Uchambuzi: Hali ya Uwanja wa ndege wa Kimataifa Chato baada ya Magufuli kustaafu

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
48,776
102,138
IMG-20171111-WA0007.jpg

IMG-20171111-WA0003.jpg

Uwanja wa ndege aliojenga Mobutu umegeuka kuwa uwanja wa popo na panya


Dikteta Mobutu aliamua kujenga Uwanja wa Gbadolite katika Jimbo la Nord-Ubangi, mwendo wa saa 5 na dakika 16 kutoka mji huo hadi kijijini Lisala (umbali wa 332km) alikozaliwa Mobutu mwenyewe, Gbadolite kilikuwa kijiji kidogo ndani ya msitu mnene chenye watu 1,500 tu, ambapo kwa maslahi yake ya kutaka umaarufu, akaubadili kuwa mji mkubwa akijenga hekalu lake kubwa, hoteli ya kitalii ya nyota tano iliyoitwa Motel Nzekele ambayo viongozi maarufu duniani kama Mfalme wa Ubelgiji, Rais wa Ufaransa Francois Mitterrand na Papa John Paul II walipata kulala.

Huku kwetu kunajengwa uwanja wa ndege wa kimataifa. Haijulikani kama uamuzi wa serikali ya Rais Magufuli umelenga maendeleo ama tu unataka kufanya jambo la kukumbukwa kwa kuanzisha ‘majiji’ mapya kama ilivyokuwa kwa Gbadolite (maarufu kama Versailles of the Jungle – yaani ‘Versailles ya Msituni’ wakifananisha na Hekalu la Versailles nchini Ufaransa).

Taarifa zilizopo zinaonyesha kwamba, uwanja huo utakuwa na eneo la kurukia ndege (runaway) wenye urefu wa meta 3,000 (sawa na kilometa 3) na upana wa meta 45, ukiwa na tofauti ndogo na uwanja wa ndege wa Gbadolite (urefu kilometa 3.2 na upana meta 60) kaskazini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo uliojengwa na Dikteta Mobutu Sese Seko mwaka 1972 ili kuruhusu midege mikubwa ya Concorde kutua na kuruka.

Hoja inakuja je,kuna hitaji lolote la kujenga uwanja huo kwa sasa?

Katika kipindi ambacho uchumi wa taifa bado haujatengemaa, ujenzi wa uwanja wa kimataifa wa ndege katika mji wa Chato wenye wakazi 17,508 tu (kwa mujibu wa Sensa ya Taifa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012) unaonekana ni uamuzi usiozingatia maslahi mapana ya taifa.

Hoja ya Mh. Sugu jana kwamba baada ya mda wa Magufuli kwisha nani ataenda kutua Chato? Ni hoja ya msingi sana

Nimelinganisha alichokifanya Mabutu miaka hiyo na kinachoendelea hivi sasa Chato ili kuleta picha ya hali itakavyokuwa mbeleni kwa mradi mkubwa kama ule.

Nini maoni yako?
 
hivi unajua chato kunanini..Chatao kuna mbuga za brigi na rubombo kwa ajili ya utalii... Chato panafunguliwa mgod mkubwa sana wa dhahabu kuliko GGM amabo utakaa miaka 30-40 life span waith high grade gold in Africa and South America. usifate ujinga wakupinga kama wabunge amabo wanalirputa bila kufanya utafiti
 
Maendeleo ya Chato ni sehemu ya Tanzania. Kama mikakati ikiwekwa hasa katika sekta ya Utalii na Wiwanda. Ndege zitatua tu hata kama Raisi wa Sasa Hatokuwepo Madarakani.
 
hivi unajua chato kunanini..Chatao kuna mbuga za brigi na rubombo kwa ajili ya utalii... Chato panafunguliwa mgod mkubwa sana wa dhahabu kuliko GGM amabo utakaa miaka 30-40 life span waith high grade gold in Africa and South America. usifate ujinga wakupinga kama wabunge amabo wanalirputa bila kufanya utafiti
Hapa ni hoja,.umeweka hoja inatosha.
 
Tunalinganisha economies of scale zilizopo Chato na sehemu kama Bukoba,Geita kama makoa na hata Mbeya,
Kuna wakati kuna watu walihoji kuwa kwa nini kila siku Dar tu ndio miundo mbinu inajengwa?? Kwa nn kusikengwe kwingine?

Sasa leo hii Chato Kunajengwa Uwanja ili walau kuwe na maendeleo sawa na Bukoba au hata Mwanza. Kwa maana huenda ikawa ndio moja ya booster ya economics development in Chato.
 
HUKO PENGINE KUNA VIWANJA TAYARI SASA SHIDA YA NINI?HATA BARABRA YA RAMI KUTOKA BUKOBA KUJA MWANZA ILIPITA CHATO MILIPIGA KELELESANA AS IF KULE NI WANYAMA.KULE KUNAKAMRADI KA MAJI KAMEANZA MMEPIGA KELELE AS IF WILAYA CHATO HAITAKIWI KUPATA MAJI YA MBOMBA..

Tunalinganisha economies of scale zilizopo Chato na sehemu kama Bukoba,Geita kama makoa na hata Mbeya,
 
mbona unawashwa sana..hivi unajua chato kunanini..Chatao kuna mbuga za brigi na rubombo kwa ajili ya utalii... Chato panafunguliwa mgod mkubwa sana wa dhahabu kuliko GGM amabo utakaa miaka 30-40 life span waith high grade gold in Africa and South America. usifate ujinga wakupinga kama wabunge amabo wanalirputa bila kufanya utafiti
kwa hivyo huko ndio zitatua Boeing kuchukua hayo madini? Kahama na shinyanga kuna migodi na geita pia na ime operate miaka mingi lakin hakukuwa na haja ya kuwa na uwanja wa mkimataifa bali ni viwaja vidogo kwa mahitaji ya eneo hilo,au nyie mnapo ambiwa uwanja wa kimataifa mmnaelewaje? Au mnadhan ni sawa na vibaraza vya kunywea madomola ?

Na hao watalii mmewachukuaje lakin , chato wanaenda kutalii kushangaa digidigi na sungura pori ambao hadi shambani kwangu wamejaa tele!! Kweli zito hakuwa na kosa hasa katika kipengere cha washaamba , na lazima wewe ni msukuma mwingine.

Weken hakiba ya maneno na huko kujipendekeza kwenu bila akili ili mje ,shuhudie huo uwanja utakapo kuwa kwa matumizi ya kuanikia dengu na kukaushia tumbaku.kama ilivyo kwa zile taa za kuongoze punda na waendesh matela ya punda. Hakujawahi tokea maendeleo bila kuwa na mipango chanya , huo uwanja ni hasara kubwa kwa taifa.
 
Hifadhi ya wanyama ya kisiwa cha Rubondo ipo Geita na kisiwa hicho kipo karibia na Chato,Mgodi wa dhahabu wa GGM upo karibia na Chato hapa kuliko mtu kutoka Geita then apite Sengerema kisha avuke maji afike wilaya ya Misungwi kisha aende Usagara kisha Buhongwa kisha Mkolani then Mkuyuni atoboe Pepsi kisha Mwanza Mjini Nara,Makongoro,apite Taqwa High School kisha kona ya bwiru aende Pasiansi kisha saba saba atoboe Ilemela ndio aingie airport Mwanza bora atoke Geita apite Buselesele kisha anaibukia Chato anakwea zake pipa
 
Kiuchumi uwanja wa Mafia ungechukua 70% ya gharama za Chato alafu 30% ikajenga air strip ya kawaida pale Chato matokeo yake yangelikuwa makubwa sana kiuchumi na kijamii kwa maeneo yote. Uwanja wa Mafia ukipata shilingi 30 billion na kuongeza kidogo kwenye miundombinu jirani basi tunaweza kuwapata zaidi ya 60% ya watalii wanaoenda Pemba, Mozambique.
Nadhani tatizo kubwa ni ccm na sote inabidi tukubali hili. Mobutu alikuwa na pesa za kukodisha Concorde lakini hakufanya mahesabu ya miaka 30 mbele, kumbuka pia hakujenga Gborite kwa pesa zake bali pesa za umma na matumizi hayo 'haramu' ndio yanaifanya DRC kuwa kama ilivyo sasa.
 
KAMA MAWAZO NI HAYA NDO MAANA STROGILLERS GORGE HAIKUJENGWA TANGIA ZAMANI KWANI WAZUNGU WALITUAMINISHA KUWA TANZANIA UCHUMI WAKE NI MDOGO SANA KUZALISHA UMEME ULE..GEITA ZAHABU ZOTE ZINATOKA HUKO UKANDA WA GEITA NA CHATO NA NIMEKWAMBIA KUNAMGONDI UTAZIDI WA GGM UTAJENGWA..eia ILITANGAZWA KAMA WIKI TATU KWENYE MAGAZETI..

Kwa wilaya ambayo shuguli kuu y uchumi ni kilimo cha kujikwamua ( subsistence farming) kujenga uwanja wa ndege tena wa kimataifa ni matumizi mabaya ya madaraka

N
 
Naona Kiki ya Lissu imebuma
sasa mnatafuta mtokee wapi tena!!
Washabikiaji bila akili hadi mmesha dumaa kiakili kila kitu ni siasa tuu hata kwa maswala ya msingi nyie mnamuwaza lissu na mbowe na Chadema tuu, hiyo ni psychological problem ingawa hamjijui nda ndiyo inayo athiri hata utendaji wa serikali maana woote mwafanana akili zenu na ndio maana hamuishi vituko.
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom