Nimesoma katika gazeti leo kuwa Chaguzi katika majimbo ya Monduli, Ukonga na Korogwe zimechukua zaidi ya Tshs.12 billioni. Bado nashangaa na siamini macho yangu kama hayo Majimbo matatu yanaweza kuchukua idadi hiyo ya fedha. Kati ya Jimbo dogo ni la Monduli ni wazi haiwezi kuchukua Tshs.4 billioni. Fedha za umma lazima zitumike kwa kufuata sheria na taratibu. Ni wakati muafaka matumizi ya hizi fedha zifuatiliwe na mamlaka kama TAKUKURU na Wananchi tupewe mrejesho.