apolycaripto
JF-Expert Member
- Feb 11, 2011
- 644
- 225
Tamko la kimaslahi, mimi ni nwanachama hai wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) hivyo ni takayo yawasilisha hapa ni kwa manufaa ya ustawi wa chama changu CCM na Taifa letu kwa ujumla.
Nimefatilia kwa umakini mchakato mzima wa uchaguzi wa viongozi wetu katika ngazi ya Serika za Mitaa. Hakika kinachoendelea huko hakina afya na pia ni hatari zaidi kwa CCM. Binafsi naamini hizi vurugu mpaka kufikia hatua baadhi ya vyama kujitoa ni aibu kubwa katika utawala wa kidemokrasia ambao kimsingi CCM ndiye mwasisi wake.
CCM imekuwa ikijipambanua kama chama bora na zaidi ni kutokana na utendaji makini wa Rais Magufuli katika kipindi hiki cha awamu ya tano. Katika uongozi wa Rais wetu mambo mengi yamefanyika ambayo sina sababu ya kuyataja hapa. Hii ilikuwa karata tosha ya kutupa ushindi wa kishindo bila ya hofu wala figisufigisu zinazotokana na Watendaji wetu huku chini.
Kimsingi watendaji hawa wa Serikali chini ya TAMISEMI, tuseme ukweli wametutia aibu. Serikali iko uchi na chama changu chenye dhamana ya Serikali na mdau mkubwa wa uchaguzi huu pia kiko uchi
Ebu tujiulize maswali machache katika sintofahamu hii na mwisho ni malizie kwa ushauri.
A. TAMISEMI
1. Je, kwa kutumia mantiki (logic) ndogo tu, TAMISEMI inaamini idadi kubwa ya wagombea wa Upinzani walioenguliwa hawana sifa?
2. Je, nini sababu hasa ya Wagombea wengi wa upinzani kushindwa kujaza fomu zao kwa ukamilfu?
3. Iwapo fomu hizo zilikuwa na ugumu wa kuzijaza, ni kwanini TAMISEMI haikuona umuhimu wa kuwa na Semina elekezi kwa wagombea?
4. Kwakuwa wasimamizi wa uchaguzi wanasimamiwa na TAMISEMI kupitia Mkurugenzi wa Halmashauri ambaye ana maslahi uchaguzi huu, Je, msimamizi huyu wa chini anakwepaje kubinya haki?
5. Tukiacha uchaguzi huu uendelee bila kujali sintofahamu iliyopo, itakuwa ni kwa manufaa ya nani?
B. CHAMA CHA MAPINDUZI
1. Chama changu kitanufaika vipi na ushindi utaotokana na ukiukwaji wa wazi wa haki?
2. Hivi ni kweli uimara wa chama changu unatokana na ulegelege ama udhaifu wa vyama pinzani?
3. Kwanini chama changu kupitia Msemaji wetu tumekuwa na papara ya kuisemea TAMISEMI juu ya uchaguzi huu?
4. Je! Ni kweli tetesi zinazozagaa huku mtaani kuwa yanayotokea sasa yalipangwa makusudi na Chama Changu?
5. Je! Ni kweli kabisa Wagombea wetu ndani ya CCM wana weledi wa kutosha hivyo kufikia hatua ya kujaza fomu pasipo kukosea?
Iwapo tutaruhusu haya yaendelee, nina wasiwasi ushindi wa kishindo wa CCM katika uchaguzi huu utakuwa ni ushindi wa mkopo ambao bila shaka malipo yake yatakuwa ya gharama kubwa baadae. Chama bora kinapaswa kukuzwa katika ushindani usio na shaka. Hatuna sababu ya kujisifia kupitia njia mbovu zinazopangwa na kutekelezwa na watendaji wetu waliopo chini ili kupata sifa na kupendwa na Mamlaka teuzi.
Nasikitika kuwa ni bahati mbaya sana leo hii nchi imekosa wa kuisemea katika ngazi ya viongozi wetu wakuu wastaafu. Yanayoendelea leo, ingekuwa enzi za uhai wa Mwalimu Nyerere, angekuwa ameishatoka na kusema jambo. Mwalimu hakuwa mtu wa kusubiri maovu yatokee ndipo baadae aingilie. Sifa bora ya viongozi wote makini duniani ni kuwa pro-active, na hii ilikuwa sifa kuu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika enzi zote za uhai wake.
Hakika hatupaswi kutoa mwanya wa Chama changu CCM kushiriki uchaguzi wenye dosari kubwa namna hii. Kwa busara na kwa manufaa ya Nchi, nashauri viongozi wakuu wa Chama changu waishauri Serikali kuhairisha uchaguzi na kutatua kwanza dosari zilizopo kwa njia ya maridhiano kisha tusonge mbele tukiwa salama na wamoja. Hatuwezi kuligawa Taifa katika misingi yenye kunyima haki kwa manufaa ya muda mfupi ya kisiasa.
Nikipata wasaa, nitakuja kuelezea athari katika USTAWI WA CHAMA CHA MAPINDUZI kutokana na sintofahamu hii iwapo mamlaka zenye dhamana katika uchaguzi huu, zitakosa kabisa utashi wa kutatua na kuacha CCM itumbukie katika uchaguzi huu wa hovyo kabisa katika historia ya nchi yetu.
Nimefatilia kwa umakini mchakato mzima wa uchaguzi wa viongozi wetu katika ngazi ya Serika za Mitaa. Hakika kinachoendelea huko hakina afya na pia ni hatari zaidi kwa CCM. Binafsi naamini hizi vurugu mpaka kufikia hatua baadhi ya vyama kujitoa ni aibu kubwa katika utawala wa kidemokrasia ambao kimsingi CCM ndiye mwasisi wake.
CCM imekuwa ikijipambanua kama chama bora na zaidi ni kutokana na utendaji makini wa Rais Magufuli katika kipindi hiki cha awamu ya tano. Katika uongozi wa Rais wetu mambo mengi yamefanyika ambayo sina sababu ya kuyataja hapa. Hii ilikuwa karata tosha ya kutupa ushindi wa kishindo bila ya hofu wala figisufigisu zinazotokana na Watendaji wetu huku chini.
Kimsingi watendaji hawa wa Serikali chini ya TAMISEMI, tuseme ukweli wametutia aibu. Serikali iko uchi na chama changu chenye dhamana ya Serikali na mdau mkubwa wa uchaguzi huu pia kiko uchi
Ebu tujiulize maswali machache katika sintofahamu hii na mwisho ni malizie kwa ushauri.
A. TAMISEMI
1. Je, kwa kutumia mantiki (logic) ndogo tu, TAMISEMI inaamini idadi kubwa ya wagombea wa Upinzani walioenguliwa hawana sifa?
2. Je, nini sababu hasa ya Wagombea wengi wa upinzani kushindwa kujaza fomu zao kwa ukamilfu?
3. Iwapo fomu hizo zilikuwa na ugumu wa kuzijaza, ni kwanini TAMISEMI haikuona umuhimu wa kuwa na Semina elekezi kwa wagombea?
4. Kwakuwa wasimamizi wa uchaguzi wanasimamiwa na TAMISEMI kupitia Mkurugenzi wa Halmashauri ambaye ana maslahi uchaguzi huu, Je, msimamizi huyu wa chini anakwepaje kubinya haki?
5. Tukiacha uchaguzi huu uendelee bila kujali sintofahamu iliyopo, itakuwa ni kwa manufaa ya nani?
B. CHAMA CHA MAPINDUZI
1. Chama changu kitanufaika vipi na ushindi utaotokana na ukiukwaji wa wazi wa haki?
2. Hivi ni kweli uimara wa chama changu unatokana na ulegelege ama udhaifu wa vyama pinzani?
3. Kwanini chama changu kupitia Msemaji wetu tumekuwa na papara ya kuisemea TAMISEMI juu ya uchaguzi huu?
4. Je! Ni kweli tetesi zinazozagaa huku mtaani kuwa yanayotokea sasa yalipangwa makusudi na Chama Changu?
5. Je! Ni kweli kabisa Wagombea wetu ndani ya CCM wana weledi wa kutosha hivyo kufikia hatua ya kujaza fomu pasipo kukosea?
Iwapo tutaruhusu haya yaendelee, nina wasiwasi ushindi wa kishindo wa CCM katika uchaguzi huu utakuwa ni ushindi wa mkopo ambao bila shaka malipo yake yatakuwa ya gharama kubwa baadae. Chama bora kinapaswa kukuzwa katika ushindani usio na shaka. Hatuna sababu ya kujisifia kupitia njia mbovu zinazopangwa na kutekelezwa na watendaji wetu waliopo chini ili kupata sifa na kupendwa na Mamlaka teuzi.
Nasikitika kuwa ni bahati mbaya sana leo hii nchi imekosa wa kuisemea katika ngazi ya viongozi wetu wakuu wastaafu. Yanayoendelea leo, ingekuwa enzi za uhai wa Mwalimu Nyerere, angekuwa ameishatoka na kusema jambo. Mwalimu hakuwa mtu wa kusubiri maovu yatokee ndipo baadae aingilie. Sifa bora ya viongozi wote makini duniani ni kuwa pro-active, na hii ilikuwa sifa kuu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika enzi zote za uhai wake.
Hakika hatupaswi kutoa mwanya wa Chama changu CCM kushiriki uchaguzi wenye dosari kubwa namna hii. Kwa busara na kwa manufaa ya Nchi, nashauri viongozi wakuu wa Chama changu waishauri Serikali kuhairisha uchaguzi na kutatua kwanza dosari zilizopo kwa njia ya maridhiano kisha tusonge mbele tukiwa salama na wamoja. Hatuwezi kuligawa Taifa katika misingi yenye kunyima haki kwa manufaa ya muda mfupi ya kisiasa.
Nikipata wasaa, nitakuja kuelezea athari katika USTAWI WA CHAMA CHA MAPINDUZI kutokana na sintofahamu hii iwapo mamlaka zenye dhamana katika uchaguzi huu, zitakosa kabisa utashi wa kutatua na kuacha CCM itumbukie katika uchaguzi huu wa hovyo kabisa katika historia ya nchi yetu.