Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Madiwani 9 wahojiwa na TAKUKURU
na Moses Ng'wat, Mbeya
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (TAKUKURU), mkoa wa Mbeya, imewakamata na kuwahoji kwa saa 10 madiwani tisa wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Wilaya ya Chunya kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa. Miongoni mwa madiwani hao yumo pia Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Chunya, Kapale Chakupewa, ambaye ni diwani wa kata ya Galula na kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana zinadai kuwa ni miongoni mwa wagombea wa nafasi ya uenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo kwenye uchaguzi unaofanyika leo.
Tukio la kukamatwa kwa madiwani hao linadaiwa kutokea jana baada ya kundi la madiwani hao, kusafiri kutoka wilayani Chunya Desemba 13 na kufikia katika nyumba mbili za kulala wageni walikokamatwa na TAKUKURU.
Hata hivyo haikuweza kufahamika mara moja kilichosababisha madiwani hao kusafiri umbali wa kilomita 90 kutoka wilayani chunya na kuja mkoani Mbeya na kufikia nyumba mbili za wageni, ikiwa ni siku moja tu kabla ya kufanyika kwa zoezi la uchaguzi.
Kamanda wa TAKUKURU mkoani Mbeya, Daniel Mtuka, alithibitisha kukamatwa kwa madiwani hao na baada ya kuwekewa dhamana na mmoja wa viongozi wa juu wa chama hicho mkoani humo na kudai kuwa idadi yao hawazidi 10 na kwamba mahojiano ya awali yalifanyika Desemba 14 kuanzia majira ya saa 3 hadi saa 10 jioni.
Kweli juzi kuna mzalendo mmoja alitupigia simu na kututaarifu kuwa kuna kundi la madiwani limetoka Chunya limekuja mkoani kwa lengo la kuwekwa sawa na mmoja wa wagombea na nafasi ya uenyekiti na tulipofuatilia tuliwabaini watu hao ni madiwani, alisema Mtuka.
Alisema kuwa madiwani hao walikutwa katika nyumba mbili za kulala wageni za Lucky Inn na Lake Nyasa ambazo zote ziko eneo la Soweto.
Kamanda Mtuka, alipotakiwa kutaja majina ya madiwani hao na kufafanua vitu walivyokamatwa navyo, hakuwa tayari kutaja na kueleza kuwa sheria namba 23 hairuhusu na suala hilo bado linafanyiwa uchunguzi na ukikamilika taarifu zitatolewa katika vyombo vya habari.
Alisema waliamua kuwahoji madiwani hao baada ya kubaini kuwepo dalili zinazoashiria vitendo vya rushwa kwa kuwa waliokamatwa ni madiwani ambao ni wapiga kura, pamoja na mmoja wa wagombea wa nafasi ya uenyekiti wa halmashauri.
CCM leo inafanya uchaguzi wa ndani wa kupata wagombea wa nafasi ya umeya na uenyekiti mikoa yote nchini watakaopambana na wagombea wa vyama vya upinzani.
na Moses Ng'wat, Mbeya
Tukio la kukamatwa kwa madiwani hao linadaiwa kutokea jana baada ya kundi la madiwani hao, kusafiri kutoka wilayani Chunya Desemba 13 na kufikia katika nyumba mbili za kulala wageni walikokamatwa na TAKUKURU.
Hata hivyo haikuweza kufahamika mara moja kilichosababisha madiwani hao kusafiri umbali wa kilomita 90 kutoka wilayani chunya na kuja mkoani Mbeya na kufikia nyumba mbili za wageni, ikiwa ni siku moja tu kabla ya kufanyika kwa zoezi la uchaguzi.
Kamanda wa TAKUKURU mkoani Mbeya, Daniel Mtuka, alithibitisha kukamatwa kwa madiwani hao na baada ya kuwekewa dhamana na mmoja wa viongozi wa juu wa chama hicho mkoani humo na kudai kuwa idadi yao hawazidi 10 na kwamba mahojiano ya awali yalifanyika Desemba 14 kuanzia majira ya saa 3 hadi saa 10 jioni.
Kweli juzi kuna mzalendo mmoja alitupigia simu na kututaarifu kuwa kuna kundi la madiwani limetoka Chunya limekuja mkoani kwa lengo la kuwekwa sawa na mmoja wa wagombea na nafasi ya uenyekiti na tulipofuatilia tuliwabaini watu hao ni madiwani, alisema Mtuka.
Alisema kuwa madiwani hao walikutwa katika nyumba mbili za kulala wageni za Lucky Inn na Lake Nyasa ambazo zote ziko eneo la Soweto.
Kamanda Mtuka, alipotakiwa kutaja majina ya madiwani hao na kufafanua vitu walivyokamatwa navyo, hakuwa tayari kutaja na kueleza kuwa sheria namba 23 hairuhusu na suala hilo bado linafanyiwa uchunguzi na ukikamilika taarifu zitatolewa katika vyombo vya habari.
Alisema waliamua kuwahoji madiwani hao baada ya kubaini kuwepo dalili zinazoashiria vitendo vya rushwa kwa kuwa waliokamatwa ni madiwani ambao ni wapiga kura, pamoja na mmoja wa wagombea wa nafasi ya uenyekiti wa halmashauri.
CCM leo inafanya uchaguzi wa ndani wa kupata wagombea wa nafasi ya umeya na uenyekiti mikoa yote nchini watakaopambana na wagombea wa vyama vya upinzani.