" na kama haitoshi hapo wakakumbatiana na kula denda. Nikahisi tu hawa watu walikuwa wana.........
huyo dem alijishushia heshima ivo?dah huyo ni cheapest not cheap.
 
mbona hamjisemi nyie wazee wa zamani kwamba siku hizi mmebadilika sana na ndo mnaongoza kwa kutembea na mabinti wadogo kama watoto wenu wa kuwazaa...hii teknologia imemuharibu kila mtu sio babu sio mjukuu
 
Wanasayansi wanakwambia 'sex ni basic need'. Sasa unategemea nini kwa hawa watu walioipokea hii idea?? Kamwe hawawezi ishi maisha ya nyuma!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom