Uchaguzi 2020 Uchaguzi tarehe 28; CHADEMA inapoteza kila kitu

Aseme nini? Hakuna cha maana kasema pale zaidi ya porojo tu, Tambua kuwa hakuna mabaya yasiyo na mwisho na sasa CCM inafika mwisho wake Nchi inaenda kupata uhuru upya tokea chato kwa Mkoloni kaburu mweusi na ndipo utawala wa haki utaingia ikulu kuleta usawa maridhiano ya kitaifa
Duh kwa ID name yako ngoja ninyamaze, I may end up exchanging my food of thought with an unmatched one.
 
Hadi sasa Magufuli anaongoza kwa 85% ✓, .. endelea kupiga kura yako kabla ya tarehe 28 kupitia Piga Kura: Nani atashinda Urais Uchaguzi Mkuu 2020? View attachment 1610970View attachment 1610972View attachment 1610974View attachment 1610971View attachment 1610973View attachment 1610975View attachment 1610976
Screenshot_20201024-183641.jpg
 
Duh kwa ID name yako ngoja ninyamaze, I may end up exchanging my food of thought with an unmatched one.
Habari za mwisho wa CCM huwa tunazizikia kila mwaka wa uchaguzi, 1995, 2000, 2005, 2010, 2015 na leo 2020! Kwa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi, utendaji ulioboreshwa , imani ya wa Tanzania hakika tuvuka 2020 na kumpa JPM miaka 5 mingine!
 
Kuna watu humu wanajipa moyo eti CHADEMA hii ya Lissu, Mbowe, Mnyika, Heche, Halima, Bulaya Matiko na Wenzake wanaweza kuishinda CCM ya Magufuli, Bashiru Ali, Mangula, na mfumo mzima wa Chama Cha Mapinduzi.

Kama Kuna mtu anawaza hivo na anamanisha na ana amini Mawazo yake hayo yanaweza kuwa uhalisia, basi huyo ana tatizo kubwa sana kifikira.

Uchaguzi huu CDM iliyopalaganyika ikiwa inamtegemea mtu mmoja inakwenda kupambana na:
1. Rais Magufuli
2.Chama Cha Mapinduzi.
3.Watanzania

1.Rais Magufuli
Rais Magufuli tangu aingie Madarakani amekuwa akifanya baadhi ya Mambo ambayo yanakuwa reflected Kama ya kwake.Hali hii imemfanya pengine awe maarufu kuliko hata Chama chake. Magufuli amejijengea ufalme wake ndani ya mioyo ya Watanzania, siyo lazima akubalike na wote na hakuna anayetegemea iwe hivo, lakini ukweli umaarufu wake unamfanya yeye Kama yeye apate kura ambazo atapigiwa yeye Kama Magufuli, na nyingi ni zile za wasio na Chama.

Hizi kelele za mitandaoni dhidi ya JPM ukizifatilia ni za wale wale, hata thread humu ukiangalia wale wale ndio wanakoment, lakini waulize je Mama zao, Dada zao, wajomba zao, shangazi zao, Babu zao na Bibi zao wanaijua Facebook, wanaijua JF, wanaijua tweeter au Instagram. Jibu wanalo, je hoja ya Uhuru na maendeleo ya vitu inaeleweka kwa Hawa watu. Mtu ambaye hakuwahi kuona umeme( sizungumzii Maria Sarungi Wala Fatuma Katume, na Hawa hawafiki hata 5000) leo kauona umeme unaweza kumueleza asimchague Magufuli eti kwakuwa amemnyima Uhuru wakati anaenda kanisani, anapiga simu, anaenda sokoni anaenda shambani Bila wasiwasi akakuelewa?.

2. Chama Cha Mapinduzi
Dubwasha linalotisha, Dude hatari Barani Africa, dude ambalo Lina historia ya kuwaweka viongozi kadhaa wa Afrika Madarakani. Hili dude Lina vichwa, Lina Consultants, lina rasilimali watu na fedha za kutosha, Lina uzoefu wa kutosha katika anga hii ya siasa. Halafu Kuna mtu anawaza linaweza kushindwa na mtu anaitwa Tundu Lissu.

Hebu angalia muundo was CCM kuanzia hapo kwenye mtaa unaoishi, angalia kwa sasa kwenye eneo lako la nyumbani kumi muundo wa CCM, angalia WanaCCM hao katika muundo huo katika eneo Hilo la nyumba kumi walivyojipanga na wanavyoendelea kuzisanya kura kwa ajiri ya CCM. Sasa unaona, Kuna kura za Magufuli ambazo atazipata yeye na kura ambazo Chama Cha Mapinduzi kitazipata. Hali hii iliwahi kutokea mwaka 2005 ambapo Jakaya Mrisho Kikwete yeye Kama yeye alipigiwa kura na CCM nayo ikapata kura zilivyounganishwa mkwere akapiga 80%. Lakini 2010 watu wakawa hawana hamu naye, lakini Chama Cha Mapinduzi kikamtafutia kura. Akapiga 61% Kama sikosei, hizi zilikuwa za Chama.

Najua wengi mmejaa kwenye Social Media, hamupo field, hamuoni huo muundo ulivyo hatari. CDM is no where, katika level hizi, CDM ipo mgongoni kwa Lissu. Upande mwingine Kuna CCM Kuna Magufuli na Kuna CCM.

Sasa ukiangalia hali ilivo Sasa unaona kabisa atapigiwa parefu, lakini bahati mbaya hata upande wa Wabunge Mambo ni magumu mno. Majimbo ambayo siku za nyuma yalikuwa ni hoja isiyobishaniwa Sasa mwaka huu ni hoja nzito, Pale Mbeya Sugu amekamatwa Ke....nde, na Dr. Tulia, Lema ameshikwa Pu....bu, na Gambo, hapo Arusha, Mbowe jasho linatirtika hadi kwenye meno, Mzee wa Kondoo wa bwana anapumulia Kisogo Cha Halima. CDM ni Kama wapo kwenye furushi ambalo tarehe 28 linadondoka.

3. Watanzania
Sisi tunayo Kariba ambayo tumejengewa na Mzee Baba mwenyewe, Mchonga, Baba wa Taifa, Julius Kambarage Nyerere. Ni Kariba ambayo unaweza iita utakavyo kulinga a na muono wako, Njema sana, Mbaya, woga, au uungwana.

Watanzania tunapenda Amani Bila kujali gharama yake, Watanzania ni wavumilivu bila kujali gharama, Watanzania tunapenda uungwana sana, hatupendi Shari, lakini mbaya zaidi tunayo Imani Kali kuwa Mabeberu ni watu hatari, na watu wabaya sana. Lakini sisi ni wanafiki, Watanzania ukiwa na sisi tutakueleza hivi, ukitoka tunafanya tofauti, Tunakutanguliza halafu tunasikilizia, upepo ukibadilika tunaingia mitini!

Watanzania ukishaonyesha dalili za ushari, dalili za kuleta uvunjifu wa Amani au ukajinasibisha na Mababeru, au ukasingiziwa Mambo hayo, basi sisi Watanzania tunachofanya, tunakukwepa.

Tarehe 28 Watanzania bila kujali gharama, bila kujari Lissu anaahidi nini Watamkwepa, watajiepusha naye.
Msisahau hapa sijazungumzia swala la CCM kuwa Chama Dora!!

Nimevaa ngao🤣🤣🤣
Ivi kwa mfano wabunge waote wakawa CCM na madiwani wooote wakawa CCM wote nal Laisi akawa ccm nn kitatokea hapo bila upinzani???
 
Back
Top Bottom