Uchambuzi wangu mdogo kuhusu uchambuzi wa Lipumba kwa Rais Samia

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,032
Katika gazeti la Raia Mwema la leo tarehe 18 Julai 2022, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba amechambua uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan akisema yeye anampa asilimia 75 ya utekelezaji.

Kwa ufupi Lipumba amechambua mambo kadhaa katika uongozi wa Rais Samia na kugusia masuala ya Demokrasia, Haki, Usawa na Utawala Bora ambapo amesisitiza kuwa sasa WATANZANIA WANAPUMUA.

Lipumba ameeleza kuwa baada ya Rais Samia kuapishwa, CUF walimshauri kusimamia misingi ya Demokrasia, lakini pia kufuta kesi zote zilizotokana na purukushani za kisiasa lakini pia asimamie mchakato wa kukamilisha upatikanaji wa Katiba mpya pamoja na kufuata kanuni za Afya za kusimamia masuala yahusuyo UVIKO19, masuala anayoeleza kuwa Rais Samia ameyafanyia kazi kw a kiasi kikubwa.

Lipumba amesisitiza kuwa andiko la Rais Samia Siku ya kuadhimisha miaka 30 ya mfumo wa vyama vingi limeongeza matumaini ya ujenzi ya demokrasia nchini huku akieleza kuwa uchaguzi wa mwaka 2020 ulikuwa mbovu kuliko yote ambayo imewahi kufanyika Tanzania/Tanganyika. Lipumba amesema uchaguzi huo uligubwika na ubakwaji mkubwa mno wa demokrasia.

Vipi wewe unaupa asilimia ngapi uchambuzi huu wa Profesa Lipumba?

Na vipi kufikia sasa, wewe unaupa asilimia ngapi uongozi wa Rais Samia Suluhu?

Lipu.jpeg
 
Mama yupo vizuri japo mtangulizi wake alikuwa na mapungufu yake.

Hapo kwenye kufuta kesi nikikumbuka ya Mbowe nasema hapana.
 
Mama yupo vizuri japo mtangulizi wake alikuwa na mapungufu yake.

Hapo kwenye kufuta kesi nikikumbuka ya Mbowe nasema hapana.
Baadhi ya Watu huwa wanashindwa kuwelewa nguvu ya Raisi, Jiwe aliitumia to the maximum. Hakukua na mwanaume mwenye uwezo wa kumzungmzia vibaya wala kumkosoa afu akaishi hapa hapa Tanzania. kila mtu alifyata mkia na raisi akawa akifanya kazi yake bila kukosolewa. Raisi Samia Suluhu ni mpole afu anaangalia response ya wananchi juu ya jambo ndio analiamua kulingana na matakwa ya wengi. Kesi ya Mbowe ilikua ishalemea upande mbaya kama sio huruma ya Rais wote tusinge amini ambacho kingetokea, we should respect that.
 
Baadhi ya Watu huwa wanashindwa kuwelewa nguvu ya Raisi, Jiwe aliitumia to the maximum. Hakukua na mwanaume mwenye uwezo wa kumzungmzia vibaya wala kumkosoa afu akaishi hapa hapa Tanzania. kila mtu alifyata mkia na raisi akawa akifanya kazi yake bila kukosolewa. Raisi Samia Suluhu ni mpole afu anaangalia response ya wananchi juu ya jambo ndio analiamua kulingana na matakwa ya wengi. Kesi ya Mbowe ilikua ishalemea upande mbaya kama sio huruma ya Rais wote tusinge amini ambacho kingetokea, we should respect that.
Hakuna cha huruma ya Rais wala nini sema upumbavu wa wanaccm wengi na rais akiwemo waliitengeneza kesi isiyo na ushahidi.
 
Baadhi ya Watu huwa wanashindwa kuwelewa nguvu ya Raisi, Jiwe aliitumia to the maximum. Hakukua na mwanaume mwenye uwezo wa kumzungmzia vibaya wala kumkosoa afu akaishi hapa hapa Tanzania. kila mtu alifyata mkia na raisi akawa akifanya kazi yake bila kukosolewa. Raisi Samia Suluhu ni mpole afu anaangalia response ya wananchi juu ya jambo ndio analiamua kulingana na matakwa ya wengi. Kesi ya Mbowe ilikua ishalemea upande mbaya kama sio huruma ya Rais wote tusinge amini ambacho kingetokea, we should respect that.
Poor
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom