Uchaguzi wa Kinondoni: Msimamizi wa Uchaguzi amenifurahisha, mpambano uanze!

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,193
25,500
Jana, kwenye mabandiko tofauti humu JF, niliyaponda na kutamani mapingamizi yote yaliyowasilishwa dhidi ya wagombea wa Ubunge wa Kinondoni yatupiliwe mbali. Lengo langu halikuwa kukiuka sheria,lilikuwa ni kutaka uchaguzi uendelee kama ulivyopangwa. Busara iongoze!

Wapo walionishambulia na kunipinga bila ya kufikiri mara mbili. Wapo pia walionipongeza na kupenda msimamo wangu. Nilisema, mapingamizi yote hayana msingi na yanapaswa kutupiliwa mbali. Nikasema pia kuwa wakati mwingine mapingamizi huwanyima wananchi viongozi bora.

Nimefurahishwa na uamuzi wa Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Kinondoni wa kuyatupilia mbali mapingamizi yote dhidi ya wagombea wa CCM,CHADEMA na SAU. Sasa, wagombea wote wanabaki na uchaguzi utafanyika vyema.

Kila la heri wana Kinondoni!
 
Tatizo mkuu nawe ueleweki upo wapi yaani full u double standards. Anyway salam zako mkuu.
 
Kwa hiyo unataka kusemaje?

....Siyo ANATAKA KUSEMAJE tayari ameshasema amefurahishwa na maamuzi ya msimamizi wa kuyatupilia mbali mapingamizi uchwara yote.....wakapambane ulingoni hukooo hakuna ushindi wa mezani hapaa....
 
Jana, kwenye mabandiko tofauti humu JF, niliyaponda na kutamani mapingamizi yote yaliyowasilishwa dhidi ya wagombea wa Ubunge wa Kinondoni yatupiliwe mbali. Lengo langu halikuwa kukiuka sheria,lilikuwa ni kutaka uchaguzi uendelee kama ulivyopangwa. Busara iongoze!

Wapo walionishambulia na kunipinga bila ya kufikiri mara mbili. Wapo pia walionipongeza na kupenda msimamo wangu. Nilisema, mapingamizi yote hayana msingi na yanapaswa kutupiliwa mbali. Nikasema pia kuwa wakati mwingine mapingamizi huwanyima wananchi viongozi bora.

Nimefurahishwa na uamuzi wa Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Kinondoni wa kuyatupilia mbali mapingamizi yote dhidi ya wagombea wa CCM,CHADEMA na SAU. Sasa, wagombea wote wanabaki na uchaguzi utafanyika vyema.

Kila la heri wana Kinondoni!
Msimamizi alikuwa hana jinsi ila ni kuiokoa FISIEM isije kupoteza mgombea wake kwani kosa lake la kutofanya mrejesho lilikuwa lina mtoa ulingoni bila ubishi.
Pingamizi la mwalim kuhusiana na stakabadhi yenye majina tofauti ilikuwa ni ishu inayoweza kurekebishwa.
Hivyo basi hii ni kama step 1 kwa FISIEM imefeli tusubirie step 2 ndani ya dimba
Lazima UKAWA kieleweke tu
9e72fe364461b6e07661ab06c3cea174.jpg
 
Jana, kwenye mabandiko tofauti humu JF, niliyaponda na kutamani mapingamizi yote yaliyowasilishwa dhidi ya wagombea wa Ubunge wa Kinondoni yatupiliwe mbali. Lengo langu halikuwa kukiuka sheria,lilikuwa ni kutaka uchaguzi uendelee kama ulivyopangwa. Busara iongoze!

Wapo walionishambulia na kunipinga bila ya kufikiri mara mbili. Wapo pia walionipongeza na kupenda msimamo wangu. Nilisema, mapingamizi yote hayana msingi na yanapaswa kutupiliwa mbali. Nikasema pia kuwa wakati mwingine mapingamizi huwanyima wananchi viongozi bora.

Nimefurahishwa na uamuzi wa Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Kinondoni wa kuyatupilia mbali mapingamizi yote dhidi ya wagombea wa CCM,CHADEMA na SAU. Sasa, wagombea wote wanabaki na uchaguzi utafanyika vyema.

Kila la heri wana Kinondoni!
Mapingamizi siyo kwamba yanawanyima wananchi viongozi bora, bali husaidia kuondoa ukakasi kwa wagombea na hivyo wapiga kura kuamua kwa usahihi bila bias yoyote. Kama mtu anahisiwa kuwa ana makandokando kwa nini huoni mantiki ya huyo mtu kuwekewa pingamizi ili pumba na mchele kujulikana?
Kwa maoni yako unashauri kila anayechukuwa form asonge mbele na wananchi ndo waamue kwenye sanduku la kura?
Wewe bila shaka ni mwanasheria/wakili, kwa upande wako kila shahidi anayesimama mahakamani dhidi yako unamkubali tu eti hakimu ndo ataamua hata kama unahisi baadhi ya details zake ni questionable?
Binafsi sioni tatizo la mapingamizi, jambo la msingi ni haki itendeke wakati wa kusikiliza na kuamua hayo mapingamizi
 
Na asije akatokea mtu kupinga uamuzi huo na kumba rufaa kwa ngazi ya juu?
 
Back
Top Bottom