Uchaguzi wa man and woman of the year JF siyo wa haki (SUperman pleaseeeeee)

kaburunye

JF-Expert Member
May 12, 2010
672
74
Wadau. Uchaguzi wa kumpata man and woman of the year hapa jamvini sio wa haki. Kwa nini wagombea binafsi haturuhusiwi??? Haiwezekani majina yetu yalipendekezwa halafu NEC ya JF mkayakata!!!! Ngoja niwasiliane na wanasheria wangu ili tusimamishe hili zoezi mpaka haki itendeke kwa kuwaruhusu wagombea binafsi.

Nataka hoja ya wagombea binafsi iruhusiwe. Kuna watu tunaona tungeweza kugombea na kuibuka washindi lakini majina yetu hayakupitishwa na tume. Superman naomba ufafanuzi kabla sijachukua hatua za kisheria. Nimepokea simu nyingi sana kutoka kwa mashabiki wangu huko nyumbani Pandagisiza Zongwinaminzi wakitishia kususia uchaguzi huu endapo jina langu halitakuwepo kati ya wagombea
 
Wadau. Uchaguzi wa kumpata man and woman of the year hapa jamvini sio wa haki. Kwa nini wagombea binafsi haturuhusiwi??? Haiwezekani majina yetu yalipendekezwa halafu NEC ya JF mkayakata!!!! Ngoja niwasiliane na wanasheria wangu ili tusimamishe hili zoezi mpaka haki itendeke kwa kuwaruhusu wagombea binafsi.

Nataka hoja ya wagombea binafsi iruhusiwe. Kuna watu tunaona tungeweza kugombea na kuibuka washindi lakini majina yetu hayakupitishwa na tume. Superman naomba ufafanuzi kabla sijachukua hatua za kisheria. Nimepokea simu nyingi sana kutoka kwa mashabiki wangu huko nyumbani Pandagisiza Zongwinaminzi wakitishia kususia uchaguzi huu endapo jina langu halitakuwepo kati ya wagombea

Nipo tayari kuwa mwanasheria wako mpaka haki itendeke, nitumie ushahidi wako uliojitosheleza nami nitalifanyia kazi hilo suala...

Nasubiri jibu...
 
Nipo tayari kuwa mwanasheria wako mpaka haki itendeke, nitumie ushahidi wako uliojitosheleza nami nitalifanyia kazi hilo suala...

Nasubiri jibu...

Nimekubali uungane na jopo la wanasheria wangu. Ushahidi ni kuwa jina langu halipo kwenye list ya wagombea. Ushahidi wa simu za ndugu zangu wa Pandagisiza nzogwinaminzi ni vigumu kuupata sababu ya urasimu wa wamiliki wa mitandao ya simu. Hebu nishauri mwanasheria wangu tufanye nini kuupata ushahidi huu muhimu. Ninazo sms zao walizoniandikia na kama tunaweza kuzitumia kama ushahidi basi niPM namba yako ya simu nikufowadie
 
Nimekubali uungane na jopo la wanasheria wangu. Ushahidi ni kuwa jina langu halipo kwenye list ya wagombea. Ushahidi wa simu za ndugu zangu wa Pandagisiza nzogwinaminzi ni vigumu kuupata sababu ya urasimu wa wamiliki wa mitandao ya simu. Hebu nishauri mwanasheria wangu tufanye nini kuupata ushahidi huu muhimu. Ninazo sms zao walizoniandikia na kama tunaweza kuzitumia kama ushahidi basi niPM namba yako ya simu nikufowadie
hahaaa holiday njema mkuu
 
Nimekubali uungane na jopo la wanasheria wangu. Ushahidi ni kuwa jina langu halipo kwenye list ya wagombea. Ushahidi wa simu za ndugu zangu wa Pandagisiza nzogwinaminzi ni vigumu kuupata sababu ya urasimu wa wamiliki wa mitandao ya simu. Hebu nishauri mwanasheria wangu tufanye nini kuupata ushahidi huu muhimu. Ninazo sms zao walizoniandikia na kama tunaweza kuzitumia kama ushahidi basi niPM namba yako ya simu nikufowadie

Ok, nimekuelewa. Kwa kuanza; kwa kuwa mimi ni mmoja tu wa wanasheria wako ningependa kufahamu wenzangu ili tuanze mara moja hili zoezi. Isitoshe kama una ushahidi wa malalamiko uliyowasilisha JEC pamoja na majibu yao ningefurahi pia kuupata. Udhaifu wa JEC kwenye huu mchakato nilishauona pia, kuna pingamizi jingine nimeliweka dhidi ya mmoja wa wagombea na sasa nasubiri uamuzi wa mwisho wa JEC kabla sijaamua kusonga mbele zaidi..
 
Wakuu wote na makamanda wa JF;

Hakika uchaguzi wa Mwaka huu umewagusa wengi tofauti na mwaka jana. Hii inaonyesha Elimu ya Uraia imewafikia wengi.

Naomba kutoa majibu ya hoja ya msingi iliyotolewa kama ifuatavyo:

Awali ya wote majibu haya yanapatikana hapa: https://www.jamiiforums.com/celebri...-of-the-year-2010-mchakato-wa-kuwapata-4.html

Naomba ninukuu na baada ya maelezo haya kama bado haieleweki nijulishwe:

Mwaka huu tunataka kuuboresha mchakato huu na tunapenda kupitia mchakato huu kupata washiriki wengi na kuipa taswira JF kuwa kuna watu wanafanya mambo makubwa.

Mwaka huu 2010 tunafanya mchakato wa kumpata JF WOMAN OF THE YEAR 2010 na pia JF MAN OF THE YEAR 2010.

Katika mchakato wa awali tutapendekeza majina mbalimbali katika kila category, na baada ya kupitia post zote za mapendekezo tutachagua watatu kutoka katika kila category na kisha kuwapambanisha kupitia JF POLLS. Mwaka huu napendekeza tutoe zawadi yenye hadhi fulani kwa washindi ili kutoa changamoto za umakini katika mabandiko haba jamvini. Tutajulishana zawadi hizi tutakapoingia katika mchakato wa Kupiga kura.

Vigezo vifuatavyo vizingatiwe katika kutoa mapendekezo ya watakaoshindanishwa katika hizi KURA ZA MAONI:

1. Kama ni category ya WOMAN lazima uwe umemdhania kuwa unayempendekeza ni Mwanamke na una ushahidi wa Kimazingira. katika hali ya mashaka, uhakikisho wa jinsia kutoka kwa muhusika aliyependekezwa utafanya akubalike. Uamuzi wa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Shindano hili utakuwa ni Final. wote mnahakikishiwa hakutakuwa na Uchakachuaji.

2. Kama ni category ya MAN lazima uwe umemdhania kuwa unayempendekeza ni Mwanaume na una ushahidi wa Kimazingira. katika hali ya mashaka, uhakikisho wa jinsia kutoka kwa muhusika aliyependekezwa utafanya akubalike.

Katika 1 na 2: Uamuzi wa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya JF (JEC) wa Shindano hili utakuwa ni Final. wote mnahakikishiwa hakutakuwa na Uchakachuaji.

3. Anayependekezwa lazima kuwe na ushahidi unaoonyesha kuwa ni Mwana JF aliyebobea hasa kutokana na Threads alizozianzisha na pia post alizozianzisha. Vyote lazima viwe na impact chanya kwa wasomaji wa JF

4. Awe ni mwenye uwezo wa kusimamia hoja zake na kuzijibu kikamilifu bila jazba na kwa umahiri wa hali ya juu pale ambapo anapata challenge toka kwa wachangiaji.

5. Awe ni mwenye ushawishi wa hali ya juu katika mabandiko anyochangia walau kwa muonekano wa wachangiaji kuunga mkono hoja zake.

6. Asibobee kwenye Jukwaa moja tu. Walau awe mchangiaji mzuri wa majukwaa yasiyopungua matatu

7. Asiwe mtu wa shari katika majibizano kiasi cha kupelekea Mods kumpa "BAN".

8. Aonekane wazi katika mabandiko yake anaweza akahisiwa kuwa Kiongozi Mzuri.

9. Awe Mchangiaji ambaye ni active walau mara moja kwa wiki. Ikiwa zaidi ni vizuri zaidi.

10. Awe ni mtu asiyeogopa kukemea mabandiko yenye lengo la kutukana, kudhalilisha, kubagua, kuleta mfarakano na kutokuelewana baina ya wanachama wa JF.

Sasa kila moja yuko huru kutoa mapendekezo yake ya nani wanastahili kuingia katika tatu bora katika kila category.

Nashauri kuwa mapendekezo ya majina yaambatane na maelezo mafupi.

Uwanja ni wenu. Karibuni.
 
Mi kwakuwa nimeanza mwaka huu mwishoni najua nitapambana mwakani mwaka huu wenu!
 
Uamuzi wa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Shindano hili utakuwa ni Final. wote mnahakikishiwa hakutakuwa na Uchakachuaji..

SUperman, asante kwa ufafanuzi lakini hoja yangu ya msingi ya mgombea binafsi hujaigusia. Pia sikubaliani na wewe kuwa uamuzi wa mwenyekiti wa tume ya shindano utakuwa final na hautaweza kupingwa "mahakama ya JF". Naona hii inafanana kabisa na katiba yetu kuukuu inayodai matokeo ya urais yakitangazwa na NEC hayapingwi mahakama yeyote. Mimi nashauri tuwe na mahakama ya JF ambayo itapitia malalamiko yote na rufaa za hapa JF maana najua mwenyekiti wa tume ya JF ni mwanadamu anaweza kughafiilka akatoa hukumu isiyo ya haki. Nashauri hata watu wanaopewa ban kama hawajaridhika na uamuzi wa mods wakate rufaa ndani ya muda fulani eg siku 10. Ikiwezekana liwepo jukwaa la mahakama na mahakimu wa JF watakaopitia rufaa wajiridhishe kama hukumu zilizotolewa ni za haki.

Ni mawazo yangu tu wadau. Bado azma yangu ya kwenda mahakamani kusimamisha zoezi la kuwapata man and woman of the year liko palepale unless Superman ulete hoja zinazoeleweka kwa nini wagombea binafsi haturuhusiwi
 
Wadau. Uchaguzi wa kumpata man and woman of the year hapa jamvini sio wa haki. Kwa nini wagombea binafsi haturuhusiwi??? Haiwezekani majina yetu yalipendekezwa halafu NEC ya JF mkayakata!!!! Ngoja niwasiliane na wanasheria wangu ili tusimamishe hili zoezi mpaka haki itendeke kwa kuwaruhusu wagombea binafsi.

Nataka hoja ya wagombea binafsi iruhusiwe. Kuna watu tunaona tungeweza kugombea na kuibuka washindi lakini majina yetu hayakupitishwa na tume. Superman naomba ufafanuzi kabla sijachukua hatua za kisheria. Nimepokea simu nyingi sana kutoka kwa mashabiki wangu huko nyumbani Pandagisiza Zongwinaminzi wakitishia kususia uchaguzi huu endapo jina langu halitakuwepo kati ya wagombea

na hao mashabiki wa huko walivyo wengi?????ilikuwa ushinde kwa kishindo...usikubali mwaya...:teeth:
 
na hao mashabiki wa huko walivyo wengi?????ilikuwa ushinde kwa kishindo...usikubali mwaya...:teeth:

Fab, you are very right. Mashabiki walitaka kuandamana lakini nimewatuliza kuwa hili suala linashughulikiwa
 
SUperman, asante kwa ufafanuzi lakini hoja yangu ya msingi ya mgombea binafsi hujaigusia. Pia sikubaliani na wewe kuwa uamuzi wa mwenyekiti wa tume ya shindano utakuwa final na hautaweza kupingwa "mahakama ya JF". Naona hii inafanana kabisa na katiba yetu kuukuu inayodai matokeo ya urais yakitangazwa na NEC hayapingwi mahakama yeyote. Mimi nashauri tuwe na mahakama ya JF ambayo itapitia malalamiko yote na rufaa za hapa JF maana najua mwenyekiti wa tume ya JF ni mwanadamu anaweza kughafiilka akatoa hukumu isiyo ya haki. Nashauri hata watu wanaopewa ban kama hawajaridhika na uamuzi wa mods wakate rufaa ndani ya muda fulani eg siku 10. Ikiwezekana liwepo jukwaa la mahakama na mahakimu wa JF watakaopitia rufaa wajiridhishe kama hukumu zilizotolewa ni za haki.

Ni mawazo yangu tu wadau. Bado azma yangu ya kwenda mahakamani kusimamisha zoezi la kuwapata man and woman of the year liko palepale unless Superman ulete hoja zinazoeleweka kwa nini wagombea binafsi haturuhusiwi

Kaburuye pamoja na kuwa hoja zako ni nzuri na nzito, kwa sasa uchaguzi utaendelea kwa kufuata katiba iliyopo. Hata hivyo unaweza kuleta hoja binafsi juu ya kuandikwa kwa katiba ambayo inaweza kutumika katika chaguzi zinazofuata.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom