PMNBuko
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 967
- 154
Waungwana wanaJF, naomba nioneshe msimamo wangu kuwa mimi ni CHADEMA damudamu, lakini kuna mambo mawili nataka niwashirikishe.
1. Wakati naangalia kipindi cha Bunge Juzi jioni niliona namna wabunge wetu wa CHADEMA wanavyopata taabu kupitisha hoja kutokana na uchache wao bungeni. Wana CCM, wabunge wanapitisha maamuzi kwa kusema NDIYOOOOOOOOOOOOOOOOOOO kubwa lakini za kinafiki huku hata waliolala huamshwa na kusema NDIYOOOOO!! Huu ni upuuzi. Lazima tuwe na idadi kubwa bungeni ili waseme NDIYOOOOOOOOOO na kushinda CCM.
2. Kutokuwepo nia ya dhati ya serikali kutoa fursa kwa vyama vya upinzani kuwa na demokrasia ya kweli katika shughuli za wanasiasa za ndani na nje ya bunge. Wabunge wetu wanadhalilishwa kwa kupindisha sheria za nchi. Idadi kubwa ya wabunge itaifanya serikali kukubaliana na maamuzi yao maana ndio watakuwa na sauti kubwa bungeni.
WanaJF, mnasemaje hapo?? Naomba michango yenu kwa kuzingatia hali halisi inavyoendelea Bungeni.
1. Wakati naangalia kipindi cha Bunge Juzi jioni niliona namna wabunge wetu wa CHADEMA wanavyopata taabu kupitisha hoja kutokana na uchache wao bungeni. Wana CCM, wabunge wanapitisha maamuzi kwa kusema NDIYOOOOOOOOOOOOOOOOOOO kubwa lakini za kinafiki huku hata waliolala huamshwa na kusema NDIYOOOOO!! Huu ni upuuzi. Lazima tuwe na idadi kubwa bungeni ili waseme NDIYOOOOOOOOOO na kushinda CCM.
2. Kutokuwepo nia ya dhati ya serikali kutoa fursa kwa vyama vya upinzani kuwa na demokrasia ya kweli katika shughuli za wanasiasa za ndani na nje ya bunge. Wabunge wetu wanadhalilishwa kwa kupindisha sheria za nchi. Idadi kubwa ya wabunge itaifanya serikali kukubaliana na maamuzi yao maana ndio watakuwa na sauti kubwa bungeni.
WanaJF, mnasemaje hapo?? Naomba michango yenu kwa kuzingatia hali halisi inavyoendelea Bungeni.