Uchaguzi wa Kesho Kinondoni na Siha: Wito kwa Chadema na CCM, Tukubali Matokeo!. Asiyekubali Kushindwa Sii Mshindani

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,463
113,537
Wanabodi,

Jumamosi ya kesho ndio siku ya uchaguzi wa marudio majimbo ya Kinondoni na Siha, japo kuna vyama vingi vinavyoshiriki uchaguzi huu, lakini ukweli ni kwamba, washindani wawili wakuu ni Chadema iliyokuwa ikiyashikilia chini ya mwamvuli wa Ukawa, na CCM, inayotaka kumpokonya mtu tonge mdomoni.
Hili ni bandiko la wito kwa mafahali wawili hawa, kukubali matokeo kwa sababu, asiyekubali kushindwa sii mshindani!.

Kwa Nini Matokeo ya Uchaguzi wa Kinondoni na Siha ni Muhimu Sana kwa Chadema
?.
Uchaguzi huu ni muhimu sana kuutumia kama kipimo cha awali cha matokeo ya jumla ya uchaguzi wa 2020. Chadema ikishindwa kuyatetea majimbo haya mawili tuu kwa sasa, then haitaweza kuyatetea majimbo yake yote 2020, hivyo matokeo haya yatatuma ujumbe mzito kwa wabunge wote wa upinzani waliopo bungeni ndani ya bunge hili, kuwa kama bado wanataka kuendelea kuwa wabunge bunge lijalo, the nao ni lazima wajiunge CCM, wasimamishwe kupitia CCM ndipo watarudi bungeni!. Ombi langu kwa watu wa aina hii, nawaomba tuu kwa sasa wawe wavumilivu, wasijitoe, kwa kuwahurumia masikini wa Tanzania, kuingia gharama za uchaguzi wa marudio, wasubirie tuu hadi 2020 bunge litakapovunjwa, waende salama.

Kwa Nini Matokeo ya Uchaguzi Huu ni Muhimu Sana Kwa CCM ndio Maana CCM Wanatumia Nguvu Kubwa Sana?.
Kwa vile CCM wanakijua walichokifanya hadi wabunge hawa kuachia ubunge wao na kuhamia CCM, hivyo ili kuhalalisha kuwa CCM inapendwa sana na inakubalika sana kwa wapiga kura, kuweza kuwanunua wabunge na madiwani wa upinzani kwa bei rahisi tuu na kuwapokonya majimbo yao, hivyo watatumia mbinu hizo hizo kuwapendesha wapiga kura, ndio maana CCM inatumia nguvu kubwa sana na line-up nzito ya heavy guards wake akiwemo mkuu wa mhimili wa Bunge. Kwenye hili la heavy guards, lazima niipongeze CCM kwa reservations za ile top brass yake, hivyo huu ni uugwana mkubwa!. Maana ile top brass ingetia timu, sijui Chadema wangeambulia nini?!. Thanks to CCM for this!.

Mshindi wa Matokeo ya Kinondoni na Siha, ni Uthibitisho Ushindi wa Usaliti, Ulaghai, Rushwa, Dhulma, Ubatili, Ufisadi na Ubadhilifu, Dhidi ya Haki, Ukweli, Uadilifu na Uzalendo.
Hakuna asiyejua kinachofanyika behind the closed doors hadi wabunge na madiwani kuhamia CCM. Hii ni vita kati ya usaliti na uzalendo, ni vita kati ya ulaghai na ukweli, ni vita kati ya rushwa na uadilifu, ni vita kati ya dhulma na haki, no vita kati ya ufisadi, ubadhirifu, na matumizi mabaya ya fedha za umma dhidi ya ukereketwa wa kweli wa umasikini wa nchi hii na rasilimali zake. Upande wowote utakaoshinda, ni kielelezo cha hivi ndivyo Watanzania tulivyo!.

Ruswa: Wahamaji ni Wasaliti na Walarushwa, Wamehongwa!. Na Huu ni Uthibitisho
!.
Mtu ukiishachaguliwa diwani au mbunge, unabeba dhamana ya wananchi wa eneo husika, kujiuzulu ni usaliti kwa watu hao. Sasa msaliti anaporudi tena kuomba nafasi ile ile aliyoisaliti, akichaguliwa tena, kunatuma ujumbe mzito type ya wapiga kura wetu!

Japo tulionyeshwa ule ushahidi wa rushwa ya wazi wazi kwenye zile video za Nasari, japo zimekataliwa ila wenye macho tumeona!.
Hii inatuma ujumbe mzito kuhusu hili lidudu linaloitwa PCCB, nalo ni shina tuu la CCM!.

Ushahidi wangu wa rushwa ni huu. Utaratibu wa kujiunga na CCM unafahamika, utaratibu wa mtu kugombea ubunge ndani ya CCM, unafahamika ni mchakato fulani. Sasa mtu anajiunga leo CCM, kesho anateuliwa mgombea bila utaratibu na mchakato kufuatwa. Huu ni uthibitisho wa rushwa ya ahadi, kisheria inaitwa "promissory estoppel" ambayo ni ushahidi usiotia shaka mtu alihongwa ahadi ya kusimamishwa yeye kama atajitoa!. Ndicho kilichofanyika Kinondoni na Siha, na kitaendelea!. Rushwa sio lazima iwe ni pesa tuu!, hata ahadi ya uteuzi ni rushwa!, halafu hili lidudu li PCCB lipo tuu, na mijitu imejazana ofisini inakula tuu kiyoyozi, eti tunapiga vita rushwa!.

Uchaguzi wa Kinondoni na Siha ni Ufisadi na Ubadhirifu Wenye Uhalali wa Kisheria Kwa Jina la Demokrasia!.

Ukizisikia gharama za chaguzi hizi za kujitakia, utakubaliana na mimi kuwa huu ni ubadhirifu na ufisadi wa kujitakia. Haiwezekani nchi masikini kama Tanzania, to spend such amounts kwa jambo la kujitakia kama hili. Hizi ndio akili zetu sisi Watanzania!.

Wito Kwa Main Players, Chadema na CCM, Fuateni Sheria, Taratibu na Kanuni za NE
C.
Huu ni wito kwa hawa two main players, hakikisheni kesho mnazingatia sheria, taratibu na kanuni. Watanzania ni wapenda amani. Tunataka uchaguzi wa amani. Kama kuna kitu hakiendi sawa, fuateni taratibu, jazeni fomu za malalamiko sio kulalamikia kwenye media pekee!.

Wito Kwa Refa, NEC, Japo Uwanja Hauka Sawa, Tendeni Haki na Haki Ionekane imetendeka!.

Kwenye hili la NEC, naomba ku declare my interest kuwa naifahamu vizuri NEC, ni Tume Huru, na pia nimetokea kumfahamu Mkurugenzi wa NEC, Ramadhani Kailima ni mtu mwenye impeccable integrity kuendesha uchaguzi huru na wa haki. Hapa NEC yeye ni refa tuu, sie yeye aliyetengeneza uwanja wa mechi, wala aliyepanga timu, yeye kazi ni kuchezesha tuu hii mechi. Ombi kwa refa wetu NEC kuwa japo uwanja wetu ni mshazari na umekaa tenge kwa kuegemea upande mmoja, tunamuomba aichezeshe mechi hii ngumu kwa haki, na haki hiyo ionekane imetendeka, ili atakayeshinda, ashinde kwa haki, na atakayeshindwa, ashindwe kwa haki, watu wayakubali matokeo na maisha yaendelee.

Mwito Kwa Wana Kinondoni na Wana Siha, Uchaguzi ni Wenu, Hatuwachagulii, na Tutaheshimu Chaguo Lenu!.

Uchaguzi ni kwa Wana Kinondoni na Wana Siha, tumieni haki yenu kuwachagua viongozi mnaowataka. Sisi wengine tumewafanyia kazi ya uelimishaji umma kwa kuamini baadhi yenu hamjui mnatakiwa kuchagua kiasi kwamba mnaweza kuletewa ujinga na mkauchagua ujinga huo kwa kutojua kuwa mmeletewa ujinga. Lakini baada ya kuelimishwa kuwa hiki ni kitu kizuri, na huu ni ujinga, mkiamua kuchagua kitu kizuri mko huru ni chaguo lenu, ila hata mkiamua kuchagua ujinga kuwa ndio chaguo lenu, sisi wengine wote tutaheshimu chaguo lenu kwa ile ile kanuni ya
"Choose your love, and love your choice", anayekijua kitanda ni anayekilala ndie ajua kunguni wake.

The choice is yours.
All the best!

Paskali
 
Wanabodi,
Niko kitandani, usingizi umekata hivyo natumia jf mobile application kupandisha uzi huu, hapa natest tuu kwanza headline kama itapanda, bandiko linafuata!.
Paskali

Tukubali matokeo ktk mazingira? Kwa hiyo chama changu pendwa kikiibinya CHADEMA wakubali tu ili kuitwa washindani? Kwa faulu hizi za tume ya uchaguzi watu wawe kondoo na kusema tumeshindwa kwa haki? Wasimamizi ni makada wa chama changu, unategemea nini? Mimi ni CCM but kwa nyendo hizi hapana kwa kweli....tunahitaji uchaguzi wa haki na ulio huru.

Test tu bandiko lako lakini ujumbe ulioko moyoni mwako tumeupata!!
 
Wanabodi,
Niko kitandani, usingizi umekata hivyo natumia jf mobile application kupandisha uzi huu, hapa natest tuu kwanza headline kama itapanda, bandiko linafuata!.
Paskali
Paskali eehh, mbona CHADEMA wameona matokeo tayari yapo NEC??? Bila ya hata fikra potofu na uchochezi inaonesha CCM wameamua na hakuna uchaguzi Kinondoni wala Siha bali ni fujo tu kama jinsi ulivyobainisha kwenye bandiko lako la juzi....
 
Kweli kabisa ....tushindane kiungwana ...nchi ni yetu sote ....naamini watu watakaojitokeza kupiga kura watakuwa wachache kuliko kawaida ....vyama vikazie watu kwenda kupiga kura ( hasa upinzani) .....wakijitokeza wachache CCM itashinda lakini mwamko ukiwa mkubwa Chadema itashinda vizuri tu ....
 
Wanabodi,

Jumamosi ya kesho ndio siku ya uchaguzi wa marudio majimbo ya Kinondoni na Siha, japo kuna vyama vingi vinavyoshiriki uchaguzi huu, lakini ukweli ni kwamba, washindani wawili wakuu ni Chadema iliyokuwa ikiyashikilia chini ya mwamvuli wa Ukawa, na CCM, inayotaka kumpokonya mtu tonge mdomoni.
Hili ni bandiko la wito kwa mafahali wawili hawa, kukubali matokeo kwa sababu, asiyekubali kushindwa sii mshindani!.

Kwa Nini Matokeo ya Uchaguzi wa Kinondoni na Siha ni Muhimu Sana kwa Chadema
?.
Uchaguzi huu ni muhimu sana kuutumia kama kipimo cha awali cha matokeo ya jumla ya uchaguzi wa 2020. Chadema ikishindwa kuyatetea majimbo haya mawili tuu kwa sasa, then haitaweza kuyatetea majimbo yake yote 2020, hivyo matokeo haya yatatuma ujumbe mzito kwa wabunge wote wa upinzani waliopo bungeni ndani ya bunge hili, kuwa kama bado wanataka kuendelea kuwa wabunge bunge lijalo, the nao ni lazima wajiunge CCM, wasimamishwe kupitia CCM ndipo watarudi bungeni!. Ombi langu kwa watu wa aina hii, nawaomba tuu kwa sasa wawe wavumilivu, wasijitoe, kwa kuwahurumia masikini wa Tanzania, kuingia gharama za uchaguzi wa marudio, wasubirie tuu hadi 2020 bunge litakapovunjwa, waende salama.

Inaendelea
Paskali
Unazungumza kama mwanahabari huru kaka.

The politicians will find a way to twist the results in their favor. Hiki ndicho kitakachotuua.

Who is the NUMBER ONE ENEMY OF THE PEOPLE?

They say: THE POLITICIANS.
 
Ushindane kiungwana wakati uchaguzi hauko huru na wa haki? Ushindane kiungwana wakati mawakala wako hawaruhusiwi kuingia kwenye vyumba vya kupigia kura ili kuangalia dosari zozote zile za wizi wa kura au wapiga kura kunyimwa haki zao za kupiga kura? Ushindane kiungwana wakati tunaona kuna kila dalili ya MACCM, NEC na polisi ccm kufanya kila hila kuiba kura? ACHANE UJINGA WA KUTETEA MAOVU NCHINI YA KUKANDAMIZA DEMOKRASI YA KWELI. Kama Muasisi wa CCM Baba wa Taifa aliona CCM inakoelekea SIKO na wakati ule hali haikuwa mbaya kama sasa na nyinyi mnaweza kabisa kufanya hivyo. Amani ikipotea nchini kutokana na shuluma kubwa inayofanyika dhidi ya vyama vya siasa na Watanzania katika kunyimwa haki zao mbali mbali wanazodai za malipo ya miaka chungu nzima, bomoa bomoa ambayo mahakama imesimamisha lakini mahakama zinadharauliwa na dhuluma kuendelea nchini basi mnatakiwa wote muweke NCHI mbele kwanza na siyo hiki chama cha wahuni ambacho sasa kimefikia hata kuua ili kushinda chaguzi kwa gharama zozote.

Acheni ujinga wenu wa kuunga mkono dhuluma kubwa zinazoendelea nchini ili kuminya haki za Watanzania, haki za vyama vya upinzani.

Kweli kabisa ....tushindane kiungwana ...nchi ni yetu sote ....naamini watu watakaojitokeza kupiga kura watakuwa wachache kuliko kawaida ....vyama vikazie watu kwenda kupiga kura ( hasa upinzani) .....wakijitokeza wachache CCM itashinda lakini mwamko ukiwa mkubwa Chadema itashinda vizuri tu ....

Wanabodi,

Jumamosi ya kesho ndio siku ya uchaguzi wa marudio majimbo ya Kinondoni na Siha, japo kuna vyama vingi vinavyoshiriki uchaguzi huu, lakini ukweli ni kwamba, washindani wawili wakuu ni Chadema iliyokuwa ikiyashikilia chini ya mwamvuli wa Ukawa, na CCM, inayotaka kumpokonya mtu tonge mdomoni.
Hili ni bandiko la wito kwa mafahali wawili hawa, kukubali matokeo kwa sababu, asiyekubali kushindwa sii mshindani!.

Kwa Nini Matokeo ya Uchaguzi wa Kinondoni na Siha ni Muhimu Sana kwa Chadema
?.
Uchaguzi huu ni muhimu sana kuutumia kama kipimo cha awali cha matokeo ya jumla ya uchaguzi wa 2020. Chadema ikishindwa kuyatetea majimbo haya mawili tuu kwa sasa, then haitaweza kuyatetea majimbo yake yote 2020, hivyo matokeo haya yatatuma ujumbe mzito kwa wabunge wote wa upinzani waliopo bungeni ndani ya bunge hili, kuwa kama bado wanataka kuendelea kuwa wabunge bunge lijalo, the nao ni lazima wajiunge CCM, wasimamishwe kupitia CCM ndipo watarudi bungeni!. Ombi langu kwa watu wa aina hii, nawaomba tuu kwa sasa wawe wavumilivu, wasijitoe, kwa kuwahurumia masikini wa Tanzania, kuingia gharama za uchaguzi wa marudio, wasubirie tuu hadi 2020 bunge litakapovunjwa, waende salama.

Inaendelea
Paskali
 
Mkuu Paskali hata kama cdm itashindwa bado ccm wana hali mbaya hiyo 2020. Hebu jiulize ccm ina mambo kibao ya kuonyesha kwa wananchi lakini inalazimika kushinda kwa kufanya rafu zote hizi unazoziona. Cdm hawana hata ofisi ya maana, wala hawana mradi wowote wa maendeleo wa kuwaonyesha wananchi lakini ccm inabidi itumie mbeleko ya tume na jeshi la polisi kushinda. Katika mazingira tuliyoaminishwa kwamba rais na chama chake wanakubalika sana, na cdm inabomoka au imechokwa, tusingeona figisu figisu za hivi.

Mkuu Paskali hakuna jambo gumu kama kulazimishwa kupendwa. Umewahi kumuona mwanamke mzee, hata ajipake wanja na kuvaa vimini bado hapendeki na hata akimpata kijana ni kwa kumuhonga au kutumia ushirikina. In short, kuvuta riziki kwa kamba ni shida tu.
 
Wosia wa Baba wa Taifa dhidi ya aliye madarakani ambaye anavunja sheria za nchi.

"Tujenge Utamaduni wa kuthibiti Viongozi wetu kama wanavunja sheria za nchi, TUSIOGOPE. Mkianza na mkiwa na woga I PROMISE YOU mtatawaliwa na dictators I PROMISE YOU mkiogopaogopa namna hii nyinyi Wabunge, nani wote na kusema Mzee wanakuwa wakali then you're making absolutely_____ that you'll be under a dictatorship." Baba wa Taifa.

 


Wanabodi,

Jumamosi ya kesho ndio siku ya uchaguzi wa marudio majimbo ya Kinondoni na Siha, japo kuna vyama vingi vinavyoshiriki uchaguzi huu, lakini ukweli ni kwamba, washindani wawili wakuu ni Chadema iliyokuwa ikiyashikilia chini ya mwamvuli wa Ukawa, na CCM, inayotaka kumpokonya mtu tonge mdomoni.
Hili ni bandiko la wito kwa mafahali wawili hawa, kukubali matokeo kwa sababu, asiyekubali kushindwa sii mshindani!.

Kwa Nini Matokeo ya Uchaguzi wa Kinondoni na Siha ni Muhimu Sana kwa Chadema
?.
Uchaguzi huu ni muhimu sana kuutumia kama kipimo cha awali cha matokeo ya jumla ya uchaguzi wa 2020. Chadema ikishindwa kuyatetea majimbo haya mawili tuu kwa sasa, then haitaweza kuyatetea majimbo yake yote 2020, hivyo matokeo haya yatatuma ujumbe mzito kwa wabunge wote wa upinzani waliopo bungeni ndani ya bunge hili, kuwa kama bado wanataka kuendelea kuwa wabunge bunge lijalo, the nao ni lazima wajiunge CCM, wasimamishwe kupitia CCM ndipo watarudi bungeni!. Ombi langu kwa watu wa aina hii, nawaomba tuu kwa sasa wawe wavumilivu, wasijitoe, kwa kuwahurumia masikini wa Tanzania, kuingia gharama za uchaguzi wa marudio, wasubirie tuu hadi 2020 bunge litakapovunjwa, waende salama.

Kwa Nini Matokeo ya Uchaguzi Huu ni Muhimu Sana Kwa CCM ndio Maana CCM Wanatumia Nguvu Kubwa Sana?.
Kwa vile CCM wanakijua walichokifanya hadi wabunge hawa kuachia ubunge wao na kuhamia CCM, hivyo ili kuhalalisha kuwa CCM inapendwa sana na inakubalika sana kwa wapiga kura, kuweza kuwanunua wabunge na madiwani wa upinzani kwa bei rahisi tuu na kuwapokonya majimbo yao, hivyo watatumia mbinu hizo hizo kuwapendesha wapiga kura, ndio maana CCM inatumia nguvu kubwa sana na line-up nzito ya heavy guards wake akiwemo mkuu wa mhimili wa Bunge. Kwenye hili la heavy guards, lazima niipongeze CCM kwa reservations za ile top brass yake, hivyo huu ni uugwana mkubwa!. Maana ile top brass ingetia timu, sijui Chadema wangeambulia nini?!. Thanks to CCM for this!.

Inaendelea
Paskali
 


Wanabodi,

Jumamosi ya kesho ndio siku ya uchaguzi wa marudio majimbo ya Kinondoni na Siha, japo kuna vyama vingi vinavyoshiriki uchaguzi huu, lakini ukweli ni kwamba, washindani wawili wakuu ni Chadema iliyokuwa ikiyashikilia chini ya mwamvuli wa Ukawa, na CCM, inayotaka kumpokonya mtu tonge mdomoni.
Hili ni bandiko la wito kwa mafahali wawili hawa, kukubali matokeo kwa sababu, asiyekubali kushindwa sii mshindani!.

Kwa Nini Matokeo ya Uchaguzi wa Kinondoni na Siha ni Muhimu Sana kwa Chadema
?.
Uchaguzi huu ni muhimu sana kuutumia kama kipimo cha awali cha matokeo ya jumla ya uchaguzi wa 2020. Chadema ikishindwa kuyatetea majimbo haya mawili tuu kwa sasa, then haitaweza kuyatetea majimbo yake yote 2020, hivyo matokeo haya yatatuma ujumbe mzito kwa wabunge wote wa upinzani waliopo bungeni ndani ya bunge hili, kuwa kama bado wanataka kuendelea kuwa wabunge bunge lijalo, the nao ni lazima wajiunge CCM, wasimamishwe kupitia CCM ndipo watarudi bungeni!. Ombi langu kwa watu wa aina hii, nawaomba tuu kwa sasa wawe wavumilivu, wasijitoe, kwa kuwahurumia masikini wa Tanzania, kuingia gharama za uchaguzi wa marudio, wasubirie tuu hadi 2020 bunge litakapovunjwa, waende salama.

Kwa Nini Matokeo ya Uchaguzi Huu ni Muhimu Sana Kwa CCM ndio Maana CCM Wanatumia Nguvu Kubwa Sana?.
Kwa vile CCM wanakijua walichokifanya hadi wabunge hawa kuachia ubunge wao na kuhamia CCM, hivyo ili kuhalalisha kuwa CCM inapendwa sana na inakubalika sana kwa wapiga kura, kuweza kuwanunua wabunge na madiwani wa upinzani kwa bei rahisi tuu na kuwapokonya majimbo yao, hivyo watatumia mbinu hizo hizo kuwapendesha wapiga kura, ndio maana CCM inatumia nguvu kubwa sana na line-up nzito ya heavy guards wake akiwemo mkuu wa mhimili wa Bunge. Kwenye hili la heavy guards, lazima niipongeze CCM kwa reservations za ile top brass yake, hivyo huu ni uugwana mkubwa!. Maana ile top brass ingetia timu, sijui Chadema wangeambulia nini?!. Thanks to CCM for this!.

Inaendelea
Paskali
 
Hata Jambazi mpora chama naye analalamika.



Wanabodi,

Jumamosi ya kesho ndio siku ya uchaguzi wa marudio majimbo ya Kinondoni na Siha, japo kuna vyama vingi vinavyoshiriki uchaguzi huu, lakini ukweli ni kwamba, washindani wawili wakuu ni Chadema iliyokuwa ikiyashikilia chini ya mwamvuli wa Ukawa, na CCM, inayotaka kumpokonya mtu tonge mdomoni.
Hili ni bandiko la wito kwa mafahali wawili hawa, kukubali matokeo kwa sababu, asiyekubali kushindwa sii mshindani!.

Kwa Nini Matokeo ya Uchaguzi wa Kinondoni na Siha ni Muhimu Sana kwa Chadema
?.
Uchaguzi huu ni muhimu sana kuutumia kama kipimo cha awali cha matokeo ya jumla ya uchaguzi wa 2020. Chadema ikishindwa kuyatetea majimbo haya mawili tuu kwa sasa, then haitaweza kuyatetea majimbo yake yote 2020, hivyo matokeo haya yatatuma ujumbe mzito kwa wabunge wote wa upinzani waliopo bungeni ndani ya bunge hili, kuwa kama bado wanataka kuendelea kuwa wabunge bunge lijalo, the nao ni lazima wajiunge CCM, wasimamishwe kupitia CCM ndipo watarudi bungeni!. Ombi langu kwa watu wa aina hii, nawaomba tuu kwa sasa wawe wavumilivu, wasijitoe, kwa kuwahurumia masikini wa Tanzania, kuingia gharama za uchaguzi wa marudio, wasubirie tuu hadi 2020 bunge litakapovunjwa, waende salama.

Kwa Nini Matokeo ya Uchaguzi Huu ni Muhimu Sana Kwa CCM ndio Maana CCM Wanatumia Nguvu Kubwa Sana?.
Kwa vile CCM wanakijua walichokifanya hadi wabunge hawa kuachia ubunge wao na kuhamia CCM, hivyo ili kuhalalisha kuwa CCM inapendwa sana na inakubalika sana kwa wapiga kura, kuweza kuwanunua wabunge na madiwani wa upinzani kwa bei rahisi tuu na kuwapokonya majimbo yao, hivyo watatumia mbinu hizo hizo kuwapendesha wapiga kura, ndio maana CCM inatumia nguvu kubwa sana na line-up nzito ya heavy guards wake akiwemo mkuu wa mhimili wa Bunge. Kwenye hili la heavy guards, lazima niipongeze CCM kwa reservations za ile top brass yake, hivyo huu ni uugwana mkubwa!. Maana ile top brass ingetia timu, sijui Chadema wangeambulia nini?!. Thanks to CCM for this!.

Inaendelea
Paskali
 
Ushindane kiungwana wakati uchaguzi hauko huru na wa haki? Ushindane kiungwana wakati mawakala wako hawaruhusiwi kuingia kwenye vyumba vya kupigia kura ili kuangalia dosari zozote zile za wizi wa kura au wapiga kura kunyimwa haki zao za kupiga kura? Ushindane kiungwana wakati tunaona kuna kila dalili ya MACCM, NEC na polisi ccm kufanya kila hila kuiba kura? ACHANE UJINGA WA KUTETEA MAOVU NCHINI YA KUKANDAMIZA DEMOKRASI YA KWELI. Kama Muasisi wa CCM Baba wa Taifa aliona CCM inakoelekea SIKO na wakati ule hali haikuwa mbaya kama sasa na nyinyi mnaweza kabisa kufanya hivyo. Amani ikipotea nchini kutokana na shuluma kubwa inayofanyika dhidi ya vyama vya siasa na Watanzania katika kunyimwa haki zao mbali mbali wanazodai za malipo ya miaka chungu nzima, bomoa bomoa ambayo mahakama imesimamisha lakini mahakama zinadharauliwa na dhuluma kuendelea nchini basi mnatakiwa wote muweke NCHI mbele kwanza na siyo hiki chama cha wahuni ambacho sasa kimefikia hata kuua ili kushinda chaguzi kwa gharama zozote.

Acheni ujinga wenu wa kuunga mkono dhuluma kubwa zinazoendelea nchini ili kuminya haki za Watanzania, haki za vyama vya upinzani.
cc Pascal Mayalla ni mara elfu bango lako lijikite zaidi kwenye suala la kutoa HAKI kunakopaswa kufanywa na NEC na CCM (CCM kwenye huu uchaguzi ni mchezaji lakini kwasababu ni chama dola pia kimejigeuza refarii ambae anamuamrisha refarii HALALI ambae ni NEC kufanya vile inavyotaka CCM ifanye)..

To be honest, CCM na NEC ndio washaonyesha dalili zote za kuharibu Uchaguzi huu..

Zungumzia kwa kukemea hili na sio hili la washindani kukubali matokeo wakati Uchaguzi umevurugwa.
 
Ahsante sana Mkuu MENGELENI KWETU. Hawa wahuni wa CCM wameanza hila za kuiba uchaguzi mapema kabisa bila hata kificho halafu huyu Pascal Mayalla anataka Chadema waendelee kudhalilishwa, kupigwa, kuuwawa na kuibiwa katika kila chaguzi.



cc Pascal Mayalla ni mara elfu bango lako lijikite zaidi kwenye suala la kutoa HAKI kunakopaswa kufanywa na NEC na CCM (CCM kwenye huu uchaguzi ni mchezaji lakini kwasababu ni chama dola pia kimejigeuza refarii ambae anamuamrisha refarii HALALI ambae ni NEC kufanya vile inavyotaka CCM ifanye)..

To be honest, CCM na NEC ndio washaonyesha dalili zote za kuharibu Uchaguzi huu..

Zungumzia kwa kukemea hili na sio hili la washindani kukubali matokeo wakati Uchaguzi umevurugwa.
 
BAK hakuna jipya kwenye chaguzi za Tanzania toka uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995. Chadema imeshiriki chaguzi zote kwa sheria hizi hizi ...figisu hizi hizi ....tena hizi chaguzi ndogo ndio kabisa mna uzoefu nazo sana ....zipo chaguzi mlizoshinda na kushindwa ndio maana mmefanya maamuzi ya kushiriki Kinondoni mkijua mnaweza kushinda. Hakuna figisu mpya mnayofanyiwa ....ndio maana wengine hatupasui kichwa na hayo maana mnayajua lakini mmeamua kushiriki na kuwapa watu matumaini kuwa mmejipanga bila kujali figisu zozote .....Kinondoni ndipo yalipo makao makuu ya chama na timu nzima kistratejia ipo hapo .....please mnatakiwa kushinda hata kama CCM watabeba kila chombo cha dola .....hata mimi nawapa asilimia kubwa kushinda ....mkishindwa hata kwa figisu nzito namna gani .....ni dalili mbaya mno ....
 
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) limetoa ujumbe wa Kwaresma wa mwaka 2018 ndani yake likitoa msimamo kuhusu masuala ya kisiasa, kiuchumi na kijamii nchini.

Ujumbe huo ulioandikwa na maaskofu wote 35 wa TEC wakiongozwa na Rais wake, Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa upo katika kitabu cha kurasa 20 ikiwa ni maandalizi ya ibada hiyo ya siku 40, kipindi ambacho ni cha mfungo wa sala kukumbuka siku 40 za Kristo kufunga na kwenda jangwani.

Hali ya kisiasa

Katika ujumbe huo, TEC imesema uamuzi wa Serikali kuzuia maandamano, mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa ni kwenda kinyume cha Katiba ya nchi.

Baraza hilo pia limeonya hatua ya Serikali kuvibana vyombo vya habari ikiwa pamoja na kuvifungia kwa sababu mbalimbali.

“Kufungiwa huku kwa vyombo vya habari kumeenda sambamba na kuminya uhuru wa Mahakama na Bunge kwa njia ya kuminya haki wabunge na kutowapa nafasi ya mikutano ya hadhara kama haki yao ya msingi ya kikatiba.”

Alipopigiwa simu ili kutoa maoni ya upande wa Serikali kuhusu ujumbe huo, Msemaji wa Serikali, Dk Hassan Abbasi alisema, “Sijaliona bado tamko husika kwa hiyo siwezi kujibu hoja ambayo sijaisoma kwa sasa.”

TEC imetoa ujumbe huo katika kipindi ambacho vyama vya siasa, hasa vya upinzani vikilalamika kuzuiwa kufanya mikutano ya hadhara baada ya Serikali kuipiga marufuku mpaka mwaka 2020, isipokuwa kwa wabunge walioshinda uchaguzi ambao wameruhusiwa kufanya mikutano kwenye majimbo yao.

Ugumu huo umetajwa na vyama hivyo kwamba unapunguza nguvu ya ushindani kwa vyama vya upinzani kukikabili chama tawala.

“Kikatiba, nchi yetu inafuata mfumo wa demokrasia ya vyama vingi. Katiba na sheria mbalimbali zimeainisha utaratibu wa kazi na shughuli za vyama vya siasa. Ili kuhakikisha kwamba shughuli za vyama vya siasa zinakuwa endelevu, vyama vyenye kukidhi vigezo hupewa ruzuku kupitia bajeti ya Serikali inayopitishwa na Bunge,” unaeleza ujumbe huo.

“Hata hivyo, shughuli za, siasa bado zinaendelea kuzuiwa kwa kutumia vyombo vya dola. Maana yake ni kwamba shughuli za kiuenezi za vyama vya siasa, kama vile mikutano ya hadhara, maandamano, makongamano, mijadala na hata mikutano ya ndani, ambayo ni haki ya kila raia, zimekoma mpaka uchaguzi mwingine. Kisheria, huu ni uvunjifu wa Katiba na sheria za nchi.”

Kuhusu vyombo vya habari, TEC imesema Serikali imepunguza wigo wa uhuru wa wananchi wa kupata habari na maoni ya kujieleza na kueleza kwamba kwa ujumla wake, mazingira hayo yatasababisha jamii kufarakana na hata kujenga chuki.

“Kumekuwapo pia hali ya vurugu katika chaguzi mbalimbali. Chaguzi hizi zinaacha nyuma uchungu, hasira, tamaa ya kulipa kisasi na hata kususia chaguzi nyingine,” unasema ujumbe huo wa TEC na kuonya kuwa kama hali hiyo itaachwa, itakuja kusababisha mifarakano mikubwa itakayobomoa amani na umoja wa kitaifa.

Kiuchumi

Kuhusu uchumi, TEC imetoa mambo sita ya kujiuliza; “Tunazitumiaje mali na rasilimali nyingine tulizokabidhiwa na Mungu kama mawakili wake? Tunalipa kodi stahiki kwa ajili ya kugharamia huduma za jamii ambazo Serikali inapaswa kutoa kwa ajili ya wananchi?”

“Wale ambao tu waajiri, tunawajali wafanyakazi na wahudumu wetu kwa kuwalipa mishahara ya halali? Wale ambao tu wafanya biashara, tunalipa kodi zote kihalali?”

“Wale ambao tumepewa jukumu la kukusanya kodi, ushuru na ada nyingine kama tunafanya hivyo kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu husika? Tunaepukaje na kishawishi cha rushwa, hongo, mulungula, magendo au aina yoyote ya ufisadi?”


Kijamii

Katika eneo la kijamii TEC imesema bado kuna kishawishi cha kupingana na azma ya kuboresha maisha ya kijamii.

“Hii inajidhihirisha kwa njia ya uhasama, ugomvi, ukatili kwa watoto na wanawake, ujambazi, na maovu mengine kama hayo miongoni mwa jamii yetu. Kama wamisionari tunaopaswa kuleta habari njema kwa ndugu zetu, kwa nini turuhusu roho ya namna hii ambayo kwa kweli ni roho ya Kaini inayouliza kwa jeuri kabisa,” unasema ujumbe huo.

Mambo matatu

Katika ujumbe wake, Baraza hilo limesema, “Kwa mwaka huu wa 2018 kipindi hiki ni cha kujitafakari mbele ya Mungu na kufanya toba hususan uhai wa amani yetu kwa njia ya matendo ya huruma, haki upendo na amani kwa jirani zetu.”

Limesema hiki ni kipindi chenye upekee wa aina yake kwake sababu ya mambo matatu;

“Ni katika mwaka huu ambapo Kanisa Katoliki Tanzania linaadhimisha na kusherehekea miaka 150 ya Ukatoliki Tanzania Bara, na kilele chake kitakuwa tarehe 2 Oktoba.

Mwaka huu pia utakuwa ni mwaka wa 50 tangu Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania watoe tamko rasmi kuhusu mwelekeo na hatima ya nchi yetu na Mwaka huu ni mwaka wa maandalizi ya utekelezaji wa haki ya msingi ya kidemokrasia ya raia wote ya kuchagua viongozi wa Serikali zetu za mitaa, vijiji na vitongoji hapo mwakani 2019.”

Kwa sababu hizo tatu, TEC imesema, “Ni vyema tafakari yetu ya Kwaresima ikalenga katika swali ambalo, kwa namna moja au nyingine, linahusu sababu hizo tatu. Kwa njia ya swali hilo mwanadamu hudiriki kumhoji na kumuuliza Mungu na Muumba wake kuhusu hali ya binadamu mwenzake. Swali hilo ni Je, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?” (Mw. 4:9).

Wanabodi,

Jumamosi ya kesho ndio siku ya uchaguzi wa marudio majimbo ya Kinondoni na Siha, japo kuna vyama vingi vinavyoshiriki uchaguzi huu, lakini ukweli ni kwamba, washindani wawili wakuu ni Chadema iliyokuwa ikiyashikilia chini ya mwamvuli wa Ukawa, na CCM, inayotaka kumpokonya mtu tonge mdomoni.
Hili ni bandiko la wito kwa mafahali wawili hawa, kukubali matokeo kwa sababu, asiyekubali kushindwa sii mshindani!.

Kwa Nini Matokeo ya Uchaguzi wa Kinondoni na Siha ni Muhimu Sana kwa Chadema
?.
Uchaguzi huu ni muhimu sana kuutumia kama kipimo cha awali cha matokeo ya jumla ya uchaguzi wa 2020. Chadema ikishindwa kuyatetea majimbo haya mawili tuu kwa sasa, then haitaweza kuyatetea majimbo yake yote 2020, hivyo matokeo haya yatatuma ujumbe mzito kwa wabunge wote wa upinzani waliopo bungeni ndani ya bunge hili, kuwa kama bado wanataka kuendelea kuwa wabunge bunge lijalo, the nao ni lazima wajiunge CCM, wasimamishwe kupitia CCM ndipo watarudi bungeni!. Ombi langu kwa watu wa aina hii, nawaomba tuu kwa sasa wawe wavumilivu, wasijitoe, kwa kuwahurumia masikini wa Tanzania, kuingia gharama za uchaguzi wa marudio, wasubirie tuu hadi 2020 bunge litakapovunjwa, waende salama.

Kwa Nini Matokeo ya Uchaguzi Huu ni Muhimu Sana Kwa CCM ndio Maana CCM Wanatumia Nguvu Kubwa Sana?.
Kwa vile CCM wanakijua walichokifanya hadi wabunge hawa kuachia ubunge wao na kuhamia CCM, hivyo ili kuhalalisha kuwa CCM inapendwa sana na inakubalika sana kwa wapiga kura, kuweza kuwanunua wabunge na madiwani wa upinzani kwa bei rahisi tuu na kuwapokonya majimbo yao, hivyo watatumia mbinu hizo hizo kuwapendesha wapiga kura, ndio maana CCM inatumia nguvu kubwa sana na line-up nzito ya heavy guards wake akiwemo mkuu wa mhimili wa Bunge. Kwenye hili la heavy guards, lazima niipongeze CCM kwa reservations za ile top brass yake, hivyo huu ni uugwana mkubwa!. Maana ile top brass ingetia timu, sijui Chadema wangeambulia nini?!. Thanks to CCM for this!.

Mshindi wa Matokeo ya Kinondoni na Siha, ni Uthibitisho Ushindi wa Usaliti, Ulaghai, Rushwa, Dhulma, Ubatili, Ufisadi na Ubadhilifu, Dhidi ya Haki, Ukweli, Uadilifu na Uzalendo.
Hakuna asiyejua kinachofanyika behind the closed doors hadi wabunge na madiwani kuhamia CCM, nitaeleza kimoja kimoja nikianzia na rushwa.

Inaendelea
Paskali
 
Wewe ni mpuuzi ndito sababu unaona hakuna jipya. Watu wanapigwa marungu, mapanga, kujeruhiwa na hata kuuwawa lakini wewe unaona hakuna jipya!!!! Angekuwa ameuwawa mtu wako wa karibu kwa vurugu za uchaguzi labda ungeona kuna jipya ambalo limesababisha hata Baraza la Maaskofu wa Kikatoliki nchini kwa mara ya KWANZA wametoa onyo kwa Serikali kwamba nchi inakoelea si kwema.

Ni miaka 56 sasa ya uhuru hili Baraza la Maaskofu halijawahi kutoa waraka kama huo ili kuikemea Serikali na pia kuitahadharisha kwamba inaweza kabisa kuwa chanzo cha vurugu kubwa nchini kufuatia dhuluma, udhalilishaji, kuteswa, kupigwa na hata kuuwawa kwa Watanzania wasio na hatia.

BAK hakuna jipya kwenye chaguzi za Tanzania toka uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995. Chadema imeshiriki chaguzi zote kwa sheria hizi hizi ...figisu hizi hizi ....tena hizi chaguzi ndogo ndio kabisa mna uzoefu nazo sana ....zipo chaguzi mlizoshinda na kushindwa ndio maana mmefanya maamuzi ya kushiriki Kinondoni mkijua mnaweza kushinda. Hakuna figisu mpya mnayofanyiwa ....ndio maana wengine hatupasui kichwa na hayo maana mnayajua lakini mmeamua kushiriki na kuwapa watu matumaini kuwa mmejipanga bila kujali figisu zozote .....Kinondoni ndipo yalipo makao makuu ya chama na timu nzima kistratejia ipo hapo .....please mnatakiwa kushinda hata kama CCM watabeba kila chombo cha dola .....hata mimi nawapa asilimia kubwa kushinda ....mkishindwa hata kwa figisu nzito namna gani .....ni dalili mbaya mno ....
 
Wanabodi,

Jumamosi ya kesho ndio siku ya uchaguzi wa marudio majimbo ya Kinondoni na Siha, japo kuna vyama vingi vinavyoshiriki uchaguzi huu, lakini ukweli ni kwamba, washindani wawili wakuu ni Chadema iliyokuwa ikiyashikilia chini ya mwamvuli wa Ukawa, na CCM, inayotaka kumpokonya mtu tonge mdomoni.
Hili ni bandiko la wito kwa mafahali wawili hawa, kukubali matokeo kwa sababu, asiyekubali kushindwa sii mshindani!.

Kwa Nini Matokeo ya Uchaguzi wa Kinondoni na Siha ni Muhimu Sana kwa Chadema
?.
Uchaguzi huu ni muhimu sana kuutumia kama kipimo cha awali cha matokeo ya jumla ya uchaguzi wa 2020. Chadema ikishindwa kuyatetea majimbo haya mawili tuu kwa sasa, then haitaweza kuyatetea majimbo yake yote 2020, hivyo matokeo haya yatatuma ujumbe mzito kwa wabunge wote wa upinzani waliopo bungeni ndani ya bunge hili, kuwa kama bado wanataka kuendelea kuwa wabunge bunge lijalo, the nao ni lazima wajiunge CCM, wasimamishwe kupitia CCM ndipo watarudi bungeni!. Ombi langu kwa watu wa aina hii, nawaomba tuu kwa sasa wawe wavumilivu, wasijitoe, kwa kuwahurumia masikini wa Tanzania, kuingia gharama za uchaguzi wa marudio, wasubirie tuu hadi 2020 bunge litakapovunjwa, waende salama.

Kwa Nini Matokeo ya Uchaguzi Huu ni Muhimu Sana Kwa CCM ndio Maana CCM Wanatumia Nguvu Kubwa Sana?.
Kwa vile CCM wanakijua walichokifanya hadi wabunge hawa kuachia ubunge wao na kuhamia CCM, hivyo ili kuhalalisha kuwa CCM inapendwa sana na inakubalika sana kwa wapiga kura, kuweza kuwanunua wabunge na madiwani wa upinzani kwa bei rahisi tuu na kuwapokonya majimbo yao, hivyo watatumia mbinu hizo hizo kuwapendesha wapiga kura, ndio maana CCM inatumia nguvu kubwa sana na line-up nzito ya heavy guards wake akiwemo mkuu wa mhimili wa Bunge. Kwenye hili la heavy guards, lazima niipongeze CCM kwa reservations za ile top brass yake, hivyo huu ni uugwana mkubwa!. Maana ile top brass ingetia timu, sijui Chadema wangeambulia nini?!. Thanks to CCM for this!.

Mshindi wa Matokeo ya Kinondoni na Siha, ni Uthibitisho Ushindi wa Usaliti, Ulaghai, Rushwa, Dhulma, Ubatili, Ufisadi na Ubadhilifu, Dhidi ya Haki, Ukweli, Uadilifu na Uzalendo.
Hakuna asiyejua kinachofanyika behind the closed doors hadi wabunge na madiwani kuhamia CCM, nitaeleza kimoja kimoja nikianzia na rushwa.

Inaendelea
Paskali
Paskali, you have missed the point. Kuna mtu alisema hivi " Gari nikupe mimi,mashahara nikulipe mimi,halafu umtangaze mpinzani ameshinda?huna kazi kuanzia siku hiyo" nukuu rais Magufuli
Nini kifanyke CDM kulinda haki yake? Wataweza mbele ya polisi, mabomu, utekeji unaofanywa na dola, mauaji yanayofanywa na dola etc? Unwashauri nini , wafanye nini kupata haki yao?
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya aomba radhi kwa Rais Magufuli baada CCM kushindwa kata ya Ibighi! Akana baada ya kuhojiwa
 
Back
Top Bottom