Uchaguzi Marekani

Mkuu nadhani matatizo ya Trump unayoyataja ndiyo yale yale yaliyokuwa yanatajwa tangu mwanzo. Alichosema mwanakijiji ndiyo hali halisi. Kwamba vyombo vya habari vilijaribu sana kuyasema hayo kwa nguvu ili kumkwamisha trump lkn vimeshindwa,labda km watakuja na mbinu mpya ukiacha hizi zilizoshindwa.

Kwa maoni yangu na kwa wamarekani hawa walioteseka na ugaidi kipindi chote cha utawala wa obama,hakuna tena wa kumzuia Trump kuwa mrithi wa obama. Wamarekani hawatakubali kumrudisha Bill clinton ikulu kwa mara ya pili.
Kuhusu suala la vyombo vya habari, hapa napata tatizo kidogo.

Trump anapenda kusikika/kuonekana katika habari kwa 'vanity and narcissism'

Haya ni mambo anayopenda yasikike, ni kwa mkakati au mazoea au tabia hatujui. Tukubaliane anapenda vyombo vya habari viwe vya kijamii au main stream.

Akiwa huko, Trump huzua 'controversy' ambazo ni chakula cha waandishi wa habari

Habari zake zinakuwa nyingi kuliko inavyotarajiwa na kuvilaumu vyombo vya habari.

Mfano mdogo, aliposhindwa na Cruz chaguzi zilizoongozana, Trump akaingiza habari za wake zao kupunguza nguvu za matokeo yaliyokuwa mabaya. Na amefanya hivyo kila mara

Kulaumu vyombo vya habari anavyovilisha habari ni jambo la kuangaliwa

Trump yupo katika uso wa jamii kama businessman na sasa Mwanasiasa.

Kuna curiosity nyingi juu yake, ni halali tu kama sehemu ya media coverage.

Kuhusu Ugaidi unaosema kwa Obama, hapa kuna vitu viwili.

i)Kuna 'lone wolf' ambao hawajulikani walipo na wanafikiri nini.
Ni mtu anaamua kama yule Meja (Fort Texas) na kuwacharanga wenzake.

Hawa lone wolf wamesababisha madhara sehemu zote kubwa duniani.

ii)Kuna ugaidi ambao ni 'organized' ndio tunayoyasikia Alshabab, Boko,ISIS, Qaeda n.k.

Unaposema Wamarekani wameteseka sana, hadi siku ya leo kuna lone wolf na siyo 'organized' ugaidi kama ule wa Sept 11, Madrid 11, London, Paris, Brussles n.k
 
Hofu yangu ni kuwa Hillary anaweza kuwa indicted maana uchunguzi wa FBI unaonekana unazidi kumsogelea kwelii kweli... na hivyo inampa nafasi Trump ya kukosa mpinzani wa maana kwa kweli.
Na tatizo kubwa zaidi ni kuwa Republican wapo nyuma ya sakata, Bernie Sanders yupo nyuma ya sakata

Hilo ndilo linamweka Sanders katika uchaguzi.
Anataka kukusanya wajumbe wengi akijua hafikii magic number ili waende convention. Huko ndipo atajenga hoja ya emails na hatari kwa Democrat

Haya anayosema ya independents ni kuficha tu dhamira, anasubiri hili la FBI

Kutakuwa na mvurugano Dem, kama hawatakuwa makini kuanzia sasa
 
Nguruvi, utaona kuwa Trump hawagawi conservatives sana anawagawa Republicans; wale ambao wanaamini chama ni chao na kuwa huyu mgeni kaja na kakichukua. Republicans hawa (kina Paul Ryan, Mitt Romney, McCain na wengine) kwa kiwango kikubwa wanaona kuwa watu wao wote ambao wangewakilisha maslahi ya chama - kina Gov. Perry, Gov. Bush n.k hawakufanikiwa. Swali ni kwanini. Hawajajua bado mood ya Wamarekani wengi.

Conservatives wengi utawaona wanasimama nyuma ya Trump kwa sababu moja - wako tayari kumchukua 40% conservative kuliko 100% republican!
Sidhani kama ni iko so straight forward kwamba ni kati ya Republicans na Conservatives kwa sababu wapo pia walio conservatives to the core wasiomkubali na ni wengi. Hivyo hivyo wapo Republicans who are not so conservatives lakini wanasita kum-endorse Trump.

Magavana wamegawanyika hivyo hivyo, maseneta wamegawanyika hivyo hivyo na wawakilishi wamegawanyika hivyo hivyo. Ni Democrats pekee unakoweza kudai establishment iko nyuma ya Clinton lakini si kwa Republicans. Huko ni kila moja na lwake.

John McCain pamoja na kutukanwa yuko tayari kum-endorse Trump, Gov. Rick Perry yuko nyuma ya Trump na kesham-endorse. Lindsay Graham anasita kum-endorse Trump akisema he is a phony na haaminiki. Lit'l Marco na na Lyin' Ted ni swala la muda tu watam-endorse.

Gov. Bush pamoja na ukoo wote wa Bush hawajamkubali Trump na hawategemewi kum-endorse, Paul Ryan hajamkataa Trump ila inavyoelekea ni swala la muda tu...wako pia Republicans ambao wame-declare kumpigia kura Clinton kama mgombea wa Republicans ni Trump.

Hata ambayo ingeitwa establishment wamegawanyika sana na sidhani kama ni sawa kusema establishment yote haimtaki Trump. Kuna mgawanyiko hata ndani ya iliyojulikana kama Tea Party ambapo wapo baadhi wanam-support na wanaoapa kutofanya hivyo.

Hata ndani ya independents kuna mgawanyiko hadi ndani ya familia kuna mgawanyiko...Siku ambayo mteule wa Democrats atajulikana wazi, ndipo hatma ya uchaguzi itakapoweza kutabirika. Changamoto zilizo kwa Democrats hazitofautiani sana na za Republicans.
 
Mkuu Mag3 nimefuatilia mwisho wa wiki hoja yako ina mashiko.
Kundi linalomuunga mkono Trump ni lile lile linaloamini katika 'Trumpisim' hili halibadiliki na kwa kiasi kikubwa sana limemsaidia Trump kupata 'nomination' ndilo lile la 30-38%

Kwa conservatives, wapo wanaomuunga mkono kwasababu tu ni Republican.
Wapo wasio muunga mkono kwasababu hawajaridhika na atakavyoweza kushinda uchaguzi.

Hawa wanaona hana zile 'elements za conservative' na hilo litawapa nafasi waliberali

Kwa upande wa establishment huko kuna mparaganyiko mkubwa sana.
Wapo wasiomtaka na wanashauri mgombea mwingine, kwa njia gani, wanajua wenyewe

Lipo kundi la establishment linaloona iwe na iwavyo, Democrat wasirudi katika madaraka

Wapo wanaoona Democrat wakishinda ni kuendeleza 3rd term ya Obama, hivyo bora Trump

John McCain akizungumza leo ni kama alimshukia speaker Ryan kwa kitendo cha kusita kumuunga mkono Trump. Inaelekea anakubaliana na 'will' lakini akiwa senior establishment kubwa analoweza kufanya ni kukwepa Cleveland.

Halafu wapo opportunists akina Gigrich, Rick Perry, Bob Jindal ambao kwao nafasi mbele.

Tatizo linakuwa kubwa pale Trump anapoanza 'vita' nao. Ni lazima akubali viongozi wana wafuasi na katika ushindani mkubwa atahitaji makundi yote.

Kazi yake kubwa ilikuwa kuleta 'harmonization' tofauti na anavyowaendea katika mikutano

DEMOCRAT
Hapa pana tatizo pengine kubwa kuliko linavyoonekana. Trump keshaanza kampeni, wakati Democrat bado wanalumbana.

Tatizo la Democrat linatengenezwa na Sanders ambaye haijulikani kwa urahisi amelenga nini. Na kwa mwendo wa wafuasi wake mitaani na mitandaoni, uharibifu unaoendelea ni mkubwa

Kampeni ya Clinton inahofia mambo mawili. Haitaki malumbano na Sanders katika kulinda wafuasi wake wanaoweza kuleta uharibifu hasa kwa mienendo yao hadi sasa

Pili, watamhitaji Sanders kama Seneta, na Clinton anataka kucheza karata ya Obama kwa Lieberman.

Tofauti ni kuwa Lieberman alitangaza kumuunga mkono McCain mwanzo kabisa na hakuwa na wafuasi. Sanders yupo ndani ya Democrat akitishia na kundi lake analoita 'independents'
Uharibifu wa Sanders ni mkubwa kuliko ule wa Lieberman

Tusemezane
 


Update
..hii hapa chini ndiyo idadi ya wajumbe wa kila mgombea hadi leo tarehe 5/9/2016

GOP -
idadi inayotak.iwa kufikiwa...1237
  1. Donald Trump...1068 - pungufu ya wajumbe...171
DEM - idadi inayotakiwa kufikiwa...2383
  1. Hillary Clinton....2228 - pungufu ya wajumbe...155
  2. Bernie Sanders...1454 - pungufu ya wajumbe...929
Bernie Sanders bado hakubali na sasa lengo lake ni kumzuia Hillary Clinton asiwapate hao wajumbe 155. Je ikiwa California peke yake inao wajumbe zaidi ya 500, kwa nini anadhani Clinton hawezi kuwapata hata nusu ya hao wajumbe?

Hata hivyo wakiondolewa super delegates, SD, Clinton anabaki na wajumbe 1705 na Sanders 1415

Hapo ndipo anapohamisha goli, hahesabu SD (super delegates) 523 wa Clinton na kudai haondoki kama Clinton hawezi kufikia wajumbe 2383 wa kuchaguliwa pekee bila SD, utaratibu ambao haujawahi kutumika wakati wowote ule!
 
Katika interview aliyofanya na Anderson Cooper, Clinton alisema mwaka 2008 alikuwa katika nafasi kama ya Sanders.

Alishinda majimbo 9 kati ya 12 katika kipindi kama hiki akiwa na ukaribu zaidi wa wajumbe kuliko tofauti iliyopo sasa.

Kwa maneno mengine alisema 'aachwe' hadi atakaporidhika

Kwa upande wa Democrat, tumejadili kuhusu kundi la Sanders.

Hili lipo katika mwendo wa 'shari' na Clinton kampeni wamejitahidi kuwakwepa. Sababu za kufanya hivyo ndiyo hizo, mosi watahitaji kundi hilo na wasingependa mtafaruku. Lakini pia watamuhitaji Sanders ikitokea Seneti inakaribiana sana

Unaweza kuona useneta wa mtu mmoja ni kidogo sana, katika seneti ya watu 60 mtu mmoja anaweza kuwa 'make or break.

Katika kupitisha ObamaCare baadhi ya Republican walifanikisha sana vinginevyo ingekuwa ngumu. Si zaidi ya 3 lakini wali influence sheria kiwango kikubwa sana

Ukiangali namba alizoleta Mag3 hata wakienda convention kutakuwa na mtafaruku

Ikitokea Sanders kashinda watawashawishi vipi watu zaidi ya milioni 10 na 2.5 zaidi wa Clinton kukubaliana na hilo?

Watashauri vipi wajumbe takribani 1700 ambao ni zaidi ya 300 alio nao Sanders kuwa maamuzi yamebadilika?

Lakini pia kutakuwa na utamaduni mpya wa kuondoa SD katika mchakato.
Hapo ni kubadilisha kanuni mchezo ukiendelea.

Clinton kampeni haitakubali. Njia itakayotumika ni ile ile ya vitabuni pledged delegates + super delegates

Zaidi ya hapo, Sanders hajafanikiwa kuwashawishi wajumbe SD kwasasakufikia 100, kuna uwezekano gani wa kuwashawishi 400 au 500 ndani ya convention?

Hata hivyo Democrat wana hofu sana, mwendo wa Sanders ni wa kumshambulia Clinton wakati Trump keshaanza mashambulizi.

Maana yake ni kuwa 'mtarajiwa' anapokea mapigo kutoka ndani na nje, jambo linalomdhoofisha

Tatizo ni kuwa kuweka pressure Sanders ajitoe ni kuamsha 'hisia na mtafaruku' ambao Sanders anautafuta. Wameamua kukaa kimya ingawa inawaumiza in 'a way'
 
DEMOCRAT W.VIRIGINA
REPUBLICAN NEBRASKA NA WV

Kulikuwa na uchaguzi wa awali katika majimbo mawili. Nebraska na West Virginia
Kwa GOP, ilikuwa 'symblolic' kwani tayari wana mgombea Donald Trump

Kwa Democrat, ilikuwa ni mtifuano West Virgia ambako Sanders alitarajiwa kushinda.
Kwanza, ni eneo lenye watu wanaompigia kura kwa wingi (white)

Pili, ni uchaguzi unaoitwa semi open kwa maana kuwa watu waliweza kujiandikisha dakika za mwisho na hilo ni sehemu kubwa ya nguvu ya Sanders

Clinton alikuwa Kentucky pengine kwa kuangalia ramani. Ni jimbo lenye wajumbe wengi.
Sanders alikuwa Oregon ambako ni jimbo linalofuata baada ya WV

Kwa west WV kulikuwa na wajumbe 29 na matokeo ya 51 kwa 36 hayawezi kutoa tofauti kubwa katika pengo la wajumbe wa kuchaguliwa miongoni mwao

Hata hivyo, Sanders amerudia kauli zake kuwa yupo kwa ajili ya ushindi na ameshinda majimbo mawili, India na WV. Sanders anajenga hoja kuhusu kura za maoni zinazoonyesha anamshinda Trump kwa point nyingi kuliko Hillary.

Hoja ya Sanders ni kuwavuta wajumbe waliobaki (Rejea bandiko la Mag3) takribani 170.

Kwa hesabu za leo, hata wote wakimuunga mkono bado pengo litakuwa lipo pale pale

Sanders amekiri kuwa katika wastani wa 45 akiwaambia wafuasi wake ugumu mbele ya safari. Hadi sasa ana SD 41 tangu uchaguzi NY, inaonyesha SD hajabadili msimamo

Kwa upande wa Clinton, kampeni inaonekana kuingiwa na ganzi.

Sababu kubwa ni Sanders. Kwamba, Clinton hawezi kwenda sambamba na Trump kama presumptive nominee Wakati huo huo hataki kuingia katika malumbano na Sanders

Hili linawaumiza Democrat. Kwa ugumu wa hesabu, ni muhimu Sanders kuendelea kumshambulia Clinton?

Ingawa Sanders anaonekana kumgeuzia kibao Trump akisema atafanya kila liwezekanalo Trump asiwe Rais, hiyo ni baada ya kupewa ujumbe anaumiza Democrat kuliko kuijenga.

Nyuma ya pazi bado anaendelea na mashambulizi dhidi ya Clinton

Trump anajijenga ingawa bado ana wakati mgumu ya kuunganisha Republican
Kazi ya kumshambulia Clinton kabaki nayo Sanders

Tusemezane
 
DEMOCRAT W.VIRIGINA
REPUBLICAN NEBRASKA NA WV

Kulikuwa na uchaguzi wa awali katika majimbo mawili. Nebraska na West Virginia
Kwa GOP, ilikuwa 'symblolic' kwani tayari wana mgombea Donald Trump

Kwa Democrat, ilikuwa ni mtifuano West Virgia ambako Sanders alitarajiwa kushinda.
Kwanza, ni eneo lenye watu wanaompigia kura kwa wingi (white)

Pili, ni uchaguzi unaoitwa semi open kwa maana kuwa watu waliweza kujiandikisha dakika za mwisho na hilo ni sehemu kubwa ya nguvu ya Sanders

Clinton alikuwa Kentucky pengine kwa kuangalia ramani. Ni jimbo lenye wajumbe wengi.
Sanders alikuwa Oregon ambako ni jimbo linalofuata baada ya WV

Kwa west WV kulikuwa na wajumbe 29 na matokeo ya 51 kwa 36 hayawezi kutoa tofauti kubwa katika pengo la wajumbe wa kuchaguliwa miongoni mwao

Hata hivyo, Sanders amerudia kauli zake kuwa yupo kwa ajili ya ushindi na ameshinda majimbo mawili, India na WV. Sanders anajenga hoja kuhusu kura za maoni zinazoonyesha anamshinda Trump kwa point nyingi kuliko Hillary.

Hoja ya Sanders ni kuwavuta wajumbe waliobaki (Rejea bandiko la Mag3) takribani 170.

Kwa hesabu za leo, hata wote wakimuunga mkono bado pengo litakuwa lipo pale pale

Sanders amekiri kuwa katika wastani wa 45 akiwaambia wafuasi wake ugumu mbele ya safari. Hadi sasa ana SD 41 tangu uchaguzi NY, inaonyesha SD hajabadili msimamo

Kwa upande wa Clinton, kampeni inaonekana kuingiwa na ganzi.

Sababu kubwa ni Sanders. Kwamba, Clinton hawezi kwenda sambamba na Trump kama presumptive nominee Wakati huo huo hataki kuingia katika malumbano na Sanders

Hili linawaumiza Democrat. Kwa ugumu wa hesabu, ni muhimu Sanders kuendelea kumshambulia Clinton?

Ingawa Sanders anaonekana kumgeuzia kibao Trump akisema atafanya kila liwezekanalo Trump asiwe Rais, hiyo ni baada ya kupewa ujumbe anaumiza Democrat kuliko kuijenga.

Nyuma ya pazi bado anaendelea na mashambulizi dhidi ya Clinton

Trump anajijenga ingawa bado ana wakati mgumu ya kuunganisha Republican
Kazi ya kumshambulia Clinton kabaki nayo Sanders

Tusemezane
Baada ya Nebraska na West Virginia hii hapa chini ndiyo idadi ya wajumbe wa kila mgombea hadi leo tarehe 5/11/2016

GOP -
idadi inayotakiwa kufikiwa...1237
  1. Donald Trump...1134 - pungufu ya wajumbe...103
DEM - idadi inayotakiwa kufikiwa...2383
  1. Hillary Clinton....2240 - pungufu ya wajumbe...143
  2. Bernie Sanders...1473 - pungufu ya wajumbe...910
Kwa sasa upande wa Democrats ni kwamba Sanders bado kakomaa na kakataa kujitoa na sababu zake hazijabadilika sana, anayo imani kwamba anaweza kuwashawishi wajumbe kumteua kwenye convention. Hata hivyo kilichojitokeza huko West Virginia ni kwamba idadi kubwa ya waliompa Sanders kura hawampi kwa sababu watampa kura kwenye uchaguzi mkuu, hapana, lengo ni kumkwamisha Clinton.

Theluthi moja wanasema wazi kura zao zitaenda kwa Donald Trump, theluthi nyingine wanasema bado hawajaamua na ni theluthi iliyobaki ndiyo inasema itamuunga mkono mgombea wa Democrats. Wengi wa hawa ingawa wamepiga kura kama Democrats lakini inaonekana ni Republicans. Hii yote ni katika kutekeleza ule msemo wa adui wa adui yako ni rafiki yako na hapa wana maana ya Sanders na Clinton.

Wanajua mgombea wao keshapita na hahitaji kura zao hivyo wanampa Sanders kumkomoa Clinton na kuleta mtafaruku miongoni mwa Democrats. Hata hivyo huko kwao nako mambo hayajatulia kihivyo kwa sababu bado vita vinaendelea na kuna hatari kubwa ya mgawanyiko kutokana na hali ya sintofahamu baina ya pande mbili zinazopingana, unaomuunga mkono Trump na ule usiomkubali kabisa.
 

trump-jpg.346954
 
Mag3
Baada ya uchaguzi wa Indiana na W.Viriginia hali nyingine inajitokeza kwa Demo. Sanders aliwahilalamika kuhusu SD na kwamba wanapaswa kuunga mkono mgombea na sehemu alizoshinda

Wakati Sanders ameshinda Caucus 7 mfululizo ambazo kimatiki si ngome ya Democrat , kauli mbiu ilikuwa 'ushindi wa majimbo 7' na aungwe mkono na SD

Baada ya uchaguzi wa NY, Clinton alishinda majimbo 5 makubwa ikiwemo Pen, Conn, Maryland, Delaware. Kwa maneno mengi alishinda majimbo 6 kati ya 7.

Hakukuwa na kauli za 'ushindi' huo mfululizo licha ya ukubwa na umuhimu wake

Sanders amebadili kauli, anatumia kura za maoni kujenga hoja.

Anasema kura za maoni zinaonyesha akimshinda Trump kwa Point 20 huku Clinton akimshinda kwa ukaribu sana

Habari za wiki hii, vyombo vingi vya habari vimeondoka katika hoja ya SD na hesabu zinazomkabili Sanders,vinazungumzia kura za maoni kati ya Dem Vs Trump

Hili linafanyika makusudi kwa maana mbili.
Kwanza, 'kuwatisha' SD kuwa Clinton ni risk kwasababu Trump anamkaribia.

Sanders anataka kushawishi SD,huko nyuma alipinga influence yao katika primaries

Pili, kuendelea kuwashawishi wapiga kura kuwa Clinton hachaguliki

Kitu ambacho ni intriguing ni namna vyombo vya habari vinavyoungana na Sanders katika kura za maoni dhidi ya Trump. Hili limechukua sehemu kubwa ya maongezi.

Tafiti zinazofanyika sasa hivi nyingi ni kuhusu Clinton/Sanders Vs Trump

Kwanini tafiti hizo zinatoka mfululizo kila siku, na kwa mpangilio fulani.
Inakuwaje watafiti walianza siku moja na kumaliza katika muda sawia?

Je, kuna mahusiano yoyote ya Sanders na wamiliki vya vyombo vya habari ambavyo kwa Marekani umiliki wake umehusishwa sana na makundi fulani ya jamii?

Je, kuna uhusiano wa watafiti na vyombo vya habari?

Tunauliza hivyo, kwasababu mwendo wa vyombo vya habari katika mazingira yaliyopo vingemuonyesha Sanders ugumu na pengine kuweka shinikizo ajitoe.

Vingeonyesha madhara yanayoendelea upande wa Democrat

Kinyume chake kumekuwa na kumtia moyo kwa kujenga hoja ambazo kila siku zinabadilika. Nini kinaendelea nyuma ya pazia na katika Democrat kwa ujumla?

Tusemezane
 
Mkuu Nguruvi3 wapo wapenzi wa Bernie Sanders hatimaye wanakiri kwamba nafasi yake ya kuteuliwa kuwa mgombea haipo na sasa wanajaribu kumshawishi kujitoa na kum-endorse Hillary Clinton. Wanasema muda muafaka wa kujitoa iwe ni baada ya California primary ili wote waweze kuelekeza nguvu za pamoja kumzuia Donald Trump wa Republicana kuutwaa Urais wa Marekani. Ifuatayo ni article ambayo imepenyezwa ndani ya gazeti la New York Times na mwandishi Yamiche Alcindor.

Hata hivyo timu ya kampeni ya Sanders imeikana hii taarifa ikiita irrelevant.

Bernie Sanders Supporters Propose ‘Mobilizing Voters’ to Beat Donald Trump

A group of Bernie Sanders supporters who have worked or volunteered for his campaign have come up with a draft proposal calling for the Vermont senator to suspend his presidential bid after the June 7 California primary, eventually concede to Hillary Clinton and build an independent organization aimed at defeating Donald J. Trump.

The three-page document addresses a question now facing Mr. Sanders’s most ardent supporters: how to harness the energy of a movement now that his presidential bid appears to be bowing to the reality that Mrs. Clinton will capture the Democratic nomination. The document suggests building “an organization, completely independent of the Clinton campaign,” to defeat Mr. Trump before focusing on other goals after the November election.

About a dozen current and former Sanders staff members and volunteers have been collaborating on the draft proposal, which was obtained by The New York Times and first reported by Politico.

While the authors believe Mr. Sanders will win the California primary, they write that “barring a miracle,” he will not become the party’s nominee. Two of the authors, who are former campaign staff members, confirmed the authenticity of the document. The authors all spoke on the condition of anonymity because they were working without the campaign’s authorization.

The draft lays out a scenario for Mr. Sanders’s leaving the race. “Senator Sanders may graciously concede and enthusiastically endorse Hillary Clinton’s bid to defeat the threatened right-wing takeover of our country by Donald Trump at this time, or may withhold that final step in anticipation of discussions with the Clinton camp before the convention,” the draft says.

Michael Briggs, a spokesman for the Sanders campaign, called the draft plan “totally irrelevant.”

“We are focused on winning the Democratic nomination,” Mr. Briggs said in an email. “This document is something that neither the senator nor anyone he works with has seen. We have no idea who wrote it. We could care less about the document.”

He added that Mr. Sanders “expects to win more delegates in the weeks ahead” and that “he is campaigning to win the nomination.”

However, the authors argue that Mr. Sanders should pivot away from trying to win the nomination after California votes. He should build an organization to “facilitate the growing voice of a new generation of activists” to focus initially on defeating Mr. Trump in November.

Such an organization would be devoted to “mobilizing voters to defend our democracy in November 2016 and beyond,” the authors of the plan write.

The draft says Mr. Sanders can help bring together “young, newly political Sanders supporters” who see “rejection of Hillary and the Democratic Party establishment as core to their identity.” They suggest that his supporters should work to influence the party’s platform at the Democratic National Convention this July in Philadelphia, and that Mr. Sanders should host his own “convention” on transforming American politics, separate from the party’s gathering.

“Coming out of their own convention, the goal will be to launch the best organized independent expenditure organization in history and give the vast (and deeply anti-establishment) base a vehicle into which they will wholeheartedly pour their energy,” the draft said.

The proposal included a section about the challenges of building an independent organization, chief among them fund-raising. They write that Mr. Sanders will have to decide whether such a group would take money from “wealthier progressives” and even suggests the possibility of creating a panel of volunteers who would decide whether to take large donations.

The group says Mr. Sanders is in a similar position as Senator Barack Obama after he energized millions of supporters during his 2008 presidential campaign. However, the authors say Mr. Obama failed to capitalize on the opportunity to change the power structure in America.

“Does Bernie Sanders and his campaign facilitate the growing voice of a new generation of activists who can rack up the defeat of Donald Trump as their first major achievement?” the draft asks. “Or does he raise hell at a party convention and leave the remains of his organization to be picked over by the existing groups on the left that, to date, have been mostly marginal to the broad majority of Americans and Sanders supporters alike?”

The authors say, “Bernie Sanders will have to decide these priorities.”
 
Mkuu Mag3 , baaadhi ya vigogo wa Democrat wameanza kuonyesha hofu na kumtaka Sanders ahitimishe kampeni yake. Sababu wanazotoa ni kuwa kuendelea kwa Sanders kunampa Clinton wakati mgumu wa kukabiliana na Trump

Mosi, kwamba independents wanachanganyikiwa na uwezekano wa kuwabidili wale wenye mwelekeo wa Republican unakumbuna na upinzani mwingine wa Sanders

Trump anaendeleza ushawishi wake kwa independents wa Sanders na kuacha kovu kwa Clinton. Tukumbuke independents wanaosema wengine ni Rep wasiokubaliana na GOP.

Senata Diaane Feinsten wa California anasema, Clinton hawezi ku focus na kuupa mboni uchaguzi mkuu kama afanyavyo Trump.

Seneta Dianne anamuungan mkono Clinton na ni mmoja wa SD.
Kauli yake ina uzito kwani mwaka 2008 yeye ndiye alileta suluhu kati ya Clinton na Obama

Senata Israel Steve, NY anasema ni wakati sasa wa kuunganisha chama mapema kabla ya kuchelewa. Seneta steve ni kiongozi aanyeshughulikia jitihada za wabunge wa Democrat kushinda bunge la Marekani, Congress. Huyu naye ni SD na ni supporter wa Clinton

Wasi wasi wa Clinton kampeni ni kuwa na ''two front effort'', kwanza kuhakikisha anakampeni katika primaries, na pili dhidi ya Trump. Wasi wasi huo unaonyeshwa na seneta wa Ohio

Wiki hii, VP Joe Biden ameeleza wazi kuhusu Clinton kuwa mgombea alipohojiwa na TV
Rais Obama ameonyesha ugumu unaomkabili Sanders kwa hesabu bila kumtaka aondoke

Senta DEbbie Stabenow wa Michigan yeye kasema wanamkaribisha Sanders katika kamati ya seneti inayohusu masula ya fedha, akimaanisha ni wakati ajitoe

Tatizo linalowakabili Biden na Obama hawawezi kuingilia kati uchaguzi unaoendelea.

Hii ina maana wasingependa kuwachukiza independents wa Sanders
Na ndivyo Clinton kampeni inavyosita kupa shinikizo la kuachia ngazi

Kwa uoande mwingine, kundi la maseneta 7 linaloshiriki chaguzi zijazo ni dalili kuwa SD hawana mpango wa kubadili mwelekeo at least kwa waliochukua upande hasa Clinton

Uchaguzi wa Oregon na Kentucky ni muhimu kwa Clinton kama anataka ongezeko la pressure
Hata hivyo, ushindi wa eneo kama Oregon haumpi nafasi kutokana na 'demography'

Kura za maoni ni chache zikiwa na mwelekeo usioonyesha uhalisia.

Tusemezane
 
KENTUCKY NA OREGON ASUBUHI YA LEO

Update na mtazamo unafuata
 
  • Thanks
Reactions: BAK
KENTUCKY
Asilimia 99 ya matokeo imepatikana, Clinton akimshinda Sanders kwa kura 1,923 katika 46.8% na 46.3%. Kwa hapa ushindi utakuwa wa Clinton ingawa matokeo hayabadilishi idadi ya wajumbe. Watagawana wajumbe 55

Hii ina maana kuwa Sanders hakuongeza wajumbe au Clinton. Kwa upande wa Clinton ni habari njema kwasababu mbili. Kwanza, amemzuia Sanders kwa kauli mbiu ya ushindi kwa sababu ushindi ni ushindi tu hata kama ni 0.1.

Pili, Hakuruhusu kupoteza hata mjumbe mmoja

OREGON
Hadi sasa asilimia ya matokeo yaliyopo ni 66 Sanders akiongoza kwa asilimia 53 kwa 47
Na update ni kuwa ameshinda Oregon

Seneta Sanders anaonge kutoka California kwa muda huu. Hoja yake kubwa ni kuhusu kura za maoni za kitaifa zinazoonyesha akimshinda Trump. Kama mtakumbuka huko nyuma tumeuliza sana kwanini Kura za moani si kati ya Sanders na Clinton bali Clinto/Sanders na Trump?

Hizi kura zinafanywa makusudi kwasababu hoja zote za Sanders zinaonekana kuwa na majibu
1. Idadi ya wajumbe wa kuchaguliwa ano wachache (300) hadi wakati huu
2. Ameshinda state chache kuliko Clinton (19)
3. Ana wapiga kura wachache kuliko Clinton kwa Zaidi ya milioni 3
4. Ana Support ya super delegates wachache

Hivyo , anasema ataendelea hadi kura ya mwisho. Ukimsikiliza na kulinganisha na yaliyotokea Nevada, ni wazi kampeni yake ipo katika vita kubwa na Clinton

Tatizo linalomkabili ni kuwa matatizo yaliyojityokeza yanayohusishwa naye yanaanza kupoteza Imani kwa SD hata waliofikiria kumuunga mkono

Katika mkutano anaoendelea nao sasa, Sanders anamshambulia kikamilifu Clinton pengine kuliko Donald Trump. Hii ina maana kaamua liwalo na liwe

Katika mjadala huu, tulijadiliana na Mkuu Mag3 tukihojia nia ya Sanders, well, dhamira yake ya kuleta mtafuruku ndani ya Democrat ipo wazi na hakika Democrat wanahofu sana

Hofu si dhidi ya ushindi wake, bali kampeni yake ambayo sasa imegeuka kuwa ya fujo mithili ya yale ya Trump. Hili linawatia hofu sana Democrat

Tutaendelea na tathmini
 
KENTUCKY
Hillary Clinton ameshinda Kentucky

BERNIE SANDERS
Mjadala uliopo ni jinsi democrat walivochanganyikiwa na Bernie Sanders
Vijana wa Sanders walifanya vurugu katika Nevada convention

Jambo hilo limewaudhi baadhi ya viongozi wa juu wa Democrat kama H.Reid ambaye ni senate minority leader, Dianne Feinsten na wengine wengi

Vijana wa Sanders walituma vitisho vya 'mauaji' kwa kiongozi wa Democrat-Nevada

Seneta Sanders amekataa kulaani vurugu zilizotokea, huku kiongozi wa kampeni yake Joan Kato akihimiza vijana 'waendelee ' na kampeni meneja wake Bw Weaver akishilia msimamo wa kutetea vijana wake

Kikubwa Zaidi ni jinsi ambavyo kampeni za Sanders zinavyomdhoofisha Hillary Clinton
Katika wakati huu mashambulizi dhidi ya Clinton yanawatia hofu kubwa Democrat

Katika mkutano wa California, Sanders ameonekana kuwashambulia viongozi wa Democrat na hasa Super delegates.

Ujumbe wake ni kuwa Democrat iruhusu 'independents' au iwaache nje.
Hapa anawachochea wafuasi wake wafanye uasi, kwa maana ya kulazimisha

Hawa independents anaozungumzia haijulikani kama ni Democrat.
Ni ukweli kuwa independents wanaweza kuwa republican au yoyote

Kauli za wafuasi wa 'Bernie or burst' ni za hatari sana.
Kwamba, kama si Bernie basi jahazi lizame

Mchambuzi Carl Bernstein akiongea na CNN amemkariri mke wa Sanders akisema 'Uchunguzi wa FBI' umefikia wapi? Hapa lipo neno ambalo halijulikani

Kwa upande mwingine, akiwa na SD 41, kitendo cha kuwashambulia wengi wao kinamweka pagumu kidogo. Kwa hali ilivyo, hakuna anayejua nini lengo hasa la Sanders

Hesabu ni ngumu sana, hadi jana alitakiwa ashinde asilimia 67 ya majimbo yaliyobaki
Ushindi wake wa Oregon haukuzidi asilimia 7, na Kentucky watagawana na Clinton

Kwa maneno mengine, ukiwaondoa SD Clinton bado atashinda

USD waipiga kura kufuatana na majimbo ya ushindi wa mgombea, Clinton ana wengi

Swali linalowasumbua Democrat, nia na dhamira ya Sanders ni kitu gani?

Tusemezane
 
KENTUCKY
Hillary Clinton ameshinda Kentucky

Tutaendelea..
Baada ya Kentucky na Oregon hii hapa chini ndiyo idadi ya wajumbe wa kila mgombea hadi leo tarehe 5/18/2016

GOP -
idadi inayotakiwa kufikiwa...1237
  1. Donald Trump...1160 - pungufu ya wajumbe...77
DEM - idadi inayotakiwa kufikiwa...2383
  1. Hillary Clinton....2291 - pungufu ya wajumbe...92
  2. Bernie Sanders...1528 - pungufu ya wajumbe...855
Kwa sasa ni vigumu kuelewa anachotafuta Sanders kwani hata angepewa wajumbe wote waliobakia hawezi kufikisha idadi inayotakiwa. Badala yake anaonekana kuongeza mashambulizi dhidi ya Clinton na Democrats wamebaki wanakuna vichwa hawajui wafanye nini.

Donald Trump wa GOP naye anaonekana kuchangamkia mashambulizi hayo ya Sanders dhidi ya Clinton na leo katoa kali kwa kumtaka Clinton ajitoe amuachie Sanders! Vituko vya kutupiana viti huko Nevada navyo vimezidi kuonesha mambo yalivyo magumu kwa DNC.

Wapenzi wa Sanders wanaonekana kuchukizwa na ukweli kwamba mtu wao hana nafasi kabisa ya kuteuliwa kuwa mgombea na hasira yao wanaimalizia kwa Clinton na uongozi wa DNC. Wamefikia hatua ya kuwatumia baadhi yao ujumbe wakiwatishia maisha yao.

Wachunguzi wanasema kwamba hali isipobadilika ndani ya DNC kuna hatari ya mtafaruku mkubwa ambao haujawahi kuonekana tangu mwaka 1968. Ingawa huko Republicans nako establishment haipendwi lakini kwa DNC hali ni mbaya zaidi...Sanders kagoma, katu hakubali.
 
Mkuu Mag3
Kinachoshangaza ni namna kampeni yake inavyoendeshwa kwa sasa
Jukwaani anatumia muda mwingine kukabiliana na Clinton kuliko Trump

Calfornia aliwaambia wafuasi wake, ili kumshinda Trump lazima wamshinde Clinton

Kauli hiyo haikuwa na matatizo, ingawa haina uhalisia. Anatoa matumaini 'feki' kwa wafuasi,matarajio yasipofikiwa frustrations zinajitokeza kama kule Nevada

Matatizo ya Nevada amekataa kuyakemea. Wakati akiendelea na mikutano anakubali kauli ya 'Bernie or Burst' akijua ni hatari , bado yupo kimya

Hakuna hesabu inayomwezesha Sanders kuwa mshindi.
Hadi Jana kabla ya matokeo, Sanders alitakiwa ashinde kwa 67% ya majimbo yaliyobaki.

Ushindi wake Oregon point 6 haukusaidia. Sasa anatakiwa ashinde kwa 68%

Nikisoma kura za maoni za polls zote kubwa, NJ Clintona anaongoza.

Haina maana Sanders hawezi kushinda, la hasha, margin haitakidhi haja ya 68%

NJ ni closed primarya,Sanders hakufanya vizuri siku za nyuma kuna colored people. Sanders akishinda kwa 55% kwa 45%, ''odd'' ya kushinda California inafikia 70%.
Je, possibility hiyo ipo?

Tunasema hivyo kwasababu Sanders alitarajiwa kuleta ushindani sana NY!!

Tatizo linalojitokeza Democrat walichukuliwa kiurahisi.

Kama utakumbuka tulisema, vijana wanaoingia midahalo kwa shari haikuwa dalili njema

Democrat wanakuna vichwa, maana Sanders kwa sehemu ya Democrat utawaumiza.

Ni kutokana na kutambua hilo, Sanders anataka kupeleka uchaguzi convention Philly n.k.

Kwenda Philladephia bila mshindi ni kutengeneza tanuru la matatizo makubwa

Kwa upande mwingine, jana amewatibua Dem kwa kuwashambulia

Pressure ya kumtaka aachie ngazi itajitokeza katika wiki hii

Tusemezane
 
Mkuu Mag3
Kinachoshangaza ni namna kampeni yake inavyoendeshwa kwa sasa
Jukwaani anatumia muda mwingine kukabiliana na Clinton kuliko Trump

Calfornia aliwaambia wafuasi wake, ili kumshinda Trump lazima wamshinde Clinton

Kauli hiyo haikuwa na matatizo, ingawa haina uhalisia. Anatoa matumaini 'feki' kwa wafuasi,matarajio yasipofikiwa frustrations zinajitokeza kama kule Nevada

Matatizo ya Nevada amekataa kuyakemea. Wakati akiendelea na mikutano anakubali kauli ya 'Bernie or Burst' akijua ni hatari , bado yupo kimya

Hakuna hesabu inayomwezesha Sanders kuwa mshindi.
Hadi Jana kabla ya matokeo, Sanders alitakiwa ashinde kwa 67% ya majimbo yaliyobaki.

Ushindi wake Oregon point 6 haukusaidia. Sasa anatakiwa ashinde kwa 68%

Nikisoma kura za maoni za polls zote kubwa, NJ Clintona anaongoza.

Haina maana Sanders hawezi kushinda, la hasha, margin haitakidhi haja ya 68%

NJ ni closed primarya,Sanders hakufanya vizuri siku za nyuma kuna colored people. Sanders akishinda kwa 55% kwa 45%, ''odd'' ya kushinda California inafikia 70%.
Je, possibility hiyo ipo?

Tunasema hivyo kwasababu Sanders alitarajiwa kuleta ushindani sana NY!!

Tatizo linalojitokeza Democrat walichukuliwa kiurahisi.

Kama utakumbuka tulisema, vijana wanaoingia midahalo kwa shari haikuwa dalili njema

Democrat wanakuna vichwa, maana Sanders kwa sehemu ya Democrat utawaumiza.

Ni kutokana na kutambua hilo, Sanders anataka kupeleka uchaguzi convention Philly n.k.

Kwenda Philladephia bila mshindi ni kutengeneza tanuru la matatizo makubwa

Kwa upande mwingine, jana amewatibua Dem kwa kuwashambulia

Pressure ya kumtaka aachie ngazi itajitokeza katika wiki hii

Tusemezane
Naomba nichukue nafasi hii kuweka bayana kiini cha malalamiko ya Bernie Sanders katika mchakato wa kutafuta mgombea wa chama cha Democrats. Tuanze kwa kutazama idadi ya wajumbe (Party Delegates) wanavyopatikana.

Jumla ya wajumbe wote wa Democrats ni 4763 na idadi hii inajumuisha wajumbe wa kuchaguliwa (pledged delegates) 4051 na wajumbe maalumu (Superdelegates) 725.

Ili mgombea ateuliwe anahitaji kupata idadi ya wajumbe (won delegates + superdelegates) 2383. Je hali ikoje hadi leo hii?

Wajumbe wa kuchaguliwa

  1. Hillary Clinton....1768
  2. Bernie Sanders...1494
Wajumbe maalum
  1. Hillary Clinton....525
  2. Bernie Sanders...39
Hadi sasa idadi ya wajumbe waliobakia ni 930. Katika hawa Sanders anahitaji wajumbe 850 ili aweze kufikisha idadi ya kuweza kuteuliwa wakati Clinton anahitaji tu wajumbe 90.

Katika wajumbe 930 waliobakia 782 ni wa kuchaguliwa na 148 ni wajumbe maalum. Ili Sanders ateuliwe anahitaji kushinda majimbo yaliyobakia na ili kuhakikisha Clinton hapati wajumbe maalum ashinde kila jimbo kwa asilimia zaidi ya 80%.

Majimbo yaliyobakia ni haya;
  1. District of Columbia - June 14... 20 (25)
  2. California - June 7.................... 475 (71)
  3. Montana - June 7....................... 21 (6)
  4. New Jersey - June 7................. 126 (16)
  5. North Dakota - June 7............... 18 (5)
  6. New Mexico - June 7................. 34 (9)
  7. South Dakota - June 7.,............ 20 (5)
  8. Puerto Rico - June 5................. 60 (7)
  9. Virgin Islands
Kama mpango huu utashindikana Sanders anataka wajumbe maalum (Superdelegates) waondolewe kwenye hesabu na kama hilo halitawezekana anadai apewe wajumbe wote kwenye majimbo aliyoshinda. Kinachowafanya Democrats wakune vichwa ni kwamba hata hayo yote yakitekelezwa bado hawezi kufikisha idadi inayotakiwa, hesabu hazikubali.

Je Sanders anataka kugombea kama Independent? Ingawa yeye anasema hawezi kufanya hivyo lakini wengi wa mashabiki wake hawako tayari kumpa kura Clinton kitu ambacho kinaweza kumpa fursa kubwa Donald Trump wa Republicans kutwaa Urais wa Marekani. Je lengo lake ni kuisambaratisha chama cha Democrats?

Na leo ametoa sharti mpya la kuwataka independents waruhusiwe kupiga kura kwenye primary ya California jambo amabalo ni kinyume kabisa na utaratibu. Je atachukua hatua gani iwapo uongozi wa DNC utakataa kubariki ombi lake hilo? Anaamini wakiruhusiwa anaweza kushinda California na kuzoa wajumbe wake wote 546.

Hata hivyo hata akifanikiwa kutwaa California yote na kama Clinton atakuwa bado anaongoza hayuko tayari kujitoa hadi Convention Philadelphia! Ndio maana amedai na kuwashauri wapenzi wake kwamba ili waweze kumshinda Trump mwezi Novemba inabidi wahakikishe wanamshinda Clinton kwanza! Homa huanza pole pole.

Swali linaloumiza kichwa ni ukweli kwamba Sanders alijua toka awali kabisa utaratibu utakaotumika kumpata mgombea ndani ya chama chake na wakati wote huo hakuwahi kutoa pingamizi lolote. Je ni kitu gani kimemfanya abadilishe msimamo katikati ya safari? Je inawezekana baada ya kuonja asali kaamua kuchonga na mzinga kabisa?
 
Na leo ametoa sharti mpya la kuwataka independents waruhusiwe kupiga kura kwenye primary ya California jambo amabalo ni kinyume kabisa na utaratibu.

Je atachukua hatua gani iwapo uongozi wa DNC utakataa kubariki ombi lake hilo?
Anaamini wakiruhusiwa anaweza kushinda California na kuzoa wajumbe wake wote 546.

Hata hivyo hata akifanikiwa kutwaa California yote na kama Clinton atakuwa bado anaongoza hayuko tayari kujitoa hadi Convention Philadelphia!

Ndio maana amedai na kuwashauri wapenzi wake kwamba ili waweze kumshinda Trump mwezi Novemba inabidi wahakikishe wanamshinda Clinton kwanza! Homa huanza pole pole.

Swali linaloumiza kichwa ni ukweli kwamba Sanders alijua toka awali kabisa utaratibu utakaotumika kumpata mgombea ndani ya chama chake na wakati wote huo hakuwahi kutoa pingamizi lolote. Je ni kitu gani kimemfanya abadilishe msimamo katikati ya safari? Je inawezekana baada ya kuonja asali kaamua kuchonga na mzinga kabisa?
Mkuu , kwa California hata afanye recruitment kubwa hawezi kuzoa wajumbe wote

Sheria za DNC zinasema ili mgombea asipate mjumbe hata mmoja ni hadi atakapokuwa na chini ya asilimia 15 ya wapiga kura katika jimbo husika.

Kwa maana kuwa Sanders lazima ashinde kwa asilimia 85.
Kwa California si Clinton au Sanders anayeweza kushinda kwa 85%

Hypothetically tufanye Sanders atashinda kwa 70%, je hiyo itabadilisha hesabu?

Hoja anayotumia ni kuwatisha DNC,wasipokubali independents kupiga kura mbele ya safari ni tatizo. Kisichojulikana hawa independents ni loyal kwa Democrat?

Ni watu kutoka wapi kiasi cha kutaka kulazimisha kupinda kanuni?

Leo Hillary Clinton alikuwa na mahojiano na Cuomo wa CNN. Katika majibu ya maswali aliyoulizwa, Clinton alisema hakuna sababu zitakazozuia asiwe mgombea wa Democrat

Kidiplomasia alisema,2008 alishinda majimbo 9 kati ya 12 katika wakati kama huu.

Akasema, ukaribu wa idadi ya wajumbe kati yake na Barack Obama ulikuwa 'close' kuliko uliopo kati yake na Sanders katika wakati kama huu

Clinton akasema, wakati huo alikuwa kura nyingi kuliko Obama.
Hata hivyo ilibidi akubali kwasababu sheria za DNC zinasema mgombea ni mwenye wajumbe wengi.

Akasema, ana kura milioni 3 Zaidi ya Sanders na wajumbe wengi wa kuchaguliwa.

Kauli za Bi Clinton zilikuwa kumweleza Sanders kuwa aliposimama wakati huu ndiko alikokuwa amesimama Clinton mwaka 2008.

Ujumbe mkubwa ni pale aliposema 'sharia za DNC zinasema hivyo'

Hiyo kauli ya 'sharia za DNC' ilikuwa kumweleza Sanders kuwa hatakubali zibadilishwe kwasababu zilitumika dhidi yake na Obama na kwamba alikubali

Tunaona kuwa kauli za Sanders kuhusu 'independents' waruhusiwe haziwezi kukubalika kirahisi na hasa kambi ya Clinton.

Interview ya leo ukiiangalia kwa undani ilikuwa majibu kwa Sanders katika lugha ya kidiplomasia, bila kuudhi lakini yenye kubeba ujumbe

Tusemezane
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom