Nachukua nafasi hii kuishukuru sana jamii Forum kwani mwezi uliopita nilituma thread ya Kuchakachuliwa kwa matokeo ya Usaili ya Uhamiaji. Kutokana na habari hiyo wengi wenye sifa sasa tumeanza kuitwa. Kwa hatua hiyo tunashukuru sana kwani kupitia Jamii forum wengi wa waliopelekwa wamebainika kukosa sifa na sisi kina yakhe sasa tumeitwa. Habari ambazo sio rasmi ni kuwa bwana Kasike aliyewachomeka watu wake baada ya mlungula amekubali ya ishe na kutema baadhi ya mlungula na hadi sasa hali yake kikazi sio nzuri ingawa bado kwa nguvu zote analindwa na kutetewa na dada yake mwanasheria. Asante sana Jamii Forum kwa kazi nzuri sana jamani mbarikiwe hatuna cha kuwalipa.
Mwana Jamii
Mwana Jamii