Uchawa unadumaza maendeleo ya nchi, unalinda ufisadi na kubariki kutokuwajibika. Taifa linaangamia

Stroke

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
34,671
40,912
Kuna ajira mpya ya kisiasa imezuka katika Taifa letu nayo inaitwa uchawa.

Uchawa ni kitendo cha kuwa mfuasi kindaki ndaki wa mtu kwa matendo na kauli zake bila kujali uhalali wa kile kinachofanywa.

Mtu huyo anaweza kuwa Kiongozi mkuu wa nchi au mwanasiasa yeyote mwenye ushawishi.

Kiongozi mwenye dhamana ya kuliongoza Taifa anao wajibu wa kikatiba kulinda maslahi ya watu wake hivyo inategemewa kwamba kila anachokifanya maslahi ya uma yanapewa kipaumbele.

Ila inapotokea kiongozi huyo akakengeuka katika maamuzi yake basi kwa mifumo ya kiutawala tuliyonayo wananchi wana haki ya kumkumbusha wajibu wake.

Kwa kutambua umuhimu wa kuwa na nafasi za kukosoana na kushauriana Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alituasa vijana tuwe na hulka ya kuhoji , kwamba pale tunapoona kuna jambo linafanyika na tunaamini linafanyika sio kwa maslahi yetu ya Taifa basi tunapaswa kuhoji.

Hali sasa ni tofauti kabisa, kizazi cha kuhoji kinapotea na ni kama hakipo kabisa kwani watu wamegeuka wabinafsi na kuangalia maslahi yao binafsi.

Kijana anaona kuliko kuhoji na kukosa fursa kwa kuonekana mtukutu bora akubaliane na kila jambo la nwanasiasa au kiongozi wa kitaifa ili akumbukwe kwa favours mbali mbali wanaita kulamba asali.

Kitendo hiki kina faida za muda mfupi ila hasara kwa muda mrefu wa vizazi vijavyo kwani kunauwezekano wa matendo ya wanasiasa kuwa ya kuliangamiza Taifa.

Kijana au mtu mwingine yeyote anapamua kuwa chawa anashiriki kuliangamiza Taifa lake kwani kiongozi husika hatakuwa na woga wa kufanya jambo lolote kwani anajua hakuna wa kumhoji kwa lolote.

Hivyo basi ni vyema tukaondoa dhana hii ya uchawa kwani inaliangamiza Taifa.
 
Kuna ajira mpya ya kisiasa imezuka katika Taifa letu nayo inaitwa uchawa.

Uchawa ni kitendo cha kuwa mfuasi kindaki ndaki wa mtu kwa matendo na kauli zake bila kujali uhalali wa kile kinachofanywa.

Mtu huyo anaweza kuwa Kiongozi mkuu wa nchi au mwanasiasa yeyote mwenye ushawishi.

Kiongozi mwenye dhamana ya kuliongoza Taifa anao wajibu wa kikatiba kulinda maslahi ya watu wake hivyo inategemewa kwamba kila anachokifanya maslahi ya uma yanapewa kipaumbele.

Ila inapotokea kiongozi huyo akakengeuka katika maamuzi yake basi kwa mifumo ya kiutawala tuliyonayo wananchi wana haki ya kumkumbusha wajibu wake.

Kwa kutambua umuhimu wa kuwa na nafasi za kukosoana na kushauriana Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alituasa vijana tuwe na hulka ya kuhoji , kwamba pale tunapoona kuna jambo linafanyika na tunaamini linafanyika sio kwa maslahi yetu ya Taifa basi tunapaswa kuhoji.

Hali sasa ni tofauti kabisa, kizazi cha kuhoji kinapotea na ni kama hakipo kabisa kwani watu wamegeuka wabinafsi na kuangalia maslahi yao binafsi.

Kijana anaona kuliko kuhoji na kukosa fursa kwa kuonekana mtukutu bora akubaliane na kila jambo la nwanasiasa au kiongozi wa kitaifa ili akumbukwe kwa favours mbali mbali wanaita kulamba asali.

Kitendo hiki kina faida za muda mfupi ila hasara kwa muda mrefu wa vizazi vijavyo kwani kunauwezekano wa matendo ya wanasiasa kuwa ya kuliangamiza Taifa.

Kijana au mtu mwingine yeyote anapamua kuwa chawa anashiriki kuliangamiza Taifa lake kwani kiongozi husika hatakuwa na woga wa kufanya jambo lolote kwani anajua hakuna wa kumhoji kwa lolote.

Hivyo basi ni vyema tukaondoa dhana hii ya uchawa kwani inaliangamiza Taifa.
MACHAWA YOTE YAPO CCM

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Uchawa ni ugonjwa mmbaya sana wa akili uliolikumba taifa letu.

Mbaya zaidi kiini chake ni maslahi binafsi yanayopatikana toka na tabia hio. Sio jambo geni nchini zamani waliitwa wapambe nuksi ila ilikuwa jambo la fedhea sana kuwa mtu wa hivyo.

Kilikuwa ni kitu kinafanywa na wapumbavu ambao hawajaenda shule ila kwa sasa ni hatari. Mtu ana degree kichwani ila ni mpambe nuksi kisa tu atapewa elfu kumi ya tumsifu mwenyekiti wetu.

Hii hali inakomaa sababu ya umaskini na kukosa fursa za kujikwamua. Ajira ngumu hivyo watu wanaona kuji enroll na upambe ni sehem ya ajira tu kufidia njaa zao.
 
Uchawa ni ugonjwa mmbaya sana wa akili uliolikumba taifa letu.

Mbaya zaidi kiini chake ni maslahi binafsi yanayopatikana toka na tabia hio. Sio jambo geni nchini zamani waliitwa wapambe nuksi ila ilikuwa jambo la fedhea sana kuwa mtu wa hivyo.

Kilikuwa ni kitu kinafanywa na wapumbavu ambao hawajaenda shule ila kwa sasa ni hatari. Mtu ana degree kichwani ila ni mpambe nuksi kisa tu atapewa elfu kumi ya tumsifu mwenyekiti wetu.

Hii hali inakomaa sababu ya umaskini na kukosa fursa za kujikwamua. Ajira ngumu hivyo watu wanaona kuji enroll na upambe ni sehem ya ajira tu kufidia njaa zao.
Hivi hawaoni aibu!!??
Nimejifunza kitu kutoka Urusi
 
Kuna ajira mpya ya kisiasa imezuka katika Taifa letu nayo inaitwa uchawa.

Uchawa ni kitendo cha kuwa mfuasi kindaki ndaki wa mtu kwa matendo na kauli zake bila kujali uhalali wa kile kinachofanywa.

Mtu huyo anaweza kuwa Kiongozi mkuu wa nchi au mwanasiasa yeyote mwenye ushawishi.

Kiongozi mwenye dhamana ya kuliongoza Taifa anao wajibu wa kikatiba kulinda maslahi ya watu wake hivyo inategemewa kwamba kila anachokifanya maslahi ya uma yanapewa kipaumbele.

Ila inapotokea kiongozi huyo akakengeuka katika maamuzi yake basi kwa mifumo ya kiutawala tuliyonayo wananchi wana haki ya kumkumbusha wajibu wake.

Kwa kutambua umuhimu wa kuwa na nafasi za kukosoana na kushauriana Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alituasa vijana tuwe na hulka ya kuhoji , kwamba pale tunapoona kuna jambo linafanyika na tunaamini linafanyika sio kwa maslahi yetu ya Taifa basi tunapaswa kuhoji.

Hali sasa ni tofauti kabisa, kizazi cha kuhoji kinapotea na ni kama hakipo kabisa kwani watu wamegeuka wabinafsi na kuangalia maslahi yao binafsi.

Kijana anaona kuliko kuhoji na kukosa fursa kwa kuonekana mtukutu bora akubaliane na kila jambo la nwanasiasa au kiongozi wa kitaifa ili akumbukwe kwa favours mbali mbali wanaita kulamba asali.

Kitendo hiki kina faida za muda mfupi ila hasara kwa muda mrefu wa vizazi vijavyo kwani kunauwezekano wa matendo ya wanasiasa kuwa ya kuliangamiza Taifa.

Kijana au mtu mwingine yeyote anapamua kuwa chawa anashiriki kuliangamiza Taifa lake kwani kiongozi husika hatakuwa na woga wa kufanya jambo lolote kwani anajua hakuna wa kumhoji kwa lolote.

Hivyo basi ni vyema tukaondoa dhana hii ya uchawa kwani inaliangamiza Taifa.
Haya yalianza na mwendazake. Hawa wengine wanaiga tu. Wakati tunapiga vita hii tabia, tutafakari kwanini mwendazake alipenda sana kusifiwa hata kwa vihoja hadi kupelekea kuasisiwa kwa tabia ya uchawa
 
Kuna ajira mpya ya kisiasa imezuka katika Taifa letu nayo inaitwa uchawa.

Uchawa ni kitendo cha kuwa mfuasi kindaki ndaki wa mtu kwa matendo na kauli zake bila kujali uhalali wa kile kinachofanywa.

Mtu huyo anaweza kuwa Kiongozi mkuu wa nchi au mwanasiasa yeyote mwenye ushawishi.

Kiongozi mwenye dhamana ya kuliongoza Taifa anao wajibu wa kikatiba kulinda maslahi ya watu wake hivyo inategemewa kwamba kila anachokifanya maslahi ya uma yanapewa kipaumbele.

Ila inapotokea kiongozi huyo akakengeuka katika maamuzi yake basi kwa mifumo ya kiutawala tuliyonayo wananchi wana haki ya kumkumbusha wajibu wake.

Kwa kutambua umuhimu wa kuwa na nafasi za kukosoana na kushauriana Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alituasa vijana tuwe na hulka ya kuhoji , kwamba pale tunapoona kuna jambo linafanyika na tunaamini linafanyika sio kwa maslahi yetu ya Taifa basi tunapaswa kuhoji.

Hali sasa ni tofauti kabisa, kizazi cha kuhoji kinapotea na ni kama hakipo kabisa kwani watu wamegeuka wabinafsi na kuangalia maslahi yao binafsi.

Kijana anaona kuliko kuhoji na kukosa fursa kwa kuonekana mtukutu bora akubaliane na kila jambo la nwanasiasa au kiongozi wa kitaifa ili akumbukwe kwa favours mbali mbali wanaita kulamba asali.

Kitendo hiki kina faida za muda mfupi ila hasara kwa muda mrefu wa vizazi vijavyo kwani kunauwezekano wa matendo ya wanasiasa kuwa ya kuliangamiza Taifa.

Kijana au mtu mwingine yeyote anapamua kuwa chawa anashiriki kuliangamiza Taifa lake kwani kiongozi husika hatakuwa na woga wa kufanya jambo lolote kwani anajua hakuna wa kumhoji kwa lolote.

Hivyo basi ni vyema tukaondoa dhana hii ya uchawa kwani inaliangamiza Taifa.
Mbona Taifa linasonga mbele haliangamii..

Onyesha lilivyoangamia kwa mtu kuwa Chawa.
 
Kwanini unaona uchawa wa sasa hivi ni mbaya kuliko uchawa wa kipindi cha mwendazake?.Au kwavile sio zamu yako kulamba asali.Kipindi ambacho wewe ulikua mfuasi wa mtu hukuona kama hicho kitendo ni kibaya,au kwavile aliyepo sasa huna maslahi naye ndo unaibuka na hoja yakujifanya huupendi uchawa.Siku tutakayoamua kuacha unafiki na kuamua kusimama na nchi badala ya mtu ndio siku tutakayoanza kupiga hatua yakulisaidia hili taifa.sasa hivi watu bado wanapokezana kulamba asali.
 
Back
Top Bottom