Uchaguzi Serikali za Mitaa: Ni huzuni, aibu, fedheha na si afya kwa Chama cha Mapinduzi(CCM)

Ukiangalia mchakato mzima na mambo yaliyotokea kuhusiana na uchaguzi wa serikali za mitaa, ni wazi kwamba ushindi wa uchaguzi wa serikali za mitaa ni ushindi ambao mwanachama yeyote wa CCM mwenye akili timamu na busara atapaswa kuuonea aibu badala ya kuushangilia.Na hata zaidi, kuna maeneo ya uchaguzi ambayo ushindi huo unapaswa kukemewa na wanaCCM wenyewe kabla ya watu wengine.

Sasa swali la kujiuliza ni kwamba, kuna wanachama wangapi wa CCM ambao ni watu wenye akili timamu na busara? Sasa hilo litakuwa wazi matokeo ya uchaguzi yatakapotangazwa
 
Mkuu kwanza nikupongeze kwa mpangilio wako wa hoja, naomba niweke wazi bila kukipendelea chama changu ccm

Mosi mimi kama kiongoz wa chama ngazi ya kata naomba nikuwekee machache ambayo wenzetu walikosea na sisi tukaona gep na tukalitumia vizuri,
Viongoz wa ccm kabla ya kuchukua form tulikaa vikao na kuanza kuzipia kanuni ambazo tayali vyama vyote vilipewa, na baada tarehe ya form kufika wagombea wetu walichukua tukakaa kuwaelimisha namna ya ujazaji wahizo form kwa kupitia kipengere kimoja hadi kingine kwa umakin mkubwa,
Baada zoezi la kuchukua na kurudisha kuisha na zikabandikwa kwenye mbao tulienda pia ili kuangalia kama wenzetu walikidhi vigezo,
Nakili kabisa kua walicho kifanya wenzetu ni vituko. Form zao nyingi zilikua na kasoro na ndo maana tukawawekea mapingamizi
Ingawa pia kwetu yalikuwepo makosa madogo madogo, lkn Hayo yote wao hawakufuatilia
wewe maiti,hivi hujui kuwa wapinzani hawaruhusiwi kufanya mkusanyiko wowote either wa ndani au nje na je nani amewazuia?
 
Wapinzani hawakufuatilia ili kuwawekea pingamizi kama walivyo wenzao was ccm
Unamaanisha kinachotafutwa ni makosa ya kujaza form, na sio sera wala malengo ya mgombea? Vipi taasisi nyingine kama bank, NIDA, vyuo vya elimu nk. wakifuata mfumo mnaoutumia ninyi kuchuja waombaji?
 
1573223163589.png


Hahaha! I say hawa jamaa mapoyoyo kweli. Yaani mtu ambae hawezi hata kuandika kiswahili ndie wakamchukua ku assess form? Angalia badala ya kusema "kutoainisha" akasema "kutoiwaisha". Afadhali hata angesema kutoainisha!

Kwanza kutoiwaisnisha sehemu sahihi anakoishi ndio kiswahili gani? Inaonyesha uduni wa elimu ya huyu mtu - yaleyale ya watu wenye akili ndogo kupewa mamlaka makubwa!
 
Raha ya ushindi ni kushindana, lakini ushindi wa kupewa ama kubebwa hauna raha yeyote. Hi aibu ni ya kiwango cha lami.
 
Wewe kweli mwehu, kwahiyo watendaji kukimbia ofisi na yenyewe ilikuwa ni maelekezo ya kwenye form?
Eti tukaenda kuangalia, ulikwenda kuangalia kama nani?
Mnazidi kujitia uchizi tu, na kuwatia hasira wananchi. Haya mmeshinda jiapisheni basi.
Mkuu kwanza nikupongeze kwa mpangilio wako wa hoja, naomba niweke wazi bila kukipendelea chama changu ccm

Mosi mimi kama kiongoz wa chama ngazi ya kata naomba nikuwekee machache ambayo wenzetu walikosea na sisi tukaona gep na tukalitumia vizuri,
Viongoz wa ccm kabla ya kuchukua form tulikaa vikao na kuanza kuzipia kanuni ambazo tayali vyama vyote vilipewa, na baada tarehe ya form kufika wagombea wetu walichukua tukakaa kuwaelimisha namna ya ujazaji wahizo form kwa kupitia kipengere kimoja hadi kingine kwa umakin mkubwa,
Baada zoezi la kuchukua na kurudisha kuisha na zikabandikwa kwenye mbao tulienda pia ili kuangalia kama wenzetu walikidhi vigezo,
Nakili kabisa kua walicho kifanya wenzetu ni vituko. Form zao nyingi zilikua na kasoro na ndo maana tukawawekea mapingamizi
Ingawa pia kwetu yalikuwepo makosa madogo madogo, lkn Hayo yote wao hawakufuatilia
 
Mkuu kwanza nikupongeze kwa mpangilio wako wa hoja, naomba niweke wazi bila kukipendelea chama changu ccm

Mosi mimi kama kiongoz wa chama ngazi ya kata naomba nikuwekee machache ambayo wenzetu walikosea na sisi tukaona gep na tukalitumia vizuri,
Viongoz wa ccm kabla ya kuchukua form tulikaa vikao na kuanza kuzipia kanuni ambazo tayali vyama vyote vilipewa, na baada tarehe ya form kufika wagombea wetu walichukua tukakaa kuwaelimisha namna ya ujazaji wahizo form kwa kupitia kipengere kimoja hadi kingine kwa umakin mkubwa,
Baada zoezi la kuchukua na kurudisha kuisha na zikabandikwa kwenye mbao tulienda pia ili kuangalia kama wenzetu walikidhi vigezo,
Nakili kabisa kua walicho kifanya wenzetu ni vituko. Form zao nyingi zilikua na kasoro na ndo maana tukawawekea mapingamizi
Ingawa pia kwetu yalikuwepo makosa madogo madogo, lkn Hayo yote wao hawakufuatilia
Hivi kweli hata Wenyeviti waliomaliza muda wao hawajui kujaza fomu!? Kweli now ni mene mene na tekeli!
 
Dr. Bashiru aitoe CCM kwenye uchaguzi huu, ibaki CUF na T ELO P.
Bashiru pamoja na kuwepo kwenye chama chenye uchafu mwingi, anajitahidi kutotumbukia mzimankama alivyotumbukia Polepole.

Siamini kama Bashiru atakuwa alishiriki kwenye huu ujinga uliotokea. Kwa kiasi kikubwa hii ni mipango iliyomhusisha mwenyekiti, mwenezi, bashite na jafo.
 
Tamko la kimaslahi, mimi ni nwanachama hai wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) hivyo ni takayo yawasilisha hapa ni kwa manufaa ya ustawi wa chama changu CCM na Taifa letu kwa ujumla.

Nimefatilia kwa umakini mchakato mzima wa uchaguzi wa viongozi wetu katika ngazi ya Serika za Mitaa. Hakika kinachoendelea huko hakina afya na pia ni hatari zaidi kwa CCM. Binafsi naamini hizi vurugu mpaka kufikia hatua baadhi ya vyama kujitoa ni aibu kubwa katika utawala wa kidemokrasia ambao kimsingi CCM ndiye mwasisi wake.

CCM imekuwa ikijipambanua kama chama bora na zaidi ni kutokana na utendaji makini wa Rais Magufuli katika kipindi hiki cha awamu ya tano. Katika uongozi wa Rais wetu mambo mengi yamefanyika ambayo sina sababu ya kuyataja hapa. Hii ilikuwa karata tosha ya kutupa ushindi wa kishindo bila ya hofu wala figisufigisu zinazotokana na Watendaji wetu huku chini.

Kimsingi watendaji hawa wa Serikali chini ya TAMISEMI, tuseme ukweli wametutia aibu. Serikali iko uchi na chama changu chenye dhamana ya Serikali na mdau mkubwa wa uchaguzi huu pia kiko uchi

Ebu tujiulize maswali machache katika sintofahamu hii na mwisho ni malizie kwa ushauri.

A. TAMISEMI
1. Je, kwa kutumia mantiki (logic) ndogo tu, TAMISEMI inaamini idadi kubwa ya wagombea wa Upinzani walioenguliwa hawana sifa?

2. Je, nini sababu hasa ya Wagombea wengi wa upinzani kushindwa kujaza fomu zao kwa ukamilfu?

3. Iwapo fomu hizo zilikuwa na ugumu wa kuzijaza, ni kwanini TAMISEMI haikuona umuhimu wa kuwa na Semina elekezi kwa wagombea?

4. Kwakuwa wasimamizi wa uchaguzi wanasimamiwa na TAMISEMI kupitia Mkurugenzi wa Halmashauri ambaye ana maslahi uchaguzi huu, Je, msimamizi huyu wa chini anakwepaje kubinya haki?

5. Tukiacha uchaguzi huu uendelee bila kujali sintofahamu iliyopo, itakuwa ni kwa manufaa ya nani?

B. CHAMA CHA MAPINDUZI
1. Chama changu kitanufaika vipi na ushindi utaotokana na ukiukwaji wa wazi wa haki?

2. Hivi ni kweli uimara wa chama changu unatokana na ulegelege ama udhaifu wa vyama pinzani?

3. Kwanini chama changu kupitia Msemaji wetu tumekuwa na papara ya kuisemea TAMISEMI juu ya uchaguzi huu?

4. Je! Ni kweli tetesi zinazozagaa huku mtaani kuwa yanayotokea sasa yalipangwa makusudi na Chama Changu?

5. Je! Ni kweli kabisa Wagombea wetu ndani ya CCM wana weledi wa kutosha hivyo kufikia hatua ya kujaza fomu pasipo kukosea?

Iwapo tutaruhusu haya yaendelee, nina wasiwasi ushindi wa kishindo wa CCM katika uchaguzi huu utakuwa ni ushindi wa mkopo ambao bila shaka malipo yake yatakuwa ya gharama kubwa baadae. Chama bora kinapaswa kukuzwa katika ushindani usio na shaka. Hatuna sababu ya kujisifia kupitia njia mbovu zinazopangwa na kutekelezwa na watendaji wetu waliopo chini ili kupata sifa na kupendwa na Mamlaka teuzi.

Nasikitika kuwa ni bahati mbaya sana leo hii nchi imekosa wa kuisemea katika ngazi ya viongozi wetu wakuu wastaafu. Yanayoendelea leo, ingekuwa enzi za uhai wa Mwalimu Nyerere, angekuwa ameishatoka na kusema jambo. Mwalimu hakuwa mtu wa kusubiri maovu yatokee ndipo baadae aingilie. Sifa bora ya viongozi wote makini duniani ni kuwa pro-active, na hii ilikuwa sifa kuu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika enzi zote za uhai wake.

Hakika hatupaswi kutoa mwanya wa Chama changu CCM kushiriki uchaguzi wenye dosari kubwa namna hii. Kwa busara na kwa manufaa ya Nchi, nashauri viongozi wakuu wa Chama changu waishauri Serikali kuhairisha uchaguzi na kutatua kwanza dosari zilizopo kwa njia ya maridhiano kisha tusonge mbele tukiwa salama na wamoja. Hatuwezi kuligawa Taifa katika misingi yenye kunyima haki kwa manufaa ya muda mfupi ya kisiasa.

Nikipata wasaa, nitakuja kuelezea athari katika USTAWI WA CHAMA CHA MAPINDUZI kutokana na sintofahamu hii iwapo mamlaka zenye dhamana katika uchaguzi huu, zitakosa kabisa utashi wa kutatua na kuacha CCM itumbukie katika uchaguzi huu wa hovyo kabisa katika historia ya nchi yetu.
Unaonekana ni mtu mwenye kupenda kufuata misingi ya Haki. Naamini una elimu nzuri ndani yako.
Unanifanya niamini si ccm wote waliooza
 
Post bora kama hivi wale praise team wanazipita kama hawazioni na kikubwa zaidi na cha muhimu kabisa.. Umetanguliza maslahi yako wazi kabisa kuwa wewe si mpinzani ni mwana CCM
Tamko la kimaslahi, mimi ni nwanachama hai wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) hivyo ni takayo yawasilisha hapa ni kwa manufaa ya ustawi wa chama changu CCM na Taifa letu kwa ujumla.

Nimefatilia kwa umakini mchakato mzima wa uchaguzi wa viongozi wetu katika ngazi ya Serika za Mitaa. Hakika kinachoendelea huko hakina afya na pia ni hatari zaidi kwa CCM. Binafsi naamini hizi vurugu mpaka kufikia hatua baadhi ya vyama kujitoa ni aibu kubwa katika utawala wa kidemokrasia ambao kimsingi CCM ndiye mwasisi wake.

CCM imekuwa ikijipambanua kama chama bora na zaidi ni kutokana na utendaji makini wa Rais Magufuli katika kipindi hiki cha awamu ya tano. Katika uongozi wa Rais wetu mambo mengi yamefanyika ambayo sina sababu ya kuyataja hapa. Hii ilikuwa karata tosha ya kutupa ushindi wa kishindo bila ya hofu wala figisufigisu zinazotokana na Watendaji wetu huku chini.

Kimsingi watendaji hawa wa Serikali chini ya TAMISEMI, tuseme ukweli wametutia aibu. Serikali iko uchi na chama changu chenye dhamana ya Serikali na mdau mkubwa wa uchaguzi huu pia kiko uchi

Ebu tujiulize maswali machache katika sintofahamu hii na mwisho ni malizie kwa ushauri.

A. TAMISEMI
1. Je, kwa kutumia mantiki (logic) ndogo tu, TAMISEMI inaamini idadi kubwa ya wagombea wa Upinzani walioenguliwa hawana sifa?

2. Je, nini sababu hasa ya Wagombea wengi wa upinzani kushindwa kujaza fomu zao kwa ukamilfu?

3. Iwapo fomu hizo zilikuwa na ugumu wa kuzijaza, ni kwanini TAMISEMI haikuona umuhimu wa kuwa na Semina elekezi kwa wagombea?

4. Kwakuwa wasimamizi wa uchaguzi wanasimamiwa na TAMISEMI kupitia Mkurugenzi wa Halmashauri ambaye ana maslahi uchaguzi huu, Je, msimamizi huyu wa chini anakwepaje kubinya haki?

5. Tukiacha uchaguzi huu uendelee bila kujali sintofahamu iliyopo, itakuwa ni kwa manufaa ya nani?

B. CHAMA CHA MAPINDUZI
1. Chama changu kitanufaika vipi na ushindi utaotokana na ukiukwaji wa wazi wa haki?

2. Hivi ni kweli uimara wa chama changu unatokana na ulegelege ama udhaifu wa vyama pinzani?

3. Kwanini chama changu kupitia Msemaji wetu tumekuwa na papara ya kuisemea TAMISEMI juu ya uchaguzi huu?

4. Je! Ni kweli tetesi zinazozagaa huku mtaani kuwa yanayotokea sasa yalipangwa makusudi na Chama Changu?

5. Je! Ni kweli kabisa Wagombea wetu ndani ya CCM wana weledi wa kutosha hivyo kufikia hatua ya kujaza fomu pasipo kukosea?

Iwapo tutaruhusu haya yaendelee, nina wasiwasi ushindi wa kishindo wa CCM katika uchaguzi huu utakuwa ni ushindi wa mkopo ambao bila shaka malipo yake yatakuwa ya gharama kubwa baadae. Chama bora kinapaswa kukuzwa katika ushindani usio na shaka. Hatuna sababu ya kujisifia kupitia njia mbovu zinazopangwa na kutekelezwa na watendaji wetu waliopo chini ili kupata sifa na kupendwa na Mamlaka teuzi.

Nasikitika kuwa ni bahati mbaya sana leo hii nchi imekosa wa kuisemea katika ngazi ya viongozi wetu wakuu wastaafu. Yanayoendelea leo, ingekuwa enzi za uhai wa Mwalimu Nyerere, angekuwa ameishatoka na kusema jambo. Mwalimu hakuwa mtu wa kusubiri maovu yatokee ndipo baadae aingilie. Sifa bora ya viongozi wote makini duniani ni kuwa pro-active, na hii ilikuwa sifa kuu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika enzi zote za uhai wake.

Hakika hatupaswi kutoa mwanya wa Chama changu CCM kushiriki uchaguzi wenye dosari kubwa namna hii. Kwa busara na kwa manufaa ya Nchi, nashauri viongozi wakuu wa Chama changu waishauri Serikali kuhairisha uchaguzi na kutatua kwanza dosari zilizopo kwa njia ya maridhiano kisha tusonge mbele tukiwa salama na wamoja. Hatuwezi kuligawa Taifa katika misingi yenye kunyima haki kwa manufaa ya muda mfupi ya kisiasa.

Nikipata wasaa, nitakuja kuelezea athari katika USTAWI WA CHAMA CHA MAPINDUZI kutokana na sintofahamu hii iwapo mamlaka zenye dhamana katika uchaguzi huu, zitakosa kabisa utashi wa kutatua na kuacha CCM itumbukie katika uchaguzi huu wa hovyo kabisa katika historia ya nchi yetu.
 
Vijana wanao anza kuonja asli ndiyo chanzo kikubwa cha haya yanayo jiri leo. Busara na hekma za wazee zilitupwa kando saana. Wazee na washauri wote wameonekana kama hawana nafasi na walipo jaribu kushauri waliambiwa wakae kimya na haya ndiyo matokeo.
 
Mleta mada unapoitaka CCM yako iondoe dosari hujuwi kuwa unataka wamuondoe rais mahana ndiye dosari yenyewe. Magu ndiye mvurugaji mwandamizi wa chaguzi za marudio na wa serekali za mitaa.
 
Tamko la kimaslahi, mimi ni nwanachama hai wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) hivyo ni takayo yawasilisha hapa ni kwa manufaa ya ustawi wa chama changu CCM na Taifa letu kwa ujumla.

Nimefatilia kwa umakini mchakato mzima wa uchaguzi wa viongozi wetu katika ngazi ya Serika za Mitaa. Hakika kinachoendelea huko hakina afya na pia ni hatari zaidi kwa CCM. Binafsi naamini hizi vurugu mpaka kufikia hatua baadhi ya vyama kujitoa ni aibu kubwa katika utawala wa kidemokrasia ambao kimsingi CCM ndiye mwasisi wake.

CCM imekuwa ikijipambanua kama chama bora na zaidi ni kutokana na utendaji makini wa Rais Magufuli katika kipindi hiki cha awamu ya tano. Katika uongozi wa Rais wetu mambo mengi yamefanyika ambayo sina sababu ya kuyataja hapa. Hii ilikuwa karata tosha ya kutupa ushindi wa kishindo bila ya hofu wala figisufigisu zinazotokana na Watendaji wetu huku chini.

Kimsingi watendaji hawa wa Serikali chini ya TAMISEMI, tuseme ukweli wametutia aibu. Serikali iko uchi na chama changu chenye dhamana ya Serikali na mdau mkubwa wa uchaguzi huu pia kiko uchi

Ebu tujiulize maswali machache katika sintofahamu hii na mwisho ni malizie kwa ushauri.

A. TAMISEMI
1. Je, kwa kutumia mantiki (logic) ndogo tu, TAMISEMI inaamini idadi kubwa ya wagombea wa Upinzani walioenguliwa hawana sifa?

2. Je, nini sababu hasa ya Wagombea wengi wa upinzani kushindwa kujaza fomu zao kwa ukamilfu?

3. Iwapo fomu hizo zilikuwa na ugumu wa kuzijaza, ni kwanini TAMISEMI haikuona umuhimu wa kuwa na Semina elekezi kwa wagombea?

4. Kwakuwa wasimamizi wa uchaguzi wanasimamiwa na TAMISEMI kupitia Mkurugenzi wa Halmashauri ambaye ana maslahi uchaguzi huu, Je, msimamizi huyu wa chini anakwepaje kubinya haki?

5. Tukiacha uchaguzi huu uendelee bila kujali sintofahamu iliyopo, itakuwa ni kwa manufaa ya nani?

B. CHAMA CHA MAPINDUZI
1. Chama changu kitanufaika vipi na ushindi utaotokana na ukiukwaji wa wazi wa haki?

2. Hivi ni kweli uimara wa chama changu unatokana na ulegelege ama udhaifu wa vyama pinzani?

3. Kwanini chama changu kupitia Msemaji wetu tumekuwa na papara ya kuisemea TAMISEMI juu ya uchaguzi huu?

4. Je! Ni kweli tetesi zinazozagaa huku mtaani kuwa yanayotokea sasa yalipangwa makusudi na Chama Changu?

5. Je! Ni kweli kabisa Wagombea wetu ndani ya CCM wana weledi wa kutosha hivyo kufikia hatua ya kujaza fomu pasipo kukosea?

Iwapo tutaruhusu haya yaendelee, nina wasiwasi ushindi wa kishindo wa CCM katika uchaguzi huu utakuwa ni ushindi wa mkopo ambao bila shaka malipo yake yatakuwa ya gharama kubwa baadae. Chama bora kinapaswa kukuzwa katika ushindani usio na shaka. Hatuna sababu ya kujisifia kupitia njia mbovu zinazopangwa na kutekelezwa na watendaji wetu waliopo chini ili kupata sifa na kupendwa na Mamlaka teuzi.

Nasikitika kuwa ni bahati mbaya sana leo hii nchi imekosa wa kuisemea katika ngazi ya viongozi wetu wakuu wastaafu. Yanayoendelea leo, ingekuwa enzi za uhai wa Mwalimu Nyerere, angekuwa ameishatoka na kusema jambo. Mwalimu hakuwa mtu wa kusubiri maovu yatokee ndipo baadae aingilie. Sifa bora ya viongozi wote makini duniani ni kuwa pro-active, na hii ilikuwa sifa kuu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika enzi zote za uhai wake.

Hakika hatupaswi kutoa mwanya wa Chama changu CCM kushiriki uchaguzi wenye dosari kubwa namna hii. Kwa busara na kwa manufaa ya Nchi, nashauri viongozi wakuu wa Chama changu waishauri Serikali kuhairisha uchaguzi na kutatua kwanza dosari zilizopo kwa njia ya maridhiano kisha tusonge mbele tukiwa salama na wamoja. Hatuwezi kuligawa Taifa katika misingi yenye kunyima haki kwa manufaa ya muda mfupi ya kisiasa.

Nikipata wasaa, nitakuja kuelezea athari katika USTAWI WA CHAMA CHA MAPINDUZI kutokana na sintofahamu hii iwapo mamlaka zenye dhamana katika uchaguzi huu, zitakosa kabisa utashi wa kutatua na kuacha CCM itumbukie katika uchaguzi huu wa hovyo kabisa katika historia ya nchi yetu.
Unawaonea hao watendaji walikuwa wanatekeleza maagizo mahsusi
 
Back
Top Bottom