Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,500
- 9,279
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza uchaguzi mdogo wa Jimbo la Ngorongoro mkoani Arusha utakaofanyika Desemba 11 mwaka huu.
Siku hiyo pia utafanyika uchaguzi mdogo wa diwani wa kata ya Naumbu, Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, mkoani Mtwara.
Hatua hiyo imetokana na Tume kupokea barua ya Spika wa Bunge akiitaarifa kuwepo kwa nafasi wazi ya ubunge katika Jimbo la Ngorongoro halmashauri ya Wilayanya Ngorongoro mkoani Arusha.
Pia imepokea barua kutoka kwa Waziri mwenye dhamana ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, ikitaarifu Tume juu ya uwepo wa nafasi wazi ya diwani.
Nafasi wazi ya ubunge imetokana na kufariki kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro, William Ole Nasha kupitia Chama Cha Mapinduzi(CCM) aliyefariki Septemba 27 mwaka huu.
Siku hiyo pia utafanyika uchaguzi mdogo wa diwani wa kata ya Naumbu, Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, mkoani Mtwara.
Hatua hiyo imetokana na Tume kupokea barua ya Spika wa Bunge akiitaarifa kuwepo kwa nafasi wazi ya ubunge katika Jimbo la Ngorongoro halmashauri ya Wilayanya Ngorongoro mkoani Arusha.
Pia imepokea barua kutoka kwa Waziri mwenye dhamana ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, ikitaarifu Tume juu ya uwepo wa nafasi wazi ya diwani.
Nafasi wazi ya ubunge imetokana na kufariki kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro, William Ole Nasha kupitia Chama Cha Mapinduzi(CCM) aliyefariki Septemba 27 mwaka huu.