Uchaguzi 2020 Uchambuzi: Tundu Lissu anaweza kumshinda Dkt. Magufuli na Maalim Seif anaweza kuibuka kidedea Zanzibar

Wasalaaam wanabodi,

Kampeni za uchaguzi mkuu zinaelekea ukingoni siku mbili zijazo nchi nzima. Tumeona Kila mgombea akijinadi kwa style yake na upekee kulingana na malengo na mikakati thabiti waliyojiwekea...
Uchambuzi wako unaakisi kiwango cha akili na weledi ulionao bahati mbaya kwa makusudi kabisa umeamua kuvitumia vibaya, kwa sababu kwa kukusudia, umeacha mambo ya msingi kabisa

IDADI YA WANACHAMA
Hawa ni ndio nguzo ya kwanza muhimu ktk kusaka kura WANACHAMA loyal and committed hawayumbishwi hata hoja iwe kali kiasi gani. Hawa sio UNDECIDED VOTERS bali ni kinyume chake hawabadiliki kwa upepo wa nyomi au ubora wa Sera.. kwao chama ni itikadi.
Je Upinzani Wana wangapi
Je CCM Wana wangapi!?

NGOME ZA KISIASA (Political stronghold regions):
NGOME za kisiasa hutengeneza base ya kuanzia mashambulizi..
Kwamba mkoa gani au kanda gani chama fulani kinapendwa na kuwa na ufuasi na ushawishi mkubwa!?

Ukichukia ACT(CUF ya zamani) Ngome yao ni Pemba ambako Wana 100% ya kuchukua majority votes kwa Urais na Wabunge wengi kuliko CCM. Hayo nia maeneo ambayo hakuna TISS, POLISI, NEC au VIFARU vinaweza kubadili matokeo bali wao ndio wanaweza ku manipulate matokeo. Je ngome kama hizo CHADEMA, ACT na CCM wanazo ngapi Kama mtaji wa kuanzia..!?

IDADI YA WBUNGE..
Kikatiba mwenye Wabunge wengi ndio anaunda Serikali, jee Kuna matarajio ya kupata angalau nusu ya Wabunge!?
Ikumbukwe kwamba Wabunge huakisi kiwango cha uungwaji mkono wa Mgombea Uraisi. Uzoefu Unaonyesha maeneo mengi ambako Kuna washindani wenye nguvu ngazi ya Ubunge huleta changamoto upande wa Urais pia. Jiulize Kuna uwezekano wa majimbo mangap mikoani!? Usizungumzie majimbo mawili matatu katika mkoa au kanda... Kwa mfano kule kanda ya ziwa Musoma, Simiyu, Mwanza, Shinyanga, Geita na Bukoba jumla mikoa 6 majimbo zaidi ya 40 lakini Upinzani hawana hata viti 8 na hakuna matumaini ya kufikisha angalau majimbo 10 mwaka huu.

Ktk Hali hiyo. Moja katibyabSifa Mgombea mwenye uwezo wa kushinda Uraisi ni uwezo wake binafsi kuwabeba Wabunge wa chama chake. Tuna tegemea Wabunge wangapi wanaobebwa na upepo wa Tundu!? Au Wabunge Wangapi Kama kina Heche watambeba Lisu!? Unategemeaje Ushindi wa Urais ktk mazingira haya!??
UPEPO WA MAKUNDI MAALUM,
Hapa namaanisha makundi rika wazee vs vijana, jinsia wanaume vs wanawake, maeneo ya makazi, Mjini vs vijijini, kiwango cha uelewa(ELIMU) wasomi vs watu wa kawaida..
Tupime kujua kundi lipi kwenye uwezo kubadili matokeo dhidi ya mingine na liko upande Gani?

POLITICAL AGENDA
Hapa kwenye agenda bado Kuna ukakasi. Kuna kundi linalazimisha agenda yake ndio ibebe garagumu la uchaguzi na wamefanikiwa kuaminsha watu uchaguzi utaamuliwa na agenda yao bila kujiuliza jinsi wananchi walivyoikubali agenda hiyo!?

Watu tunaaminishwa ati agenda kuu ni UHURU NA HAKI. Tunasahau kwamba CCM chini ya JPM imetoa Uhuru na HAKI kwa raia ya kawaida kuliko kipindi chochote ktk Historia ya Nchi hii. Tuliimba sana kule nyuma juu ya CCM kuwa Kama kambale baba ndevu mtoto ndevu tukimaanisha kuwa hata balozi au mtendaji wa Kijiji anaweza kukunyanyasa na usipate msaada. Leo sio mtendaji tu bali hata Mkuu wa Mkoa au Waziri hawezi kukunyanyasa ukiwa na ujasiri wa kudai haki yako.

Wahanga wakubwa wa UHURU na HAKI ni wanasiasa, wanaharakati na wanahabari, Kwa kuwa Wana access na media wanataka Wananchi tuwapiganie vita vyao huku wakituaminisha eti na sisi ni wahanga watarajiwa..
Jamani kila mmoja ajifunze kupigana vita yake. Leo hii Mimi Raia wa kawaida nahudumiwa vzr zaidi, nasikilizwa vizuri zaidi, napata haki zangu kwa urahisi zaidi, nina Uhuru zaidi mbele viongozi wa ngazi yangu kuliko kipindi chochote ktk Historia ya Nchi hii kwani KAMBALE MWENYE NDEVU amebaki ni JPM pekee, makamu wake na PM Majaliwa, FULL STOP. Kwa hiyo agenda ya UHURU NA HAKI sio hitaji au agenda ya Raia wa kawaida bali Social Media Na Opposition wanatulisha maneno.

Nimalizie kwa kusema kwamba huenda uchaguzi Ukawa na matokeo tofauti sana na mtazamo wa baadhi ya watu kwani wanakimbia towards wrong direction wakiamini eti the commons watawafuata. Wakifika mwisho wa mwendo watashanga watakapogeuka nyuma na kukuta Raia walikimbia opposite direction.
Tujiandae kisaikolojia
 
tuna nguvu za ku control huu upepo, maadam ni upepo, utapita tuu.
P
Mku kwa hali ilivyo sijui kwani sio kabisa.

Nakumbuka andiko lako moja linalouliza juu ya Congress kuwaandikia baadhi Marais Barua na baadhi ya hao marais hawapo duniani tena.

Na katika hilo uliuliza swala je Congress wanamtaka Mwenyekiti wetu hapa majibu hatuna kabisa.
Hili la nguvu ya umma limekaa vibaya kwani hata Mzee wetu Bashiru aliwahi kuliongelea juu ya Sudan.

Mpenye umetukalia vibaya kwani maonye ya Tasisi za kimataifa yamekuwa mengi mno Mku
 
kwani wakati lowasa angombania uraisi lissu hakuwepo chadema? kuna mtu alikua anafuatilia bunge na asijui tundu lissu wa chadema?
- wacha nkuchambulie, lowasa kama lowasa ndie alieleta machafuko ccm, yeye ndo aliesababisha mpasuko, yeye ndo alienda chadema na wengine ccm wakamfuata nyuma, na yeye ndo alirudi ccm na wakina sumaye wakamfuata nyuma...
hiv ni ukawa ipi ya 2015 ambayo haipo kwenye 'ukawa' hii ya 2020?!! ni nccr ndo haipo? ni cuf au ni udp? ni ipi. navoelewa ukawa ya 2015 ipo ndani ya cdm(haswa bara) na act(haswa zanzibar). kiukweli kabisa ukawa ya 2020 ni kamilifu na compact zaid kuliko ya 2015.

hiyo kazkazin unayoongelea kwenye ngome ya ccm ni kaskazin ipi hiyo? arusha? au moshi? au tanga? i wap hiyo ngome ya ccm kaskazini? huku kaskazinilikuwaga kidogo tanga ndiko ccm wakipumulia kwa kuwadanganya na kuwagawanya waislamu lakin mwaka huu mbona hata hiyo tanga ya ccm kwishabomoka?

Kuna mwislamu atapigia kura ccm inayowatesa mashakhe wake mahabusu miaka nenda rudi bila kosa?!!!! wewe labsa umaanishe tume na polisi wameweka ngome zaidi kaskazini kwa ajili ya kuiba kura...hapo utaeleweka.
 
Wasalaam wanabodi,

Kampeni za uchaguzi mkuu zinaelekea ukingoni siku mbili zijazo nchi nzima. Tumeona Kila mgombea akijinadi kwa style yake na upekee kulingana na malengo na mikakati thabiti waliyojiwekea...
hebu nipe line up japo ya mawaziri 5 kutoka Chadema kama wanashinda
 
hebu nipe line up japo ya mawaziri 5 kutoka CDM kama wanashinda
achilia mbali hilo unalosema kwanza hata tu serikali na bunge la sasa limeundwa kwa kiasi kikubwa na wanachadema kupitia ccm. isitoshe jpm kachukua watu kibao mtaani(waliokuwa nje ya mfumo wa serikali) kawapa madaraka kinyume cha utaratibu watu wasiojua hata basic ethics za governance!!!! pia utambue serikali siyo ccm. tatizo lenu jingine wanaccm mnafikiri(gi) eti serikali ni ccm na ccm ni serikali. hizi ni hangover za siasa za ujamaa.

unapouliza kama cdm wana watu wa kuunda serikali unamaanisga nini hasa? kwamba watanzania milion 60 hakuna wa kuunda serikal nje ya ccm? hoja yako hapa nini?
 
Wasalaam wanabodi,

Kampeni za uchaguzi mkuu zinaelekea ukingoni siku mbili zijazo nchi nzima. Tumeona Kila mgombea akijinadi kwa style yake na upekee kulingana na malengo na mikakati thabiti waliyojiwekea.
Chama tawala CCM walianza kwa kishindo kikubwa pale dodoma na kuonesha ukubwa wa idadi ya wafuasi wake walijipanga kutetea kiti Chao. Kadiri siku zilivyozidi kwenda utamu wa kampeni za chama tawala ulinoga kupita zilizotangulia.

Msingi wao mkubwa ulikuwa nyomi la watu na uwezo wa kufika vijijini zaidi. Tofauti na miaka yote mgombea wao amefika MAENEO mengi ya mijini zaidi kuliko vijijini ukilinganisha na 2015. Ukifanya SWOT Analysis utayaona haya:

Strength:

CCM huwezi kuitenganisha na Sola na pia huwezi kuitenganisha na serikali , na hapo ndipo utagundua kwa Nini NEC Ni watiifu Sana kwa CCM.

WEAKNESS

Kundi kubwa Lina wageni ambao sio wajuvi wa siasa za majukwaa na uwezo wa kubashiri yajayo kwa uyakinifu. Hii imewagharimu Sana kiasi hawajui kuwa mbaya wao Ni Seif sharrif Hamad au Tundu Lissu au ubovu wa kumsimamisha Mwinyi.

Si hivyo tu pia kushindwa kujua kuwa Kuivuruga CUF, CHADEMA na kununua wabunge wa upinzani ingelikuwa njia nyepesu ya wao kushinda Bila kupingwa au kushinda kwa kishindo kikubwa. Mpaka Sasa timu ya kampeni ya CCM imeshinda kuondoa udhaifu huu na unawagharimu kwenye field sababu kubwa walisahau kuwa upinzani Ni mioyo na hisia za watu na sio vyama. Hivyo mziki wa upinzani bado unagonga spika zao kwa Kasi Sana.

NGUVU YA UMMA

Inaonekana wazi LISSU na SEIF hawatanii hata kidogo jinsi walivyojipanga kutumia nguvu ya Umma. Kwa mwenye macho mapana .Umma haujawahi kushinda DHIDI ya watawala na Kama kweli basi hiki kitisho kikubwa Sana kwa CCM.

OPPORTUNITY

Fursa kubwa na ya pekee Ni kutumia Dola .

Pili mtaji wa fedha na rasilimali watu

TECHNICALLY

Hapa namaanisha MBINU za kiufundi za kushinda uchaguzi siku ya uchaguzi. MBINU ya kwanza NEC,hii imewapa wabunge zaidi ya 20

NEC na CCM ni watu wamoja wanaongea lugha Moja pia wanaweza kwa hiyari tu Kuivuruga ngome ya wapinzani na matokeo Yao kwa sababu hawana pa kushtakiwa popote kwa kuwa wao wanatoa tamko la mwisho.(namaanisha wakurugenzi) na dalili zishaonekana tayari.

CHADEMA NA ACT

Wote kwa pamoja na wajadili Bila kuwatenganisha ili nihitimishe vizuri. Ni ukweli usiopingika kuwa Zambarau wameiteka Zanzibar na CDM wameiteka Tanganyika.

Ubora wa viongozi wao wakuu wawili MBOWE & SEIF SHARRIF HAMAD umejidhihirisha wazi kwenye uchaguzi huu kwa kuruka mamii ya vihunzi na kuilaghai serikali mchana kweupeeee.

Hebu nikurudishe nyuma kidogo, siku Maalim Seif alipokwenda ikulu kumsalimia Rais huku MBOWE akipambana kesi ya Akwilina. Kila mtu alijua Maalim ameunga juhudi mkono na shughuli anayo mwamba. Sasa ndio nang'amua kwamba kumbe Ile Ni MBINU ya kimedani ya kuwalaghai watawala waamini upo pamoja nao. Ile ndio siku ya USHINDI wa SEIF Kama ikitokea atashinda Zanzibar kesho kutwa.

Hisia zinaniambia kwamba mwamba na mwalimu waliwaingiza Chaka CCM na Membe wao huku wakijua wamemficha mfukoni Lissu.
Tuachane na hayo hebu tuwafanyie SWOT na wao wapoje.
STRENGTH

NGUVU YA UMMA

Umma umewaelewa Sana ACT &CHADEMA na ushahidi wa Watanzania kuwachangia pesa wahalifu wasiende jela badala yake walipiwe faini na warudi uraiani Ni ishara Tosha upo tayari kufanya lolote lenye kuwalinda Chadema kwa upande wa bara. Jambo Hili liliwatia kiwewe IKULU na kesho yake Rais aliamua kumlipia msigwa kuonesha Kwamba Rais Ana huruma na wapinzani. Kama watu walichanga dusko dusko namaanisha kiasi Cha 1k -10k kinyume chake hizi buku buku Ni idadi ya wapiga kura wa upinzani. Sasa kazi yako chukua kikokotoo halafu tafuta majibu Ni watu wangapi wanasapoti Chadema. Zenji siongei Kila mtu ameona NGUVU ya Maalim kaondoka na wanachama wake kwenda ACT so like amevimbisha msuli kwa mamlaka.

UWEZO WA KUNUSA HATARI

Tukio la Membe kuachwa kwenye mataa na hajielewi linathibitisha uwezo wa wapinzani KUNUSA HATARI.
Waliujua mtego wa CCM na wao wakatega wa kwao kwenda ikulu na kuleta picha kwamba Seif Ni mshkaji na MBOWE mkorofi kumbe Ni mtego wa Kumlinda LISSU na kunifanya Membe aonekane punguani asiyejua anataka nn.
Membe Ni ujio hatarishi kwa upinzani na Lissu anatafutwa na watesi wake asirudi kwenye siasa. Inaonesha wazi Kuna makubaliano kwamba ACT na CDM wote waingize wagombea ili mmoja akikatwa aungwe mkono mwingine na ndicho kinachoendelea Sasa.

Wanachama 9M according to MBOWE

WEAKNESS
Hawana Dola Wala serikali na hawajahi kushinda uchaguzi ngazi ya Rais

NEC haipo upande wao

UWEZO mdogo wa ulinzi na USALAMA wa viongozi wake, Ni rahisi kumteka au kumkata au kuzuia mkutano wa upinzani.

Ukosefu wa rasilimali fedha

OPPORTUNITY

MPASUKO wa CCM baada ya kura za MAONI. Huu Ni mtaji mkubwa Sana wa upinzani na dalili zimeonekana wazi Kanda ya ziwa na Zanzibar. Maamuzi ya Dodoma huenda yakawafanya CCM kupoteza majimbo 35-50 ya uchaguzi wasipotumia utemi.

KULINDA KURA VITUONI

Wakiwekeza NGUVU imara ya KULINDA KURA CCM hawana Chao. Naamini Lissu anamaanisha na ujumbe umewafikia walengwa. Wameanza kujibu maneno

MAKUNDI MAALUM YALIYOUMIZWA NA SERIKALI

Hapa nawaweka wahanga wote wa utawala wa awamu ya tano. Wafanyakazi hewa,waliobomolewa,waliotoswa walimu, wafanyakazi wa serikali, waliokosa mshahara n.k

Hawa Ni game changers watatoa USHINDI 5%-7% kwa Lissu sababu Wana maumivu Yao.

TECHNICALLY

MAANDAMANO YASIYO KIKOMO

Ukifuatilia vizuri utagundua MBINU pekee ya wapinzani kuingia ikulu Ni MAANDAMANO YASIYO na KIKOMO. Hii ndio MBINU ya kiufundi yenye chanya na imewasaidi wapinzani wa nchi jirani kuingia na kushika serikali punde tu baada ya uchaguzi.

Hakuna serikali ya kiafrika imeyashinda MAANDAMANO YASIYO KIKOMO. Kiufundi wapinzani wako vyedi.

MATAMKO NA VITISHO VYA VIKWAZO
tangu wiki iliyopita mataifa makubwa yamekuwa na spidi ya MATAMKO na baru ya into kwa serikali ya Tanzania Ni wazi wapinzani kwenye MBINU hii wako mbali Sana. Yakitokea tusiyoyaomba wanatusua mapema.

Baaada ya mtazamo huo Sasa najikita kueleza kwa Nini Lissu 49% na Magufuli 47%.

Sympathy
Umaarufu wa Magufuli umeporomoka Sana baada ya kura za MAONI. Wakati huohuo umaarufu wa Chadema umekuwa mkubwa kupindukia sababu watu waliaminishwa kuwa upinzani umekufa na kinyume chake umekuwa zaidi kwa sababu ya huruma kuwa wanaonewa.

Kifungo Cha viongozi wa Chadema mwezi Machi kiliibua hisia za huruma kwa wananchi na kuamsha Ari ya huruma kwa wapinzani. Ujio wa Lissu umeikuza sympathy ya Chadema na ACT kwa pamoja na hivi tunavyoongea waliopewa kazi kushughulika na wapinzani wanalala na viatu.Hii itawapa kura sawa na 21%

Waislamu

Hapa Sina lengo la udini Ila hakuna asiyejua michango ya waislamu hapa bongo. Ujio wa sheikh Ponda Ni pigo kwa CCM na faida upinzani.

Sheikh ponda kashawagawa na Hili litawapa wapinzi USHINDI Zanzibar na pwani na mikoa ya kusini ambapo CCM imewakwaza kwa kiasi kikubwa kupitia korosho. Hili litapunguza 45% kwenye kura za waislam zilizotakiwa kwenda ccm

KOROSHO

sekeseke la korosho linaonekana Ni shida kubwa Sana kiasi Cha kuitikisa ngome ya CCM na hii ikikutana na impact ya ponda itawaumiza CCM zaidi na kuwanufaisha wapinzani.

Low turnover
Mwitiko mdogo wa wapiga kura siku ya uchaguzi, Ni pigo kingine kwa CCM na msaada kwa upinzani. Kuna uwezekano turn over ya wapiga kura ikawa watu 9M -11M

Hapa ndio kifo Cha CCM kinaanzia na hiili litawapunguzia 50% kura zote walizotarajia kupata kwenye uchaguzi huu.hii Ni faida kwa upinzani kwa sababu wao wanategemea sababu za hapo juu kupindua meza.

Common interest za Wazanzibar
Ikumbukwe watu wa visiwani wakitaka Lao hawashindwi licha ya utofauti wa vyama. Ni wazi CCM na ACT wote Lao Ni Moja ingawaje kwa nje wanashambuliana Jana kwamba wanapigana Vita ya 3 ya dunia. Seif anakwenda kushinda uchaguzi kwa sababu wazenji wote Wana ongozwa na common interest kuiona CCM Ni kikwazo kwao so best way Ni kumpa seif na sio Mwinyi.

Membe ATAPATA 1.1%
Lipumba & other 0.9%
Kuharibika kura 2%
Tutarajie mchuano mkali na matokeo ndio hayo hapo juu.

Karibuni kwa mjadalaa
Utopolo kichwani, Lissu hawezi kuwa Rais wa Watanzania milele.
 
Utopolo kichwani, Lissu hawezi kuwa Rais wa Watanzania milele.
saga chupa mezea na maji ya bomba.
kila Mtanzania mwenye vigezo na sifa za kugombea urais kama zilivyoainishwa kwenye sheria anaweza kuwa rais. Lisu kapitishwa na Tume kuwa ametimiza vigezo hivyo na kwa hiyo anaweza kuwa rais vizur tu. intataprengenyua awe na uwezo wa kuwa rais halafu mwanasheria nguli ashindwe kwa lip hasa?!!!
 
Uwezekano wa Tundu Lissu kushinda uchaguzi upo lakini je atatangazwa kama kashinda kweli.
Kwa Zanzibar Hilo halina majadala Maalimu seif atashinda je atatangazwa au ndiyo yaleyale ya Jeche 2015.

Hadi Sasa tume ya uchaguzi ktk imeonyesha upendeleo, uonevu ktk uchaguzi... Huku Ni kuharibu uchaguzi na kuongeza chuki kwa raia...
 
saga chupa mezea na maji ya bomba.
kila Mtanzania mwenye vigezo na sifa za kugombea urais kama zilivyoainishwa kwenye sheria anaweza kuwa rais. Lisu kapitishwa na Tume kuwa ametimiza vigezo hivyo na kwa hiyo anaweza kuwa rais vizur tu. intataprengenyua awe na uwezo wa kuwa rais halafu mwanasheria nguli ashindwe kwa lip hasa?!!!
CCM hawakubaliani na uhalisia au wanategemea mazoea. Maana Kila mwana CCM anakuwa mkali tu Bila sababu
 
hebu nipe line up japo ya mawaziri 5 kutoka CDM kama wanashinda
MBOWE -waziri mkuu
Matiko - waziri wa Afya
Nyalandu - Mambo ya nje
Mrema -tamisemi
Mdee- ARDHI

Vipi tuongeze sauti
 
kwani wakati lowasa angombania uraisi lissu hakuwepo chadema? kuna mtu alikua anafuatilia bunge na asijui tundu lissu wa chadema?
- wacha nkuchambulie, lowasa kama lowasa ndie alieleta machafuko ccm, yeye ndo aliesababisha mpasuko, yeye ndo alienda chadema na wengine ccm wakamfuata nyuma, na yeye ndo alirudi ccm na wakina sumaye wakamfuata nyuma

- sifanyi siasa ushabiki ni mahesabu ya kawaida sana, lowasa kama lowasa kwa mtu anaefuatilia siasa anajua nguvu alionayo kwenye hizi siasa ndo maaana, lowasa ndo richmond, lowasa ndo EPA!

- basi sasa kwa mafupi nliokupa uelewe kwamba lowasa kama lowasa ana asilimia 18% ya all tanzania voters,
(na hii imefanyika research na ndo maana lisu ameipresent apo, sio maneno ya vijiwe ni watu walilipwa kufanya huu uchungizi)
na ndo maaana chadema walimpigia magoti aende chadema, (kama una mabishano bado, lissu ndo amesema mwenyewe ubishane nae sasa kama unataka maaana wao ndo walitoa ela ya uchunguzi)
: sasa basi kwa kua umeshaambiwa lowasa kama lowasa ana 18% likability yeye kama yeye(kupendwa): basi ulichoandika chote ni rubbish
hapo tumamaliza

2) 2015 kura hazikua za chadema peke yake, kura zilikua za UKAWA! wacha kujiongeza sana una hali mbaya
3) chadema ina nguvu sana mikoa ya kaskazini, 2015 chadema ilibebwa sana na mikoa ya kaskazini, leo hii ukiongelea mikoa ya kaskazini unaongelea ngome kurudi ccm

kwa hayo mafupi nakusogezea kipaza sauti
Kama msingi wa tafiti Ni personality Lowassa kwa Sasa Hana na Wala haweiz athiri chochote.
Kama msingi Ni yupo wapi mbatia na NCCR? CUF ya huku bara?

mbona kazi Ni nyepesi tu.

Unakitetea Ni sawa na mtu anayemtetea Juma Nature wa kale na Diamond wa Leo kwa kusema Juma Nature akiandaa show atajaza kuliko Mond wakati kashapoteza mvuto.

Au wema sepetu na Amisa Mobeto
Au
Mange na kigogo .

Kwenye siasa siku 2 Ni nyingi Sana sembuse miaka 5.
 
Hizi ni ndoto za mchana. Mmejaribu kumnadi Lissu lakini watanzania wamemkataa, hawataki wakala wa mabeberu. Watanzania wameamua kwenda na JPM kwamiaka mingine mitano. Utafiti uliofanywa kisayansi juzi na Taasisi ya IBC Research International imegundua JPM anashinda kwa 89.5 na Lissu ataambulia tu 8.2% ya kura zote. Nakuhurumieni sana wana Ufipa, pengine ndoto hizi za mchana unazokuja nazo ni sehemu yenu ya kujifariji. Kila Mahali ni kura ya ndiyo kwa JPM. Hakuna mtanzania wa kumchagua Lissu . Tunakwenda na JPM .
Labda wameamua kwenda naye chato na si ikulu tena akusanye kilichochake mapema
 
Kuna mtu kanambia anauhakika Lissu atashinda nikamwambia mimi sio mwanasiasa wala mtabiri ila Magufuli atashinda.
Nikamuomba tuweke dau la milioni mojamoja ili ambae kauli yake itakua ilikua yakweli achukue milioni mbili kakataa nikajua kumbe ananiambia maneno asio na uhakika nayo kabisa na anaujua ukweli.

Sent from my Infinix X603 using JamiiForums mobile app
Ukute wkt huo hata jero huna mfukoni ndio maana akakupuuza namna hiyo
 
Wasalaam wanabodi,

Kampeni za uchaguzi mkuu zinaelekea ukingoni siku mbili zijazo nchi nzima. Tumeona Kila mgombea akijinadi kwa style yake na upekee kulingana na malengo na mikakati thabiti waliyojiwekea.
Chama tawala CCM walianza kwa kishindo kikubwa pale dodoma na kuonesha ukubwa wa idadi ya wafuasi wake walijipanga kutetea kiti Chao. Kadiri siku zilivyozidi kwenda utamu wa kampeni za chama tawala ulinoga kupita zilizotangulia.

Msingi wao mkubwa ulikuwa nyomi la watu na uwezo wa kufika vijijini zaidi. Tofauti na miaka yote mgombea wao amefika MAENEO mengi ya mijini zaidi kuliko vijijini ukilinganisha na 2015. Ukifanya SWOT Analysis utayaona haya:

Strength:

CCM huwezi kuitenganisha na Sola na pia huwezi kuitenganisha na serikali , na hapo ndipo utagundua kwa Nini NEC Ni watiifu Sana kwa CCM.

WEAKNESS

Kundi kubwa Lina wageni ambao sio wajuvi wa siasa za majukwaa na uwezo wa kubashiri yajayo kwa uyakinifu. Hii imewagharimu Sana kiasi hawajui kuwa mbaya wao Ni Seif sharrif Hamad au Tundu Lissu au ubovu wa kumsimamisha Mwinyi.

Si hivyo tu pia kushindwa kujua kuwa Kuivuruga CUF, CHADEMA na kununua wabunge wa upinzani ingelikuwa njia nyepesu ya wao kushinda Bila kupingwa au kushinda kwa kishindo kikubwa. Mpaka Sasa timu ya kampeni ya CCM imeshinda kuondoa udhaifu huu na unawagharimu kwenye field sababu kubwa walisahau kuwa upinzani Ni mioyo na hisia za watu na sio vyama. Hivyo mziki wa upinzani bado unagonga spika zao kwa Kasi Sana.

NGUVU YA UMMA

Inaonekana wazi LISSU na SEIF hawatanii hata kidogo jinsi walivyojipanga kutumia nguvu ya Umma. Kwa mwenye macho mapana .Umma haujawahi kushinda DHIDI ya watawala na Kama kweli basi hiki kitisho kikubwa Sana kwa CCM.

OPPORTUNITY

Fursa kubwa na ya pekee Ni kutumia Dola .

Pili mtaji wa fedha na rasilimali watu

TECHNICALLY

Hapa namaanisha MBINU za kiufundi za kushinda uchaguzi siku ya uchaguzi. MBINU ya kwanza NEC,hii imewapa wabunge zaidi ya 20

NEC na CCM ni watu wamoja wanaongea lugha Moja pia wanaweza kwa hiyari tu Kuivuruga ngome ya wapinzani na matokeo Yao kwa sababu hawana pa kushtakiwa popote kwa kuwa wao wanatoa tamko la mwisho.(namaanisha wakurugenzi) na dalili zishaonekana tayari.

CHADEMA NA ACT

Wote kwa pamoja na wajadili Bila kuwatenganisha ili nihitimishe vizuri. Ni ukweli usiopingika kuwa Zambarau wameiteka Zanzibar na CDM wameiteka Tanganyika.

Ubora wa viongozi wao wakuu wawili MBOWE & SEIF SHARRIF HAMAD umejidhihirisha wazi kwenye uchaguzi huu kwa kuruka mamii ya vihunzi na kuilaghai serikali mchana kweupeeee.

Hebu nikurudishe nyuma kidogo, siku Maalim Seif alipokwenda ikulu kumsalimia Rais huku MBOWE akipambana kesi ya Akwilina. Kila mtu alijua Maalim ameunga juhudi mkono na shughuli anayo mwamba. Sasa ndio nang'amua kwamba kumbe Ile Ni MBINU ya kimedani ya kuwalaghai watawala waamini upo pamoja nao. Ile ndio siku ya USHINDI wa SEIF Kama ikitokea atashinda Zanzibar kesho kutwa.

Hisia zinaniambia kwamba mwamba na mwalimu waliwaingiza Chaka CCM na Membe wao huku wakijua wamemficha mfukoni Lissu.
Tuachane na hayo hebu tuwafanyie SWOT na wao wapoje.
STRENGTH

NGUVU YA UMMA

Umma umewaelewa Sana ACT &CHADEMA na ushahidi wa Watanzania kuwachangia pesa wahalifu wasiende jela badala yake walipiwe faini na warudi uraiani Ni ishara Tosha upo tayari kufanya lolote lenye kuwalinda Chadema kwa upande wa bara. Jambo Hili liliwatia kiwewe IKULU na kesho yake Rais aliamua kumlipia msigwa kuonesha Kwamba Rais Ana huruma na wapinzani. Kama watu walichanga dusko dusko namaanisha kiasi Cha 1k -10k kinyume chake hizi buku buku Ni idadi ya wapiga kura wa upinzani. Sasa kazi yako chukua kikokotoo halafu tafuta majibu Ni watu wangapi wanasapoti Chadema. Zenji siongei Kila mtu ameona NGUVU ya Maalim kaondoka na wanachama wake kwenda ACT so like amevimbisha msuli kwa mamlaka.

UWEZO WA KUNUSA HATARI

Tukio la Membe kuachwa kwenye mataa na hajielewi linathibitisha uwezo wa wapinzani KUNUSA HATARI.
Waliujua mtego wa CCM na wao wakatega wa kwao kwenda ikulu na kuleta picha kwamba Seif Ni mshkaji na MBOWE mkorofi kumbe Ni mtego wa Kumlinda LISSU na kunifanya Membe aonekane punguani asiyejua anataka nn.
Membe Ni ujio hatarishi kwa upinzani na Lissu anatafutwa na watesi wake asirudi kwenye siasa. Inaonesha wazi Kuna makubaliano kwamba ACT na CDM wote waingize wagombea ili mmoja akikatwa aungwe mkono mwingine na ndicho kinachoendelea Sasa.

Wanachama 9M according to MBOWE

WEAKNESS
Hawana Dola Wala serikali na hawajahi kushinda uchaguzi ngazi ya Rais

NEC haipo upande wao

UWEZO mdogo wa ulinzi na USALAMA wa viongozi wake, Ni rahisi kumteka au kumkata au kuzuia mkutano wa upinzani.

Ukosefu wa rasilimali fedha

OPPORTUNITY

MPASUKO wa CCM baada ya kura za MAONI. Huu Ni mtaji mkubwa Sana wa upinzani na dalili zimeonekana wazi Kanda ya ziwa na Zanzibar. Maamuzi ya Dodoma huenda yakawafanya CCM kupoteza majimbo 35-50 ya uchaguzi wasipotumia utemi.

KULINDA KURA VITUONI

Wakiwekeza NGUVU imara ya KULINDA KURA CCM hawana Chao. Naamini Lissu anamaanisha na ujumbe umewafikia walengwa. Wameanza kujibu maneno

MAKUNDI MAALUM YALIYOUMIZWA NA SERIKALI

Hapa nawaweka wahanga wote wa utawala wa awamu ya tano. Wafanyakazi hewa,waliobomolewa,waliotoswa walimu, wafanyakazi wa serikali, waliokosa mshahara n.k

Hawa Ni game changers watatoa USHINDI 5%-7% kwa Lissu sababu Wana maumivu Yao.

TECHNICALLY

MAANDAMANO YASIYO KIKOMO

Ukifuatilia vizuri utagundua MBINU pekee ya wapinzani kuingia ikulu Ni MAANDAMANO YASIYO na KIKOMO. Hii ndio MBINU ya kiufundi yenye chanya na imewasaidi wapinzani wa nchi jirani kuingia na kushika serikali punde tu baada ya uchaguzi.

Hakuna serikali ya kiafrika imeyashinda MAANDAMANO YASIYO KIKOMO. Kiufundi wapinzani wako vyedi.

MATAMKO NA VITISHO VYA VIKWAZO
tangu wiki iliyopita mataifa makubwa yamekuwa na spidi ya MATAMKO na baru ya into kwa serikali ya Tanzania Ni wazi wapinzani kwenye MBINU hii wako mbali Sana. Yakitokea tusiyoyaomba wanatusua mapema.

Baaada ya mtazamo huo Sasa najikita kueleza kwa Nini Lissu 49% na Magufuli 47%.

Sympathy
Umaarufu wa Magufuli umeporomoka Sana baada ya kura za MAONI. Wakati huohuo umaarufu wa Chadema umekuwa mkubwa kupindukia sababu watu waliaminishwa kuwa upinzani umekufa na kinyume chake umekuwa zaidi kwa sababu ya huruma kuwa wanaonewa.

Kifungo Cha viongozi wa Chadema mwezi Machi kiliibua hisia za huruma kwa wananchi na kuamsha Ari ya huruma kwa wapinzani. Ujio wa Lissu umeikuza sympathy ya Chadema na ACT kwa pamoja na hivi tunavyoongea waliopewa kazi kushughulika na wapinzani wanalala na viatu.Hii itawapa kura sawa na 21%

Waislamu

Hapa Sina lengo la udini Ila hakuna asiyejua michango ya waislamu hapa bongo. Ujio wa sheikh Ponda Ni pigo kwa CCM na faida upinzani.

Sheikh ponda kashawagawa na Hili litawapa wapinzi USHINDI Zanzibar na pwani na mikoa ya kusini ambapo CCM imewakwaza kwa kiasi kikubwa kupitia korosho. Hili litapunguza 45% kwenye kura za waislam zilizotakiwa kwenda ccm

KOROSHO

sekeseke la korosho linaonekana Ni shida kubwa Sana kiasi Cha kuitikisa ngome ya CCM na hii ikikutana na impact ya ponda itawaumiza CCM zaidi na kuwanufaisha wapinzani.

Low turnover
Mwitiko mdogo wa wapiga kura siku ya uchaguzi, Ni pigo kingine kwa CCM na msaada kwa upinzani. Kuna uwezekano turn over ya wapiga kura ikawa watu 9M -11M

Hapa ndio kifo Cha CCM kinaanzia na hiili litawapunguzia 50% kura zote walizotarajia kupata kwenye uchaguzi huu.hii Ni faida kwa upinzani kwa sababu wao wanategemea sababu za hapo juu kupindua meza.

Common interest za Wazanzibar
Ikumbukwe watu wa visiwani wakitaka Lao hawashindwi licha ya utofauti wa vyama. Ni wazi CCM na ACT wote Lao Ni Moja ingawaje kwa nje wanashambuliana Jana kwamba wanapigana Vita ya 3 ya dunia. Seif anakwenda kushinda uchaguzi kwa sababu wazenji wote Wana ongozwa na common interest kuiona CCM Ni kikwazo kwao so best way Ni kumpa seif na sio Mwinyi.

Membe ATAPATA 1.1%
Lipumba & other 0.9%
Kuharibika kura 2%
Tutarajie mchuano mkali na matokeo ndio hayo hapo juu.

Karibuni kwa mjadalaa
Kaka umechambua vyema bila upendeleo. Hongera mzee kwa kufanya utafiti makini na SWOT analysis iloyo balance mizani.
 
Hizi ni ndoto za mchana. Mmejaribu kumnadi Lissu lakini watanzania wamemkataa, hawataki wakala wa mabeberu. Watanzania wameamua kwenda na JPM kwamiaka mingine mitano. Utafiti uliofanywa kisayansi juzi na Taasisi ya IBC Research International imegundua JPM anashinda kwa 89.5 na Lissu ataambulia tu 8.2% ya kura zote. Nakuhurumieni sana wana Ufipa, pengine ndoto hizi za mchana unazokuja nazo ni sehemu yenu ya kujifariji. Kila Mahali ni kura ya ndiyo kwa JPM. Hakuna mtanzania wa kumchagua Lissu . Tunakwenda na JPM .
Hivi ni wakati gani wazungu wanakuwa wafadhili na ni wakati gani hao hao wanakuwa mabeberu?
 
Kama msingi wa tafiti Ni personality Lowassa kwa Sasa Hana na Wala haweiz athiri chochote.
Kama msingi Ni yupo wapi mbatia na NCCR? CUF ya huku bara?

mbona kazi Ni nyepesi tu.

Unakitetea Ni sawa na mtu anayemtetea Juma Nature wa kale na Diamond wa Leo kwa kusema Juma Nature akiandaa show atajaza kuliko Mond wakati kashapoteza mvuto.

Au wema sepetu na Amisa Mobeto
Au
Mange na kigogo .

Kwenye siasa siku 2 Ni nyingi Sana sembuse miaka 5.


Utaacha kufanya siasa za mahaba lini sasa, anyway will see who projected well, jiandae for 20% - 30%
 
Back
Top Bottom