Kwa rehma zake Mwenyezi Mungu ni matumaini yangu sote tutaumaliza Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan salama salimin na hakika yeye ndiye mwenye kurehemu riziki zetu kubwa na ndogo na hapana mwingine apaswaye kuabudiwa. Tumuombe sote atuepushe na kila lisokuwa na kheri kwetu. Ameen.
Nina hakika siku ya leo tutasikia SIFA kemkem za mafuta ya tin na zaitun zitamiminika kupamba na kusifia hotuba ya rais wa JMT Mama Samia Suluhu Hassan kwa sababu imewagusa watu wote katika mazingira tofauti katika mwelekeo mpya wa dira ya Awamu hii ya sita ikitekeleza kauli mbiu ya KAZI IENDELEE.
Mimi binafsi, niseme ukweli wangu kutoka moyoni ya kuwa sii mshabiki wa rais Mama Samia Suluhu Hassan toka hotuba yake ya kwanza alipo apishwa kama rais wa Awamu ya sita. Huu ndio ukweli wangu! Na sababu zangu ni ndogo kabisa, nilimsoma toka mwanzo mwelekeo na Dira yake Kitaifa, dira ambayo Kiitikadi, mimi sii muumini wake na hupingana na nadharia zinazofungamana zaidi na UBEPARI badala ya UJAMAA wa Mwafrika.
Hivyo unaponisoma hapa ni muhimu Uzingatie kuwa mimi ni muumini wa UJAMAA wa Mwafrika na naamini Maendeleo ya Tanzania yataletwa na WATANZANIA wenyewe badala ya WAWEKEZAJI kutoka nje. Imani ya kwamba maendeleo yetu yanahitaji kuweka masharti rahisi ili kuvutia Wawekezaji ni sawa na fikra za.Kitumwa za Mababu zetu walokubali kupewa na wakoloni Shanga na vilemba ili tupendeze huku wagenu wakiondoka na madini mali ghafi na nyara zetu za Kitaifa.
Niseme wazi kwamba binafsi yangu naiona tofauti kubwa sana baina ya Hayati rais wa awamu ya Tani John Pombe Magufuli na Mama Samia Suluhu Hassan na kwamba hawa sii kitu kimoja hata kidogo. Tofauti zinazotokana na ahadi za mabadiriko makubwa ya SERA na SHERIA ambazo Chama cha Mapinduzi na Hayati Magufuli walizitumia kupata ushindi mkubwa katika Uchaguzi wa mwaka 2020. Niseme kwa nini nasema hivi?
Haina Shqka kabisa, Hayati Magufuli alikuwa rais anayepigania maslahi ya Wananchi Wanyonge kwa maana ya Watanzania Maskini dhidi ya Wawekezaji Mabeberu tofauti kabisa na Dira na Mwelekeo wa Mama Samia anayetazama zaidi viwashwishi kwa maslahi ya WAWEKEZAJI pamoja na dhana ya UKUONGEZA UZALISHAJI wa Mazao kwa WINGI zaidi (Quantity) badala ya fikra za Magufuli kudhamiria Kuanzisha viwanda vya ndani ili Kuongeza thamani ya Mazao yetu ya Asili yalokuwa BORA zaidi (Quality).
Nimalizie tu kwa kusema, rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan awe makini sana na dhana hizi, kwani hatukuanza jana wala juzi. Tulifuata mrengo ule toka wakati wa Rais Ally Hassan Mwinyi, akaja Mh. Benjamin Mkapa na Mwishowe mstaafu Jakaya Kikwete, na kote huko nyuma tulifanya makosa mengi sana kwa dhana ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Biashara. Matokeo yake tukaunda Matabaka ya Walionacho na wasiona nacho baina ya Wainanchi wenyewe. Ndipo Ufisadi na rushwa viliposhamiri kwani hapana alotaka kubakia katika kundi la wasionacho (Maskini)
Maoni ya rais kuhusu matumizi ya mbinu za kisasa katika Kilimo, kuna hatari kubwa ya nchi yetu kurudi kutawaliwa tena Kiuchumi kutokana na ujio wa mbegu za maabara ambazo zitaondoa kabisa rutuba ya Ardhi yetu, ubora wa mbegu zetu (Organic) na kubwa zaidi kumikilisha Mashirika ya nje nguzo za Uchumi wetu Kitaifa.
Maasalaam,
- Ramadhan Kareem
Nina hakika siku ya leo tutasikia SIFA kemkem za mafuta ya tin na zaitun zitamiminika kupamba na kusifia hotuba ya rais wa JMT Mama Samia Suluhu Hassan kwa sababu imewagusa watu wote katika mazingira tofauti katika mwelekeo mpya wa dira ya Awamu hii ya sita ikitekeleza kauli mbiu ya KAZI IENDELEE.
Mimi binafsi, niseme ukweli wangu kutoka moyoni ya kuwa sii mshabiki wa rais Mama Samia Suluhu Hassan toka hotuba yake ya kwanza alipo apishwa kama rais wa Awamu ya sita. Huu ndio ukweli wangu! Na sababu zangu ni ndogo kabisa, nilimsoma toka mwanzo mwelekeo na Dira yake Kitaifa, dira ambayo Kiitikadi, mimi sii muumini wake na hupingana na nadharia zinazofungamana zaidi na UBEPARI badala ya UJAMAA wa Mwafrika.
Hivyo unaponisoma hapa ni muhimu Uzingatie kuwa mimi ni muumini wa UJAMAA wa Mwafrika na naamini Maendeleo ya Tanzania yataletwa na WATANZANIA wenyewe badala ya WAWEKEZAJI kutoka nje. Imani ya kwamba maendeleo yetu yanahitaji kuweka masharti rahisi ili kuvutia Wawekezaji ni sawa na fikra za.Kitumwa za Mababu zetu walokubali kupewa na wakoloni Shanga na vilemba ili tupendeze huku wagenu wakiondoka na madini mali ghafi na nyara zetu za Kitaifa.
Niseme wazi kwamba binafsi yangu naiona tofauti kubwa sana baina ya Hayati rais wa awamu ya Tani John Pombe Magufuli na Mama Samia Suluhu Hassan na kwamba hawa sii kitu kimoja hata kidogo. Tofauti zinazotokana na ahadi za mabadiriko makubwa ya SERA na SHERIA ambazo Chama cha Mapinduzi na Hayati Magufuli walizitumia kupata ushindi mkubwa katika Uchaguzi wa mwaka 2020. Niseme kwa nini nasema hivi?
Haina Shqka kabisa, Hayati Magufuli alikuwa rais anayepigania maslahi ya Wananchi Wanyonge kwa maana ya Watanzania Maskini dhidi ya Wawekezaji Mabeberu tofauti kabisa na Dira na Mwelekeo wa Mama Samia anayetazama zaidi viwashwishi kwa maslahi ya WAWEKEZAJI pamoja na dhana ya UKUONGEZA UZALISHAJI wa Mazao kwa WINGI zaidi (Quantity) badala ya fikra za Magufuli kudhamiria Kuanzisha viwanda vya ndani ili Kuongeza thamani ya Mazao yetu ya Asili yalokuwa BORA zaidi (Quality).
Nimalizie tu kwa kusema, rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan awe makini sana na dhana hizi, kwani hatukuanza jana wala juzi. Tulifuata mrengo ule toka wakati wa Rais Ally Hassan Mwinyi, akaja Mh. Benjamin Mkapa na Mwishowe mstaafu Jakaya Kikwete, na kote huko nyuma tulifanya makosa mengi sana kwa dhana ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Biashara. Matokeo yake tukaunda Matabaka ya Walionacho na wasiona nacho baina ya Wainanchi wenyewe. Ndipo Ufisadi na rushwa viliposhamiri kwani hapana alotaka kubakia katika kundi la wasionacho (Maskini)
Maoni ya rais kuhusu matumizi ya mbinu za kisasa katika Kilimo, kuna hatari kubwa ya nchi yetu kurudi kutawaliwa tena Kiuchumi kutokana na ujio wa mbegu za maabara ambazo zitaondoa kabisa rutuba ya Ardhi yetu, ubora wa mbegu zetu (Organic) na kubwa zaidi kumikilisha Mashirika ya nje nguzo za Uchumi wetu Kitaifa.
Maasalaam,
- Ramadhan Kareem