Ufipa-Kinondoni
JF-Expert Member
- Jan 3, 2012
- 4,582
- 2,783
Kuna sura ya wazi ndani ya chama chetu cha CHADEMA inapokuja kushughulikia mambo ya ndani ya chama. Kimekuwa kinaendesha mambo kwa mikimiki sana na hata kuonyesha sura halisi ya chama kama ndo kingekuwa chama dola.
Miaka mingi nimekuwa nafuatilia uchaguzi wa chama unapokaribia huwa unambatana na kufukuzana kwa sana na kuwekena katika nafasi za maamuzi. Hili limekuwa likitafsiriwa kama kuweka wasiopinga fikra za mwenyekiti wetu, Mr. Mbowe.
Mwaka 2014/5 hali hii ilijionyesha zaidi kwa kumfukuza ZZK ndani ya chama pamoja na wenyeviti wengi wa Mikoa na Wilaya walioonyesha hisia za kutokubaliana na uongozi wa mwenyekiti.
Mwaka huu pia tumeanza ona yale yaliyokuwepo huko nyuma, na ifikapo 2019 zaidi ya nusu ya wenyeviti wa mikoa na wilaya na wasaidizi wake wanaweza kuwa wamefukuzwa uanachama na kuweka viongozi wa muda watakao mchagua mwenyekiti.
Hii ina maana mwenyekiti wa chadema huwa anajiteua kwa mgongo wa wajumbe alio waweka yeye kumpigia kura.
Kilichotokea hapa Kyela, cha kumteua mzee wa CCM wa miaka 80 kuwa mwenyekiti ni hatua moja ya Mbowe kuendelea kushika nafasi yake mpaka afe madarakani au achoke kuongoza.
Miaka mingi nimekuwa nafuatilia uchaguzi wa chama unapokaribia huwa unambatana na kufukuzana kwa sana na kuwekena katika nafasi za maamuzi. Hili limekuwa likitafsiriwa kama kuweka wasiopinga fikra za mwenyekiti wetu, Mr. Mbowe.
Mwaka 2014/5 hali hii ilijionyesha zaidi kwa kumfukuza ZZK ndani ya chama pamoja na wenyeviti wengi wa Mikoa na Wilaya walioonyesha hisia za kutokubaliana na uongozi wa mwenyekiti.
Mwaka huu pia tumeanza ona yale yaliyokuwepo huko nyuma, na ifikapo 2019 zaidi ya nusu ya wenyeviti wa mikoa na wilaya na wasaidizi wake wanaweza kuwa wamefukuzwa uanachama na kuweka viongozi wa muda watakao mchagua mwenyekiti.
Hii ina maana mwenyekiti wa chadema huwa anajiteua kwa mgongo wa wajumbe alio waweka yeye kumpigia kura.
Kilichotokea hapa Kyela, cha kumteua mzee wa CCM wa miaka 80 kuwa mwenyekiti ni hatua moja ya Mbowe kuendelea kushika nafasi yake mpaka afe madarakani au achoke kuongoza.