Uchaguzi Urais, USA - 2020: Anavyopigwa Donald Trump (R) katika Ballot Box, ndivyo ambavyo alikuwa anapigwa John P. Magufuli (CCM)..

Mfanano wa chaguzi hizi mbili:
1. Wote, Donald Trump (Republican) na John Magufuli (CCM) ni incumbent presidents waliokuwa wanatetea nafasi zao..

2. Wote ni maRais wasema ovyo na wasiopenda kulaumiwa kwa makosa yao..

3. Wote ni wapenda sifa na wakati mwingine kutaka sana kupenda "kuabudiwa"..

4. Wote ni wapenda kusema uongo na kulazimisha watu waamini uongo wao...

Utofauti wao;
1. Rais Donald Trump anatawala chini ya mamlaka na taasisi zenye uhuru mkubwa wa kumdhibiti, hafurukuti hawezi kuzitumia kumpendelea. Magufuli Pombe, ndiye anayezitawala, kuzielekeza cha kufanya mamlaka na taasisi za udhibiti kama polisi, NEC nk. Anazilamisha kumpendelea yeye na kuwakandamiza wapinzani wake..

2. Rais Trump ndiye anahaha kutafuta haki mahakamani kwa kudhani kuwa kuna wizi wa kura dhidi yake. Kwa Magufuli, hilo halipo, halikuwepo.!!

Nini Kinaendelea sasa?
1. Rais Trump Donald anaelekea kupoteza Mamlaka ya Urais wake. Mpaka sasa mpinzani wake Joe Biden (D) anaongoza kwa kura (Electoral College) 264 huku counting ya kura kwenye baadhi ya majimbo ukiendelea, Joe Biden akiwa anaongoza ktk kura hizo zinazoendelea kuhesabiwa sasa..

2. Donald Trump haamini kinachoendelea. Haamini kuwa pamoja na "maendeleo ya vitu" aliyowaletea wamarekani, cha ajabu wanamkataa kwenye sanduku la kura. Hajui amewakosea nini...!!

Kwa nini hapa Tanzania, Magufuli (CCM) tumeambiwa "ameshinda?"
1. Kwa hakika, kama uchaguzi mkuu wa Tanzania 2020 ungefanyika ktk mazingira ya uwazi kama USA, Magufuli asingeshinda na angepigwa kama ambavyo mwenzake Trump ananyongwa mchana kweupe..!

2. Tanzania na Magufuli wa CCM ili kujipatia ushindi "wenye mashaka" makubwa, ilibidi afungulie "giza totoro" ili kuruhusu mifumo yake ya "kumshindisha" ifanye kazi..

3. Kufungwa kwa mtandao wa internet; kuzuia zaidi ya mawakala 57,000 wa vyama pinzani katika vituo vya kupigia zaidi ya 80,000 kuwakilisha wagombea wao ktk vituo vya kupigia kura; kukamata baadhi ya wagombea wa vyama pinzani na kuwaweka ndani (selo za polisi) kabla na siku ya uchaguzi yenyewe nk nk ni miongoni mwa mikakati ya kumpa ushindi "fake" Magufuli na CCM kwa ujumla...!
................................................

US - Updates Presidential Election results as at 21:00EAT
View attachment 1621656

Georgia State with 16 Electoral Colleges votes is under "votes recounting"..

Obviously, Joe Biden (D) atashinda...
Asante sana mkuu kwa ufafanuzi mzuri. Moja ya kitu kinatugharimu sana Tanzania ni woga wetu uliopitiliza mipaka, hasa kwa upande wa Tanzania Bara. itafika siku watu watachoka kutupigania na kutusemea!
 
..Donald Trump ni Amiri Jeshi dhaifu na bwege sijapata kuona.

..Inawezekana vipi Joe Biden afanye kampeni muda wote na hatujasikia hata mara moja amepigwa mabomu ya machozi, au kuswekwa mahabusu?

..Amiri Jeshi Mkuu gani asiyeweza kutumia DOLA kubaki madarakani?
Ile white house sio black house kama ya meko? Anajikuta yuko juuu ya sheria
 
Huwezi kushinda kwa kura mil 1 labda visiwa vya shelisheli ... sio Tanzania 🇹🇿 mnajaa mikutanoni kupiga kura hamuendi alafu mnalalamika mmeibiwa heri ya Lowasa kuliko huyu hata angekua anataka urais Dar asingeweza kupata kwa kura mil 1
 
Tufanye Ccm wameiba technically walikua wanaongeza kura za JPM labda alipata mil 5 wakaongeza 7 ... hawakua wanafuta waka kuchana za Lissu ... kwa kura mil 1 asingeweza kushinda hata asingeibiwa hata moja
 
Huwezi kushinda kwa kura mil 1 labda visiwa vya shelisheli ... sio Tanzania 🇹🇿 mnajaa mikutanoni kupiga kura hamuendi alafu mnalalamika mmeibiwa heri ya Lowasa kuliko huyu hata angekua anataka urais Dar asingeweza kupata kwa kura mil 1
Wacha ujinga mwamba,, kura zilizopigwa kwenye vituo vilivyozuia mawakala kuingia hazikuhesabiwa, walihesabu zilizokuwa kwenye mabegi! Mimi nilikuwa mmoja wa wasimamizi kwenye halmashauri moja!
 
Wacha ujinga mwamba,, kura zilizopigwa kwenye vituo vilivyozuia mawakala kuingia hazikuhesabiwa, walihesabu zilizokuwa kwenye mabegi! Mimi nilikuwa mmoja wa wasimamizi kwenye halmashauri moja!
Wewe kama msimamizi ulikua ni wajibu wako kuhakikisha taratibu na sheria zinafatwa ... huu ndio unafiki wa vijana MANYUMBU mnaangalia TUMBO na sio maslahi ya CHAMA ... snitch mkubwa kabisa
 
Biden; "Ni wakati wa kuacha kuwachukulia wapinzani wetu kama maadui"

"Nitawaunganisha wamarekani wote".
Qs44tWPw.jpg
 
Wewe kama msimamizi ulikua ni wajibu wako kuhakikisha taratibu na sheria zinafatwa ... huu ndio unafiki wa vijana MANYUMBU mnaangalia TUMBO na sio maslahi ya CHAMA ... snitch mkubwa kabisa
Kwa ufupi tumeona wazi kabisa CCM haipendwi na wananchi, tofauti kabisa na tunavyodanganywa!
 
26 Reactions
Reply
Back
Top Bottom