Uchawi, Wanawake vyatajwa kuwa chanzo kikubwa cha Mafanikio ya Diamond..!!

Money Stunna

JF-Expert Member
Aug 9, 2011
13,054
6,281
dia.PNG
MEBAINIKA kwamba msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania,Nassib Abdul Mohamed maarufu kwa jina la (Diamond Platnumz) anatumia nyota za wanawake katika kujipatia umaarufu, habari za ndani zinazomhusu msanii huyo zinadai kwamba amekuwa akitumia nyota za wasichana mbalimbali nchini kujipatia umaarufu.


Taarifa za ndani zilizonaswa na Papaprazi wetu kutoka kwa watu wake wakaribu zinadai kwamba msanii huyo ana amini katika ushirikina na kwamba anamganga wake wa kienyeji anayemtengezea nyota yake, kutokana na nyota za wasichana anao kuwa nao kimapenzi, ambapo anatumia nguo zao za ndani ,leso zao za kujifutia jacho pamoja na picha zao za kiganjani.

Taarifa zaidi zinaeleza kwamba baada ya Diamond kupeleka vitu hivyo kwa mganga wake, ambaye huviingiza katika luninga yake na kupiga ramri yenye nguvu ya kutambua nyota za msichana husika, baada ya hapo Diamond hudumu na msichana huyo mpaka atakapobaaini kwamba amekomba bahati zake zote kisha anatafuta sababu za kumuacha.

"Diamond hafai kabisa ni mshirikina ni mchawi, anaroga watu hususan wanawake,Diamond akikutaka kimapenzi ujue kwamba ukiachana naye lazima ufirisike ama uyumbe na kama ukiwa maarufu lazima umaarufu wako uporomoke, epu fanya utafiti kuanzia kwa wasicha wote aliowahi kutembea nao, tangu alipopata umaarufu mfano, alipokuwa na Wolper kila mtu anajua maisha ya Wopler pamoja na umaarufu wake ulivyokuwa,mtizame Wolper alivyo hivi sasa kama vile kachanganyikiwa"kilisema chanzo chetu na kuongeza:



DIAMO1.PNG


diamondd.PNG


Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya Tanzania Diamond Platnumz
"Mtizame Jokate wakati akiwa na Diamond maisha yake yalikuwaje, Jokate alikuwa na maisha ya juu lakini tangu alipoachana naye tu mambo yake yakaanza kuyumba, kuliko alivyokuwa awali, mtu mwingine ni Penny ambaye ni mtangazaji wa Luninga ya DTV, yule demu ukimwona hivi sasa huwezi kuamini, kwanza amechanganyikiwa kabisa, mtu mwingine ni Wema Sepetu kila siku ni majanga, inasemekana kwamba nyota ya Wema bado ina nguvu kwa Diamond kuliko wanakwake zake wote, lakini kwa masharti ya mganga wake ni kukaa na kila msichana kwa muda usiozidi miaka miwili ndiyo maana Wema bado anamuota Diamond hadi leo".

Hata hivyo Chanzo hicho kilidokeza kwamba, msanii huyo amegonga mwamba kwa Lulu kwa sababu Lulu hivi sasa anadaia kuwa na mtalaam mmoja mkali anayemtengenezea mambo yake, tangu alipo haribu nyota yake kutokana na kifo cha Kanumba na kwamba moja ya masharti yake kwa sasa ni kutokuwa na mahusiano ya kimapenzi na Diamond kwa sababu msanii huyo ndiye aliyempa mikosi tangu alipokuwa na Kanumba.

"Kama utakumbuka vizuri siku ya ugonvi wa Kanumba na Lulu kabla ya kifo kutokea Lulu alikuwa na ahadi ya kukutana na Diamond na akawa na mipango ya kutoroka usiku lakini kwa kuwa jamaa alishtukia mpango wake akawa anajaribu
 
Hao waganga anawajua yeye tu?acheni wivu wa kivivu,mtu akifanikiwa lazima mseme maneno ya kivivu,nenda nawe kaloge,tuone kama utaweza kuimba kama dogo au umpite kabisa.
 
Ina maana huyo mganga ame-specialize kwa Diamond peke yake, au? Hakuna bahati mbaya duniani kama kuzaliwa Mwafrika na ukawa na 100% Pure African Brain.
 
He is truly NUMBER ONE, at least for 2013. Wema is also her Best woman ever.
 
Halafu nyimbo kama hii halafu mtu useme Diamond anaroga ndo maana ana-hit!
Uchawi wa Diamond kwa mashabiki wake huu hapa
  • Ubunifu
  • Kujituma
  • Hakurupuki katika kazi zake
  • Anaelewa mashabiki wake wanataka nini
  • Anaheshimu na kuthamini kazi yake
Uthibitisho Angalia Hapa "nataka kulewa"
 
Last edited by a moderator:
Diamond anajituma na anajua mziki halafu skendo zake zinampandisha chati
 
Uchawi wa Diamond kwa mashabiki wake huu hapa
  • Ubunifu
  • Kujituma
  • Hakurupuki katika kazi zake
  • Anaelewa mashabiki wake wanataka nini
  • Anaheshimu na kuthamini kazi yake
Uthibitisho Angalia Hapa "nataka kulewa"

Kbisaaaaaa; you're 100%+1 RIGHT!!
 
Last edited by a moderator:
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom