Uchaguzi mkuu 2010 kuvurugika

KakaNanii

JF-Expert Member
Sep 28, 2008
325
52
Yaani huwezi amini. Zikiwa zimebaki siku 5 tu kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA bado hawajafahamika mpaka sasa.

Mimi nipo katika mkoa wa Dar es salaam. Na nimefuatilia kwa karibu sana zoezi hili la kuchagua wasimamizi wa vituo vya kupigia kura. Lakini nimeona kuna ujanja mkubwa unafanywa ili kuingiza wasimamizi ambao kwa namna moja au nyingine watapendelea chama tawala.


Ukienda kwa mkurugenzi wa manispaa iwe ya Temeke, Kinondoni hata Ilala. Ukaulizia majina ya Wasimamizi wa vituo vya kupigia kura atakwambia , majina hayo yameshapelekwa katika Kata husika. Ukienda kwenye kata yako nao wanakwambia hatujaletewa bado hayo majina ya Wasimamizi wa vituo vya kupigia kura kutoka kwa mkurugenzi .

Lakini katika pita pita zangu mitaani nimepata taarifa kwamba tayari hayo majina yameshatoka na watu sasa hivi wapo kwenye semina za namna ya kusimamia vituo vya kupigia kura na namna ya kuiba kura.

Kama unabisha nenda sasa kwa ama mkurugenzi wa manispaaa husika au kwenye kata yako waulizie hayo majina wameyabandika wapi uone kama watakupa.

Huku viongozi wetu wa siasa wakiwa wamejikita katika kufanya kampeni tu, wakifikiri ndo watashinda , lakini hiyo ni kama kujaza maji kwenye tenga. Maana wenzenu chama tawala mwaka huu wa 2010 watatumia Wasimamizi wa vituo vya kupigia kura katika KUCHAKACHUA matokeo ya uchaguzi. Hivyo vyama vya upinzani "kalaga baho" na kubobea katika kupiga kampeni tu, wakati mchakato mzima wa kuwapata Wasimamizi wa Vituo vya Kupigia Kura unafanywa katika misingi ya KUCHAKACHUA matokeo !!!!

Mwisho ningependa kusema kwamba Zoezi zima la kuwapata WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA mwaka huu katika jiji la Dar es salaam limejaa UFISADI MTUPU !!!

MUNGU IBARIKI DAR ES SALAAM !!!
 
Yaani huwezi amini. Zikiwa zimebaki siku 5 tu kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA bado hawajafahamika mpaka sasa.

Mimi nipo katika mkoa wa Dar es salaam. Na nimefuatilia kwa karibu sana zoezi hili la kuchagua wasimamizi wa vituo vya kupigia kura. Lakini nimeona kuna ujanja mkubwa unafanywa ili kuingiza wasimamizi ambao kwa namna moja au nyingine watapendelea chama tawala.


Ukienda kwa mkurugenzi wa manispaa iwe ya Temeke, Kinondoni hata Ilala. Ukaulizia majina ya Wasimamizi wa vituo vya kupigia kura atakwambia , majina hayo yameshapelekwa katika Kata husika. Ukienda kwenye kata yako nao wanakwambia hatujaletewa bado hayo majina ya Wasimamizi wa vituo vya kupigia kura kutoka kwa mkurugenzi .

Lakini katika pita pita zangu mitaani nimepata taarifa kwamba tayari hayo majina yameshatoka na watu sasa hivi wapo kwenye semina za namna ya kusimamia vituo vya kupigia kura na namna ya kuiba kura.

Kama unabisha nenda sasa kwa ama mkurugenzi wa manispaaa husika au kwenye kata yako waulizie hayo majina wameyabandika wapi uone kama watakupa.

Huku viongozi wetu wa siasa wakiwa wamejikita katika kufanya kampeni tu, wakifikiri ndo watashinda , lakini hiyo ni kama kujaza maji kwenye tenga. Maana wenzenu chama tawala mwaka huu wa 2010 watatumia Wasimamizi wa vituo vya kupigia kura katika KUCHAKACHUA matokeo ya uchaguzi. Hivyo vyama vya upinzani "kalaga baho" na kubobea katika kupiga kampeni tu, wakati mchakato mzima wa kuwapata Wasimamizi wa Vituo vya Kupigia Kura unafanywa katika misingi ya KUCHAKACHUA matokeo !!!!

Mwisho ningependa kusema kwamba Zoezi zima la kuwapata WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA mwaka huu katika jiji la Dar es salaam limejaa UFISADI MTUPU !!!

MUNGU IBARIKI DAR ES SALAAM !!!

Mkuu naamini maneno yako, habari nilizozipata ambazo sio rasmi zinasema kuwa waendaji wa TISS wamemwagwa nchi nzima na ndio watakuwa wasimamizi wa vituo vya kupigia kura. Habari zinaendelea kusema kuwa hii imetokana na ccm kugundua kuwa baadhi ya maofisa wa ngazi za juu TISS wamewasaliti na kusaidia upinzani, hivyo wameagiza vijana wasambazwe. Siuji kitatokea nini lakini mawakala wa vyama vya upinzani kaeni chinjo, saa mbaya yaja.
 
Mkuu naamini maneno yako, habari nilizozipata ambazo sio rasmi zinasema kuwa waendaji wa TISS wamemwagwa nchi nzima na ndio watakuwa wasimamizi wa vituo vya kupigia kura. Habari zinaendelea kusema kuwa hii imetokana na ccm kugundua kuwa baadhi ya maofisa wa ngazi za juu TISS wamewasaliti na kusaidia upinzani, hivyo wameagiza vijana wasambazwe. Siuji kitatokea nini lakini mawakala wa vyama vya upinzani kaeni chinjo, saa mbaya yaja.

Tuweke wazi ndugu yangu usiiogope sisiemu hiyo TISS ndo nini hiyo ???
 
mkuu naamini maneno yako, habari nilizozipata ambazo sio rasmi zinasema kuwa waendaji wa tiss wamemwagwa nchi nzima na ndio watakuwa wasimamizi wa vituo vya kupigia kura. Habari zinaendelea kusema kuwa hii imetokana na ccm kugundua kuwa baadhi ya maofisa wa ngazi za juu tiss wamewasaliti na kusaidia upinzani, hivyo wameagiza vijana wasambazwe. Siuji kitatokea nini lakini mawakala wa vyama vya upinzani kaeni chinjo, saa mbaya yaja.

kwanini muwe na wasiwasi hali mgombea wenu slaa alishasema kuwa nusu ya usalama wa taifa huripoti kwake?
Ama kweli mfa maji heshi kutapatapa na mwaka huu ndio mwisho wa chadema na sijui zile milioni 12 alizoahidiwa slaa kulipwa kila mwezi sijui zitatoka wapi!!!!
 
kwanini muwe na wasiwasi hali mgombea wenu slaa alishasema kuwa nusu ya usalama wa taifa huripoti kwake?
Ama kweli mfa maji heshi kutapatapa na mwaka huu ndio mwisho wa chadema na sijui zile milioni 12 alizoahidiwa slaa kulipwa kila mwezi sijui zitatoka wapi!!!!
Tunamchangia na tutaendelea kumchangia, Tena umenikumbusha jana sikumchangia. Endelea na maswali, upo Zubedaaa???
 
kuna mtu alisema humu kuwa ccm inategema kuweka mawakala wake na kununua mawakala wa chadema......


ni kweli bana hii kitu imefichwa sana
 
kwanini muwe na wasiwasi hali mgombea wenu slaa alishasema kuwa nusu ya usalama wa taifa huripoti kwake?
Ama kweli mfa maji heshi kutapatapa na mwaka huu ndio mwisho wa chadema na sijui zile milioni 12 alizoahidiwa slaa kulipwa kila mwezi sijui zitatoka wapi!!!!

Watch out. Si uchangiaji wenye tija. Ungetujuvya ukweli au uongo wa thread. Halafu unajikanganya kwenye kauli zako. Hili sio jamvi la mambumbu.
 
sasa hao vijana sio Watanzania jamani???? yaani wao hawaoni Taifa letu linavyokwenda mrama???? NAAMINI KABISA SEMINA WATAPEWA LAKINI MUNGU ATATUSIMAMIA - WATAKOSA UJASIRI WA KUIBA HIZO KURA

Naamini hata wao wanahitaji MABADILIKO; hata WAO WAMEICHOKA CCM, CHAMA KISICHO NA SERA BALI CHENYE AHADI HEWA

Mungu ibariki siku ya uchaguzi Tanzania - iwe ya HAKI, AMANI NA UTULIVU - tupate matokeo yetu mazuri ya KURA NYINGI KWA DR. SLAA
 
Ee Mwenyezi Mungu, Ninawaombea wale wote walio na nia ya kuiba au kuchakachua kura kwa namna yeyote ile ili kutowapa watu walio wengi kiongozi wanayemtaka waamke jpili wakiwa na ugonjwa wa kuhara, kila baada ya dakika mbili watakiwe kwenda ****** ili wasipate muda wa kufanya ufedhuli wao... Amen
 
Wewe unawatafuta wanini hawa wasimamizi?

swali zuri sana...waache wasimamizi wakila chama wafichwe..wakitajwa ndio watasumbuliwa(kwa vitisho) na vyombo vya dola, ni bora wasifahamike mpaka siku ya mwisho wafanye kazi yao vizuri.....ila ni wajibu wa kila chama kuhakikisha wasimamizi wao wapo kwenye vituo vyao , ila kwa sasa majina ya baki na wahusika tu!
 
sasa hao vijana sio Watanzania jamani???? yaani wao hawaoni Taifa letu linavyokwenda mrama???? NAAMINI KABISA SEMINA WATAPEWA LAKINI MUNGU ATATUSIMAMIA - WATAKOSA UJASIRI WA KUIBA HIZO KURA

Naamini hata wao wanahitaji MABADILIKO; hata WAO WAMEICHOKA CCM, CHAMA KISICHO NA SERA BALI CHENYE AHADI HEWA

Mungu ibariki siku ya uchaguzi Tanzania - iwe ya HAKI, AMANI NA UTULIVU - tupate matokeo yetu mazuri ya KURA NYINGI KWA DR. SLAA


wee waache laana iwapate maana KILA ATAKAYE IBA KURA AU KUHUJUMA HAKI ZA WANANCHI MWAKA HUU HAKIKA ATAKUFA...... HUU NI UFUNUO MZEE MEMBE MHESHIMIWA WA KUCHAKACHUA WEWE NA KIZAZI CHAKO HATA KIZAZI CHA NNE KAA CHONJO............
 
Wenzenu wako busy on the ground kwa kampeni ya nguvu,kuwatafuta vijana na wanawake na kuwahamasisha wakapige kura, mnalia kuibiwa kura na uchaguzi kuvurugika mapema. Consipiracy theories za nini kama kutafuta sababu za kushindwa?
 
Mwisho ningependa kusema kwamba Zoezi zima la kuwapata WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA mwaka huu katika jiji la Dar es salaam limejaa UFISADI MTUPU !!!

Uchaguzi huu ni wakung'oa ufisadi kila mahali.........mawakala safi na sisi wapigakura mita 100 nje ya vituo vya kupigia kura......mchezo umekwisha hapo.
 
Hata kama wasipotoa nafasi ya kusimamia uchaguzi kwa wanaharakati, yao ngumu mwaka huu. Kuna vijana kibao walioandaliwa rasmi wajifanye wako CCM, kumbe ni CHADEMA full. Najua hao wengi wataaminiwa na kupewa nafasi hizo. Sasa wabaki vinywa wazi baada ya matokeo.
 
Ukweli ni kwamba chama tawala watakuwa wanafuatilia kwa ukaribu mwenendo wa kura hasa za urais na wakiona mwelekeo unaonesha Kiwete kushindwa basi watavuruga uchaguzi kwa kuwaruhusu Green guards waanzishe vurugu na hivyo kusababisha uchaguzi kuahilishwa!! Mbinu hizi walizitumia mwaka 1995 mkoa wa Dar es salaam walipoona NCCR wanaelekea kuchukua majimbo yote wakazua balaa na kuahirisha uchaguzi; pia wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa pale Kawe Mzimuni, ccm walipoona wanashindwa wakazusha fujo na kijana wao aitwae kwa jina Azimio akavuruga sanduku la kura mbele ya polisi na hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi ya ke na uchaguzi ukahalibika!! Hizo ndizo mbinu chafu za ccm inapoelekea kushindwa na kama alivyosema Dr. Slaa ni wao CCm ndio watakaoanzisha vurugu kwenye uchaguzi huu jumapili. Tungoje tuone utabili huu.
 
Back
Top Bottom