only83
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 5,343
- 2,525
Katika kile kinachoonekana ni mpango wa maandalizi kwa ajili ya uchaguzi wa NEC ya CCM mwakani na uchaguzi wa Raisi na wabunge 2015 kuna maandalizi makubwa na yakutisha yameanza kuonekana….Juzi nilikuwa mkoa mmoja wa kaskazini na kufanikiwa kukutana na ndugu wa karibu kabisa na Edward Ngoyai Lowasa,nilijaribu kumdadisi kuhusu michakato wa EL kugombea uraisi mwaka 2015…Bila kuficha akaniambia bado jamaa ana hayo mawazo tena kwa asilimia 95…Na akaendelea kuniambia kuwa kwasasa EL ana michakato ya kutia mkono wake katika uchaguzi wa NEC-CCM mwakani…Hili kufanikisha hili,wiki hii EL halikuwa Ujerumani,ambapo inasemekana mipango inasukiwa huko ili kukwepa watu wanaoweza kuingilia mpango huu kama ungefanyika hapa nchini..Jamaa huyu wa karibu na EL aliniambia kuwa kuna mpango madhubuti wa kuhakikisha kuwa NEC inashikwa na kambi yake na RA ili kuweza kufanikisha mpango wake wa kuingia ikulu..Jamaa huyu,japo kwa kusita nilipojaribu kumdadisi kuhusu 111 bilioni ambazo TANESCO wamehamrishwa kuilipa DOWANS kama fidia ya kuvunja mkataba,Je si mlolongo wa mipango iliyoandaliwa kukusanya pesa kwa ajili ya uchaguzi huo,akasema inawezekana ila hana uhakika sana,isipokuwa mipango ya kukusanya hela ipo na inendelea kupitia wafanyabiashara na watu wengine wenye uwezo……………