Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 3,768
- 1,817
Nimeisikiliza kwa makini sana hotuba ya Rais Magufuli wiki iliyopita kwa wahandisi. Raisi kawatupia mawe sana wahandisi na kuwaona kama hawafai na waliojaa nadharia wanazoshindwa kuzitekeleza kivitendo. Kalaumu mengi ikiwa pamoja na makisio feke ya gharama za ujenzi wa miradi mbali mbali. Kifupi kasema mengi ambayo binafsi nimeyaona kama siasa za maji taka, siasa nyepesi zenye kuhitaji kuzoa umaarufu kwa wananchi hasa wasio na utaalam katika taaluma hiyo. Nitaeleza kwanini nayasema hayo.
Siasa ndio dira kubwa ya maendeleo ya nchi ikiwemo na fani ya uhandisi. Unaponadi ILANI ya chama, kifupi unaeleza jinsi dira ya maendeleo itavyoelekezwa ikiwepo pamoja na sekta ya uhandisi. Wahandisi hata wakiwa maprofesa na ujuzi wote katika taaluma hiyo hawawezi kufanya lolote kama ILANI za vyama tawala haviwabebi. Zingatia kuwa kwa bahati nzuri tumekuwa na chama kimoja kikitawala Tanzania kwa zaidi ya miaka 50 na Rais magufuli akiwepo katika uwaziri kwa takribani miaka 20. Je ILANI za CCM chaguzi hata chaguzi ziliibebaje taaluma ya UHANDISI? Ilikuwa na mipango gani ya muda mrefu kwa wahandisi kwa maendeleo ya nchi? Hivi ni wahandisi ndio walioingia mikataba ya kuchimba dhahabu na wageni, ujenzi wa bara bara ya Mtwara korido na nyinginezo?
Rais Magufuli amekuwa waziri wa Ujenzi kwa miaka mingi ya uwaziri wake. Na ni wizara hii iliyo na wahandisi wengi kuliko wizara nyingine zote. Na ni wizara hii yenye Miradi mingi katika taaluma ya uhandisi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa bara bara. Je alianzisha kampuni yenye high tech ya watanzania katika kufanya shughuli hizo? Si ndio hawa hawa CCM wakigawa miradi ya ujenzi wa bara bara za mijini na vijijini kwa wana CCM ambao hata hawakuwa na Magreda (vijiko) kama caterpillar. Ukweli ni kwamba miaka 50 yote ilikuwa ni ya ulaji tu katika sekta hiyo, huku wakibadilisha majina tu toka TRM (Watanzani tuliita- Tule Raha Mijini) mpaka leo Tanroad. Katika hali hiyo ya chama chashika hatamu unatarajia wahandisi wafanye nini? Nao waliamua kula na kipofu. Mfano Songambele (darasa la nne) alikuwa mwenyekiti wa CCM TANESCO, Molell (mhandisi) meneja wa TANESCO. Maamuzi ya Molell yalikuwa hayapita bila kukubaliwa na Songambele- Kiutendaji ni kama Songambele ndio alikuwa Meneja. Hiyo ni picha tu ya sehemu moja katika 100.
China (Mao) ilipoamua kujitegemea, kitu cha kwanza kabisa iliwaita wahandisi wake wote maarufu wa ndani na waliokuwa nje ya nchi na kuwauliza hivi hiki na hiki tunaweza wenyewe. Kama mnaweza kufanya huko nje ni nini kinachofanya mshindwe hapa? Wote wakamjibu tunaweza! Ila tusaidie hiki na kile. Akatekeleza na nchi ikaenda. Hali kadhalika Urusi, Vietnam n.k.
Kwa mantiki hiyo, Rais magufuli hana udole wa kuwalaumu wahandisi katika mipango mibovu ya miaka 50 ya chama chake. Kinyume chake ni ukweli inabidi awaombe msamaha wahandisi kwa chama chake CCM kutowajali wasomi ikiwa ni pamoja na wahandisi. Tena afanye hivi mara moja ili wahandisi waweze kufanya kazi. Wahandisi wetu leo wamejaa Botswana, Namibia, Swaziland na Afrika kusini na wanasifa nzuri sana huko. Iweje leo wakija katika ardhi ya Tanzania wanakuwa wabovu. CCM ijisafishe kwanza ndani kabla ya kupaka matope wengine.
Siasa ndio dira kubwa ya maendeleo ya nchi ikiwemo na fani ya uhandisi. Unaponadi ILANI ya chama, kifupi unaeleza jinsi dira ya maendeleo itavyoelekezwa ikiwepo pamoja na sekta ya uhandisi. Wahandisi hata wakiwa maprofesa na ujuzi wote katika taaluma hiyo hawawezi kufanya lolote kama ILANI za vyama tawala haviwabebi. Zingatia kuwa kwa bahati nzuri tumekuwa na chama kimoja kikitawala Tanzania kwa zaidi ya miaka 50 na Rais magufuli akiwepo katika uwaziri kwa takribani miaka 20. Je ILANI za CCM chaguzi hata chaguzi ziliibebaje taaluma ya UHANDISI? Ilikuwa na mipango gani ya muda mrefu kwa wahandisi kwa maendeleo ya nchi? Hivi ni wahandisi ndio walioingia mikataba ya kuchimba dhahabu na wageni, ujenzi wa bara bara ya Mtwara korido na nyinginezo?
Rais Magufuli amekuwa waziri wa Ujenzi kwa miaka mingi ya uwaziri wake. Na ni wizara hii iliyo na wahandisi wengi kuliko wizara nyingine zote. Na ni wizara hii yenye Miradi mingi katika taaluma ya uhandisi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa bara bara. Je alianzisha kampuni yenye high tech ya watanzania katika kufanya shughuli hizo? Si ndio hawa hawa CCM wakigawa miradi ya ujenzi wa bara bara za mijini na vijijini kwa wana CCM ambao hata hawakuwa na Magreda (vijiko) kama caterpillar. Ukweli ni kwamba miaka 50 yote ilikuwa ni ya ulaji tu katika sekta hiyo, huku wakibadilisha majina tu toka TRM (Watanzani tuliita- Tule Raha Mijini) mpaka leo Tanroad. Katika hali hiyo ya chama chashika hatamu unatarajia wahandisi wafanye nini? Nao waliamua kula na kipofu. Mfano Songambele (darasa la nne) alikuwa mwenyekiti wa CCM TANESCO, Molell (mhandisi) meneja wa TANESCO. Maamuzi ya Molell yalikuwa hayapita bila kukubaliwa na Songambele- Kiutendaji ni kama Songambele ndio alikuwa Meneja. Hiyo ni picha tu ya sehemu moja katika 100.
China (Mao) ilipoamua kujitegemea, kitu cha kwanza kabisa iliwaita wahandisi wake wote maarufu wa ndani na waliokuwa nje ya nchi na kuwauliza hivi hiki na hiki tunaweza wenyewe. Kama mnaweza kufanya huko nje ni nini kinachofanya mshindwe hapa? Wote wakamjibu tunaweza! Ila tusaidie hiki na kile. Akatekeleza na nchi ikaenda. Hali kadhalika Urusi, Vietnam n.k.
Kwa mantiki hiyo, Rais magufuli hana udole wa kuwalaumu wahandisi katika mipango mibovu ya miaka 50 ya chama chake. Kinyume chake ni ukweli inabidi awaombe msamaha wahandisi kwa chama chake CCM kutowajali wasomi ikiwa ni pamoja na wahandisi. Tena afanye hivi mara moja ili wahandisi waweze kufanya kazi. Wahandisi wetu leo wamejaa Botswana, Namibia, Swaziland na Afrika kusini na wanasifa nzuri sana huko. Iweje leo wakija katika ardhi ya Tanzania wanakuwa wabovu. CCM ijisafishe kwanza ndani kabla ya kupaka matope wengine.