Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Status
Not open for further replies.
Mimi, kama 'President Elect', niko tayari kuvaa gwanda endapo CHADEMA kitafanikiwa kushinda uchaguzi mdogo, jimbo la Igunga.
Hii ni changamoto kwa CHADEMA na wapambe wao hapa JF, ambao macho na masikio yao yanafuatilia uchaguzi wa Igunga.
Jimbo la Igunga ni karata dume, ambayo CCM wanayo mikononi mwao. Kazi kwenu CHADEMA kuwapokonya, na kama mtafanikiwa, basi na mimi nitavaa gwanda, kama ilivyo kwa mh. Freeman Mbowe au mh. Zitto Kabwe. Nasema tena, kazi kwenu CHADEMA!

So what? Kuvaa kwako gwanda kutaisaidia nini CDM?
 
Ila tutakushonea magwanda ya bluu yenye drafti ya njano,na alama ya jembe na nyaundo mgongoni
 
Fanya hishima na adabu ni kipi kibaya alichokiongea? hiyo ni changamoto kwa magwanda. Hata FF alisema humu cdm ikishinda Igunga anahamia huko.
<br />
<br />
Yaani we Zombie na dadako FF wala hatuwahitaji CDM maana nyie ni vilaza kuliko hata Shibuda! Bakini huko huko na magamba yenu kila kukicha mna kashfa mpya ya ufisadi! Yaani kila gamba na kashfa yake. Lol!
 
Nadhani President Elect umetumwa kuja kuchafua hali ya hewa huku, wewe sio bure. cdm ina watu makini tayari, hategemei mtu makini yeyote atokee magambani. hao wachache tu walokuja kutoka magamba tunajuuuuuta kuwafahamu na kuwapokea.

Wewe inaonyesha umeshadhamiria kuja kuvaa gwanda mana unajua wazi kuwa CDM ushindi Igunga ni lazima. hilo dau unaloweka ni kama vile ushamake up your mind kuja CDM.
 
Kama wote ulivyosema!ni sahihi kabisa kwakua najua wajua mbinu gani wenzetu wanazitumia!kam ni mfuatiliaji mzuri wa mambo,kwenye kura za maoni tu ndani ya chama chao wenzetu washakamatana na rushwa!wangekua wapinzani ndio wamefanya mchezoo huu mchafu ungesikia!nashangaa kama unatupima kwa jimbo la igunga unahitaji msaada uelewe nini malengo ya chamachetu.
 
Safari hii CCM inabidi ijipange kisawasawa kwa kuwa historia ya jimbo hili kuwa wazi ni tofauti na chaguzi ndogo zilizopita, CCM ilikuwa na uhakika wa kuyatetea kwa vile aidha yaliachwa wazi kutokana na vifo au kubatilishwa kwa matokeo hivyo kuwaacha CCM wakiwa wamoja na kusaidiwa na sympath ya wenyeji, this time jimbo limeachwa kwa shutuma, visa na aliyeondoka ameondoka kwa kinyongo they have to put this in mind hivyo lazima kuna makundi yamejengeka ndiyo maana hata mwandishi anasema CCM wana nafasi ndogo tena kaandika (sana) ya kushinda.
 
Mimi, kama 'President Elect', niko tayari kuvaa gwanda endapo CHADEMA kitafanikiwa kushinda uchaguzi mdogo, jimbo la Igunga.<br />
<br />
Hii ni changamoto kwa CHADEMA na wapambe wao hapa JF, ambao macho na masikio yao yanafuatilia uchaguzi wa Igunga.<br />
<br />
Jimbo la Igunga ni karata dume, ambayo CCM wanayo mikononi mwao. Kazi kwenu CHADEMA kuwapokonya, na kama mtafanikiwa, basi na mimi nitavaa gwanda, kama ilivyo kwa mh. Freeman Mbowe au mh. Zitto Kabwe. Nasema tena, kazi kwenu CHADEMA!
<br />
<br />

Sanity is insanity
No!
Insanity is sanity
Yes, it is
 
We nani kwanza tukujue. Pili kuvaa gwanda ni swala la maamuzi yako mwenyewe halihusiani na CDM waweza vaa gwanda la mgambo, gwanda la polisi, gwanda la mjeda au hata gwanda la mfungwa.

Vaa tu gwanda ndugu. CDM hatutaki shobo. CDM hatufanyi kampeni ili kushinda uchaguzi na kufurahisha watu, ila CDM nia kubwa ni kuleta ukombozi kwa watanzania.
 
Hivi nani kawaambia ufisadi wa CCM ni kigezo cha kuchagua upinzani?
Gurudumu huwezi kuingia uchaguzi wowote bila kuwa na hot issue ya kuuza, ninavyoona mimi kwa sasa hot issue ya kuuzika rahisi ni ufisadi, bila kuficha hoja ya ufisadi ndiyo iliyompandisha Slaa na Chadema ndio maana CCM mwaka jana waka-risk baadhi ya wabunge wao ili waiteke walijua inalipa, wengi kama si wote walio-risk sasa ni manaibu waziri au mawaziri kamili.

Hadi leo hii ufisadi bado ni hoja inayolipa kwa upinzani wanaweza kuitumia kwenye uchaguzi wa Igunga, hata chama tawala wanaweza wakijua kuitumia mfano ulio wazi ni wa wao kujivua gamba imetokana na hoja ya ufisadi.
 
mh! huko Igunga kazi ipo, kila chama hat SAU kinajinasibu kushinda Igunga, ngoja tusubiri na tuone yatakayotokea
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom