makoye2009
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,638
- 1,218
Kwa wenye access na Channel Ten, watch kipindi cha Channel Ten on Monday Live!, Mwenyekiti wa Chadema, Mhe. Freeman Mbowe yuko hewani...
Mwenyekiti Mbowe amesema uchaguzi huo haukuwa huru na wa haki, ndio sababu ya msingi ya mgombea wa Chadema kususia kusaini ile karatasi ya matokeo na hivyo Chadema kitakwenda mahakamani kuyapinga matokeo hayo.
Mhe. Mbowe amesema, uchaguzi huo umeendeshwa na Tume isiyo huru ya Uchaguzi ambayo imekiuka kwa makusudi baadhi ya sheria, taratibu na kanuni kulikowaondolea haki ya kupiga kura, watu wengi wenye haki hiyo.
Pia serikali, imekiuka sheria, taratibu na kanuni, kwa kuingia Igunga kama serikali, wakati serikali haukupaswa kujiingiza kwenye direct campaingn za CCM.
Mbowe amesema, Chadema itakwenda mahakamani sio kwa lengo la kutaka matokeo ya Igunga yabatilishwe, bali inakwenda mahakamani ili mahakama kama chumbo huru, kihakikishe haki inatendeka kwa kuimuru Tume ya Uchaguzi itende haki na kupress kupatikana kwa Tume huru ya uchaguzi ili kuweka presedence kwa chaguzi nyingine zitakazofuatia.
Mbowe ameshamaliza kuhojiwa na sasa ni wachangiaji wakichangia kuu iitwayo "Uchaguzi wa Igunga, Tumejifunza Nini?.
Mhe. Mbowe is correct.
Mimi naomba CHADEMA wafanye haraka kupeleka hiyo kesi Mahakamani. Kuna vipengele kadhaa ambavyo vilikiukwa kwa uwazi kabisa na CCM kwenye kampeni za Uchaguzi wa Igunga.
- CCM wamekiuka matumizi ya Bajeti ya Uchaguzi iliyoidhinishwa na Msajili wa Vyama ambayo ilitakiwa iwe au isizidi Tshs.milioni 80. CCM wametumia zaidi ya Tshs.Bilioni 10!
- CCM wametumia Resources za Serikali kufanya kampeni Igunga. Tumeshuhudia Mawaziri na viongozi wengi waandamizi wa serikali wakitumia magari ya Serikali yenye namba ST(X) kuifanyia CCM kampeni ambayo ni kinyume cha sheria za Uchaguzi.
- CCM wamefanya Kampeni wakiwa na SILAHA kama bastola kinyume cha sheria ya Uchaguzi. Ushahidi ni upo wa kina Aden Rage(MB-Tabora mjini-CCM) na Aesh(MB-Sumbawanga-CCM).
- CCM wametumia RUSHWA kwenye Kampeni za Igunga. Wamehonga PESA na MAJI kuwarubuni wananchi wa Igunga wawape kura. Ushahidi upo kwamba MAJI yalikatwa mjini na yakaelekezwa VIJIJINI ili wanavijiji wapate maji na kuna gari la CCM lililokamatwa likiwa na Tshs.Milioni 20 siku ya Uchaguzi likigawa pesa kwa wapiga kura.