Uchawi na muujiza ni mapacha

Kuna mambo mawili hayajakaa vizuri
1.Umekuwa ukirudiarudia kwamba uchawi na nduguyake miujiza,hilo neno siokweli bali uchawi aduiyake miujiza, na hawana udugu wowote.
2.Umetoa ushahidi wa kivitendo namna manabii wanatekeleza miujiza,lakini umeshindwa kuelezea namna wachawi wanavyotekeleza mambo,muda,vitu,mahala na kwa ikiwezekana hata kutaja jina la mchawi mwenyewe,kama Mwanamalundi n.k.
Mosi,,,,
Nimesema ndugu na sijasema marafiki,,,, katika hali ya kawaida marafiki wanagomba na kushindana ndio seuze kwa ndugu?

Nina mifano mingi ya ndugu wamekuwa hawapatani kabisa, mfano Yakobo na Esahu, walianza kupigana tangu wakiwa tumboni mwa mama yao.

Kwa hivyo ni sawa kabisa Uchawi na muujiza ndugu pamoja na kwamba ni maadui. Kwanini nasema ndugu????

Nasema ndugu sababu uchawi haukujiumba, alikadhalika muujiza pia haukujiumba, bali vyote viwili vimeumbwa na Mungu mwenyewe.

Kuna baadhi ya watu wanataka kutuaminisha kuwa shetani kaumba uchawi, si kweli, shetani uchawi kaukuta, anachofanya shetani ni kuutumia tu.

Katika mada yangu ya msingi nimetaja aya kadhaa za kutoka katika biblia na quran zikionesha Mungu ni muumba wa kila kitu(uchawi moja kati ya vitu hivyo)

Ndio maana Mfalme Suleiman amesema katika methali zake kuwa "Bwana amefanya kila kwa kusudi lake, hata ubaya kwa siku ya ubaya"

rejea mithali 16:4

Pili.
Si kweli kuwa nimeshindwa kutoa ushahidi wa vitendo jinsi watu walivyokuwa wanafanya uchawi kwa mujibu wa biblia, naomba soma vizuri mada yangu unaweza kuona.

Nimeeleza jinsi Farao alivyotumia waganga kufanya uchawi kupambana na Mussa, Watu wa Farao walifanya uchawi ili kugeuza fimbo zao kuwa nyoka.

Kwa kuongezea hapo, Sauli baada ya kukataliwa na Mungu, na baada ya kukosa neno la unabii juu ya nini anatakiwa kufanya na nini asifanye, alienda kwa mganga wa kienyeji, ambaye alikuwa anatumia pepo wa utambuzi (jini mpiga ramli), ili aweze kuwasiliana na Samweli ambaye tayari ameshakufa, ili sasa Samweli amweleze nini anatakiwa kufanya.

Yule mganga aliweza kuitafuta roho ya Samweli kwa kutumia uchawi, na akaiona na kaongea naye, na hapo Sauli akajua nini atakiwa kufanya.

Rejea 1 Samweli 28:3-14

Hata hivyo, huenda hoja yako ni kuwa, biblia haijaonesha ni mambo gani ya kiuchawi walifanya watu Farao katika kugeuza fimbo kuwa Nyoka au mambo gani ya kichawi alifanya yule mwanamke mwenye pepo la utambuzi hata akaweza kuongea na roho ya Samweli.

Kama ndio hoja yako.

A. Elewa biblia na quran hazijaacha kitu juu ya ulimwengu, ila vitabu hivi havijaandika kila kitu kwa kina, na kama kitabu kimoja kingeandika kwa kina kila kitu, ukubwa kitabu hicho ungeizidi si dunia yetu tu lakini mfumo mzima wa jua(solar System)

Mathalani, "Mungu akasema iwe nuru"

Hivi ni kweli kuwa Mungu aliposema iwe nuru na nuru ikawa? Hakuna jambo lolote lilofanyika zaidi ya hiyo kauli? Kuna mambo yalifanyika na hapa nataka nikupe ushahidi.

HAPA KUNA NAMNA MBILI
NAMANA YA KWANZA.

Kwa mujibu wa biblia tunaweza kusema kuwa mungu alitumia siku moja kuumba NURU.

Lakini kwa mujibu wa biblia pia siku moja kwa mungu kwetu ni miaka elfu moja. Kama ndivyo tunaweza kusema kuwa Mungu alitumia miaka eflu moja kuumba NURU, hivi kwa miaka yote hii eflu moja Mungu alikaa tu au kuna mambo alokuwa anayafanya kuhakikisha NURU inakuwa? jawabu ndio, na uumbaji wa mungu ni zaidi ya "kuwa" kisha ikawa.

NAMNA YA PILI.

huenda kweli pia kuwa Mungu aliumba NURU kwa kitendo cha kufumba na kufumbua, yaani, "kuwa" kisha ikawa.

Lakini kwa nikirejea kuwa siku moja kwa mungu kwetu sawa na miaka elfu, na jaalie kitendo cha kufumba na kufumbua ni sawa na kitendo cha sekunde moja, kwa hivyo hapo ni sawa na kujiuliza sekunde moja kwa mungu kwetu ni sawa muda gani? ukikokotoa mahesabu utapata sekunde moja kwa mungu kwetu sawa siku 4 na masaa yake matatu.

Kwahivyo naweza kusema kufumba nakufumbua kwa mungu kwetu ni sawa na siku 4. Hivi kwa kusiku nne zote Mungu alitumia kutamka "kuwa nuru" alitamka alafu kukawa hakuna mambo mengine yanafanyika? Jawabu kuna mambo yalikuwa yanafanyika kinyume chake hakuhitaji siku nne.



ZINGATIA: kila kitu kipo ndani ya quran, lakini quran haijaandika kila kitu. Hata biblia pia.

B.
Mungu hapendi tuujue au tuufanye uchawi, ndio maana katika vitabu vyake amefafanua zaidi jinsi muujiza unavyofanyika na kuushinda uchawi lakini haoneshi jinsi uchawi unavyofanyika.

Mathalan wakati Mungu anataka kuwakomboa wana Israeli kutoka Misri alipata ushindani mkubwa sana kutoka kwa uchawi, lakini ule uchawi ulio kuwa unashinda na muujiza hatukuoneshwa bali tulioneshwa muujiza tu kupitia mapigo kumi na mbili.

Pigo la mwisho wana wa Israeli walitakiwa wachinje kondoo au mbuzi, wale wakiwa wamesimama, na mboga za uchungu, damu wapake katika miimo ya milango. Lakini wakati wana wa Israeli wanafanya hivi wachawi wa Farao kuna yao wakuwa wanayafanya si biblia wala si quran ilo onesha kinagaubaga nini Wachawi wa Farao walikuwa wanafanya.

Vitabu hivi vinaonesha kushindwa kwa Farao baada ya kila mzaliwa ea kwanza wa Misri kufa.

ILA UJUE.
Yale walio kuwa wanayafanya wamisri waliya rekodi katika vitabu vyao na mengi waliyaandikia vitabu maalum vya uchawi vya ngazi(hatua au milango) mbalimbali.

Mfano kuna kitabu cha uchawi, book of spells kinaitwa "Book of Dead" kilianza kutumika na wamisri kwenye mwaka 1550BC na baadhi ya spells zilianza kutumika na wamisri wenyewe zaidi ya miaka 1500 kabla hata ya kuandikwa kitabu hicho.

Ikiwa Mussa alizaliwa mwaka 1400 BC utagundua kitabu kilikuwako kabla hata ya Mussa kuzaliwa. Yaliyo andikwa katika kitabu hichi hayakuandikwa kitika biblia wala quran. Na kwa kupitia kitabu hiki ndipo pakapatikana vitabu vingi vya uchawi na ramli mfano satal habar.

Ngoja niishie hapa, sababu nachelea kuingilia sehem ya pili ya mada yangu, ambayo hivi karibuni nitaanza kuandika.
 
Kwahiyo mungu wa wakristo ndio kaumba mwanadamu?

Na miungu wengine ni feki sio?People are christian-centric....

Kuna dini za mungu mmoja na kuna dini za miungu wengi,kuna madhehebu zaidi ya 30,000 ya kikristo,bado millions of other religions na kila dini ina amini mungu wake ni sahihi wa wengine ni hovyo....ya nini tuamini mmoja na kumkubali mwingine?Kuna uwezekano mmoja akawa wa kweli na wengine wakawa feki?Wa kweli ni yupi?Hatutakaa tujue,kwavile umelelewa kwa mfumo wa abrahmic religion point of view utasema ni ukristo au uislam,kumbuka china,india,japan,russia,etc hawatambui huu ujinga wa abrahmic religilions,na it is not their fault...dini zote ni za kufuta period!

Kuna makanisa 37,000 ya kikristo! Kwa kuwa hayapatani katika mafundisho yao huenda kila kanisa lina mungu wake maana Biblia inasema Mungu si wa machafuko.Ndiyo maana wengine husema Yesu ndiye Mungu,Wengine Roho mtakatifu ,wengine Mungu baba,wengine Utatu mtakatifu.Jibu la Biblia ni Yehova ndiye Mungu wa kweli Muumba wa Mbingu na Dunia.Zaburi 83:18,Kutoka 6:2
 
kwanza nipende kumpongeza kipekee mtoa mada kwa kufikiri sana na kuibuka na andiko hili refu sana lenye mrengo wa kidini ambao kwa kweli amekiri ndio msingi wa andiko lake hili kwanza ameweka msawazo kwenye uwanja wa hoja kwa kuainisha nguvu mbili zinazosukuma mambo duniani yaani UCHAWI na MIUJIZA,sina shaka kukukubaliana na maana alizodadavu kuhusu Dhana hizi mbili na ya kwamba ni nani wapo nyuma wakipull strings ili yatokee yanayoitwa MIUJIZA na UCHAWI pia nakubaliana kimsingi kabisa na hoja ya UCHAWI kama ni udenguzi ama ukiushi wa kaida zinazoongoza mambo yatokee katika maumbile ya kawaida lakini yakisimamiwa na mkuu wa nguvu za giza lakini umejichanganya ulipokuwa ukijibu hoja za ndugu tofyo
ukasema mwazilishi wa uchawi sio shetani kwa maana ameukuta uchawi na hivyo akautumia kuenda kinyume na Maumbile halisi ambayo Mungu aliyaumba
excuse me!!!!
Biblia inamtaja shetani kama muasisi wa dhambi(uchawi)maana dhambi ni uasi wa sheria na sheria ndio msingi wa maisha ya binadamu
mkuu wa Miujiza ambaye ameshikilia Sheria zinazoongoza maisha ya sayari na ulimwengu wote yaani Mungu ndiye hasa wa kuinuliwa juu ya muujiza wowote ule unaotendeka kwa jina la Yesu.
Shetani alichofanya ni kuleta Bandia miujiza bandia,Neno bandia theology bandia na sheria bandia ili tu kutaka kujitwalia kiti cha Mungu pambano kubwa sana ambalo Binadamu anagombaniwa hapa lilianzia mbinguni chanzo kikuu ni Ibada shetani akitumia mtindo wake wa kwanza ushawishi.
Akatupwa toka huko Mbinguni wala mahali pake hapakuonekana huko mbinguni.
Kwahivyo swala la uchawi ni swala la shetani kikwelikweli kabisa hapakuwahi kuwa na mauzauza mahali pengine kabla shetani hajaasi mbinguni
ikumbukwe alikuwa malaika wa nuru hivyo nguvu na uwezo wake havikutwaliwa toka mikononi mwake.
pambano na Uchawi na miujiza linaenda likishabihiana kabisa na Dhana ya WEMA na UOVU/UBAYA hili ndio pambano kubwa hasa la leo tunapoelekea mwisho wa wakati
Swali la kujiuliza ni je Umepata nguvu ya kimungu ili ubainishe bayana dhana hizi mbili maana wapo waalimu wengi humu duniani wenye mfano wa Utakatifu lakini wakizikana nguvu za Mungu
Hitimisho!
katika muujiza wowote jiulize?
Waende sawasawa na sheria(torrah) na Shuhuda(yale ambayo manabii wa haki wa MwenyeziMungu wameyaandika)kama hawasemi sawasawa kwao hapana asubuhi!
 
Cjamaliza kusoma Inaboa sana. All I can say Acheni Uchawi kama mnataka kujifunza. Mungu ni mmoja tu.
 
Mtoa mada yupo vizuri anajua anachokisema kwakweli..hateterki mana kapigwa swali hapo kajibu mpaka nacheka mwenyewe...vitu vyenye mantiki kabisa..inatakiwa kufikiri zaidi na zaidi..asantr sana mtoa mada
 
kwanza nipende kumpongeza kipekee mtoa mada kwa kufikiri sana na kuibuka na andiko hili refu sana lenye mrengo wa kidini ambao kwa kweli amekiri ndio msingi wa andiko lake hili kwanza ameweka msawazo kwenye uwanja wa hoja kwa kuainisha nguvu mbili zinazosukuma mambo duniani yaani UCHAWI na MIUJIZA,sina shaka kukukubaliana na maana alizodadavu kuhusu Dhana hizi mbili na ya kwamba ni nani wapo nyuma wakipull strings ili yatokee yanayoitwa MIUJIZA na UCHAWI pia nakubaliana kimsingi kabisa na hoja ya UCHAWI kama ni udenguzi ama ukiushi wa kaida zinazoongoza mambo yatokee katika maumbile ya kawaida lakini yakisimamiwa na mkuu wa nguvu za giza lakini umejichanganya ulipokuwa ukijibu hoja za ndugu tofyo
ukasema mwazilishi wa uchawi sio shetani kwa maana ameukuta uchawi na hivyo akautumia kuenda kinyume na Maumbile halisi ambayo Mungu aliyaumba
excuse me!!!!
Biblia inamtaja shetani kama muasisi wa dhambi(uchawi)maana dhambi ni uasi wa sheria na sheria ndio msingi wa maisha ya binadamu
mkuu wa Miujiza ambaye ameshikilia Sheria zinazoongoza maisha ya sayari na ulimwengu wote yaani Mungu ndiye hasa wa kuinuliwa juu ya muujiza wowote ule unaotendeka kwa jina la Yesu.
Shetani alichofanya ni kuleta Bandia miujiza bandia,Neno bandia theology bandia na sheria bandia ili tu kutaka kujitwalia kiti cha Mungu pambano kubwa sana ambalo Binadamu anagombaniwa hapa lilianzia mbinguni chanzo kikuu ni Ibada shetani akitumia mtindo wake wa kwanza ushawishi.
Akatupwa toka huko Mbinguni wala mahali pake hapakuonekana huko mbinguni.
Kwahivyo swala la uchawi ni swala la shetani kikwelikweli kabisa hapakuwahi kuwa na mauzauza mahali pengine kabla shetani hajaasi mbinguni
ikumbukwe alikuwa malaika wa nuru hivyo nguvu na uwezo wake havikutwaliwa toka mikononi mwake.
pambano na Uchawi na miujiza linaenda likishabihiana kabisa na Dhana ya WEMA na UOVU/UBAYA hili ndio pambano kubwa hasa la leo tunapoelekea mwisho wa wakati
Swali la kujiuliza ni je Umepata nguvu ya kimungu ili ubainishe bayana dhana hizi mbili maana wapo waalimu wengi humu duniani wenye mfano wa Utakatifu lakini wakizikana nguvu za Mungu
Hitimisho!
katika muujiza wowote jiulize?
Waende sawasawa na sheria(torrah) na Shuhuda(yale ambayo manabii wa haki wa MwenyeziMungu wameyaandika)kama hawasemi sawasawa kwao hapana asubuhi!
Kama Mungu hakuumba uchawi basi pia ukubali Mungu hakuumba kila kitu, pamoja na hayo una ushahidi wowote kuonesha kuwa Ibilis kaumba uchawi?
 
Mtoa mada nashukuru kwa jibu lako zuri.lakini kusudio "A" la swali langu linaowana na dhamira "B" ya swali langu.
Rejea kauli hii"mchawi au miujiza anatakiwa ajue anataka kufanya nini,wapi na vitugani vinavyotakiwa kuchanganya"ambayo umeiweka hapo juu.
sasa katika muktadha huo umeelezea yesu alivyochanganya tope,kisha ukaonyesha ya Ezekieli na kunyoa kwa panga na kufanya alivyofanya.Lakini hii ni upande mmoja wa miujiza.sasa ilituweze kufanya comperative ya Udugu au Umapacha kama ulivyosema,naomba unionyeshe na mchanganyo na vitu vinavyotumika kwenye uchawi.
Katika hoja hii ni kwamba Mungu kaumba kilakitu lakini suala la udugu au mapacha ni mpaka hivyo vitu viwe vinanasaba iliosawa.Kwasababu Tui la nazi linafanana na maziwa kwani vitu hivyo ni ndugu????lakini nini nasaba zao???
Ninachokitaka mimi unionyeshe udugu wao.na sinashaka kwamba nguvu hizi zinatoka kwa mmoja.Lakini kama miujiza ilikuja kama hoja ya kupinga uchawi since kwamba uchawi unatumiwa kama hoja kupotosha watu .wapi uduguwao?
 
Uchawi, miujiza, mazingaombwe, kiini macho.... Vyote hivi ni kitu kimoja. Ni kama vile unakuta mtu ana jina la utani, Jina la ubatizo, jina la mtaani nk
 
Mtoa mada nashukuru kwa jibu lako zuri.lakini kusudio "A" la swali langu linaowana na dhamira "B" ya swali langu.
Rejea kauli hii"mchawi au miujiza anatakiwa ajue anataka kufanya nini,wapi na vitugani vinavyotakiwa kuchanganya"ambayo umeiweka hapo juu.
sasa katika muktadha huo umeelezea yesu alivyochanganya tope,kisha ukaonyesha ya Ezekieli na kunyoa kwa panga na kufanya alivyofanya.Lakini hii ni upande mmoja wa miujiza.sasa ilituweze kufanya comperative ya Udugu au Umapacha kama ulivyosema,naomba unionyeshe na mchanganyo na vitu vinavyotumika kwenye uchawi.
Katika hoja hii ni kwamba Mungu kaumba kilakitu lakini suala la udugu au mapacha ni mpaka hivyo vitu viwe vinanasaba iliosawa.Kwasababu Tui la nazi linafanana na maziwa kwani vitu hivyo ni ndugu????lakini nini nasaba zao???
Ninachokitaka mimi unionyeshe udugu wao.na sinashaka kwamba nguvu hizi zinatoka kwa mmoja.Lakini kama miujiza ilikuja kama hoja ya kupinga uchawi since kwamba uchawi unatumiwa kama hoja kupotosha watu .wapi uduguwao?
nitakuja inshallah
 
Ukisoma Biblia inasema ni Yehova.Zaburi 83:18
Ukisoma Quran inasema ni Allah.
Biblia ilianza kuandikwa mwaka 1513 BCE Yaani miaka 2,000 kabla ya kuran kuandikwa.Quran inanukuu vifungu vingi kutoka katika Biblia kama mada inavyoonyesha.
kwa hiyo Biblia imetangulia Quran.
Hivi wewe unajua maana ya ALLAH?? WAKRISTO WA MASHARIKI YA KATI UNAJUA KUSEMA MUNGU WANASEMAJE?? Kwa taarifa yako tamko Allah kwa kiswahili maana yake ni Mwenyezi MUNGU na wakristo wanaotumia lugha ya kiarabu husema Allah wakimaanisha Mwenyezi MUNGU. Jifunze utaelewa. Ulichoeleza hapo ni kama vile kusema Almighty GOD na Mwenyezi MUNGU ni vitu tofauti kumbe ni kitu kimoja tofauti ni lugha. Mwenyezi MUNGU jina lake limejipambanua kwa sifa zake. Huwezi kusema MUNGU wangu ni mbuzi muumba wa mbingu na ardhi, wenzako watamchinja yule mbuzi wamle nyama halafu watakuuliza mungu wako tumemla utampata wapi mungu mwingine!! Kama Ibrahimu alivopasua masanamu akaacha limoja, walivomuuliza nani kafanya hivyo?, akasema, liulizeni lile kubwa lao kama lenyewe ni MUNGU na lisema nani kawavunja wenzake; wakashikwa na aibu kubwa maana halikuweza kuongea wala kuwatetea wala kuwadhuru! Kwa mantiki hiyo nadiriki kusema Mwenyezi MUNGU kajipambanua kwa sifa zake sio kwa jina, ukitaka kumwita jina lake wala usipate taabu, unawezatumia sifa zake kwa kusema tu "Ee Muumba wa Mbingu na ardhi..." aliyeumba mbingu na ardhi atakuitikia sawasawa na imani yako juu yake.
Ni vyema ifahamike kuwa Quran haijawahi kukataa ukristo wala uyahudi na wala usilamu si dini mpya bali ni dini ileile ya Ibarahim na Ismail na Is haka na Yakobo na mitume na manabii. Wala Quran si neno jipya bali linasadikisha yaliyokuwepo kabla yake na ni ukumbusho kwa wachamungu waliopotoka. Ukumbuke wachamungu walikuwepo kabla hata ya kuja muhammad na neno la Mwenyezi MUNGU lilikuwepo tangu zama za Nuhu, lkn wengi katika wachamungu walikuwa kwa nyakati fulani wanaanza kwenda kinyume na maandiko au wanashindwa kutafsiri maandiko, huvyo Mwenyezi MUNGU alikuwa akiwaleta mitume kwa nyakati tofauti kulikumbushia neno lake lililokuwepo tangu awali na kuwaelekeza mengine mapya. Labda nikukumbushe kuwa mitume wote walitamka neno moja tu "Mcheni Mwenyezi MUNGU na nitiini mimi" Hapana mtume ama nabii yeyote aliyewahi sema "nicheni mimi" ama "muabuduni asiyekuwa Mwenyezi MUNGU". Ipo wazi kabisa kuwa MUNGU wa wachawi na wasio na dini na wenye dini na wema na waovu ni MUNGU mmoja tu, yeye ameumba kila kitu na kwake tutarejeshwa sote.
Quran ipo wazi kabisa kuwa kabla yake vilikuwepo vitabu vya Injiri, torati, na zaburi na vingine vilivyoshuka kwa manabii wengi waonyaji. Kifupi wakristo na waislamu tofauti zetu zimejikita kwenye namna ya kumfikia huyu muumba na kamwe hatuna muumba tofauti na Mwenyezi MUNGU aliyeumba mbingu na nchi na vyote vilivyomo.
Aidha, quran haijanukuu vifungu vya biblia hata kimoja ila imenukuu baadhi ya matamko ya manabii moja kwa moja waliyoyatamka kuwaambia watu wao. Ikumbukwe kuna manabii wametajwa kwenye quran lkn biblia haijawahi kutamka na kuna matendo ya manabii yametajwa kwenye quran lkn biblia hajawahi kutamka; mfano Yesu kuumba ndege ipo kwenye quran lkn biblia ipo silent; yesu kuzungumza katika uchanga wake ipo kwenye quran lkn biblia haijawahi kutamka. Ni kukosa uelewa kusema quran imenukuu biblia.
 
Mhhh hapa inabidi mtu akimbie.
Maswali mengine magumu hadi mtu anazikataa aya za kitabu kitakatifu kinachosema Mwenyezi MUNGU kaumba kila kitu including wema na ubaya. Mimi naamini Mwenyezi MUNGU kaumba kila kitu hadi uchawi. Na uchawi hauna mamlaka ya kufanya kazi popote ila hadi yeye aridhie. Hebu tupate nukuu kutoka kwenye Quran;
"Hakika shetani hana nguvu (mamlaka) juu ya walioamini na wanaomtegemea Mola wao" (quran 16: 99)
"Wala mchawi hafaulu popote afikapo" ( Quran 20: 69).
"Mwenyezi MUNGU ndiye muumba wa kila kitu na Yeye ndiye mlinzi wa kila kitu" (Quran 39: 62).
Kwa waliomwasi Mwenyezi MUNGU ridhaa ya wao kukumbwa na uchawi ipo wazi kwa maana wao hawamtegemei Mola wao hivo shetani ana nguvu juu ya nafsi zao. Adha, hata wanao mchamungu uchawi unaweza kuwapata kama mtihani kwao mfano ni Nabii Ayubu alilogeka, Mwenyezi MUNGU aliruhusu nguvu za shetani zifanye kazi kwake na alifaulu mtihani huu hatimaye Mwenyezi MUNGU alimponya na kumuinua zaidi.
 
Mtoa mada nashukuru kwa jibu lako zuri.lakini kusudio "A" la swali langu linaowana na dhamira "B" ya swali langu.
Rejea kauli hii"mchawi au miujiza anatakiwa ajue anataka kufanya nini,wapi na vitugani vinavyotakiwa kuchanganya"ambayo umeiweka hapo juu.
sasa katika muktadha huo umeelezea yesu alivyochanganya tope,kisha ukaonyesha ya Ezekieli na kunyoa kwa panga na kufanya alivyofanya.Lakini hii ni upande mmoja wa miujiza.sasa ilituweze kufanya comperative ya Udugu au Umapacha kama ulivyosema,naomba unionyeshe na mchanganyo na vitu vinavyotumika kwenye uchawi.
Katika hoja hii ni kwamba Mungu kaumba kilakitu lakini suala la udugu au mapacha ni mpaka hivyo vitu viwe vinanasaba iliosawa.Kwasababu Tui la nazi linafanana na maziwa kwani vitu hivyo ni ndugu????lakini nini nasaba zao???
Ninachokitaka mimi unionyeshe udugu wao.na sinashaka kwamba nguvu hizi zinatoka kwa mmoja.Lakini kama miujiza ilikuja kama hoja ya kupinga uchawi since kwamba uchawi unatumiwa kama hoja kupotosha watu .wapi uduguwao?
Hebu jiongeze kidogo nawewe mkuu. Udugu wao ni kuwa aliyeumba hivyo ni mmoja ambaye ni Mwenyezi MUNGU. Tofauti yao ni kuwa watumiaji ndio wako tofauti, waliomwasi Mwenyezi MUNGU hutumia uchawi na wanaomtii Mwenyezi MUNGU hutumia muujiza. Anayewahadaa wanadamu watumie uchawi si yeye muumba bali ni yule mwovu mdanganyifu shetani
 
Mtoa mada upo vzuri sana. Hongera kwa taaluma hii. Umeshuka vitu hadi akili inakubali.
 
Muendelezo afu mbona whatsap haupo?
View attachment 352087

View attachment 352088

UCHAWI na MUUJIZA ni masuala tata katika jamii, pamoja na utata wake lakini yamekuwa ni masuala ya kawaida kusikika. Ni kawaida kusikia fulani ni mchawi au nimefanyiwa uchawi. Pia ni kawaida kusikia kuwa fulani ana miujiza au nimefanyiwa miujiza. Uchawi ni nini? Muujiza ni nini? Ipi tafauti kati ya uchawi na muujiza?

Kwanza kabisa naomba nikiri mapema kuwa, mambo haya ni ya kiimani zaidi. Kwakuwa ni ya kiimani, na mimi ufafanuzi wangu utategemea rejea za imani zinazokubali uwepo wa uchawi na muujiza, hususani toka kitabu cha qur-an na biblia.

Katika dini zote, hadi zile za kipagani, zina amini kuwa ulimwengu na vilivyomo ndani yake vimeumbwa na MUNGU. Si ukweli hata kidogo kuwa mungu ni mmoja, kwani kuna watu wanasema kuwa mungu ni mmoja.

Kila dini iko na mungu wake, na kila dini inaamini kuwa mungu wake ndiye aliyeumba ulimwengu na vilivyopo ndani ya huo ulimwengu. Kwakuwa kila dini iko na mungu wake, na kwakuwa dini ziko nyingi, iweje sasa mungu awe mmoja?

“Sema: Enyi makafiri! Siabudu mnacho kiabudu; Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu. Wala sitaabudu mnacho abudu. Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu. Nyinyi mna dini yenu, nami nina Dini yangu.” Qur-an 109:1-6

“Wakamwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri, wakafuata miungu mingine, baadhi ya miungu ya watu wale waliokaa karibu nao pande zote, wakajiinamisha mbele yao; wakamkasirisha Bwana, akaghadhibika. Wakamwacha Bwana, wakamtumikia Baali na Maashtorethi” Waamuzi 2:12-14

Pamoja na mambo mengine aya hizo kutoka katika qur-an na biblia zinatufunza kuwa, kuna miungu mingi na dini ziko nyingi pia. Kila mtu anaona mungu wake yuko sahihi kuliko mungu wa mwenziwe. Jambo la kuzingatia ni hili, kwa kiwango kile ambacho mtu huona mungu wake ni sahihi, basi ni kwa kiwango hicho hicho mungu huyo huonekana na watu wengine si lolote.

Si lengo la andishi hili kuelezea miungu na dini sanjari na uhalali wake, lakini nimelazimika kuelezea kwa kifupi ili nikija kuzungumzia masuala ya nani hasa aliyeumba ulimwengu nisiwachanganye watu.

Nataka watu wajue kuwa MUNGU ndiye aliumba ulimwengu, huyo mungu anaweza kuwa Yesu, Allah[s.w], Yehova, mzimu, mlungu, nk. Hii itategemea katika dini yako mungu wako ni nani, kama ni Yesu, basi Yesu ndiye atakayekuwa kaumba ulimwengu kwa mujibu wa imani yako, na si vinginevyo!

Mungu ameumba ulimwengu, ulimwengu ambao umegawanyika katika mapute mawili. Pute la kwanza linaundwa na maada(matter & dark matter) Pute la pili limeundwa na sheria zinazotawala hizo maada(energy & dark energy).

Ndani ya sheria za kimaumbile kuna proglamu zinazoamrisha[command] maada zifanye yale tunayoyajua na tusiyoyajua. Cha kuzingatia ni kuwa, hizi sheria ni sehemu ya ulimwengu, na zimeumbwa makhususi ili kuzifanya maada zisikiuke matakwa ya MUNGU.

Upande wa maada ndio kuna (matter &dark matter)
Upande wa sheria za kimaumbile ndio kuna (energy & dark energy)

Vyote kwa pamoja ndio vinafanya ulimwengu.

“Je! Waweza kuziongoza Sayari kwa wakati wake? Au waweza kuongoza Dubu na watoto wake? Je! Unazijua amri zilizoamuriwa mbingu? Waweza kuyathibitisha mamlaka yake juu ya dunia?” Ayubu 38:32-33

“Hakika Mola Mlezi wenu ni Mwenyezi Mungu aliye ziumba mbingu na ardhi katika siku sita. Kisha akatawala juu ya Kiti cha Enzi. Huufunika usiku kwa mchana, ufuatao upesi upesi. Na jua, na mwezi, na nyota zinazo tumika kwa amri yake. Fahamuni! Kuumba na amri ni zake. Ametukuka kabisa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote” qur-an 7:54

Hiyo “amri ” inayotajwa katika aya hizo ndio sheria za kimaumbile(energy &dark energy), yaani nguvu za mvutano na zinginezo ambazo zipo kuyaongoza magimba na nyota mbali mbali zipite katika njia ambazo zimepangiwa na zifanye mambo yaliyoamriwa kuyafanya. Sheria hizo ndizo zinazotawala maada yanayounda ulimwengu.

Hizi sheria za kimaumbile zilianza kuumbwa kabla hata ya ulimwengu kuwako. Ni vigumu sheria hizi kuvurugwa au kushindwa dhidi ya vitimbi vya waja. Mfano, mtu anapochinjwa shingo hata kichwa kitengane na kiwiliwili ni lazima huyo mtu afe, sababu sheria za kimaumbile zinazotawala mwili huamrisha[command] mwili ufe pindi ukipatwa na tukio hilo. La kuzingatia ni kuwa, kila kitu na kila tukio hutawaliwa na sheria za kimaumbile.

Pamoja na ugumu uliopo katika kuzikiuka na kuzishinda sheria za kimaumbile haiondoi ukweli kuwa watu, majini, malaika na mungu mwenyewe wamekuwa wakizikiuka na kuzishinda sheria hizi mara nyingi tangu ziliposimikwa.

Uchawi ni nini? Uchawi ni ile hali ya kukiuka au kuzishinda sheria za kimaumbile pasina kupata kibali au ruhusa kwa mmiliki wa sheria hizo. Mmiliki wa sheria hizo Mungu. Mtu yoyote anayekiuka au kuzishinda sheria hizo katika muktadha huo huitwa MCHAWI.

Mfano mtu akichinjwa katika namna niliyoeleza hapo juu, na bado akiendelea kuwa hai huku kichwa kikilalamika kwa kitendo cha kuchinjwa, basi jua kuwa sheria za kimaumbile zimekiukwa na kushindwa kufanya kazi yake. Tukio hilo litakuwa ni uchawi endapo aliyefanikisha ukiukwaji na ushindwaji wa sheria hizo hakupewa kibali na ruhusa toka kwa Mungu.

Muujiza nini? Muujiza ni ile hali ya kukiuka au kuzishinda sheria za kimaumbile kwa kupata kibali na ruhusa toka kwa mmiliki wa sheria hizo. Tukio nililolitaja hapo juu, la mtu kuchinjwa na kisha kichwa chake kilalamike kwa kufanyiwa hivyo, utakuwa ni muujiza endapo aliyefanikisha ukiukwaji na ushindwaji wa sheria hizo alipata kibali na ruhusa toka kwa Mungu.

“Bwana akanena na Musa na Haruni, akawaambia, Farao atakaponena nanyi, na kuwaambia, Jifanyieni miujiza; ndipo utakapomwambia Haruni, Shika fimbo yako, uibwage chini mbele ya Farao, ili iwe nyoka. Basi Musa na Haruni wakaingia kwa Farao, wakafanya vivyo kama Bwana alivyowaambia; Haruni akaibwaga fimbo yake chini mbele ya Farao, mbele ya watumishi wake, ikawa nyoka. Ndipo Farao naye akawaita wenye akili na wachawi; na hao waganga wa Misri wakafanya vivyo kwa uganga wao. Wakabwaga chini kila mtu fimbo yake, nazo zikawa nyoka; lakini fimbo ya Haruni ikazimeza fimbo zao.” Kutoka 7:10-12

“Wakasema: Ewe Musa! Je! Utatupa wewe, au tutakuwa sisi wa kwanza kutupa? Akasema: Bali tupeni nyinyi! Tahamaki kamba zao na fimbo zao zikaonekana mbele yake, kwa uchawi wao, kuwa zinapiga mbio. Basi Musa akaingia khofu nafsi yake. Tukasema: Usikhofu! Hakika wewe ndiye utakaye shinda. Na kitupe kilicho katika mkono wako wa kulia; kitavimeza walivyo viunda. Hakika walivyo unda ni hila za mchawi tu, na mchawi hafanikiwi popote afikapo. Basi wachawi wakaangushwa wanasujudu. Wakasema: Tumemuamini Mola Mlezi wa Harun na Musa! “ Qur-an 20:65-70

Aya za hapo juu toka katika qur-an na biblia zinaelezea kisa cha Firauni na Musa[a.s] kwa ufupi. Watu wa Firauni walitupa fimbo na kamba zao, kisha zikageuka kuwa nyoka. Naye Musa[a.s] akatupa fimbo yake, nayo ikawa nyoka na ikawameza wale nyoka wengine. Kitendo cha fimbo kutoka katika umbile lake na kuwa nyoka ni kitendo kilichosababishwa na ukiukaji wa sheria za kimaumbile. Kitendo hichi alipokifanya Musa[a.s] kiliitwa “MUUJIZA” na kilipofanywa na watu wa Firauni kiliitwa “UCHAWI” ingawa kimsingi tukio ni moja, na si lingine, bali ni fimbo kugeuka kuwa nyoka!

Uchawi na muujiza ni watoto mapacha na wana fanana sana. Kutokana na kufanana huku ndio maana wakati mwingine watu hujikuta “uchawi” wanauita “muujiza” na “muujiza” wanauita “uchawi”, lakini ukweli uko wazi kuwa “uchawi” na “muujiza” ni vitu viwili tafauti pamoja na kufanana kwao. Aya za hapa chini kutoka katika Qur-an zinaonesha jinsi Firauni alivyoshindwa kutafautisha kati ya “uchawi” na “muujiza”. Aliuita muujiza ni uchawi. Yawezekana alishindwa kutafautisha kutokana kibli chake au ndio upeo wake wa kufikiri ulikuwa umefikia kikomo katika suala husika hata asijue ule ulikuwa ni muujiza na si uchawi.

Ama, kwa kuwa dini ya Farao haikuwa ndio ya Mussa, na kwa vyovyote vile Mungu wa Mussa hakuwa ndio Mungu wa Farao, kama ndivyo, ni sawa muujiza wa Mussa uonekane uchawi kwa Farao, na yale ya Farao mwenyewe aone muujiza.

“Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri. Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao. (Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu. Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?” Qur-an 26:32-35

Yale mambo yote yasiyoyakawaida aliyoyafanya Yesu Kristo huitwa ni “miujiza”, kwani imethibiti mara chungu nzima katika qur-an na biblia kuwa Yesu alizikiuka sheria za kimaumbile. Alikiuka sheria za kimaumbile kwa kufufua wafu, kuponya viziwi, vipofu, wagonjwa na kwa kulisha maelfu ya watu kwa chakula cha kidogo kabisa. Pia alitembea juu ya bahari pasina kuzama, hata ile saumu yake ya siku arobani bila kula hata kidogo ni muujiza pia.

“Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari. Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu. Mara Yesu alinena, akawaambia, Jipeni moyo ni mimi; msiogope” Mathayo 14:25-27

"Na pale Mwenyezi Mungu atapo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Kumbuka neema yangu juu yako, na juu ya mama yako, nilipo kutia nguvu kwa Roho Takatifu, ukazungumza na watu katika utoto na utuuzimani. Na nilivyo kufunza kuandika na hikima na Taurati na Injili. Na ulipo tengeneza udongo sura ya ndege, kwa idhini yangu, kisha ukapuliza ikawa ndege kwa idhini yangu; na ulipo waponesha vipofu na wakoma kwa idhini yangu; na ulipo wafufua wafu kwa idhini yangu; na nilipo kukinga na Wana wa Israili ulipo wajia na hoja zilizo wazi, na wakasema walio kufuru miongoni mwao: Haya si lolote ila ni uchawi mtupu" Qur-an 5:110

"Akasema Isa bin Maryamu: Ewe Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wetu! Tuteremshia chakula kutoka mbinguni ili kiwe Sikukuu kwa ajili ya wa mwanzo wetu na wa mwisho wetu, na kiwe ni Ishara itokayo kwako. Basi turuzuku, kwani Wewe ndiye mbora wa wanao ruzuku." Qur-an 5:114

"Akawaagiza makutano waketi katika majani; akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akabariki, akaimega ile mikate, akawapa wanafunzi, wanafunzi wakawapa makutano. Wakala wote wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate, vikapu kumi na viwili, vimejaa. Nao waliokula walikuwa wanaume wapata elfu tano, bila wanawake na watoto." Mathayo 14:19-21

Nafikiri hadi kufikia hapa tutakuwa tushafahamu maana ya uchawi na muujiza japo kidogo, si hivyo tu tutakuwa tumeshajua jinsi uchawi na muujiza unavyotafautiana na kufanana. Sasa nataka tujue asili ya uchawi na muujiza. Asili ya uchawi na muujiza ni Mungu mwenyewe.

Tanbihi: nikizungumzia asili ya kitu fulani, jua kuwa nazungumzia muumbaji wa kitu hicho. Mungu ndiye aliyeumba “uchawi” na huo “muujiza” Uchawi na muujiza ni viumbe wa Mungu kama vilivyo viumbe vingine, kama tikikataa kuwa uchawi na mujiiza sio viumbe wa mungu, basi tukubali kuwa kuna “kitu” kingine tafauti na “MUNGU” ndio kimeumba uchawi na muujiza, jambo ambalo halikubaliki katika dini zote, yaani, hata zile za kipagani.

“Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote;” Qur-an 1:2

“Bwana amefanya kila kitu kwa kusudi lake; Naam, hata wabaya kwa siku ya ubaya.” Mithali 16:4

“Mwenyezi Mungu ndiye aliye umba mbingu na ardhi na viliomo baina yao kwa siku sita, na akatawala kwenye Kiti cha Enzi. Nyinyi hamna mlinzi wala mwombezi isipo kuwa Yeye tu. Basi, je, hamkumbuki?” Qur-an 31:4

“Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.” Yohana 1:3

Katika aya za hapo juu zote zinadhihirisha kuwa MUNGU ndiye aliyeumba viumbe vyote ikiwemo na uchawi na nduguye muujiza. Mfano katika andiko hilo la Mithali 16:4, Mfalme Suleiman[a.s] anatuambia kila kitu kimefanywa[kimeumbwa] na MUNGU kwa makusudi yake, kwa vyovyote vile hata uchawi kwa siku ya uchawi na muujiza kwa siku ya muujiza. Sitaki nijikite katika sababu zilizopelekea MUNGU kuumba uchawi na muujiza, kwani nachelea kutoka nje ya mada, kwa ufupi naomba mridhike kuwa MUNGU ndiye aliyeviumba vitu hivi kama nilivyothibitisha kwa kutumia misahafu yetu.

Hivi uchawi na muujiza unafanyaje kazi hata uweze kushinda sheria za kimaumbile? Ili tuweze kujua namna uchawi na muujiza unavyofanya kazi, ni lazima tujue Mungu alitumia nini kuumba ulimwengu. Imethibiti katika dini zote, hadi zile za kipagani kuwa MUNGU alitumia “NENO” katika kuumba ulimwengu, yaani aliposema na iwe bahari, basi papo hapo na ikawa bahari. Tunaweza kusema hiyo papo hapo ni sawa na kitendo cha kufumba na kufumbua.

“Yeye ndiye Muumba wa mbingu na ardhi pasina ruwaza; na anapo taka jambo basi huliambia tu: Kuwa! Nalo huwa” Qur-an 2:117

“Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru. Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza” Mwanzo 1:3-4

Muda kwa upande wa MUNGU haupimwi kwa kutegemea vitendo vifanyavyo na jua, mwezi na dunia, bali hupimwa kwa utaratibu ambao MUNGU mwenyewe ndio anaujua. Ndio maana Mungu alianza kuhesabu siku katika uumbaji wake hata kabla ya kuumbwa jua, mwezi na dunia. Muda kwa upande wa kibinadamu hupimwa kwa kwa kutegemea mzunguko wa dunia katika mhimiri wake, kitendo cha dunia kuzunguka jua na mwezi kuzunguka dunia, kwa MUNGU ni tafauti, utafauti huu ndio hufanya siku moja kwa MUNGU kwa binaadamu ni miaka elfu moja. Je. Kufumba na kufumbua kwa MUNGU kwa binaadamu ni sawa na miaka mingapi?

“Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja” 2 Petro 3:8

“ Maana miaka elfu machoni pako Ni kama siku ya jana ikiisha kupita, Na kama kesha la usiku.” Zaburi 90:4

Hii ina maanisha nini? Hii ina maanisha kuwa “NENO” lina nguvu na kasi ya ajabu katika utekelezaji wa majukumu yake, jambo ambalo limefanywa kwa siku moja na “NENO” litatugharimu miaka elfu sisi kulifanya, tena kwa vyovyote vile katika kipindi chote cha hiyo miaka elfu moja itatupasa tuache kufanya kila kitu, yaani hata kula, na kisha tujikite katika utafiti. Je, yupo mwenye uwezo kuishi miaka elfu moja kwa kufanya utafiti tu? Kutokana na sababu hii ndio maana nasema ni vigumu kwa mja kuzikiuka sheria za kimaumbile ili hali yuko mwenyewe.

Pamoja na ugumu huo, lakini waja wangali wanazikiuka sheria za kimaumbile kila uchao. Wanazikiuka sheria hizi si kwa kutumia uwezo wa kibinaadamu, bali inawapasa wawe zaidi ya binaadamu wakati wakizikiuka sheria hizi, kinyume chake kamwe binaadamu hawezi. Kwakuwa ulimwengu na sheria za kimaumbile zimeumbwa na MUNGU kwa kutumia “neno” basi binaadamu hulazimika kutumia “neno” wakati akitaka kukiuka sheria za kimaumbile.

“Yesu akanyosha mkono, akamgusa, akisema Nataka; takasika. Na mara ukoma wake ukatakasika” Mathayo 8:3

Nataka “takasika” hilo neno nililoliwekea funga na fungua semi ndio neno lilotumika kumponya huyo mtu mwenye ukoma. Ili neno lipate kukiuka sheria za kimaumbile ni lazima liwe na pumzi ya MUNGU aliye hai; Hivyo neno hilo “takasika” lilikuwa na pumzi ya mungu wakati ule linatamkwa na Yesu Kristo, na ndio maana likaweza kukiuka sheria za kimaumbile na hatimaye likasababisha muujiza wa kuondoa ukoma katika mwili wa mhitaji. Hata wachawi hutumia “neno” lenye pumzi ya mungu wakati wakifanya mambo yao ya kichawi, sema wao wanatumia neno hilo pasina kupewa kibali au ruhusa na mungu.

Pamoja na kwamba “neno” ndio kila kitu katika shughuli za kimuujiza na kichawi, lakini haindoi ukweli kuwa kuna vitu vingine hutumika pamoja na neno katika kukamilisha mambo ya kichawi na ya kimuujiza. Kikubwa mfanyaji uchawi au muujiza ni lazima ajue anataka kufanya nini, kwa wakati gani, kwa nani na vitu gani vitahitajika katika kukamilisha huo muujiza au uchawi.

Labda niseme kitu kimoja “nyakati” na “idadi" ya vitu, mambo, vitendo au matukio katika shughuli za kichawi na muujiza ni muhimu sana, usipojua matumizi sahihi ya vitu hivyo inawezekana uchawi au muujiza wako usifanikiwe, au usifanyike kama vile ambavyo ulivyotaka.

“Alipokwisha kusema hayo, alitema mate chini, akafanya tope kwa yale mate. Akampaka kipofu tope za macho, akamwambia, Nenda kanawe katika birika ya Siloamu, (maana yake, Aliyetumwa). Basi akaenda na kunawa; akarudi anaona”

Kwa vyovyote vile Yesu Kristo aliona kuwa pindi akitumia “neno” tupu pasina tope lililotokana na udongo na mate yake, yule mtu asingepona ukoma aliokuwa nao. Katika andiko hilo halionekani neno lenye pumzi alilolitumia Yesu Kristo, lakini haiondoi ukweli kuwa alitumia neno pia; kwa maana nia ya kutaka uponyaji ujengwa na “neno” ndani ya moyo, na Yesu alikuwa na nia ya kutaka kufanya muujiza. Nia ambayo kimsingi ndio “neno” katika muktadha huu sanjari na tope ndio vilivyowezesha kukamilisha tukio la muujiza.

“Nawe, mwanadamu, ujipatie upanga mkali, kama wembe wa kinyozi ujipatie, ukaupitishe juu ya kichwa chako na ndevu zako; kisha ujipatie mizani ya kupimia, ukazigawanye nywele hizo. Theluthi ya hizo utaiteketeza katikati ya mji, siku za mazingiwa zitakapotimia; nawe utatwaa theluthi, na kuipiga kwa upanga pande zote; nawe utatawanya theluthi ichukuliwe na upepo, nami nitafuta upanga nyuma yake. Nawe twaa nywele chache katika hizo, na kuzifunga katika upindo wa mavazi yako. Nawe utatwaa tena baadhi ya hizo, na kuzitupa katikati ya moto, na kuziteketeza katika moto huo; kutoka nywele hizo moto utakuja na kuingia katika nyumba yote ya Israeli” Ezekieli 5:1-4

Katika aya za hapo juu Mungu anamwambia nabii Ezekieli afanye mambo hayo ili apate kuuchoma moto nyumba za watenda maovu katika Israeli kwa kutumia muujiza. Katika kutekeleza huo muujiza, Ezekieli aliambiwa afanye yafuatayo, aliambiwa awe na upanga, kisha kwa kutumia huo upanga anyoe nywele na ndevu. Swali la kujiuliza, kwanini Mungu alitaka atumie upanga kunyolea hizo nywele na ndevu badala ya wembe ambao ndio kitu makhususi kwaajili ya kunyolea? Kwa vyovyote vile kama ungetumika wembe huo muujiza usingekuwa kama vile alivyotaka Mungu.

Kisha akaambiwa hizo nywele na ndevu azigawe katika mafungu matatu kisha na azifanye kama alivyoambiwa. Yaani zingine azitupe kwenye maji[sijui kama aliambiwa mtoni au baharini], zingine azipeperushe kwa kutumia upanga, na zingine katika fungu la tatu kidogo azifunge katika upindo wa vazi[hirizi] na zingine azichome moto. Pindi akitekeleza mambo haya basi nyumba za waovu katika Israeli zitashika moto. Kwanini Mungu alitaka nabii Ezekieli afanye yote haya badala ya kutumia neno tu? Hapo ndipo utakapogundua kuwa muujiza wakati fulani hauwezi kutimia kwa kutumia “neno” tu.

Hata uchawi nao hutumia “neno” na baadhi ya vitu vingine, na hii inategemea na huyo mchawi anataka kufanya nini, kwa nyakati gani na kwa nani. Kuna baadhi ya mambo ya kichawi yanafanikiwa pindi yakifanyika mchana kuliko hata usiku, mengine yanataka saa maalumu , mengine yanataka mahali maalum, mengine yanataka mavazi maalum na mengine yanataka matukio maalum, kwa mfano siku ya tukio la kupatwa jua au mwezi kuna baadhi ya mambo ya kichawi yanataka yafanyike siku ya matukio hayo. Aya ya hapo chini inatujilisha ni kwa namna gani baadhi ya vitu hutumika pamoja na “neno” katika kutimiza mambo ya kichawi.

“Useme, Bwana MUNGU asema hivi; Ole wao wanawake wale, washonao hirizi katika viungo vyote vya mikono, wawekao leso juu ya vichwa vya kila kimo, ili wawinde roho za watu; je! Mtaziwinda roho za watu wangu, na kuzihifadhi hai roho zenu wenyewe?” Ezekieli 13:18

Kumbuka kuwa nilisema anayefanya uchawi hufanya hivyo kwa kutumia "neno" lenye pumzi ya Mungu pasina kupewa kibali na Mungu mwenyewe. Yale mambo aliyoyafanya Ezekieli anaweza kuyafanya mtu mwingine na akafanikiwa kutimiza kama alivyofanya Ezekieli. Ni kawaida sana kwa wachawi kutumia nywele, kufunga hirizi, kuchoma mafusho, kutupa vitu baharini au mtoni, kuchinja wa nyama, na mambo kadha wa kadha katika kutekeleza shughuli zao za kichawi.

Kwanini wachawi wanaroga? ipi tiba ya uchawi? Kwanini Yesu alilazimika kumponya kipofu kwa kutumia tope? Kuna uhusiano gani kati ya jini na uchawi? Kuna uhusiano gani kati ya uchawi na biblia? Kuna uhusiano gani kati uchawi qur-an? Kuna uhusiano gani kati ya uchawi na Mungu? Kuna uhusiano gani kati ya majina yetu na uchawi/muujiza?

USIKOSE SEHEMU YA PILI.

ASANTENI NA UNGU AWABARIKI.

Dotto Rangimoto Chamchua(Njano5)
Whatspp/call 0622845394
 

Similar Discussions

11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom