Uchaguzi wa wanafunzi UD wadorora!

Mwafrika wa Kike

JF-Expert Member
Jul 5, 2007
5,185
56
Kulingana na hii report toka kwa mwanabulogi hakingowi. Uchaguzi wa serikali ya wanafunzi anaotaka Mukandala hatimaye umefanyika bila yule mgombea mwenye umaarufu na ambaye dikiteta mukandala hakutaka kumruhusu agombee na kupelekea machafuko na uonevu wa FFU wiki jana.

Hatimaye Mukandala ameonyesha its true colors kwa kulazimisha kile anachotaka yeye kwenye throats za wanafunzi huku akijinadi kuwa mtetezi na mwendelezaji wa demokrasia Tanzania. No wonder ni mshauri wa Kikwete na serikali ya ccm iliyowapiga wafuasi wa Chadema siku chache kabla ya uchaguzi wa kiteto.


KUTOKUWEPO kwa jina la mgombea urais wa serikali ya wanafunzi (DARUSO) katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Odong’ Odwar raia wa Uganda aliyekuwa akikubalika na wanachuo walio wengi, baada ya jina lake kuondolewa katika kinyang’anyiro hicho kwa madai kuwa hakuwa na sifa ya kuwa chuoni hapo kimesababisha wanafunzi wengi kususia uchaguzi huo.

Pamoja na wanafunzi wengi kususia uchaguzi ila wachache waliojitokeza kupiga kura waliongozwa na wasichana, huku wavulana wengi wakionekana kuvinjari sehemu mbalimbali katika vituo vya kupigia kura chuoni hapo bila kupiga kura.Hata hivyo ilielezwa kuwa sababu kubwa iliyofanya wavinjari katika vituo hivyo ni kuwabainisha wenzao ambao walidhaniwa kuwa wangekaidi na kusaliti msimamo wao.

Mwitikio wa uchaguzi haukuwa mkubwa baada ya wapiga kura wengi kukataa kupiga kura kwa kile walichodai kuwa mgombea waliyekuwa wanamtaka hakuwepo hivyo hawakuwa na sababu ya kupiga kura kumchagua mtu asiye chaguo lao.Hata hivyo kulikuwa na kampeni ya chinichini chuoni hapo iliyolenga kuzua wanafunzi kutopiga kura ingawa baadhi yao walionekana wakivinjari katika vituo vya kupigia kura bila kupiga kura.Habarii hii na Jackson Odoyo na Christopher Maregesi


kwa habari zaidi na picha za matukio click hapa au visit blog ya hakingowi
 
Akitoa maoni yake kuhusu uchaguzi huo, Mwendamseke alisema kwa hali iliyojitokeza, Rais mpya wa Daruso atakuwa na kazi ngumu katika uongozi wake, kwa sababu idadi kubwa ya wabunge ni wale waliokuwa wanamuunga mkono Odwar.


Alisema anatakiwa kuchanga karata zake vizuri, kwani chuo hicho kina wanafunzi zaidi ya 15,000, lakini waliopiga kura ni 730 tu na rais kushinda kwa kura 395..

HII NI AIBU KWA TAIFA, UCHAGUZI GANI WALIOMCHAGUA RAIS NI ASILIMIA 2 na nukta kadhaa tu ya WAPIGA KURA? HAINA TOFAUTI NA ZILE KURA ZA MARUHANI KULE PEMBA. HIZI NI PROTEST VOTES BY ABSCONDENCE. ILA IPENDEZA ZAIDI KAMA WOTE ELFU 15 WANGEKWENDA NA KUPIGA KURA ZA HAPANA! HATA HIVYO UJUMBE UMEFIKA KWA WATAWALA, HAO WAGOMBEA HAWATAKIWI. NA KWANINI HILO BUNGE LISIPIGE TU KURA YA KUTOKUWA NA IMANI YA HUYO RAIS MPYA UCHAGUZI UKARUDIWA TENA? AU KWANINI YASIFANYIKE MAPINDUZI TU?

Asha
 
Akitoa maoni yake kuhusu uchaguzi huo, Mwendamseke alisema kwa hali iliyojitokeza, Rais mpya wa Daruso atakuwa na kazi ngumu katika uongozi wake, kwa sababu idadi kubwa ya wabunge ni wale waliokuwa wanamuunga mkono Odwar.


Alisema anatakiwa kuchanga karata zake vizuri, kwani chuo hicho kina wanafunzi zaidi ya 15,000, lakini waliopiga kura ni 730 tu na rais kushinda kwa kura 395..

HII NI AIBU KWA TAIFA, UCHAGUZI GANI WALIOMCHAGUA RAIS NI ASILIMIA 2 na nukta kadhaa tu ya WAPIGA KURA? HAINA TOFAUTI NA ZILE KURA ZA MARUHANI KULE PEMBA. HIZI NI PROTEST VOTES BY ABSCONDENCE. ILA IPENDEZA ZAIDI KAMA WOTE ELFU 15 WANGEKWENDA NA KUPIGA KURA ZA HAPANA! HATA HIVYO UJUMBE UMEFIKA KWA WATAWALA, HAO WAGOMBEA HAWATAKIWI. NA KWANINI HILO BUNGE LISIPIGE TU KURA YA KUTOKUWA NA IMANI YA HUYO RAIS MPYA UCHAGUZI UKARUDIWA TENA? AU KWANINI YASIFANYIKE MAPINDUZI TU?

Asha

Jamani jamani! Kwa nini mnapenyeza hizi siasa zenu tenganishi na gombanishi kwenye masuala ya wanafunzi? Waacheni wanafunzi waendeshe mambo yao huko shuleni, sasa ninyi wanasiasa kwa nini mnawavuruga? Mnazungumzia bunge sijui kitu gani, bunge la shuleni ni bunge? Hebu acheni utani! Haya mambo ya viranja wa shule mnayaingilia ya nini kama si tu kupenda fujo? Huko hakuna wabunge wala chochote, kuna viranja na wasaidizi wao, basi! Na sifa ya kwanza ya kuwa kiranja shuleni ni lazima kwanza uwe mwanafunzi, ukifeli shule au ukifukuzwa kwa utovu wa nidhamu na ukiranja wako utaisha (hata kama umejibandika fancy titles kama "rais", "waziri", "mbunge" etc, vyote hivi ni delusional).

Binafsi nimeshachoshwa kabisa na hii mijadala ya viranja wa shule hapa JF. Na tena kuna elements za grandiosity zinazoambatana na hii kitu, maana sioni viranja wa vyuo vikuu vingine wakijadiliwa hapa, bado kuna watu wanadhani Tanzania kuna chuo kikuu kimoja tu! Wanafunzi wa chuo kikuu Mlimani mtabakia kujadili mambo ya viranja wenu kutwa kucha hapa, wakati wenzenu wa Tumaini, St Augustine, Dodoma, Morogoro Muslim nk wanapiga kitabu kisawasawa, mwishowe wao watafaulu na kutoka na degree nzuri na kuchukua nafasi muhimu za ajira, ninyi mtabaki na ujinga wa kugombea uchaguzi wa viranja! Upuuzi tu! Na nimefurahi sana kuona taasisi mbalimbali zikiwaajiri bila uaguzi wahitimu wa vyuo vyetu vikuu vingine zaidi ya Mlimani, nimeona mawakili, tutorial assistants (hata Mlimani wapo wa kutoka Tumaini), waalimu, madaktari na wataalamu wengine.

Kalieni migomo tu, mkisusa wenzenu wanakula!
 
Akitoa maoni yake kuhusu uchaguzi huo, Mwendamseke alisema kwa hali iliyojitokeza, Rais mpya wa Daruso atakuwa na kazi ngumu katika uongozi wake, kwa sababu idadi kubwa ya wabunge ni wale waliokuwa wanamuunga mkono Odwar.


Alisema anatakiwa kuchanga karata zake vizuri, kwani chuo hicho kina wanafunzi zaidi ya 15,000, lakini waliopiga kura ni 730 tu na rais kushinda kwa kura 395..

HII NI AIBU KWA TAIFA, UCHAGUZI GANI WALIOMCHAGUA RAIS NI ASILIMIA 2 na nukta kadhaa tu ya WAPIGA KURA? HAINA TOFAUTI NA ZILE KURA ZA MARUHANI KULE PEMBA. HIZI NI PROTEST VOTES BY ABSCONDENCE. ILA IPENDEZA ZAIDI KAMA WOTE ELFU 15 WANGEKWENDA NA KUPIGA KURA ZA HAPANA! HATA HIVYO UJUMBE UMEFIKA KWA WATAWALA, HAO WAGOMBEA HAWATAKIWI. NA KWANINI HILO BUNGE LISIPIGE TU KURA YA KUTOKUWA NA IMANI YA HUYO RAIS MPYA UCHAGUZI UKARUDIWA TENA? AU KWANINI YASIFANYIKE MAPINDUZI TU?

Asha



Naamini wanakusoma hapa hao wana Chuo .Si wajinga naamini hawataenda tena kubeba mabango ya CCM I hope .Ngoma chini wacha tuone .Mukandala Oyeeeee CCM oyeeeeeeeeeeee
 
Jamani jamani! Kwa nini mnapenyeza hizi siasa zenu tenganishi na gombanishi kwenye masuala ya wanafunzi? Waacheni wanafunzi waendeshe mambo yao huko shuleni, sasa ninyi wanasiasa kwa nini mnawavuruga? Mnazungumzia bunge sijui kitu gani, bunge la shuleni ni bunge? Hebu acheni utani! Haya mambo ya viranja wa shule mnayaingilia ya nini kama si tu kupenda fujo? Huko hakuna wabunge wala chochote, kuna viranja na wasaidizi wao, basi! Na sifa ya kwanza ya kuwa kiranja shuleni ni lazima kwanza uwe mwanafunzi, ukifeli shule au ukifukuzwa kwa utovu wa nidhamu na ukiranja wako utaisha (hata kama umejibandika fancy titles kama "rais", "waziri", "mbunge" etc, vyote hivi ni delusional).


Mkuu Kithuku,

demokrasia ya kuchagua viongozi wa chama cha wanafunzi wa vyuo vikuu haifai kuachiwa ikaingiliwa na watu wasioamini uhuru wa boz la kura. Wakiachiwa mlimani watakwenda kwingine na mchezo utakuwa the same.

Binafsi nimeshachoshwa kabisa na hii mijadala ya viranja wa shule hapa JF. Na tena kuna elements za grandiosity zinazoambatana na hii kitu, maana sioni viranja wa vyuo vikuu vingine wakijadiliwa hapa, bado kuna watu wanadhani Tanzania kuna chuo kikuu kimoja tu! Wanafunzi wa chuo kikuu Mlimani mtabakia kujadili mambo ya viranja wenu kutwa kucha hapa, wakati wenzenu wa Tumaini, St Augustine, Dodoma, Morogoro Muslim nk wanapiga kitabu kisawasawa, mwishowe wao watafaulu na kutoka na degree nzuri na kuchukua nafasi muhimu za ajira, ninyi mtabaki na ujinga wa kugombea uchaguzi wa viranja! Upuuzi tu! Na nimefurahi sana kuona taasisi mbalimbali zikiwaajiri bila uaguzi wahitimu wa vyuo vyetu vikuu vingine zaidi ya Mlimani, nimeona mawakili, tutorial assistants (hata Mlimani wapo wa kutoka Tumaini), waalimu, madaktari na wataalamu wengine.

Kalieni migomo tu, mkisusa wenzenu wanakula!

Bado hakuna report kuwa uongozi wa vyuo vingine ulivyotaja hapa umeingilia chaguzi za wanafunzi. Hiyo ikitokea utasikia the same dozier ikitokea hapa kama kawa.

Kwa nini uongozi wa chuo ambao kwa miaka mingi umekuwa unawapa wanafunzi uhuru wa kuchagua viongozi wao leo all of the sudden baada ya Mukandala kuwa VC umeamua kuingilia power ya box la kura na kutaka kuweka mtu wanayempenda wao?
 
Hii nayo kali jamani
Katiba ya Daruso inasemaje kuhusu kura za kumchagua rais??
au hata akishinda kwa kwa asilimia 2 ya wanachuo waliotakiwa kupiga kura anachukua urais??

Haya bwana kweli kazi hipo hapo???

Hata kama watu wawili tu wangempigia kura kati ya wanafunzi maelfu wa UD bado Mukandala angefurahi kuwa anaendeleza demokrasia chuoni na Tanzania kwa ujumla.

Inachekesha kweli na kusikitisha baba
 
Mkuu Kithuku,

demokrasia ya kuchagua viongozi wa chama cha wanafunzi wa vyuo vikuu haifai kuachiwa ikaingiliwa na watu wasioamini uhuru wa boz la kura. Wakiachiwa mlimani watakwenda kwingine na mchezo utakuwa the same.



Bado hakuna report kuwa uongozi wa vyuo vingine ulivyotaja hapa umeingilia chaguzi za wanafunzi. Hiyo ikitokea utasikia the same dozier ikitokea hapa kama kawa.

Kwa nini uongozi wa chuo ambao kwa miaka mingi umekuwa unawapa wanafunzi uhuru wa kuchagua viongozi wao leo all of the sudden baada ya Mukandala kuwa VC umeamua kuingilia power ya box la kura na kutaka kuweka mtu wanayempenda wao?

Uongozi wowote makini wa taasisi ya elimu (shule au chuo) lazima uhakikishe kuwa viranja wanaochaguliwa kuongoza wanafunzi wenzao ni miongoni mwa watu wanaoweza kufanya nao kazi. Kiranja yuko baina ya wanafunzi wenzake na uongozi wa chuo, kwa hiyo viongozi wa chuo ni wadau muhimu, hawawezi kupuuzwa katika suala la upatikanaji wa viranja. Vyuo vyote huwa vinahusisha maofisa wao katika hatua fulanifulani za mchakato wa kupata viranja, na hii pia ni sehemu ya malezi ya hao wanafunzi, hawawezi kuachwa wajipeleke tu wanavyotaka, lazima taratibu na kanuni zizingatiwe, zikiwamo za malezi. Kama menejimenti ya UDSM walikuwa na sababu za kuamini kuwa mtu fulani miongoni mwa wanafunzi hawawezi kufanya naye kazi kama kiranja, hakuna mtu nje ya chuo mwenye mamlaka ya kuwaingilia katika uendeshaji wa chuo, wanafunzi ndio wanaopaswa kujadili na walimu wao na wafikie muafaka, kwani wao(wanafunzi na walimu) ndio wadau. Ninavyoelewa mimi na kwa uzoefu wangu kama mwalimu, mwanafunzi asiyekubalika kwa walimu na utawala wa chuo kamwe hafai kuwa kiranja, na iwapo kwa bahati mbaya amepitishwa kitakachofuatia ni fujo tu, maana badala ya kuendesha mambo kwa faida ya wadau wote wa chuo, atakuwa kila siku na ugomvi na utawala na watakaoumia zaidi ni wanafunzi wenzie, na matokeo yake hata viwango vya elimu vitashuka. Na hakuna mwalimu anayependa kuona kiwango cha ufanisi wake kinashuka sababu tu ya kiranja fulani.

Napenda kukutaarifu kuwa vyuo vyote makini hufuatilia uchaguzi wa wanafunzi kuhakikisha wanapatikana wawakilishi wanaoweza kufanya kazi vizuri na wadau wote chuoni, na ndio maana maofisa wa chuo kama Dean of Students huhusika katika mchakato na hutoa taarifa kwa uongozi wa juu. Sasa chuo kikiwa legelege na kumbeleza demokrasia feki (ambayo mimi naona ni mdebwedo tu), matokeo yake ni kuruhusu watu wenye fujo kuingia katika uongozi wa wanafunzi na kuharibu kabisa dhana nzima ya uwakilishi wa wanafunzi katika masuala ya uendeshaji wa chuo.
 
Uongozi wowote makini wa taasisi ya elimu (shule au chuo) lazima uhakikishe kuwa viranja wanaochaguliwa kuongoza wanafunzi wenzao ni miongoni mwa watu wanaoweza kufanya nao kazi. Kiranja yuko baina ya wanafunzi wenzake na uongozi wa chuo, kwa hiyo viongozi wa chuo ni wadau muhimu, hawawezi kupuuzwa katika suala la upatikanaji wa viranja. Vyuo vyote huwa vinahusisha maofisa wao katika hatua fulanifulani za mchakato wa kupata viranja, na hii pia ni sehemu ya malezi ya hao wanafunzi, hawawezi kuachwa wajipeleke tu wanavyotaka, lazima taratibu na kanuni zizingatiwe, zikiwamo za malezi.

Hadi hapa tuko pamoja

Kama menejimenti ya UDSM walikuwa na sababu za kuamini kuwa mtu fulani miongoni mwa wanafunzi hawawezi kufanya naye kazi kama kiranja, hakuna mtu nje ya chuo mwenye mamlaka ya kuwaingilia katika uendeshaji wa chuo, wanafunzi ndio wanaopaswa kujadili na walimu wao na wafikie muafaka, kwani wao(wanafunzi na walimu) ndio wadau.

So far ni wanafunzi ndio walilalamika kuhusu suala la uongozi wa chuo kuwaingilia katika uchaguzi wao. Hao watu wa nje unaowasema hapa ni kina nani?

Ninavyoelewa mimi na kwa uzoefu wangu kama mwalimu, mwanafunzi asiyekubalika kwa walimu na utawala wa chuo kamwe hafai kuwa kiranja, na iwapo kwa bahati mbaya amepitishwa kitakachofuatia ni fujo tu, maana badala ya kuendesha mambo kwa faida ya wadau wote wa chuo, atakuwa kila siku na ugomvi na utawala na watakaoumia zaidi ni wanafunzi wenzie, na matokeo yake hata viwango vya elimu vitashuka. Na hakuna mwalimu anayependa kuona kiwango cha ufanisi wake kinashuka sababu tu ya kiranja fulani.

NI vigezo gani unavyotumia kusema kuwa mwanafunzi hakubaliki na uongozi wa chuo?

Napenda kukutaarifu kuwa vyuo vyote makini hufuatilia uchaguzi wa wanafunzi kuhakikisha wanapatikana wawakilishi wanaoweza kufanya kazi vizuri na wadau wote chuoni, na ndio maana maofisa wa chuo kama Dean of Students huhusika katika mchakato na hutoa taarifa kwa uongozi wa juu. Sasa chuo kikiwa legelege na kumbeleza demokrasia feki (ambayo mimi naona ni mdebwedo tu), matokeo yake ni kuruhusu watu wenye fujo kuingia katika uongozi wa wanafunzi na kuharibu kabisa dhana nzima ya uwakilishi wa wanafunzi katika masuala ya uendeshaji wa chuo.

Strong word hapa ni kufuatilia (na kusimamia ikibidi) na sio kuingilia na kuamua nani agombee na nani asigombee. Huo ni udikiteta!

Next.....
 
Uongozi wowote makini wa taasisi ya elimu (shule au chuo) lazima uhakikishe kuwa viranja wanaochaguliwa kuongoza wanafunzi wenzao ni miongoni mwa watu wanaoweza kufanya nao kazi. Kiranja yuko baina ya wanafunzi wenzake na uongozi wa chuo, kwa hiyo viongozi wa chuo ni wadau muhimu, hawawezi kupuuzwa katika suala la upatikanaji wa viranja. Vyuo vyote huwa vinahusisha maofisa wao katika hatua fulanifulani za mchakato wa kupata viranja, na hii pia ni sehemu ya malezi ya hao wanafunzi, hawawezi kuachwa wajipeleke tu wanavyotaka, lazima taratibu na kanuni zizingatiwe, zikiwamo za malezi. Kama menejimenti ya UDSM walikuwa na sababu za kuamini kuwa mtu fulani miongoni mwa wanafunzi hawawezi kufanya naye kazi kama kiranja, hakuna mtu nje ya chuo mwenye mamlaka ya kuwaingilia katika uendeshaji wa chuo, wanafunzi ndio wanaopaswa kujadili na walimu wao na wafikie muafaka, kwani wao(wanafunzi na walimu) ndio wadau. Ninavyoelewa mimi na kwa uzoefu wangu kama mwalimu, mwanafunzi asiyekubalika kwa walimu na utawala wa chuo kamwe hafai kuwa kiranja, na iwapo kwa bahati mbaya amepitishwa kitakachofuatia ni fujo tu, maana badala ya kuendesha mambo kwa faida ya wadau wote wa chuo, atakuwa kila siku na ugomvi na utawala na watakaoumia zaidi ni wanafunzi wenzie, na matokeo yake hata viwango vya elimu vitashuka. Na hakuna mwalimu anayependa kuona kiwango cha ufanisi wake kinashuka sababu tu ya kiranja fulani.

Napenda kukutaarifu kuwa vyuo vyote makini hufuatilia uchaguzi wa wanafunzi kuhakikisha wanapatikana wawakilishi wanaoweza kufanya kazi vizuri na wadau wote chuoni, na ndio maana maofisa wa chuo kama Dean of Students huhusika katika mchakato na hutoa taarifa kwa uongozi wa juu. Sasa chuo kikiwa legelege na kumbeleza demokrasia feki (ambayo mimi naona ni mdebwedo tu), matokeo yake ni kuruhusu watu wenye fujo kuingia katika uongozi wa wanafunzi na kuharibu kabisa dhana nzima ya uwakilishi wa wanafunzi katika masuala ya uendeshaji wa chuo.

Kithuku kama nimekuelewa ina maana wewe unakubaliana na yale ambayo yametokea UDSM kwa kuwaondoka na kuweka wale wanao watakiwa na uongozi wa Chuo .Je na wale wanao ongozwa na hao viranja ama Kiranja itakuwaje kama kiranja hawampendi ila anapendwa na uongozi wa Chuo? By the way nani kapita kuwa Rais hapo UDSM ?
 
Nasema hivi, na naomba nieleweke vizuri. Anapoteuliwa mtu kuwa mkuu wa taasisi ya kielimu, anakabidhiwa dira, mwelekeo na malengo ya taasisi hiyo na anawajibika kwa aliyemteua kuhusu utekelezaji. Mimi nikipewa nafasi kama hiyo, siwezi kuruhusu kamwe mazingira yoyote yatakayonisababisha nishindwe kutimiza wajibu wangu ipasavyo. Miongoni mwa mazingira kama hayo, ni viongozi wa wanafunzi wenye hulka ya kupenda migogoro, ambayo inaweza kwa hakika kuwaharibia kazi viongozi wa chuo na waalimu. Kwa hiyo uongozi wa chuo una wajibu wa kuwashauri wanafuzi na kuwasaidia kimalezi ili wachague viongozi wanaokubalika na wanaoweza kufanya kazi na utawala wa chuo. Jitihada za kushauri zikishindikana (mfano kutokana na kiburi cha wanaoshauriwa), basi ni wajibu wa uongozi wa chuo kuweka msimamo wazi kuwa mtu fulani hatumtaki, na kama hilo mnaita kuingilia basi sioni ubaya wa kuingilia huko. Siwezi kumkubali mtu wa kuja kuniharibia kazi, eti nabembeleza demokrasia, huo ni upuuzi! Demokrasia ya wanafunzi chuoni ina mipaka, na mipaka yake inaishia kwenye misingi, kanuni, viwango na taratibu ambazo utawala wa chuo ndio unaosimamia. Pale ambapo nina mamlaka (mfano kama ni sehemu ya utawala wa chuo), sitamkaribisha kwenye uongozi mtu wa kuja kuniharibia kazi, huyo hatapata uongozi hata akifanya nini, maana mambo yakiharibika chuoni hawaulizwi viranja wa wanafunzi (hawa ni wa kupita tu, kila mwaka wanachaguliwa wapya), watakaoulizwa ni utawala wa chuo. Kwa hiyo utawala una haki na wajibu wa kulinda viwango vya taaluma, nidhamu, na kusimamia misingi na dira ya chuo. Mwanafunzi asiyefaa uongozi kwa maoni ya utawala wa chuo (ambao wameaminiwa na taifa kama walezi wa wanafunzi hao) kamwe asiruhusiwe kuwa kiongozi chuoni, anaweza kwenda kuwa kiongozi mahali pengine huko atakapoondoka chuoni, anaweza kwenda kuwa diwani huko au chochote atakachoweza huko kwingine ambako uongozi wa chuo hauhusiki, lakini ndani ya chuo ni lazima mamlaka ya chuo iheshimiwe. Huo ndio msimamo wangu.
 
HII NI AIBU KWA TAIFA, UCHAGUZI GANI WALIOMCHAGUA RAIS NI ASILIMIA 2 na nukta kadhaa tu ya WAPIGA KURA? HAINA TOFAUTI NA ZILE KURA ZA MARUHANI KULE PEMBA. HIZI NI PROTEST VOTES BY ABSCONDENCE. ILA IPENDEZA ZAIDI KAMA WOTE ELFU 15 WANGEKWENDA NA KUPIGA KURA ZA HAPANA! HATA HIVYO UJUMBE UMEFIKA KWA WATAWALA, HAO WAGOMBEA HAWATAKIWI. NA KWANINI HILO BUNGE LISIPIGE TU KURA YA KUTOKUWA NA IMANI YA HUYO RAIS MPYA UCHAGUZI UKARUDIWA TENA? AU KWANINI YASIFANYIKE MAPINDUZI TU?

Asha

dada Asha.. ni 0.26%
 
dada Asha.. ni 0.26%

Heeeeeeeh. Afanaleki! Hilo ndio somo la DEMOKRASIA watoto wetu wanalojifunza CHUO KIKUU chini ya Mkuu wa Chuo ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi ya UTAFITI WA DEMOKRASIA(REDET)?

Ama kweli, tatizo sio Bodi ya Mikopo ila ni Serikali ya KISHKAJI ya JK

Asha
 
Nasema hivi, na naomba nieleweke vizuri. Anapoteuliwa mtu kuwa mkuu wa taasisi ya kielimu, anakabidhiwa dira, mwelekeo na malengo ya taasisi hiyo na anawajibika kwa aliyemteua kuhusu utekelezaji. Mimi nikipewa nafasi kama hiyo, siwezi kuruhusu kamwe mazingira yoyote yatakayonisababisha nishindwe kutimiza wajibu wangu ipasavyo. Miongoni mwa mazingira kama hayo, ni viongozi wa wanafunzi wenye hulka ya kupenda migogoro, ambayo inaweza kwa hakika kuwaharibia kazi viongozi wa chuo na waalimu. Kwa hiyo uongozi wa chuo una wajibu wa kuwashauri wanafuzi na kuwasaidia kimalezi ili wachague viongozi wanaokubalika na wanaoweza kufanya kazi na utawala wa chuo. Jitihada za kushauri zikishindikana (mfano kutokana na kiburi cha wanaoshauriwa), basi ni wajibu wa uongozi wa chuo kuweka msimamo wazi kuwa mtu fulani hatumtaki, na kama hilo mnaita kuingilia basi sioni ubaya wa kuingilia huko. Siwezi kumkubali mtu wa kuja kuniharibia kazi, eti nabembeleza demokrasia, huo ni upuuzi! Demokrasia ya wanafunzi chuoni ina mipaka, na mipaka yake inaishia kwenye misingi, kanuni, viwango na taratibu ambazo utawala wa chuo ndio unaosimamia. Pale ambapo nina mamlaka (mfano kama ni sehemu ya utawala wa chuo), sitamkaribisha kwenye uongozi mtu wa kuja kuniharibia kazi, huyo hatapata uongozi hata akifanya nini, maana mambo yakiharibika chuoni hawaulizwi viranja wa wanafunzi (hawa ni wa kupita tu, kila mwaka wanachaguliwa wapya), watakaoulizwa ni utawala wa chuo. Kwa hiyo utawala una haki na wajibu wa kulinda viwango vya taaluma, nidhamu, na kusimamia misingi na dira ya chuo. Mwanafunzi asiyefaa uongozi kwa maoni ya utawala wa chuo (ambao wameaminiwa na taifa kama walezi wa wanafunzi hao) kamwe asiruhusiwe kuwa kiongozi chuoni, anaweza kwenda kuwa kiongozi mahali pengine huko atakapoondoka chuoni, anaweza kwenda kuwa diwani huko au chochote atakachoweza huko kwingine ambako uongozi wa chuo hauhusiki, lakini ndani ya chuo ni lazima mamlaka ya chuo iheshimiwe. Huo ndio msimamo wangu.

Mkuu, mbona unanitisha? Unafananisha shule ya msingi na Chuo Kikuu? Hao unaowazungumzia sio viranja kama unavyowaita bali ni watu wazima wanaotakiwa kuendesha serikali (ndio, serikali na sio kamati ya viranja)yao. Kumbuka tunapozungumzia wanafunzi wa chuo kikuu ni kuanzia wale wa digrii ya kwanza hadi hao wanaochua masomo ya Ph.D. Hawa si watoto wadogo bali ni watu wenye busara zao.Nchi zote duniani, serikali za wanafunzi zinapewa heshima kubwa na utawala (nadhani jina sahihi ni uongozi) maana inatambulika kuwa wao ni watu wazima na wana haki sawa na hao wakufunzi.

Heshima unayoitaka wewe ni ya mabavu ambayo tumeizoea kwenye jamii yetu (kuanzia kwenye familia hadi serikalini). Kwa taarifa yako katika demokrasia na utawala makini, heshima inakuwa 'earned' na hata siku moja hailazimishwi (heshima si kuamkiwa shikamoo tu kama tunavyodhani). Kwa bahati mbaya msimamo kama wa kwako wa kujiona vimungu mtu kwa sababu tu ni mkubwa na chochote unachosema ni sahihi ndiyo uliotufikisha hapa si chuoni tu bali katika jamii nzima.Chuo Kikuu si mali ya utawala bali ni mali ya jumuia nzima.Dhamana haiko kwa uongozi pekee yao bali wote wanaohusika hapo chuoni, wanafunzi na waajiriwa wengine.

Unapokuwa na uongozi wa wanafunzi unaokubalika nao unafanya kazi ya kuongoza chuo kuwa rahisi zaidi maana maamuzi yakifanywa kwa kuwashirikisha yatakubalika na wanafunzi. Migogoro na migomo inatokana na utawala wa kimabavu usiotaka kuulizwa wala kuwashirikisha wanafunzi katika maamuzi kwa maana wao ndio wanaowajibika! Uongozi kama huo umepitwa na wakati kama vile kuvaa suruali vipande vyuoni na kuchapana viboko! Utawala hauna nafasi katika Chuo Kikuu bali ni uongozi makini unaotakiwa. Chuo Kikuu ni sehemu ambapo tunawajenga wale ambao tunategemea kuja kuwa viongozi hapo baadae. Tunataka viongozi wenye udadisi na wasio na uoga wa kupinga maovu pale yanapotokea bila kujali nani ameyafanya. Tunataka viongozi ambao wako tayri kukabiliana na uovu kwa kila namna bila kuogopa. hatutaki viranja ambao kazi yao ni kubeba mikoba ya waliowaweka.

Huwezi kupinga demokrasi kamili katika Chuo kikuu halafu ukajidai ni mtetezi wa demokrasia kwenye jamii.

Amandla!
 
Fundi Mchundo,

Bado hujafanikiwa kunishawishi kubadili msimamo wangu. Dhamana ya uongozi wa chuo hukabidhiwa kwa viongozi wa chuo na si kwa viongozi wa wanafunzi. Wanafunzi wako pale kufundishwa na kulelewa kwa mujibu wa kanuni na mitaala iliyowekwa, na wala hawana madaraka yoyote katika mambo hayo, wanayakuta chuoni na ni lazima wayafuate kama yalivyo. Kama kungekuwa na hiyo demokrasia ya wanafunzi unayodai basi wangechagua hata mkuu wa chuo na kushiriki kupanga mitaala chuoni, lakini sivyo!

Hakuna serikali ya wanafunzi kama unavyodai, hata katika vyuo vikuu vya huku nje. Hiyo dhana ya kuwa na "serikali" ni mojawapo ya grandiosities za wanafunzi wa Mlimani! Ile ya Mlimani ni "Students' Organization" (sasa kama kwako na kwa wanafunzi wa Mlimani "organization" ni "serikali", hilo ni tatizo lingine!). Hiyo DARUSO haikuandikishwa kisheria kama "serikali", imeandikishwa kama umoja wa wanafunzi kwa mujibu wa sheria ya iliyoanzisha Chuo Kikuu cha Dar es salaam, na wala haina madaraka wala mamlaka ya "kiserikali". Hapa UK taasisi kama hiyo ya wanafunzi huitwa "Students' Union". Umoja wa wanafunzi wala siyo chama, maana hakuna hiari katika kujiunga, kwani ukishakuwa mwanafunzi basi automatically ni member. Hiyo DARUSO huko Dar kwa mfano, hakuna mwanafunzi mwenye hiari ya kujitoa, na kulipa ada ni lazima (actually ni sehemu ya zile fees ambazo lazima mwanafunzi alipe kabla ya kudahiliwa). Sasa huu uanachama wa lazima wewe unaita demokrasia?

Ni kweli kuwa wanafunzi wapo wa viwango mbalimbali kuanzia shahada ya kwanza hadi PhD, lakini practically na kwa uzoefu, hao wafanya fujo hapo Mlimani ni wanafunzi wa shahada za kwanza ambao bado wana hang over za sekondari, na wanapaswa kulelewa kwa kanuni madhubuti (strictness) hadi hangover hiyo iwatoke. Sijawahi kuona mwanafunzi yeyote wa shahada ya uzamili au uzamivu kwenye hizi fujo za DARUSO. Kimsingi wanafunzi wa shahada za uzamili wana matatizo makubwa pengine kuliko hao wa shahada za kwanza (kukosa fedha za utafiti, mambo ya kazini kwao, wengine wana familia tayari zinawategemea, wakati mwingine mikwaruzano na supervisors, ukata, mishahara midogo isiyokidhi mahitaji ilhali akiwapo masomoni hana tena ule muda wa kujitafutia fedha za ziada, nk), lakini huwa wanayatatua kwa busara bila kufanya fujo. Kwa maana hiyo, "serikali" unayodai ya wanafunzi (ambayo kwangu ni feki) haihusishi wanafunzi wa shahada za uzamili na uzamivu, na wala si washirika wao ima katika matamko yao wala katika fujo zao.

Narudia msimamo wangu, hakuna "serikali" ya wanafunzi, kuna mkusanyiko (organization au union) wa kurahisisha mawasiliano na utatuzi wa matatizo ya wanafunzi ambazo ni kazi za kawaida za viranja shuleni. Hizo fancy titles za "rais", "waziri mkuu" nk zilikuwa zinatumika hata kule Weruweru sekondari, na hazikuwafanya wawe tofauti na viranja wengine. Wanafunzi, ikiwa ni pamoja na viongozi wao ni lazima, narudia, ni LAZIMA watii,kufuata na kuheshimu sheria, kanuni na taratibu za chuo wanachosoma maana ndizo zinazowapa hiyo status ya uanafunzi, na kamwe "demokrasia" yao haiwezi kupindukia mipaka na kutaka kuizidi mamlaka ya chuo. Nimemaliza.
 
Kithuku mbona hao akina Mukandala wasikate kwa maelezo ya wazi kama yako kwamba hawawataki wale viongozi wengine bali wanawataka ama wanamtaka huyu aliyechaguliwa basi badala ya kuwapiga na kuanza kuuliza uhalali wao wa kuwepo Chuoni hapo ?Mbinu hizi nawe ungaliweza kuzitumia ili kumridhisha bwana wako ambaye amekupa madaraka usionekane kushindwa ?
 
Bado, Mkuu, nami haujani'convince' kuwa kwa sababu wao ni wanafunzi wenye grandiose titles basi menejimenti ya chuo ndiyo wenye mamlaka ya kuwachagulia viongozi! Kwa msimamo wako, basi hawa vijana wageuzwe idara ya Chuo ili uongozi waweze kufanya wanachotaka. Hakuna mahali ambapo uongozi unaingilia mambo ya wanafunzi, period, isipokuwa pengine China na Zimbabwe! Ni hiki kiburi kwa wale wanaoongoza cha kutokuwasikiliza wanafunzi ati kwa sababu wao ndio waliopewa dhamana ya kuongoza ndiko kunakopelekea migomo na malumbano yote kuanzia kwenye Vyuo Vikuu (hata hicho cha Tumaini pamewahi kutokea malumbano) hadi shule za msingi. Ni lazima wale wanaopewa dhamana ya kuongoza wajifunze kuwaheshimu wanaowaongoza. Vitisho na ubabe havina nafasi katika jamii ya leo. Kuwaita viranja ni kuwatukana.

Hizo students unions unazozizungumzia ni kwenye mifumo iliyokuwa na vyuo vikuu kwa miaka mingi na zimeweza kufikia mahali pa kuweza kujiendesha bila kutegemea ada kutoka kwa wanafunzi. Student union hizo zinamiliki mabweni, clubs na kadhalika na hauwezi kuzilinganisha hata siku moja na DARUSO.

Unachodai wewe si kuheshimu sheria, bali ni kuwanyenyekea viongozi. Masuala ya uchaguzi, kukosekana kwa maji, n.k. vinaingiaje kwenye huko kutii sheria?
 

Kithuku,
Na ukifuatilia historiaya hizo Students Union utakuta na wao walianza kama wanavyofanya wenzao hapo UDSM. Wanafunzi katika vyuo vikuu hawajawahi hata siku moja kukubali kuwa mouth piece wa uongozi. Wanafunzi wameuawa Marekani hadi ufaransa katika mapigano dhidi ya hao waliojiona wana dhamana ya kuongoza vyuo vikuu.Mtizamo kama wa kwako nina wasiwasi unaweza kutufikisha pabaya.

Amandla.
 
Kithuku mbona hao akina Mukandala wasikate kwa maelezo ya wazi kama yako kwamba hawawataki wale viongozi wengine bali wanawataka ama wanamtaka huyu aliyechaguliwa basi badala ya kuwapiga na kuanza kuuliza uhalali wao wa kuwepo Chuoni hapo ?Mbinu hizi nawe ungaliweza kuzitumia ili kumridhisha bwana wako ambaye amekupa madaraka usionekane kushindwa ?

Kama Mukandara alitumia mbinu chafu kuwakataa viongozi fulani, tujadili hilo na kumshutumu kama inapasa. Kikubwa nafurahi kuwa umeona uhalali wa uongozi wa chuo kukataa aina fulani ya viongozi wa wanafunzi, cha kujadili ni njia bora za kuwakataa hao viongozi badala ya mbinu chafu za kuwasingizia mambo mabaya. Lakini tuna ushahidi wowote kuwa huyo mwanafunzi aliyeuliziwa uhalali wa kuwa chuoni hakuwa na kasoro hizo? Mkuu Lunyungu ni kwamba unapoamua kugombea uongozi hata kama ni wa serikali ya mtaa, unawapa nafasi wadau kukujua kuliko walivyokuwa wanakujua kabla. Inawezekana ni kweli huyo mwanafunzi alikuwa na matatizo hayo lakini hayakujulikana kabla (kutokana na udhaifu wa chuo ambao pia bado unapaswa kukemewa sana), lakini kitendo cha kugombea urais kilitoa mwanya kwa hayo masuala kugundulika! Mie sijui, lakini inawezekana ndivyo. Na kama sivyo, bado anayo nafasi ya kufuata mkondo wa sheria na kurudishiwa haki yake.

Nikupe mfano mwingine, unamkumbuka Kihiyo yule aliyewahi kuwa mbunge wa Temake? Alikuwa amefanikiwa kufoji cheti kuwa ana shahada ya uhandisi (B.Eng), na alikula kiulaini kwa miaka mingi kwa kutumia cheti hicho bila kustukiwa, lakini mambo yalikuja kubumburuka alipogombea na kushinda ubunge Temeke 1995. Ilikuja kugundulika kuwa hata cheti cha FTC cha Dar Tech alichodai anacho alighushi kwani hakuwahi kusoma chuoni hapo, achilia mbali B.Eng aliyofoji kuwa kaipatia Ujerumani! Hadi leo neno "kihiyo" limegeuka kuwa msamiati kumaanisha wanaoghushi vyeti vya shule. Haya yote yaliweza kujulikana kutokana na kujiweka kwenye mazingira yaliyosababisha afuatiliwe. Inawezekana huyo mwanafunzi wa UDSM aliingia katika mtego kama huo.
 
Bado, Mkuu, nami haujani'convince' kuwa kwa sababu wao ni wanafunzi wenye grandiose titles basi menejimenti ya chuo ndiyo wenye mamlaka ya kuwachagulia viongozi! Kwa msimamo wako, basi hawa vijana wageuzwe idara ya Chuo ili uongozi waweze kufanya wanachotaka. Hakuna mahali ambapo uongozi unaingilia mambo ya wanafunzi, period, isipokuwa pengine China na Zimbabwe! Ni hiki kiburi kwa wale wanaoongoza cha kutokuwasikiliza wanafunzi ati kwa sababu wao ndio waliopewa dhamana ya kuongoza ndiko kunakopelekea migomo na malumbano yote kuanzia kwenye Vyuo Vikuu (hata hicho cha Tumaini pamewahi kutokea malumbano) hadi shule za msingi. Ni lazima wale wanaopewa dhamana ya kuongoza wajifunze kuwaheshimu wanaowaongoza. Vitisho na ubabe havina nafasi katika jamii ya leo. Kuwaita viranja ni kuwatukana.

Hizo students unions unazozizungumzia ni kwenye mifumo iliyokuwa na vyuo vikuu kwa miaka mingi na zimeweza kufikia mahali pa kuweza kujiendesha bila kutegemea ada kutoka kwa wanafunzi. Student union hizo zinamiliki mabweni, clubs na kadhalika na hauwezi kuzilinganisha hata siku moja na DARUSO.

Unachodai wewe si kuheshimu sheria, bali ni kuwanyenyekea viongozi. Masuala ya uchaguzi, kukosekana kwa maji, n.k. vinaingiaje kwenye huko kutii sheria?

Fundi Mchundo,

Tatizo ninaloliona kwako na kwa wengine wanaochangia mjadala huu ni kwamba wanaangalia upande wa wanafunzi tu, wanasahau pia kuna waalimu na menejimenti ambao wana haki pia. Huwezi kumpa mmoja uhuru na haki pasipo na mipaka kwa gharama ya uhuru na haki za wengine. Wakati wanafunzi wanadai hayo wanayoyadai na ni haki yao, walimu na menejimenti pia wanayo haki na wajibu wa kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa ajira zao na kujiweka kwenye mazingira bora ya ufanisi kama taasisi na kama watu binafsi pia. Sasa haya hayawezi kupatikana kwa kuruhusu wanafunzi wajifanyie watakayo, wafanye vurugu na fujo bila kudhibitiwa, ati kisa demokrasia, demokrasia gani?
 
Kithuku: usije ukaingia kwenye kundi la kutetea yasiyoteteeka. Piga ua mkuu, utaandika mengi sana, lakini hakuna utakayemshawishi akubaliane na wewe kwamba uongozi wa chuo una haki ya kuweka vigezo vya kiongozi wa wanafunzi wanavyovitaka wao. Halafu umefanya utumbo wangu utetemeka kabisa unaposema eti uongozi wa chuo hauwezi kukubali achaguliwe kiongozi anayependa migomo-how do they know kwamba huyu anapenda migomo na huyu hapendi? And more importantly, nani amesema kwamba kuna mwanafunzi anapenda migomo? Migomo inajulikana, popote pale sio chuoni tu, kuwa ni njia ya dharura ya kuwakilisha madai fulani. Sasa nani anakwambia unaweza kupanga dharura?

Kama viongozi wa chuo wangekubaliana na mawazo yako haya, siamini kwamba kuna kiongozi wa chuo pale mlimani anaweza kufikiri kama ulivyosema hapa, basi ingebidi waifute DARUSO na wa-adopt system inayotumika primary school kuchagua hao viongozi wa wanafunzi.

In fact watu wenye mawazo yako haya ndio wanaochochea migomo chuoni maana mawazo haya yanasababisha vijana wetu wawachukie viongozi wa chuo pasipo sababu za msingi. Mawazo ya namna yamejengwa kwenye minanjili ya ubabe na woga na hayawezi kumaliza migomo hata siku moja.

Sasa hivi kweli wewe unaamini kwa chuo kuruhusu kiongozi wa wanafunzi achaguliwe na wanafunzi chini ya 1% kwamba kimefanikiwa kuzima migomo pale mlimani?

In short, I am puzzled and dumbfounded by your views about the ongoing crisis at UDSM. I can't believe it is you who is writing this!
 
Back
Top Bottom