UCHAWI: Upo au haupo?

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,606
696,727
Mojawapo ya dhana zinazotikisa katika jamii yetu ni hii dhana ya uchawi KWAMBA UPO AMA HAUPO!...Na Kwakweli unapoongelea kuhusu uchawi unaonekana mtu usiyeelimika kabisa ama mtu fulani wa kuogopwa
Ndani ya dunia kuna;

1. Ulimwengu unaoonekana
Huu ni ulimwengu wa ithibati za kisayansi, ulimwengu wa formula, ulimwengu wa halisi (sio uhalisia) ulimwengu wa mwili wa nyama.,ulimwengu wa vinavyoonekana kwa macho na kugusika kwa mikono.

2. Ulimwengu usioonekana, ulimwengu usio na ithibati za kisayansi, ulimwengu wa roho, ulimwengu wa nafsi. Ulimwengu wa kiza... Ulimwengu huu ndio injini ya ulimwengu unaoonekana yaani ndio unaoendesha dunia ya sayansi na ithibati

4f80492adf3f0e6df2d1f5659f18f894.jpg


Sina tatizo hata kidogo na watu wasioamini uchawi kama hawamwamini Mungu mmoja (wapagani), lakini nina tatizo na mashaka makubwa na wale wenye imani kamili juu ya Mungu mmoja, muumba wa mbingu na nchi na vyote vilivyomo (ukiwemo uchawi)! Shida yao hii hapa! Aidha wanasoma misahafu yao kwa kukakiriri bila kuelewa, ama wanapotoshwa na wengine.....

Vile vile inawezekana kabisa wengi wanajichanganya kwenye kuamini uchawi kama dhana ya msingi na kuamini waganga wa kienyeji. ...iko hivi unaweza uamini katika uchawi lakini usiamini katika wachawi na waganga wa kienyeji
Maranyingi tumeona wale wasiomini wakitoa changamoto ya kurogwa kama kweli uchawi upo! Huku ni kupotoka kabisa na kukosa uelewa wa mambo..

Kuwepo kwa uchawi ni kitu cha kwanza lakini kuwepo na mtu akaweza kuutumia huo uchawi kwa muktadha fulani ni kitu kingine kabisa
Malumbano mengi pia yametokea kwenye kutaka ithibati za kuwepo kwa uchawi! Hizi ni fikra tengefu..

Ulimwengu wa roho ni software huwezi kuuona kwa macho ya mwili wala kuushika kwa mikono yako...tusichanganye vinavyoonekana na visivyoonekana, tukafanya hiki ndio kile na kile ndio kile
-simu unayo na unafanya mawasiliano yote ninini kinafanyika mpaka umudu kufanya hayo yote?

-Akili unayo na ukiulizwa hutabisha je ukiambiwa ionyeshe utaweza?
-Usingizi unao je kufumba macho ndio kulala usingizi?
Ni vema kuelewa kwama uchawi ni sehemu ya ulimwengu usioonekana, upo lakini hauna ithibati za kisayansi kwakuwa huwezi kuushika nk ....

Kama ilivyo nguvu iliyopo kwenye mashine yoyote ana mwanga kwenye taa yoyote ama software kwenye kifaa chochote cha kielectronic...kama ulivyo uhai ndani ya mwili
Tafakari....!

Jr
 
Dah mkuu ni nitoe hofu kwanza hii si ndo mida yenyewe ya wanga? mimi nimeamka kula daku vp mwenzangu hukulala ama umeamka kwa kuandka uzi tuu?au u mchawi na kama sio mbna thread zako unapost mida hii ?nijb kaka mana nimeota ndoto mbya sana kabla ya kuamka araf nashka smu nakutana na post yako!
 
Dah mkuu ni nitoe hofu kwanza hii si ndo mida yenyewe ya wanga? mimi nimeamka kula daku vp mwenzangu hukulala ama umeamka kwa kuandka uzi tuu?au u mchawi na kama sio mbna thread zako unapost mida hii ?nijb kaka mana nimeota ndoto mbya sana kabla ya kuamka araf nashka smu nakutana na post yako!
Mimi sio mchawi wala mshirikina pia sio mwanga wala mlozi ila kazi yangu kuna wakati naingia shift...hivyo hupendelea kufanya meditation usiku mwingi kazi zinapopungua na baada ya hapo kuandika makala ili waliolala wakiamka wapate cha kusoma
Kwenye ulimwengu wa roho ndoto mbaya huja kati ya SAA saba usiku na SAA tisa kwakuwa ndio muda ambao roho zinazotangatanga huvinjari kwa wingi
 
Mimi sio mchawi wala mshirikina pia sio mwanga wala mlozi ila kazi yangu kuna wakati naingia shift...hivyo hupendelea kufanya meditation usiku mwingi kazi zinapopungua na baada ya hapo kuandika makala ili waliolala wakiamka wapate cha kusoma
Kwenye ulimwengu wa roho ndoto mbaya huja kati ya SAA saba usiku na SAA tisa kwakuwa ndio muda ambao roho zinazotangatanga huvinjari kwa wingi
Sawa mkuu nimetoka kuota mtu ananilazimisha kula nyama tena vipande vya nyama kama sikosei ni maini,nlpostuka jasho linantoka sna ,vp maana yake nini hii?yan nimechoka hadi dakika hii sielew elew mkuu ukzngatia npo mkoan
 
Sawa mkuu nimetoka kuota mtu ananilazimisha kula nyama tena vipande vya nyama kama sikosei ni maini,nlpostuka jasho linantoka sna ,vp maana yake nini hii?yan nimechoka hadi dakika hii sielew elew mkuu ukzngatia npo mkoan
Michezo ya wanga na wachawi shukuru Mungu hukula. ..watu wengi hulishwa nyama za watu na wa nyama kupitia ndoto kama hizo!
Ingetokea ukala kesho undeshinda vibaya huku tumbo likiwa limejaa na kujisikia hovyo hovyo tuu
 
mshana jr nitakushitaki, ohooooo. Nimesoma Makala yako nikiwa bado kitandani maana majirani wameniamsha wakigombea daku. Cha kushangaza nikasikia kama mtu anapiga jiwe juu ya bati, natoka nichungulie naona bonge la bundi linanitizama.....namuuliza wewe ni mshana jr akageuka kuwa kishada (kite) na kupotea ghafla. Eee bwana tusileteane masikhara kihivi, unatuogopesha wenzio.
 
mshana jr nitakushitaki, ohooooo. Nimesoma Makala yako nikiwa bado kitandani maana majirani wameniamsha wakigombea daku. Cha kushangaza nikasikia kama mtu anapiga jiwe juu ya bati, natoka nichungulie naona bonge la bundi linanitizama.....namuuliza wewe ni mshana jr akageuka kuwa kishada (kite) na kupotea ghafla. Eee bwana tusileteane masikhara kihivi, unatuogopesha wenzio.
 
ukitaka nijue kama upo au haupo hebu fanya rihanna awe mke wangu! au kama hauwezi mwambie mganga yoyote afanye hivyo
 

Similar Discussions

19 Reactions
Reply
Back
Top Bottom