Uchawi bungeni wafika Usalama wa Taifa, Polisi

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Uchawi bungeni wafika Usalama wa Taifa, Polisi

Stella Nyemenohi, Dodoma | June 15, 2008

Ofisi ya Spika imewasilisha taarifa kwa Polisi na Usalama wa Taifa ili washughulikie madai yaliyojitokeza hivi karibuni kuhusu Mbunge na Ofisa mmoja Mwandamizi wa Bunge kukutwa ndani ya Ukumbi wa Bunge wakifanya vitu vinavyodhaniwa kuwa ni ushirikina.


Tukio hilo lililoripotiwa jana na baadhi ya vyombo vya habari, linadaiwa kufanyika Jumatatu wiki iliyopita likimhusisha Mbunge na Ofisa wa Bunge, ambao hata hivyo, hawakutajwa ni akina nani.

Imedaiwa kuwa watu hao walinaswa wakinyunyizia vitu visivyojulikana katika kila kiti cha Mbunge na kuishia cha Spika. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuahirishwa semina ya

Wajumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi mjini hapa, Spika Samuel Sitta alisema Kamanda wa Polisi mkoani hapa na Usalama wameanza kufuatilia zaidi tangu juzi ili kubaini ukweli wa suala hilo .

Ingawa alisema bado suala hilo ni uvumi na kwamba halina budi kusubiri kukamilika uchunguzi wa vyombo hivyo vya usalama , Sitta alisema hata hivyo tahadhari zote zinachukuliwa katika Ukumbi wa Bunge.

Hata hivyo, alisema kwa upande mwingine, tahadhari zinaweza kuwa ngumu ikizingatiwa kuwa wanaohusishwa ni watu ambao hawana kipingamizi cha kuingia katika ukumbi huo.

Akizungumzia juu ya tukio hilo , Spika alisema, Inashangaza. Lakini ni suala la uvumi, linachunguzwa. Tusubiri RPC na Usalama wa Taifa wakamilishe uchunguzi waotahadhari zote zinachukuliwa, alisema.

Kwa mujibu wa taarifa zilizoandikwa na baadhi ya magazeti, tukio hilo la ushirikina, linadaiwa kufanyika siku moja kabla ya kikao cha kwanza cha Mkutano wa 12 wa Bunge kuanza Jumanne iliyopita.

Spika alisema wakati wa tukio hilo, kamera sita zilizokuwa katika ukumbi huo, hazikuwa zimewashwa. Isipokuwa inadaiwa, kamera moja ya studio ndiyo iliyoonyesha watu hao.

Hata hivyo, Sitta alisema kamera hiyo ilionyesha picha iliyofifia ambayo ni vigumu kubaini wahusika. Hata hivyo, alisema anaamini kuwa ikifikishwa kwa wataalamu, ndiyo watakaoweza kubaini wahusika.

Alipoulizwa na waandishi kuhusu mantiki ya kuhusisha tukio hilo la ushirikina na ugonjwa wa ghafla wa Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe (CCM), Spika alisema halihusishwi ikizingatiwa kuwa taarifa za daktari, zilionyesha kuwa alikuwa na uchovu.

Kwa mujibu wa Spika, Dk. Mwakyembe alianza kujisikia anaishiwa nguvu Alhamisi dakika chache wakati akijaribu kuwasiliana na Spika ndani ya Bunge. Alitoka nje ya ukumbi kwa msaada wa Mbunge mwenzake na kupelekwa hospitalini.

Baada ya Mwakyembe kukabiliwa na maradhi hayo ya ghafla, kesho yake (juzi) ulienea uvumi kuwa amefariki. Wakati Sitta alisisitiza jana kuwa afya yake inaendelea vizuri, HabariLeo ilimshuhudia Mbunge huyo jana akiwa katika viwanja vya Bunge katika hali ya kawaida.

Wakati huohuo, semina ya NEC-CCM ilianza jana na inatarajiwa kumalizika leo mjini Dodoma. Kwa mujibu wa Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi ya CCM John Chiligati alisema miongoni mwa waliotoa mada ni pamoja na Gavana wa Benki Kuu (BoT), Profesa Beno Ndullu.

"Hatujamaliza semina. Inaendelea hadi kesho (leo). Kwa hiyo, maazimio yote yatakayofikiwa, tutatoa taarifa kesho saa 11," Chiligati aliwaambia waandishi na kusisitiza kuwa lengo la semina hiyo ni kuhusu masuala ya uchumi, hususan kilimo.
 
Katika Usalama Wa Taifa Au Chochote Hatuamini Katika Uchawi Wala Imani Za Kishirikina Wala Chochote Kinachohusu Uficho Wa Kitu Fulani ,kazi Ni Mtindo Moja Tu ,kumlinda Mwananchi Na Mali Zake , Kupeana Na Kupashana Habari Kuhakikisha Nchi Inaendelea Kuwa Na Amani ,mshikamano ,undugu Na Upendo Kama Ilivyosiku Zote
 
Katika Usalama Wa Taifa Au Chochote Hatuamini Katika Uchawi Wala Imani Za Kishirikina Wala Chochote Kinachohusu Uficho Wa Kitu Fulani ,kazi Ni Mtindo Moja Tu ,kumlinda Mwananchi Na Mali Zake , Kupeana Na Kupashana Habari Kuhakikisha Nchi Inaendelea Kuwa Na Amani ,mshikamano ,undugu Na Upendo Kama Ilivyosiku Zote

Kama ndiyo hivyo kulikuwa na haja gani hiyo ofisa ya spika kuwaambia Watanzania kwamba imewasilisha ripoti ya uchawi polisi ili waifanyie uchunguzi? Ofisi ya spika haiyajui hayo uliyoandika hapo juu au ni katika kudanganya wadanganyika?
 
Ndio Hivyo Umeshadanganywa Kama Ni Wewe Nenda Vituo Vyote Vya Polisi Uulize Kuhusu Uchawi Au Ushirikina Uone Utajibiwa Nini ,mada Zingine Hazina Masihali Kwa Jamii Forum
 
Ndio Hivyo Umeshadanganywa Kama Ni Wewe Nenda Vituo Vyote Vya Polisi Uulize Kuhusu Uchawi Au Ushirikina Uone Utajibiwa Nini ,mada Zingine Hazina Masihali Kwa Jamii Forum

Kinachochunguzwa sio uchawi wenyewe bali ni nia ya mtu kufanya mambo ya kishirikina kama alivyoainishwa kwenye sheria ya mambo ya kishirikina(yaani witchcraft ordinance) kwa lengo la kuwadhuru watu hao ambao wewe na wenzio mmesema mnawalinda.Sasa unabisha nini?kama huyajui mambo si utulie ukalale?isitoshe wewe ni kama ni wale wa kuambiwa tu fanya hiki fanya kile.Iistoshe hata akijulikana muhusika sio lazima ashughulikiwe kijinai hiyo inaweza pia kumuwezesha spika kumshughulikia administratively(kimaadili na nidahmu ya bunge).
 
Katika Usalama Wa Taifa Au Chochote Hatuamini Katika Uchawi Wala Imani Za Kishirikina Wala Chochote Kinachohusu Uficho Wa Kitu Fulani ,kazi Ni Mtindo Moja Tu ,kumlinda Mwananchi Na Mali Zake , Kupeana Na Kupashana Habari Kuhakikisha Nchi Inaendelea Kuwa Na Amani ,mshikamano ,undugu Na Upendo Kama Ilivyosiku Zote

Yule mtoto aliyekutwa na kichwa cha mtoto na akaanza kukila pale Muhimbili polisi walimkamata na kumtia ndani ambako yuko hadi hii leo na huku kesi yake ikiendelea mahakamani. Sasa kama polisi ni sehemu ya usalama wa Taifa kulikoni mpaka wakamkamata yule kijana na kumuweka rumande hadi sasa kama wao hawaamini uchawi? Unapotaka kujadili hakikisha una facts za kusupport kile unachokisema vinginevyo utaonekana unabwabwaja tu!
 
Jamani hili bunge lishughulikie mambo ya maana ya kuongoza nchi .tuwache itikadi .mjue tuu serekali hairogwi
 
Jamani hili bunge lishughulikie mambo ya maana ya kuongoza nchi .tuwache itikadi .mjue tuu serekali hairogwi

Maneno mema...

Moja: Serikali ni nini? na inajumuisha vitu vingapi ili iweze kuitwa serikali?

Mbili: Baada ya kuacha itikadi tutafuata mwelekeo gani?

Tatu: Je Tanzania tuna Witchcraft Act? Kama ndio ni ya nini na inaisaidiaje Serikali?

Uchawi ni silaha muhimu sana ya Maangamizi sema tumeamua itumia vibaya na kujaribu itumia angamiza wale wema...Kungekuwa na chuo cha uchawi ningeenda nipate ujuzi kisha niwekane sawa na hawa mafisadi wanaodharau wapiga kura wao na kujivisha Umungu!
 
Maneno mema...

Moja: Serikali ni nini? na inajumuisha vitu vingapi ili iweze kuitwa serikali?

Mbili: Baada ya kuacha itikadi tutafuata mwelekeo gani?

Tatu: Je Tanzania tuna Witchcraft Act? Kama ndio ni ya nini na inaisaidiaje Serikali?

Uchawi ni silaha muhimu sana ya Maangamizi sema tumeamua itumia vibaya na kujaribu itumia angamiza wale wema...Kungekuwa na chuo cha uchawi ningeenda nipate ujuzi kisha niwekane sawa na hawa mafisadi wanaodharau wapiga kura wao na kujivisha Umungu!
Dhana kwamba serikali hairogiw ni nadharia tu,ambayo ukweli wake ni kuwa serikali haiwezi anguka kwa kurogwa yaani viongozi wote wa serikali wafe siku moja,lakini cha kujiuliza?serikali inaundwa na nani?kama jibu ni watu je,watu wanarogeka?kama jibu ni ndiyo basi serikali inarogeka.Uchawi upo? je jibu ni ndiyo au hapana?kwa Tanzania jibu ni ndiyo na je,unatambulika na serikali kuwa upo?jibu ni ndiyo upo na ndiyo maana katika sheria za Tanzania kuna Witchcraft Act, iwapo serikali isingekuwa inaamini uchawi upo basi sheris hii ingefutwa zamaniiiiiiiiiiiii,kwani mbali ya kupigiwa kelele na wasomi na watetezi wa haki za binadamu kuwa ifutwe na imepitwa na wakati bado serikali inaikumbatia na imekuwepo tokea enzi za mkoloni.
Uchawi na influence zake upo mahali pote ndiyo maana hata wenzetu waingereza wanaogopa na katu hawatalala kwenye chumba namba 13 na kutokana na hilo hoteli zote duniani za hadhi ya kitalii duniani hazina namba hiyo.Pili waingereza wenyewe wana sikukuu yao inaiwa haloween hii ni sherehe ya mizimu na kuna matambiko hufanyika ili wasidhurike na winta isiwe mbaya.Tatu wakati wa summer kama kipindi hiki ni imani ya waingereza kuwa kila ulapo nyama (barbeque) choma lazima uchomee nje ili moshi ufuke uende juu ukahanikize mizimu ili summer iwe nzuri na winta isiwe mbaya kwa upande wao. Hizizote ni imani za kishirikina na hazipo tz tu hata wenzetu waloendelee.
 
Taifa linalozungumzia the so called uchawi!karne hii ya 21!kwa kweli lazima uboubt na uwezo wa wananchi pamoja na viongozi wake!Ndo maana mtu mweupe anawasiwasi na uwezo wa mtu mweusi!
 
Katika Usalama Wa Taifa Au Chochote Hatuamini Katika Uchawi Wala Imani Za Kishirikina Wala Chochote Kinachohusu Uficho Wa Kitu Fulani ,kazi Ni Mtindo Moja Tu ,kumlinda Mwananchi Na Mali Zake , Kupeana Na Kupashana Habari Kuhakikisha Nchi Inaendelea Kuwa Na Amani ,mshikamano ,undugu Na Upendo Kama Ilivyosiku Zote
.......???
 
Voodoo, poison threats: Bunge still trembling under shadow of fear

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

THE recently reported incident of witchcraft rituals allegedly performed by a senior MP and a parliament official inside the National Assembly (Bunge) Hall in Dodoma has sparked concern among other members of parliament over a possible poison attack targeted at certain legislators.

The Kigoma North MP, Zitto Kabwe (CHADEMA), said yesterday that the incident could be more than just a simple matter of voodoo rituals, but possibly an outright attempt to poison someone or some people in the House.

According to Zitto, the incident could even be directly linked to the sudden sickness that has apparently befallen Kyela legislator Dr Harrison Mwakyembe, who was abruptly taken ill while attending a parliamentary session last week.

Mwakyembe was chairman of the Bunge committee that probed the Richmond power generation scandal and delivered a scathing report that led to the resignation of former prime minister Edward Lowassa and two senior cabinet ministers, Nazir Karamagi and Dr Ibrahim Msabaha.

The Kyela MP and other members of the committee are already on record as having publicly declared that they received death threats during the course of the probe.

In Zitto's opinion, special medical tests need to be conducted on Mwakyembe to conclusively establish whether or not he might have been somehow poisoned in Dodoma.

''I personally don't believe that there are witchcraft rituals in parliament...It is possible we are deliberately being diverted from what might actually be the real issue, that some kind of poison could have been spilled inside the House,'' he told THISDAY.

Likewise, the Tarime legislator also on a CHADEMA ticket, Chacha Wangwe, described the reported Bunge vodoo rituals as ''suspicious'' and warranting a deeper investigation.

Mwakyembe himself has been unreachable since last week's reports that he had suddenly fallen ill after an alleged ''witchcraft ritual'' was performed on his seat inside the Bunge Hall, at a time when parliament was not in session.

The Speaker of the National Assembly, Samwel Sitta, has said his office has already informed the police and security/intelligence authorities about the incident, and asked for a formal investigation into the matter.

There were conflicting reports regarding whether or not the alleged perpetrators of the decidedly un-parliamentary behaviour were actually caught on the surveillance cameras installed in parliament.
 
Back
Top Bottom