Kikwete leo amefungua kikao cha NEC ya CCM kilichotanguliwa na Kamati Kuu na Kamati ya Usalama na Maadili. Amewaacha mdomo wazi akina Lowassa aliposema wamekata majina ya watu wengine japo wanazo sifa na wengine wamepungukiwa sifa kwa makusudi ili kujenga chama chenye ari mpya na vijana wengi wasomi ambao ndiyo future ya chama hicho. Aliwamaliza zaidi aliposema "tunaunda timu ya ushindi wa chama na si timu ya ushindi wa mtu." hapa kama ni kisu basi kimegonga mifupa ya akina Lowassa wakabaki midomo wazi nilikuwa nawatazama vizuri walivyokaa katika siti moja Lowassa, Sumaye na Kingunge huku wapambe wao akina Mgeja wakilia kupoteza nafasi. Tena Kikwete amewaeleza anajua mjadala wa kwa nini fulani kakatwa jina na mwingine yupo utakuwepo lakini chama kwanza na anayetishia kuondoka ccm kwa kukatwa jina atangulie mapema wanamtakia kila la kheri, anasema anashangazwa na mtu anapoanza kusema chama kibaya pale anapokosa fursa ya uongozi. Ritz upo? asubuhi niliona umeleta uzi wa kumsifu Lowassa.
"Bora mimi sijasema"Fitina
sijakusikia vizuri, unasema Kinana yumo kwenye kashfa ya kutorosha wanyama na kuingiza wageni wasiodhibitiwa na Idara ya Uhamiaji pale KIA? Au sijaelewa?
Hata mimi sijaona ni kivipi amemkatisha tamaa,JK anakula kotekote ili yeyote atakayeshinda asimbugudhi.JK will never be straight,si JK huyu tunayemfahamu.Hawezi kumgeuka EL moja kwa moja na wakati dili la Richmond lilikuwa lao wote na alijiuzulu kumnusuru.JK ni msanii msiingie mkenge,wapi magamba aliyomtuma Nape atoe siku 90?Hamna kitu hapo.
Kwani toka alipompigia kampeni ni kipi kimebadilika?RA ni woga wake tu,hata yeye angeweza kugoma,sema kunguru mwoga ukimbiza bawa lake.
Then switch off computer!!delete.... empty recycle bin
exit
Mkuu mimi watu wanafiki nawachukia kama wauwaji tu,JK ni mnafiki vibaya mno!Sasa kumbe EL alimshtukia?Ngoja tuone ni kivipi watamtimua EL kama wana ubavu huo,wataishia kutulia wanyolewe.Otherwise chama kitampasukia mikononi,uzuri wa unafiki ni kwamba una mwisho wake.Na mnafiki mara zote huumbuka kwasababu at the end hakuna anachokisimamia.Mkuu hata RA sio uoga alitumika kwa makubaliano ili kuwatisha wezake kina Vijisnti na EL waogope wamwage manyanga...lkn jamaa wakachanganya na za kwao
Hao vijana wanaondaliwa ni wepi, Nchemba? au Ngeleja? Au Adam Malima?
Mkuu hata RA sio uoga alitumika kwa makubaliano ili kuwatisha wezake kina Vijisnti na EL waogope wamwage manyanga...lkn jamaa wakachanganya na za kwao