Uchawi au Majini hayapo! Nani ameshawahi kukutana na jini

I have meets with this guys,they are so cool and humble "THIS IS CREATURES OF SPECIAL PRINCIPLES...DO YOU WISH TO SEE? ARE YOU CLEAN ENOUGH?,DO YOU WANT TO POSSESS ONE?I HAVE MANY I CAN GIVE YOU A LITTLE ONE.
Shame on ,next time try to use the language that your competent,don't say/ write "I have meets,but say,I have met, also this is creatures was supposed to be "these are creatures"
 
Na wewe utupe facts kwanza kama uchawi na majini havipo fact hupingwa na fact kuna kitu nimejifunza kwenye maisha haya ignorance yako kuhusu jambo fulani inaweza isibadilishe uhalisia kwani wewe unavyoamini kuna mungu unaweza kututhibitishia
 
Hizo ni mental /brain disorders tu!

Kwa Tanzania, matatizo ya akili ni mpaka mtu aokote makopo.

Mtu mwenye auditory hallucinations watu watasema amepandwa na mashetani!

Mwenye tactile hallucinations watadai wachawi wanamtekenya!

Tatizo ni ujinga. Mambo tusiyoyajua au tusiyoyaelewa, tunayabatiza uchawi!
Hapana, nimeona nguvu za giza kwa macho yangu mawili.

Mwanzoni nilikuwa najidai mimi ni msomi na mbishi juu ya haya mambo lakini nilipoyashuhudia ubishi ukanitoka.

Wala sio ugonjwa wa akili.
 
Leo unajifanya hujawahi kuliona jini mbona limefukiwa juzi tu hapa. Nalitoto lake lina henyeshwa kule kisongo.
 

Unataka kujua ya majini na ilihali ndoa yako ina shida, mtoto wako hajafanana na wewe umeliws wewe
Kumbe! 🙆🏾‍♂️😬😬😬
 
Hicho kisaidizi cha akili utakitumia bila kutumia akili?
Mbona unauliza swali ambalo nimeshalijibu ?

Akili lazima iwepo,kuna kaida ya kiusuli inasema hivi "Tunatumia akili kuifata na kuuelewa ufunuo na si ufunuo ufate akili".
Huko kuhoji utahoji bila kutumia akili?
Nasisitiza ya kuwa uwe unasoma na kuelewa ninacho kiandika sababu kimejibu swali lako. Kufanya hivyo kutakuwa kuna kusaidia wewe kuto poteza muda.
Nikikwambia mimi ndiye Mungu, na kanusho lako lolote halitafaa kwa sababu ukweli huo, kwamba mimi ndiye Mungu, umepita uwezo wa akili yako kuelewa, utakanushaje hilo?
Unarudia swali. Rejea jibu nililo kujibu.
Chochote utakachokanusha kimepitia akili yako, na mimi nishakwambia akili yako haiwezi kuelewa ukweli huu kwamba mimi ndiye Mungu.
Hili nimekujibu.

Inaonekana husomi ninacho kiandika.
Utakanushaje?
Unarudia swali.
 
Hata kama sijauona live huo uchawi ama hao wachawi, ila tangu nizaliwe hadi nilipofikia sahi, najua upo, sio story tu. Evidence zipo kwenye vitabu vya dini, na kupitia watu wenye kupitia experiences za kichawi. So, kama haujawahi uona/waona, usidhanie havipo 'chini ya maji'.
 
Baadhi wanasema kuna majini wazuri na majini wabaya, wazuri hua wanasali na kumuomba mungu na wabaya hadi ma atheist wapo

Wapo wanaodai kua kuna elimu juu ya utengenezaji wa hivyo viumbe.

Kuna siku nilisikia redioni mkufunzi akitoa somo namna ya kuita jini kwa kutamka maneno fulani hivi ya kiarabu.

Yale maneno niliyanukuu vyema nikawa naya practice maana mdau alisema unatakiwa uende njia panda usiku wa maneno kisha utamke hayo maneno

Nikiwa na tumaini kua leo ndio siku ambayo najithibitishia kua majini yapo, nikafika njia panda nikaanza kuyatamka hayo maneno kwa kuyarudia rudia zaidi ya mara 100 lakini hakukua na respond yeyote kutoka third party system

Wakati nikiendelea kutamka yale maneno nilishtukizwa na roba flani matata upande wa nyuma, mwanzo nilidhani ni ujio wa jini kumbe ni kibaka wa mtaa na alikua anapiga patrol

Aisee nilimlaumu sana yule jamaa wa redioni
Labda kuna masharti ulikosea.
 
You are good at debates!

Lakini ukitaka kujuzwa ukweli lazima ulegeze shingo kidogo!

Ukigangamara na midahalo utaishia kwenye ubishi tu.

Na wewe najua huwa hushindwi.

Kwa tuliokumbana na nguvu za giza tunatizama tu tunasema Hiiiiiiiii....
"Nguvu za giza" ni nini?

Na unajuaje hizo ni nguvu za giza, si kitu kingine tofauti tu ambacho hujakijua?
 
Huu ni ujinga, unakuja JamiiForums uthibitishiwe uwepo wa UCHAWI???... Kitu chochote kina njia zake za uthibitisho,,,, mfano UMEME hauonekani kwa MACHO ila kuna vitu vinaashiria uwepo wa UMEME,, sasa kama unataka kuona UCHAWI tafuta panapopatikana UCHAWI wakuonyeshe...
Asante wasiokuelewa hapa hawatakaa wakuelewe
 
Mbona unauliza swali ambalo nimeshalijibu ?

Akili lazima iwepo,kuna kaida ya kiusuli inasema hivi "Tunatumia akili kuifata na kuuelewa ufunuo na si ufunuo ufate akili".

Nasisitiza ya kuwa uwe unasoma na kuelewa ninacho kiandika sababu kimejibu swali lako. Kufanya hivyo kutakuwa kuna kusaidia wewe kuto poteza muda.

Unarudia swali. Rejea jibu nililo kujibu.

Hili nimekujibu.

Inaonekana husomi ninacho kiandika.

Unarudia swali.
Nikikwambia kwamba mimi ni Mungu, ila wewe huwezi kujua hilo, kwa sababu ukweli huo umepita uwezo wa akili yako kujua, utabishaje?

Chochote utakachobisha, mimi nitakujibu "huwezi kujua ukweli huu, kwa sababu ukweli huu umepita uwezo wa akili yako kujua".

Huoni hizo habari za "ukweli huu umepita uwezo wa akili yako kuujua" ni kichaka cha kuficha uongo wowote ule?
 
Hata kama sijauona live huo uchawi ama hao wachawi, ila tangu nizaliwe hadi nilipofikia sahi, najua upo, sio story tu. Evidence zipo kwenye vitabu vya dini, na kupitia watu wenye kupitia experiences za kichawi. So, kama haujawahi uona/waona, usidhanie havipo 'chini ya maji'.
Vitabu vya dini vinakuambia mababu na mabibi zako wote waliozaliwa kabla ya Yesu na Mtume, na hata waliozaliwa baada lakini hawakuwajua wageni hawa na dini zao kwa sababu ya umbali huko Africa watachomwa na moto wa milele na Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, kwa kuwa hawakumjua huyo Mungu, kwa kuwa hawakupewa ufunuo wa vitabu hivyo vya dini kumjua huyo Mungu.

Unaamini hili nalo?
 
Mpaka sasa hakuna mtu aliye define uchawi ni nini.

Achilia mbali kuthibitisha uchawi upo.Hakuna aliye define uchawi ni nini!

Tunawezaje kufanya mjadala wa maana kuhusu kitu ambacho hata hatujaki define?

Kwa sababu, inawezekana kwa mtu mmoja, kumuua mtu kwa kutumia cyanide ni uchawi.

Halafu, kwa mtu mwingine, kumuua mtu kwa kutumia cyanide si uchawi, ni Kemia tu.

Sasa, kabla hatujakubaliana uchawi ni nini, tutawezaje kujadiliana kuhusu uchawi?
 
Vitabu vya dini vinakuambia mababu na mabibi zako wote waliozaliwa kabla ya Yesu na Mtume, na hata waliozaliwa baada lakini hawakuwajua wageni hawa na dini zao kwa sababu ya umbali huko Africa watachomwa na moto wa milele na Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, kwa kuwa hawakumjua huyo Mungu, kwa kuwa hawakupewa ufunuo wa vitabu hivyo vya dini kumjua huyo Mungu.

Unaamini hili nalo?
🙄🤷🏾‍♂️🤷🏾‍♂️🤷🏾‍♂️
 
Back
Top Bottom