Happy nation
JF-Expert Member
- Apr 19, 2015
- 679
- 591
Habari nilizopata kutoka kwa rafiki yangu wa karibu, jana Mheshimiwa JPM alisema anafahamu baadhi ya watu wanachakachua vocha za pembejeo ya wakulima masikini na safari hii atahakikisha wale wote wanaohusika na dhuluma hiyo wanachukuliwa hatuwa za kisheria na atahakisha ukaguzi unafanyika kuanzia mahali wanapodai kuzinunua mbegu na hadi vijiji vinavyo pelekwa. Hii imenifurahisha sana kwa sababu uwizi huu wa mabilioni ya fedha za uma umekuwa ni wa kawaida, kuna maeneo mengi mbegu hazipelekwi na ikipelekwa ikipelekwa situka au kilima za sh 2500 kwa kilo badala ya seedco ya sh 6000, sehemu zingine kama katoro na sengerema vocha zime yeyuka.