Uchu wa madaraka tu utaweza kuiua UKAWA... vinginevyyo CCM haina lake 2015

Dopas

JF-Expert Member
Aug 14, 2010
1,151
392
Wana JF
Kwa hali ilivyo sasa kisiasa Tanzania, matumaini makubwa ni kuiombea UKAWA isimame imara... ni kete pekee ya kuiondoa CCM madarakani uchaguzi ujao. Ni kete pekee kwa sababu ni nguvu ya upinzani iliyounganishwa, na ikiwa haitaingiliwa na ibilisi wa tamaa ya madaraka, basi ni wazi CCM hawana lao tena uchaguzi ujao. Ni vema basi nguvu hii ikadumishwa kwa kuanza kupanga mikakati ya kuachiana nafasi ya kugombea kutoka ngazi ya madiwani, ubunge hadi kumweka mgombea moja tu wa Urais.

Hofu ni kuwa CCM sasa matumbo moto wanaweza kupenyeza mapandikizi wa kuchafua hali ya hewa katika UKAWA.
Ila ni imani yangu kuwa kama hawataingiliwa na uchu wa madaraka, na kama mikakati ya kuachiana kata, majimbo, na hata ngazi ya urais. Matumaini ya kuingia kwenye Nchi ijaayo maziwa na asali yapo karibu kuliko ilivyokuwa utitiri wa vyama vya upinzani kuwagawana kura.
Ni maoni yangu tu, msomaji uko huru kukubaliana nami au la.
Mungu ibariki UKAWA.
 
Mkuu hapa lazima mvutano utakuwepo, hebu fikiria vijana wengi wa BAVICHA na CHASO wana ndoto za kugombea nafasi za ubunge 2015, sasa hapo bado hatujachanganya na vijana wa CUF na NCCR aiseee hapa tuwe makini isijetokea kizaazaa hasa ukizingatia vijana wengi ni sample ya Kisandu na Mtela ambao kwao kuropoka kwny media sio shida na weng hawana uvumilivu wa kisiasa.

ALL IN ALL MWISHO WA SIKU UKOMBOZI UTAPATIKANA TU.
 
Mkuu hapa lazima mvutano utakuwepo, hebu fikiria vijana wengi wa BAVICHA na CHASO wana ndoto za kugombea nafasi za ubunge 2015, sasa hapo bado hatujachanganya na vijana wa CUF na NCCR aiseee hapa tuwe makini isijetokea kizaazaa hasa ukizingatia vijana wengi ni sample ya Kisandu na Mtela ambao kwao kuropoka kwny media sio shida na weng hawana uvumilivu wa kisiasa.

ALL IN ALL MWISHO WA SIKU UKOMBOZI UTAPATIKANA TU.
Kwani hauwezi kuitumikia Chadema mpaka ugombee ubunge, naona unataka kupingana na Mbowe angalia usifukuzwe.
 
Mkuu hapa lazima mvutano utakuwepo, hebu fikiria vijana wengi wa BAVICHA na CHASO wana ndoto za kugombea nafasi za ubunge 2015, sasa hapo bado hatujachanganya na vijana wa CUF na NCCR aiseee hapa tuwe makini isijetokea kizaazaa hasa ukizingatia vijana wengi ni sample ya Kisandu na Mtela ambao kwao kuropoka kwny media sio shida na weng hawana uvumilivu wa kisiasa.

ALL IN ALL MWISHO WA SIKU UKOMBOZI UTAPATIKANA TU.

UKAWA ina watu makini kuliko inavyotarajiwa. Criteria ya kisayansi itatumika kuachiana kugombea.
 
Mkuu hapa lazima mvutano utakuwepo, hebu fikiria vijana wengi wa BAVICHA na CHASO wana ndoto za kugombea nafasi za ubunge 2015, sasa hapo bado hatujachanganya na vijana wa CUF na NCCR aiseee hapa tuwe makini isijetokea kizaazaa hasa ukizingatia vijana wengi ni sample ya Kisandu na Mtela ambao kwao kuropoka kwny media sio shida na weng hawana uvumilivu wa kisiasa.

ALL IN ALL MWISHO WA SIKU UKOMBOZI UTAPATIKANA TU.

kweli kabisa.. turudi kwenye nafasi ya mwenyekiti wa UKAWA TAIFA, mpambano kati ya dj Mbowe. mchumi Lipumba na msomi Mbatia sijui utakuwaje,,Hakuna wa kukubali kushindwa..hahaha,..yetu macho
 
kweli kabisa.. turudi kwenye nafasi ya mwenyekiti wa UKAWA TAIFA, mpambano kati ya dj Mbowe. mchumi Lipumba na msomi Mbatia sijui utakuwaje,,Hakuna wa kukubali kushindwa..hahaha,..yetu macho

Kamanda acha uchochezi, jadili uhalisia wa hoja, wasiwasi hapa sio uongozi wa juu sababu ni watu wanaojitambua pia wana experience ya kutosha kuhusu siasa na uongozi hivyo si rahisi kutokea mvutano.
Tatizo ni huku chini kwa vijana ambapo huwa hakuna uvumilivu bali ni fighting bila suluhu.
 
Kamanda acha uchochezi, jadili uhalisia wa hoja, wasiwasi hapa sio uongozi wa juu sababu ni watu wanaojitambua pia wana experience ya kutosha kuhusu siasa na uongozi hivyo si rahisi kutokea mvutano.
Tatizo ni huku chini kwa vijana ambapo huwa hakuna uvumilivu bali ni fighting bila suluhu.

bado sikubaliani na wewe mkuu..hivi hukumbuki ule mvurugano uliotokea baada ya zito kuchukua fomu ya.kugombea uenyekiti taifa? mi nina uhakika kwenye uongozi wa juu ndio.itakuwa shida zaidi..hivi chadema watakubali mwenyekiti atoke cuf wakati wanadai wanakubalika zaidi?
 
UKAWA ina watu makini kuliko inavyotarajiwa. Criteria ya kisayansi itatumika kuachiana kugombea.

Mkuu sio Jambo rahisi sana kama unavyolichukulia, Kuna watu wamegombea urais toka mwaka 1995 mpaka sasa hakijaeleweka na wako ndani ya UKAWA. Pia kuna watu waliacha ubunge kwa mkataba kuwa kama asipokuwa Rais alipwe maslahi sawa na ya mbunge wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania , Watu hawa wote bado wako ndani ya UKAWA, na wanataka kufanikisha malengo yao ya kuwa viongozi wakuu wa Nchi kupitia UKAWA. Je hiyo dhana ya kuachiana unadhani ni rahisi hapo?
 
UKAWA muda si mrefu wataanza vita ya wao kwa wao, katika kugombea nyadhifa mbalimbali.
 
Mkuu hapa lazima mvutano utakuwepo, hebu fikiria vijana wengi wa BAVICHA na CHASO wana ndoto za kugombea nafasi za ubunge 2015, sasa hapo bado hatujachanganya na vijana wa CUF na NCCR aiseee hapa tuwe makini isijetokea kizaazaa hasa ukizingatia vijana wengi ni sample ya Kisandu na Mtela ambao kwao kuropoka kwny media sio shida na weng hawana uvumilivu wa kisiasa.

ALL IN ALL MWISHO WA SIKU UKOMBOZI UTAPATIKANA TU.
Wewe bavicha unamatatizo kweli unataka ubunge kwa akili yako kama hii kweli chadema na ukawa ni bonge la tatizo kwa tanzania.
 
mkuu. hivi mzee mtei atakubali mwenyekiti wa Ukawa Taifa awe Lipumba?


Ndugu yangu naona hujaelewa modus operandi ya UKAWA, UKAWA haitakuwa na mwenyekiti wake!! Vyama vyote vitaendelea kuwepo na kupewa rusuku zake kama kawaida, ila watak kwenye vikao vya makubaliano kuhusu kumsimamisha mgombea enbeo fulani, awe diwani, mbunge au Rais wa nchi!!! Jambo la kusema eti Mtei atakubaloi Lipumba awe mwenyekiti wa ukawa? Hilo mbona sio shida kabisaaa, mwenyekiti wa Ukawa tuuu ----Naomba muelewe UKAWA sio chama cha siasa ni forum ya kuwaunganisha vyama vya upinzani katika objective za kutaka kuwatumikia wananchi wa tanzania. naomba tuelewe!!
 
Hivi hii ukawa mnadhani itavuka hata daraja la salenda?


Hivi kwanini mtu kama wewe unachangia humu? So negative, eti ukawa haivuki daraja la salender, kwani zimewahi kutokea Ukawa ngapi zikashindwa kuvuka daraja la salender, mbona una argument za kiganga na kizeee??? Be positive and necer say never!!!
 
bado sikubaliani na
wewe mkuu..hivi hukumbuki ule mvurugano uliotokea baada ya zito kuchukua
fomu ya.kugombea uenyekiti taifa? mi nina uhakika kwenye uongozi wa juu
ndio.itakuwa shida zaidi..hivi chadema watakubali mwenyekiti atoke cuf
wakati wanadai wanakubalika zaidi?

Uwelewa wako ni mdogo sana na umesababishwa na chama unachoshabikia.

Ukawa ni ushirikianao wa vyama vya upinzani na wenyeviti wa vyama shiriki wanahaki sawa katika uenyekiti wa Ukawa
 
UKAWA muda si mrefu wataanza vita ya wao kwa wao, katika kugombea nyadhifa mbalimbali.

Ukiwa na akili finyu kero sana.

Zanzibar-CUF (Maalim Seifu)
Tanganyika- NCCR (Mbatia)
Tanzania-CHADEMA (Dr. Slaa)

Ni chungu ila ndio ukweli.
 
Ukiwa na akili finyu kero sana.

Zanzibar-CUF (Maalim Seifu)
Tanganyika- NCCR (Mbatia)
Tanzania-CHADEMA (Dr. Slaa)

Ni chungu ila ndio ukweli.

lipumba kwa hiyo mmemchinjia baharini? Lipumba ni mgombea wa kudumu wa nafasi ya urais..
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom