Uchaguzi Mkuu 2020: Msimu mwingine wa ulaji kwa waganga washirikina

HORSE POWER

JF-Expert Member
Feb 22, 2015
2,067
1,386
Habari zenu wanaJF,

Kama ilivyo ada kwa mujibu wa Katiba yetu, mwaka huu pia kutakua na Uchaguzi Mkuu hapo mwezi Octoba.Ni fursa kwa wananchi kuchagua Rais, Wabunge na Madiwani.Ni katka harakati hizi za kusaka 'uheshimiwa' tutashuhudia minyukano, kejeli, matusi, vitisho n.k.

Lakini pia tutashuhudia pia wale wanasiasa wachovu na wasio jiamini wakigawa rushwa kama peremende hasa majimboni na katani.Wapo watakaohonga khanga, vitenge, ubwabwa, tshirt n.k.Lakini kuna wale watakaoenda mbali zaidi hapo.

Hawa watajiongeza maradufu maana wataona Mwenyezi Mungu hatoshi kuwafanikishia malengo yao hivyo watahamia kwa 'waona mbali' ili mambo yawe mepesi.

Wanasiasa hawa waliofilisika sera, hoja, maono na ushawishi, matumaini yao watayahamishia kwa hawa 'waona mbali' ambao wengi wao ni waganga washirikina.Huko tena makafara ya ajabu ajabu yatafanyika na mahela yatatapanywa.

Yatapishana mashangingi huko kutafuta madaraka na ulaji.Kwa hakika ni msimu mnono na kabambe kwa hawa waganga washirikina...!!

"Na atakayemfanya shetani ndiye kiongozimsaidizi wake, hakika amepata hasara iliyokuwa wazi."

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Makanisani na misikitini Sasa wataanza kuonekana wako wale ambao miaka yote toka wachaguliwe hawajawahi onekana kanisani Wala msikitini Sasa hivi wataonekana
 
Tumuombe Mungu atuepushe na mabalaa yote katika kipindi hiki. Kila mtu kwa imani yake, popote alipo aombe. Tume ya uchaguzi na idara zote husika zitende kazi kwa mujibu wa sheria za uchaguzi na haki kuliepusha taifa kutumbukia katika machafuko tokana na baadhi ya wananchi kuhisi kudhulumiwa , AMINA 🙏
 
Matukio ya Albino kukatwa mikono na kupotea yataanza
Na maajali ya ajabu ajabu ya makafara na watu kufiwa kwa kafara za wazazi na watoto au ndugu wa karibu wa waheshimiiwa kutaanza !!!!

Maeneo.kama mlingotini bagamoyo kutafurika waheshimiiwa wageni

Barabara za kuelekea bagamoyo Kutakuwa na foleni
 
Na maajali ya ajabu ajabu ya makafara na watu kufiwa kwa kafara za wazazi na watoto au ndugu wa karibu wa waheshimiiwa kutaanza !!!!

Maeneo.kama mlingotini bagamoyo kutafurika waheshimiiwa wageni

Barabara za kuelekea bagamoyo Kutakuwa na foleni
Acha tu maisha ya mifugo yako hatari ni, kuku, mbuzi, kondoo na ng’ombe
 
Acha tu maisha ya mifugo yako hatari ni, kuku, mbuzi, kondoo na ng’ombe
Soko la kuku ,mbuzi,kondoo kwa ajili ya kafara litapanda

Tutaona njia panda nyingi zikiwa na vitu vya ajabu ajabu na ajali za ajabu ajabu

Serikali iweke kamera kwenye njia panda zote za barabara kuwanulika Hawa wawangaji wa kisiasa usiku na watoa makafara njia panda.

Pale salender bridge mataa patakuwa na wageni wengi usiku.Watu huwanga usiku pale mataa hawajali Wakati kituo Cha polisi Kiko hatua kumi tu toka wanapowangia.Pilika pilika zitakuwa nyingi Sana pale
 
Back
Top Bottom