Uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 nini tutarajie?

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,556
29,640
Kuanzia mwezi Septemba 2019 hekahela za kinyang'anyiro cha uchaguzi wa serikali za mitaa nchi nzima zitakuwa katika peak.

Uchaguzi huu unatarajia kutupatia wenyeviti wa mitaa, vijiji na vitongoji pamoja na Halmashauri za mitaa kwa kipindi kingine cha miaka mitano hadi 2014. Kwa hali inavyoendelea sasa inaonyesha wanaharakati wamejipanga vilivyo kuibana serikali kuhusiana na utaratibu mzima wa chaguzi za serikali za Mitaa, vijiiji na Vitongoji nchi nzima. Hukumu ya hivi karibuni kuhusiana na usimamizi wa chaguzi zetu imeelekeza kutowatambua wakurugenzi wa Manispaa na Watendaji wa Serikali ambao siyo waajiriwa wa Tume ya Uchaguzi kusimamia chaguzi hizi. nimepata maswali mawili hapa ambayo natamani wenye ufahamu wa taratibu za chaguzi ama waliopo jikoni (NEC) kunipatia uelewa.

1. Je Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji unasimamiwa na sheria ya Tume Huru ya Uchaguzi au upo chini ya TAMISEMI?

2. Kama jibu la swali la kwanza ni kuwa NEC husimamia chaguzi hizi, utaratibu wa usimamizi wa Chaguzi za mwaka huu upoje? Namaanisha kuwa, Wakurugenzi wa wilaya na watendaji hawatahusika na usimamizi?

Ahsante
 
Yaani hili swali lako ni jepesi kama yale maswali ya kwanza kwanza kwenye exam papers.
Hivi wewe Sheria ya Tume Huru imetungwa lini..??
Alafu mbona mnaangaika na hizi "chaguzi" wakati mara nyingi "washindi hewa/bure kabisa" wanateuliwaga na kutangazwa holela holela..??

Nasubiria siku ambayo wananchi watakuwa wametambua nguvu ya wingi wao.. Nguvu ya maamuzi yao... Ya kwamba wakinyanyuka kama wananchi kwa ujumla na umoja wo wanaweza kupinga haya matukio ya kisanii sanii yafanyikayo nchini kwa sasa..!!
Sijuhi ni lini tu.. Lakini ipo siku yaja... Na haipo mbali.. Siku ambayo wananchi watakuwa na uwezo wa hali ya juu kabisa katika kuchagua na kuwawajibisha viongozi wao.

Hadi siku hiyo; haya mengine ni sawa na episodes za bongo muvie..!
 
Kuanzia mwezi Septemba 2019 hekahela za kinyang'anyiro cha uchaguzi wa serikali za mitaa nchi nzima zitakuwa katika peak.

Uchaguzi huu unatarajia kutupatia wenyeviti wa mitaa, vijiji na vitongoji pamoja na Halmashauri za mitaa kwa kipindi kingine cha miaka mitano hadi 2014. Kwa hali inavyoendelea sasa inaonyesha wanaharakati wamejipanga vilivyo kuibana serikali kuhusiana na utaratibu mzima wa chaguzi za serikali za Mitaa, vijiiji na Vitongoji nchi nzima. Hukumu ya hivi karibuni kuhusiana na usimamizi wa chaguzi zetu imeelekeza kutowatambua wakurugenzi wa Manispaa na Watendaji wa Serikali ambao siyo waajiriwa wa Tume ya Uchaguzi kusimamia chaguzi hizi. nimepata maswali mawili hapa ambayo natamani wenye ufahamu wa taratibu za chaguzi ama waliopo jikoni (NEC) kunipatia uelewa.

1. Je Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji unasimamiwa na sheria ya Tume Huru ya Uchaguzi au upo chini ya TAMISEMI?

2. Kama jibu la swali la kwanza ni kuwa NEC husimamia chaguzi hizi, utaratibu wa usimamizi wa Chaguzi za mwaka huu upoje? Namaanisha kuwa, Wakurugenzi wa wilaya na watendaji hawatahusika na usimamizi?

Ahsante
Je tuna tume huru ya uchaguzi
 
Hahaha tutarajie wagombea wa ccm kupita bila kupingwa.
Vyombo vya dola vyao, tume ya uchaguzi yao nchi yao, hakuna kulialia.
 
Back
Top Bottom