Uchambuzi: Adhabu kwa wabunge Silaa na Gwajima ni funzo kubwa kwa watanzania

Gwajima amekosea kuropoka kuwa mama Samia kapokea hongo kutoka kwa mabeberu kuingiza chanjo feki nchini ili kuwaua watanzania. Na pia kakosea kusema kwamba mama Samia aliigiza kuchanja kumbe hakuchanja. Wewe kwa uelewa wako haya sio makosa?
Hakuna kosa yule aliyedhani kwamba kilichosemwa sivyo alitakiwa kutoa ushaidi wa kuthibisha hapo nguvu sawa (aliyetuhumu hakutoa 'substantial evidence' ambayo ni 'reliable and credible' halikadhalika aliyetuhumiwa hakuonesha uthibitisho wenye ushahidi kwamba kilichotuhumiwa ni uongo; kwa hiyo kwa dhana hiyo hakuna mwenye mamlaka hapo kumchukulia hatua za aina yoyote mwingine ila labda ubabe wa madaraka na kanuni kandamizi
 
Wewe ni nani hadi useme haya mataputapu mkuu? Mwacheni Gwajima avune alichopanda. Kama wewe ni mmoja misukule wake, nenda kanisani jumapili ijayo ukamlambe miguu tapeli mwenzako.
Obtuse argument with intellectual disability to scale along the tolerable nuisance level.
 
Am not fanatic, nani ka kwambia mimi naamini hayo ya mtandaoni ya commoners...I know deeper than those petty things...Ukiwa na facts acha zijitete usijitete nafsi yako...

Mimi sijakuhukumu unajihukumu mwenyewe kwakua huamini katika unayoyasema...

Commoners wana express a genuine fear, but they have a point even though they cannot come up with facts...

Nimejiteteaje nafsi yangu? Ni kwa vipi siamini katika ninayosema?
 
USA ingekuwa na approach ya kipuuzi kama yao, basi American conservative talk show hosts wote sasa hivi wangekuwa gerezani kwa misinformation and disinformation campaign wanayoiendesha kuhusu chanjo, ambayo imechangia wafuasi wengi sana wa Trump kukataa chanjo na matokeo yake ndio waliofurika ICU kwa COVID-19.
Kwa mantiki hii, wewe huoni kuna umuhimu wa kumdibiti Gwajima asiendelee kuipotosha misukule yake isije ikafurika ICU kwa kuumwa covid-19? Pointi yako ni ipi sasa mkuu?:oops::oops::oops:
 
Nakubaliana na wewe. Kinachonishangaza sijui watanzania elimu yetu ni ya namna gani...mimi ni mfanyakazi mbali ya Basic Salary yangu kuna sitahiki zingine kama house rent allowance nk. vinaunganishwa na mshahara wangu na kukatwa kodi. Kwahiyo Mhe. Jerry Silaa ana hoja ya msingi kwamba zile posho wanazopata wabunge nje ya mshahara wao zijumuishwe na kukatwa kodi kama wafanyakazi wengine wa umma na binafsi. Jiulize, kama mbunge anapewa posho kwa ajili mishahara ya wasaidizi wake je, akishawalipa PAYE yao anaipeleka TRA au inakuwaje?

PAYE, short for Pay-As-Your-Earn, is a Tanzanian withholding tax applied on taxable incomes of applicable employees. Every employer in Tanzania is required, by law, to deduct the tax from an employee's taxable salaries or wages and submit such deductions to the Tanzania Revenue Authority

Ndio maana Basic Salary na sitahiki zote ni mapato kutoka kwa mwajiri wako ni lazima yakatwe kodi. Kinachonisikitisha sheria zipo lakini watanzania wengi hawajui hii PAYE inapatikaje, Pathetic. Hivyo basi kama hizo posho zingine za wabunge hazikatwi kodi basi ni wakati mwafaka kubadili sheria iliyopo na kuanza kukatwa kodi kama wafanyakazi wanavyokatwa posho za mafuta ya gari na posho ya kwa ajili ya pango (rent).
Mkuu umeongea vizuri sana. Wabunge walifanya ujanja wa kuficha mishahara yao kwenye posho ili isikatwe kodi. Ni wakati muafaka sasa posho hizi zihamishiwe kwenye mishahara ili zikatwe kodi. Haya majitu ni ya ajabu sana. Eti yenyewe hayataki yakatwe kodi lakini yanalazimisha tu wanyonge ndio wakatwe. Mapuuzi sana haya majamaa aisee! :oops: :oops: :oops: :oops:
 
Kwa mantiki hii, wewe huoni kuna umuhimu wa kumdibiti Gwajima asiendelee kuipotosha misukule yake isije ikafurika ICU kwa kuumwa covid-19? Pointi yako ni ipi sasa mkuu?:oops::oops::oops:
Kafanye rapid appraisal uone walioko ICU ni kutoka kundi gani la jamii? Kisha rudi kutuambia kwamba anawapotosha...
 
Kwa mantiki hii, wewe huoni kuna umuhimu wa kumdibiti Gwajima asiendelee kuipotosha misukule yake isije ikafurika ICU kwa kuumwa covid-19? Pointi yako ni ipi sasa mkuu?:oops::oops::oops:

Mapepo ya ujinga hayatolewi kwa kutumia Polisi na Mahakama. Kujaribu kufanya hivyo ni ujinga zaidi!
 
Umeongea vizuri juu ya slaa ila kwa gwaji Ndio umeteleza hata yeue yupo ok
Jambo la chanjo hadi sasa hata Mimi naliona Kama Bado Ni dillema tu nadhani hata dunia yote bado haina uhakika na chanjo hizo
Na ukitaka kuthibitisha hili fuatilia habari za chanjo na maambukizi mapya ya covid ulaya hapo ndipo utakapoona gwajima ana reason
Mkuu ibanezafrica , Askofu Gwajima (kama anavyojiita) alikuwa na kesi nyingi za kujibu sio kesi ya upotoshaji wa COVID 19 tu. Alikuwa na kesi nyingine 2 kama ifuatavyo:
1. Kumtuhumu mama Samia kuhongwa na mabeberu kupokea chanjo ili kuwaua watanzania.
2. Kumtuhumu mama Samia na viongozi wengine wa serikali kwa kuigiza kuchomwa chanjo ilhali hawakuchomwa (kwa mujibu wa Gwajima).

Haya makosa mawili ni zaidi ya uhaini. Kama Gwajima angetenda makosa haya akiwa China, angepigwa risasi za kichwa hadharani na kufa papo hapo.
 
I stand with Gwajima!
Japo mi si muumini wake!

Ila Hakuna marefu yasiyokua na ncha!
Slaa ana kosa gani?
Viongozi hawapendi kuambiwa ukweli?
On whay ground bro? Gwajima ni sawa na hadithi za kusadikika tu. Watu wanaweka scientific proof yeye anabaikia ana bwabwaja tu.

Ni sawa leo wale wanapata cerebral malaria wanaibuka na hoja kuwa wamerogwa.

Kuhusu Slaa, bunge letu ni ovu na lisio na weredi.
Ilibidi wajibu hoja, na ikiwezekana Slaa nae azungumze mle bungeni baada ya wabunge kuweka hoja zao.
 
Ujinga sana ,unafikiri ikiwa wewe ni Rais basi uko sawa, viongozi wangapi duniani wanaangamiza wananchi wao,
,for me Gwajima is right
G.boy anaweza kuwa sawa au awe amekosea muhimu hayo ni matokeo ya uchaguzi wa 2020

20210904_182908.jpg
 
G.boy anaweza kuwa sawa au awe amekosea muhimu hayo ni matokeo ya uchaguzi wa 2020

View attachment 1925436
Mkuu napenda nikukumbushe kuwa 2020 hakukuwa na uchaguzi bali uchafuzi na ushetani mkubwa uliofanywa na mwendazake (Mungu anamuona huko aliko). Uchafuzi huu ndio uliotuletea majitu ya ajabu kama Gwajima.
 
Hakuna kosa yule aliyedhani kwamba kilichosemwa sivyo alitakiwa kutoa ushaidi wa kuthibisha hapo nguvu sawa (aliyetuhumu hakutoa 'substantial evidence' ambayo ni 'reliable and credible' halikadhalika aliyetuhumiwa hakuonesha uthibitisho wenye ushahidi kwamba kilichotuhumiwa ni uongo; kwa hiyo kwa dhana hiyo hakuna mwenye mamlaka hapo kumchukulia hatua za aina yoyote mwingine ila labda ubabe wa madaraka na kanuni kandamizi
Sote tunakubaliana kwamba chanjo ni HIYARI. Sasa Gwajima anapowashawishi watanzania (anaowaita waumini wake) wasichanje wewe unaona sawa? Suppose Gwajima angekuwa Mbowe, je kanisa lake si lingekuwa limefungiwa? Lazima angefungiwa na kufunguliwa kesi ya ugaidi kwa kuwa makusudi ya kuanzisha kanisa sio anayoyahubiri. Gwajima anatamba tu kwa sababu ni mmoja wa watu waliomo kwenye chama chetu. Angekuwa hayumo ndani ya chama chetu, angeweza hata kupotezwa na watu wasiojulikana kama Antipas Lissu alivyonusurika kuuawa.
 
Naona orodha ya wahanga inazidi kuongezeka. Safari hii Polepole naye kaingia nyavuni. Tuwaache wafu wakawazike wafu wao bila shuruti.
 
Back
Top Bottom