Uchaguzi 2020 Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge wa 2020 utakuwa ni wa kufariji na kuadhibu

maramia

JF-Expert Member
Jul 17, 2015
2,030
1,344
Kwa namna hali ilivyo na inavyoonekana uchaguzi mkuu wa Rais na Wabunge wa 28 Oktoba 2020 kwa namna unavyoonekana utakuwa ni uchaguzi ambao wapiga kura wataongozwa na mambo makubwa mawili wakati wa kupiga kura yao.

1. Kuna wapiga kura watakaopiga kura yao kwa chuki ya kuuadhibu utawala ulioko madarakani kutokana na uonevu na maovu waliyofanyiwa. Hawa ni wale;

√ waliotumbuliwa, kuachishwa na kufukuzwa kazi kwa uonevu.

√ wanaochukizwa na utungwaji wa sheria za kujipendelea na upendeleo kwa watawala. Wanaoona Kama sheria ya kinga ya viongozi ilikuwa njia ya kujihami kwa watakayofanya.

√ waliokutwa na majanga wakapuuzwa, wakakejeliwa na wakanyimwa misaada walliyochangiwa na watanzania ndugu zao.

√ wale waliojitolea kuwasaidia wahanga wa matukio na majanga mbali mbali lakini misaada yao haikuwafikia wale waliokusudiwa.

√ watumishi waliofukuzwa kazi au KUNYIMWA mishahara yao kwa sababu walienda kugombea uongozi katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, kitu ambacho hakijawahi kuwepo.

√ wafugaji waliouziwa mifugo yao kwa sababu mbali mbali na wakulima walionyang'anywa mazao au ambao walichukuliwa mazao yao lakini hawakulipwa.

√ waliobambikizwa kesi na kutakiwa kwenda kutubu kwa DPP walikolipa mamilioni na mabilioni ya fedha bila kufikishwa mahakamani.

√ ambao walikamatwa wakateswa, wakapotea na hata kuuawa na watu wanaoitwa "wasiojulikana"

√ kuna watanzania watakaopiga kura kama huruma na faraja kwa Tundu Lissu wanaomwona kama ni mtetezi wao aliyeonewa na kutaka kuuawa kwa sababu ya misimamo yake ya kutetea haki na uhuru wa watanzania na raslimali zao.

√ walionyimwa fursa ya kufanya siasa katika nchi yao wakati ni haki yao ya kidemokrasia.

Wahanga hao wote wanao makumi, mamia na maelfu ya jamaa, ndugu na watanzania chungu nzima nyuma yao ambao kura yao itakuwa ngumu sana kuitoa kwa CCM.
 
Kwa namna hali ilivyo na inavyoonekana uchaguzi mkuu wa Rais na Wabunge wa 28 Oktoba 2020 kwa namna unavyoonekana utakuwa ni uchaguzi ambao wapiga kura wataongozwa na mambo makubwa mawili wakati wa kupiga kura yao.

1. Kuna wapiga kura watakaopiga kura yao kwa chuki ya kuuadhibu utawala ulioko madarakani kutokana na uonevu na maovu waliyofanyiwa. Hawa ni wale;

√ waliotumbuliwa, kuachishwa na kufukuzwa kazi kwa uonevu.

√ wanaochukizwa na utungwaji wa sheria za kujipendelea na upendeleo kwa watawala. Wanaoona Kama sheria ya kinga ya viongozi ilikuwa njia ya kujihami kwa watakayofanya.

√ waliokutwa na majanga wakapuuzwa, wakakejeliwa na wakanyimwa misaada walliyochangiwa na watanzania ndugu zao.

√ wale waliojitolea kuwasaidia wahanga wa matukio na majanga mbali mbali lakini misaada yao haikuwafikia wale waliokusudiwa.

√ watumishi waliofukuzwa kazi au KUNYIMWA mishahara yao kwa sababu walienda kugombea uongozi katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, kitu ambacho hakijawahi kuwepo.

√ wafugaji waliouziwa mifugo yao kwa sababu mbali mbali na wakulima walionyang'anywa mazao au ambao walichukuliwa mazao yao lakini hawakulipwa.

√ waliobambikizwa kesi na kutakiwa kwenda kutubu kwa DPP walikolipa mamilioni na mabilioni ya fedha bila kufikishwa mahakamani.

√ ambao walikamatwa wakateswa, wakapotea na hata kuuawa na watu wanaoitwa "wasiojulikana"

√ kuna watanzania watakaopiga kura kama huruma na faraja kwa Tundu Lissu wanaomwona kama ni mtetezi wao aliyeonewa na kutaka kuuawa kwa sababu ya misimamo yake ya kutetea haki na uhuru wa watanzania na raslimali zao.

√ walionyimwa fursa ya kufanya siasa katika nchi yao wakati ni haki yao ya kidemokrasia.

Wahanga hao wote wanao makumi, mamia na maelfu ya jamaa, ndugu na watanzania chungu nzima nyuma yao ambao kura yao itakuwa ngumu sana kuitoa kwa CCM.
Umeandika hali halisi,lakini ngoja watetezi wa fly over waje
 
Naona Jambo la pili hujalimalizia ngoja nikusaidie;
Kuna watakaopiga kura ya ndio kutokana na;

a. Kuletewa huduma ya Afya karibu Yao

b.kuletewa huduma ya maji ya uhakika

c.kuletewa umeme vijini na mijin kwao.

d.nchi Yao kupandishwa Uchumi wa Kati.

e.Kuvushwa salama kwenye janga la Corona linaloendelea kutesa mataifa Mengine duniani.

f.kujengewa miradi mikubwa na yenye tija kwa Taifa lao hata vizazi na vizazi km vile SGR.

g. Elimu bure

h. Amani na utulivu katika makazi yao(hasa kukoma kwa uvamizi wa siraha).

I. Kulifanya Taifa lao kuwa na ndege zake zinazofanya safari za ndani na nje.

J. Heshima yao kama wanyonge na kufuta kauli za kipuuzi zilizokuwepo Kama "UNANIJUA KUWA MIMI NINAN? NITAKUFUNGA.

k. Kupunguzwa na kuthibitiwa kwa wimbi la rushwa na ufisadi katika nchi Yao.

L. Fly over na madaraja ya kisasa

m. Stand na masoko ya kisasa.

N. Uhuru wa biashara wa mama ntilie, machinga na wengine wote

Na Mengine mengi ambayo siwezi kuyamaliza kwa kuyataja kwenye bandiko langu maana yanaweza tengeneza Uzi kabisa na mimi sijaanzisha Uzi Bali nimechangia/nimekamilisha Uzi wako tu.
 
"claw back clause"
Maendeleo hayana chama ila HAKIKA chama kinafahamu strategy ya kuyafikia Maendeleo
 
Naona Jambo la pili hujalimalizia ngoja nikusaidie;
Kuna watakaopiga kura ya ndio kutokana na;

a. Kuletewa huduma ya Afya karibu Yao

b.kuletewa huduma ya maji ya uhakika

c.kuletewa umeme vijini na mijin kwao.

d.nchi Yao kupandishwa Uchumi wa Kati.

e.Kuvushwa salama kwenye janga la Corona linaloendelea kutesa mataifa Mengine duniani.

f.kujengewa miradi mikubwa na yenye tija kwa Taifa lao hata vizazi na vizazi km vile SGR.

g. Elimu bure

h. Amani na utulivu katika makazi yao(hasa kukoma kwa uvamizi wa siraha).

I. Kulifanya Taifa lao kuwa na ndege zake zinazofanya safari za ndani na nje.

J. Heshima yao kama wanyonge na kufuta kauli za kipuuzi zilizokuwepo Kama "UNANIJUA KUWA MIMI NINAN? NITAKUFUNGA.

k. Kupunguzwa na kuthibitiwa kwa wimbi la rushwa na ufisadi katika nchi Yao.

L. Fly over na madaraja ya kisasa

m. Stand na masoko ya kisasa.

N. Uhuru wa biashara wa mama ntilie, machinga na wengine wote

Na Mengine mengi ambayo siwezi kuyamaliza kwa kuyataja kwenye bandiko langu maana yanaweza tengeneza Uzi kabisa na mimi sijaanzisha Uzi Bali nimechangia/nimekamilisha Uzi wako tu.
Haya nayo ni kweli ila ukikosa tu uhuru wa kufanya siasa inayoleta hayo umeharibu kila kitu.
 
Kutokana na sifa zilizotolewa na Mr Tyang wapiga kura watakuwa wanakwenda kumchagua "boss" lakini kutokana na sifa zilizotolewa na Maramia wapigakura watakuwa wanakwenda kumchagua "leader"
tapatalk_1592626220087.jpeg
 
Yetu macho, mwaka huu tutashuhudia mengi sana, na kwakweli uchaguzi huu nadhani ni miongoni mwa chaguzi ngumu kuwahi kutokea.
 
Back
Top Bottom