Mikael Aweda
JF-Expert Member
- Dec 17, 2010
- 2,973
- 3,901
Naibu katibu mkuu Chadema, Naibu kiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni, mkiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirka ya Umma na Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe ndo mgeni rasmi atakayezindua kampeni ya Chadema kata ya Vjibweni Leo.
Wakati Zitto akisubiriwa kuzindua kampeni hizo leo mchana, atalazimika kukabiliana na hoja za ccm dhidi ya Chadema zilizotemwa na Abdulrahamani Kinana ambaye ndiye aliyezindua kampeni za Chama hicho jumatano wiki. Viongozi wa kata wameelekezwa kukusanya hoja hizo ambazo ataelezwa Zitto kabla hajasimama na kuzijibu zile zenye mantiki
ZITTO pia tumempangia kuongea na wazee wa vijiwen kabla hajahutubia. Utaratibu huu unaandaliwa na viogozi wa kata.
RAFU ZA CCM NI ZIPI?
Kwa mujibu wa ratiba ya NEC, kampeni zinaanza leo nchi nzima. Hata hivyo, Kinana aliweza kufanya mkutano mkubwa wa Hadhara na kumnadi mgombea wa CCM tangu jumatano wiki HII, kinyume na utaratibu uliowekwa na NEC.
Sisi tuliamua kukata rufaa kuhusu jambo hili. Cha kushangaza Mtendaji wa kata akasema kwamba hiyo ni ratiba ya vyama, kwa hiyo, haina tatizo.
Pili, akasema nikipokea barua yenu, ina maanisha kuwa na ninyi hamtazindua kampeni yenu ijumaa hadi rufaa itakapoamuliwa. Tulipewa hilo sharti gumu ambalo kwa kweli halina msinigi wo wote WALA MANTIKI.
Tulitafakari hilo, huku tukiwa hatuko tayari kuchelewesha kampeni, pili tunajua tunaweza tusimpate tena Zitto kwa sababu hatujui amepangiwa Kwenda wapi baada ya leo na CHAMA. Tukaamua kuachana na rufaa. Tulihisi wangeweza kujadili hiyo rufaa kwa wiki 2, kampeni ikawa wiki mmoja. CCM kila kitu kinawezekana.
Zitto PIA amepangiwa kuongea na wazee wa Vibweni kabla ya kuhutubia mchana wa Leo. utaratibu huu unaandaliwa na viongozi wa kata.
KATIKA HALI YA KUSHANGAZA.
Wiki iliyopita, sikumbuki tarehe, kulikuwa na masuala ambayo tulitaka ufafanuzi kutoka kwa msimamizi wa uchaguzi ambaye ndiye mtendaji wa Kata. Tulimpigia simu bila yeye kujua kwamba alipigiwa simu na nani na ana tatizo gani LA kiofisi? Akatuelekeza alipo. Tulimkuta yuko na vionogozi wa ccm kata ya vijibweni, Viongozi wa ccm ngazi ya wilaya na mfadhili wa ccm wa kata hiyo. Huyu mfadhili ni mhinidi aliyewekeza sana ktk fukwe za kata hiyo. Tukajiuliza, viongozi wa ccm, msimamizi wa uchaguzi na mfadhili wa ccm saa kumi mchana ndani ya Hotel wanakula au wanajadili nini? Mimi sitaki kuwa shehe Yahya, ila kuna utata.