Uchaguzi Mkuu 2025, NECTA ihesabu kura badala ya NEC

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,214
3,587
Ninapendekeza ili kuruhusu haki kutendeka kwenye matokeo ya kuhesabu kura katika chaguzi za nchi yetu, serikali ipeleke Bungeni kwa hati ya dharura kuomba mabadiliko ya sheria ili kuondoa jukumu la kuhesabu kura toka NEC na kuhamishia jukumu hilo NECTA na majukumu mengine ya uchaguzi hadi kutangaza matokeo yabaki kuwa chini ya NEC.

NECTA ambayo sasa hivi inaongoza Afrika kwa mfumo imara wa kuratibu mitihani inao uwezo wa kitaalam, kiufundi, kiusalama, kiteknolojia kuratibu uhesabuji wa kura bila dosari yoyote na bila kuingiliwa na mtu au mamlaka yoyote ile kama inavyofanya kwenye utungaji mitihani, usimamizi wake, usahihishaji wake, utoaji alama na utangazaji matokeo. NEC izuiliwe na sheria kuingilia zoezi la uhesabuji kura utakaofanywa na NECTA na ikiwezekana hata matokeo yatangazwe na NEC kwenye uwepo wa NECTA kama shahidi. Chaguzi za ndani ya vyama pia zinaweza kufanyika kwa mfumo huu wa uhesabuji kura ili kupata wagombea wenye sifa ambao hawatokani na matokeo ya kuhesabu kura zilizohujumiwa.

1638695315483.png

Kura zikihesabiwa kwa mikono. Taswira kwa hisani ya google.
 
Ingekuwa ccm ina ushawishi kwa umma haya mapendekezo yako yangekubaliwa. Lakini ccm hii inayaoona aibu na fedheha ya kushindwa haiwezi kukubali. Machafuko pekee ndio njia iliyobaki ya kuwatoa ccm madarakani.
 
Ingekuwa ccm ina ushawishi kwa umma haya mapendekezo yako yangekubaliwa. Lakini ccm hii inayaoona aibu na fedheha ya kushindwa haiwezi kukubali. Machafuko pekee ndio iliyobaki ya kuwatoa ccm.
Duh! Mkuu umefumua mshono. Huo ujumbe wako na signature yako vinamfikirisha mtu mambo mawili:-
1. Kuomba passport kwa dharura.
2. Kurejesha kadi ya uanachama.
 
Shule ulisoma ujinga hujui sheria za kuanzishwa kwa taasisi hizo

USSR
 
Shule ulisoma ujinga hujui sheria za kuanzishwa kwa taasisi hizo

USSR
Mkuu, wewe hiyo shule yako ulifundishwa kuwa duniani kuna sheria ambayo ni Msahafu (haibadiliki). Zamani BVR zilipingwa duniani hasa Afrika zisitumike kwenye mchakato wa uchaguzi, kukawa na chagizo kwa baadhi ya nchi ili zirekebishe sheria ili BVR zitambulike rasmi kisheria. Pole sana mkuu wangu, kumbe hujapona kifafa cha mimba yako!
 
Tunataka katiba mpya itakayozaa time huru aya Mambo ya kuungaunga hatutaki ,uko Necta linapokuja swala la uchaguzi ni pabovu kuliko Nec iliyopo ,huko wale wa suti nyeusi, na wale wa PGO Ndo hujazana kule ,

Lakini pia NECTA ipo chin ya wizara ya Elim, ambayo ni serikali yenyewe bado, hii ni sawa kuluka mkojo na kukanyaga kinyesi,

Wazo lako nalipinga KWa asilimia 200
 
Kwahiyo, unashauri NEC (inayotumia walimu kuhesabu kura) iondolewe iwekwe NECTA ( inayotumia walimu) kuhesabu kura. Ahahahahahaha! Walimu waendelee kuenziwa Tanzania maana sifa zote nzuri za utendaji mzuri wa NECTA ni walimu hao hao!
 
Tunataka katiba mpya itakayozaa time huru aya Mambo ya kuungaunga hatutaki ,uko Necta linapokuja swala la uchaguzi ni pabovu kuliko Nec iliyopo ,huko wale wa suti nyeusi, na wale wa PGO Ndo hujazana kule ,

Lakini pia NECTA ipo chin ya wizara ya Elim, ambayo ni serikali yenyewe bado, hii ni sawa kuluka mkojo na kukanyaga kinyesi,

Wazo lako nalipinga KWa asilimia 200
Siyo lazima NECTA ikahesabu kura, ila NEC inaweza kutumia mfumo wa NECTA kuhesabu kura. Walimu wako humu JF, wanaweza kuwa mashahidi wazuri wa umahiri na usalama wa mfumo wa NECTA kuliko mfumo wa NEC. Ni bahati nzuri kwamba Walimu ni rasilimaliwatu wanaoshiriki kwenye operesheni za taasisi zote hizi za NECTA na NEC. Naamini kiasi kikubwa tutakuwa tumejinasua na mifumo binafsi isiyo rasmi ya kudukuwa hesabu za kura kwenye vituo vya siri-kali (vya kujumulisha matokeo) na kupotosha matokeo ya mwisho.
 
Walim nao wezi wa kula KWani hujui,kwenye kura wezi Kama wezi wengi alafu KILA siku ndo wakulalamika na kuangushiwa jumba bovu,

TUNATAKA TUME ISUKWE NA KUANZA UPYAAAA, alisema Mbunge Bwege
 
Ingekuwa ccm ina ushawishi kwa umma haya mapendekezo yako yangekubaliwa. Lakini ccm hii inayaoona aibu na fedheha ya kushindwa haiwezi kukubali. Machafuko pekee ndio njia iliyobaki ya kuwatoa ccm madarakani.
asante umeniuunga mkono.

kamwe na katu sisiemu haitokuja kutoka madarakani mpka machafuko na d@mu pekee

ila tuombe MUNGU atunusuru na haya

Sisiem oyeee
 
Sio lazima damu imwagike, ila machafuko kwamba hawatakiwi ndio watajua wamefika mwisho.
e umeniuunga mkono.

kamwe na katu sisiemu haitokuja kutoka madarakani mpka machafuko na d@mu pekee

ila tuombe MUNGU atunusuru na haya

Sisiem oyeee
 
asante umeniuunga mkono.

kamwe na katu sisiemu haitokuja kutoka madarakani mpka machafuko na d@mu pekee

ila tuombe MUNGU atunusuru na haya

Sisiem oyeee

Halafu sina popote ninapokuunga mkono kwenye umwagaji damu, usitake kunichomekea ushetani wako. Kawatafute wa hivyo uwalishe maneno. Kama umeagiziwa waambie huwa sichomekewi hizo.
 
NECTA hii hii ambayo mifumo yake kwa nyakati zaidi ya 10+ imekuwa ikikosea katika upangaji na ugawaji madaraja kwa majina yenye asili ya Mashariki ya Kati na Asia hadi Waziri wa wizara iliyo na uratibu NECTA kuthibitisha?
 
Back
Top Bottom