Facilitator
JF-Expert Member
- Oct 30, 2010
- 2,280
- 1,763
Kufuatia tukio la mlipuko jana jumamosi Arusha, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeahirisha chaguzi za madiwani katika kata zote nne (4) jijini arusha hadi jumapili ya tar 30/6/2013.
Poleni wote mlioguswa na tatizo hili.
-----------------------------
Poleni wote mlioguswa na tatizo hili.
-----------------------------
Tume ya taifa ya Uchaguzi imesimamisha kufanyika kwa uchaguzi mdogo wa udiwani ktk kata nne jijini Arusha. Akizungumza kwa njia ya simu na Radio TBC FM,kutoka Zanzibari mwenyekiti huyo wa tume ya uchaguzi alisema kua wameamua kusimamisha uchaguzi huo ili kuwapa nafasi vyombo vya usalama kuchunguza swala hilo.
Alisema kua sheria inawapa mamlaka kufanya hivyo pale wanapogundua kuwa hakutakua na uhuru wa mpiga kura kwenda kupiga kura. Alisema haiwezekani uchaguzi ufanyike ktk hali kama hiyo huku kukiwa na wasiwasi.
Kwa wale waliokua wanasema ni uongo basi sio uwongo ni kweli.
Source: Radio TBC FM.
Tume ya Uchaguzi Tanzania imeahirisha uchaguzi uliokuwa umepangwa kufanyika leo hii katika kata 4 za Mkoa wa Arusha. Kata zingine 22 zitaendelea na uchaguzi kama kawaida. Hii inatokaana na mlipuko wa bomu wa hapo jana.Sasa utafanyika jumapili tarehe 30.6.2013