Uchaguzi 2020 Uchaguzi wa 2020 unaenda kuitambulisha Tanzania ya miaka 100 ijayo

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Huu uchaguzi una maana kubwa sana kwa taifa la Tanzania. Ni uchaguzi unaoenda kui 'define' Tanzania kwa karne moja ijayo. Nchi hii iko katika njia panda, kuna hatma za aina mbili au tatu nchi inayoweza kuzifuata na yote hayo yanategemea mambo kadhaa. Ila ninachoweza kusema ni kuwa haijalishi nani atashinda kinyanganyiro cha Urais, haijalishi ni chama gani kitafanikiwa, jambo la muhimu kutambua ni kuwa huu uchaguzi ni 'referendum' ya sauti ya Mtanzania kutokana na hali ya nchi wanavyoiona.

Wakionyesha kwa sauti kuu kuwa hawajaridhishwa na muelekeo wa nchi hii itaonekana kuanzia katika kampeni hadi katika sanduku la kura na kama kutakuwa na mizengwe huko, wataionyesha kwa njia nyingine. Vivyo hivyo kama watataka waonyeshe kuwa wanaridhishwa na kila ambacho kimekuwa kinafanyika hasa katika nyanja zinazowagusa moja kwa moja, pia itaonekana.

Kwa msisitizo tu ni kuwa uchaguzi wowote wa kisiasa huwa unatoa fursa ya sauti na hoja ambazo huwa hazisikiki kusikika na kipimo cha uungwaji mkono wa hoja hizo huwa ni idadi ya kura, bila kujali kama wagombea wa sauti hizo wameshinda ama la. Hili jambo ndiyo linanifanya niamini kuwa uchaguzi huu si wa kawaida. Unaenda kuibadilisha Tanzania kwa namna ambayo wanahistoria wataikumbuka kwa sababu kuna hoja za msingi sana zinazolitambulisha ziko mezani huku kukiwa na mvutano mkali wa pande mbili zinazokinzana.

It is the best of times, it is the worst of times.
 
Baada ya uchaguzi wa 2015 CCM ingeweza kukaa miaka mingi Sana bila kupata upinzani mkubwa kama Magufuli angekuwa kiongozi mzuri.

Lkn kwa namna alivyoongoza nchi amegeuka kuwa kichocheo kikubwa Sana Cha upinzani usioweza kizuiwa kwa Sasa. Magufuli amewachefua Sana watu. Wamedhamiria kumpumzisha.
 
Baada ya uchaguzi wa 2015 CCM ingeweza kukaa miaka mingi Sana bila kupata upinzani mkubwa kama Magufuli angekuwa kiongozi mzuri.

Lkn kwa namna alivyoongoza nchi amegeuka kuwa kichocheo kikubwa Sana Cha upinzani usioweza kizuiwa kwa Sasa. Magufuli amewachefua Sana watu. Wamedhamiria kumpumzisha.

Na inshallah ATAPUMZISHWA come October 28, 2020!
Amen
 
CCM kuwa rasmi Chama cha upinzani Tanzania kuanzia October 2020. Chadema kuwa chama Tawala na kufanya reformations ambazo zitai define Tanzania kama nchi ya maendeleo kweli in the coming years. Hiki ndo ninachokiona mwaka huu
 
Ni kipindi sahihi cha kufanya mageuzi ya sera na mikakati ya kimaendeleo nchini. Mipango ya CCM ya kimaendeleo ipo taratibu sana na wanaitimiza katika njia ya kuwahadaa watanzania ili miaka na miaka waendelee kuitawala hii nchii.
Ni muda muafaka ambao wananchi wanataka kuona njia mbadara na mageuzi ya kisiasa. Na hili linawezekana, ni swala la wananchi kuamua
 
CCM kuwa rasmi Chama cha upinzani Tanzania kuanzia October 2020. Chadema kuwa chama Tawala na kufanya reformations ambazo zitai define Tanzania kama nchi ya maendeleo kweli in the coming years. Hiki ndo ninachokiona mwaka huu
Mawazo yangu na yako hayajapishana mkuu. Inahitajika reformation kubwa and true transition sio ya aeamu hii yakulishana data za uongo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom