Uchaguzi CWT: Wakuu wa Shule na Ma-MEK hawafai

chamilo nicolous

JF-Expert Member
Mar 10, 2016
1,991
1,364
-Wengi wao ni vibaraka wa Wakurugenzi na Maafisa Elimu (DEO);Wametumwa
--Wakuu wa shule, Waratibu Elimu Kata (MEK) hawafai kuchaguliwa


Siku na Tarehe ya kufanya uchaguzi wa kupata viongozi wa Chama Cha Walimu (CWT) utatangazwa muda wowote, hii ikiwa ni baada ya tarehe ya awali kuhairishwa kufuatia tishio la ugojwa wa CORONA. Poleni kwa usumbufu uliojitieza.

Wapiga kura (Walimu wawakilishi wa kila shule) kuweni makini sana na aina ya Walimu waliojitokeza kugombea nafasi ndani ya chama.Miongoni mwa Walimu waliojitokeza baadhi yao ni Wakuu wa shule na Waratibu Elimu Kata (MEK), na hawa wanaonekana wanahushawishi wa kifedha kwa sababu ya posho ya madaraka, hivyo elfu kumi, kumi kwao sio shida.

NIWAKUMBUSHE WALIMU: Miongoni mwa watu wanaofanya kazi ya ualimu kuwa ngumu ni wakuu wa Shule na Waratibu Elimu Kata. Hii inanipa kigugumizi , kundi hili la viongozi wanaotaka tena uongozi watawatetea vipi walimu ikiwa migogoro mingi ya walimu inatengenezwa na Wakuu wa shule na Waratibu Elimu Kata? Walimu mlioko mashuleni mnalijua hili. Walimu wengi wanaohoji masuala ya msingi kama vile mapato na matumizi ya shule, wakuu wa shule huwajengea hoja kuwa ni walimu wakorofi na wasumbufu, na wanaanza kuwaandikia barua mbaya za kuwachafua.

LAKINI: Wakuu wa shule na Waratibu Elimu Kata (MEK), kwa sababu ya posho ya madaraka huwa mnajisahau kuwa na ninyi ni walimu kama walivyo walimu wengine. Mnabadilika kuwa vibaraka wa Wakurugenzi na Maafisa Elimu (DEO). Mnadiliki muda mwingine kutoa maneno ya shombo kwa walimu wenzenu wanapotoa madai ya msingi, mara nyingine mnaficha barua za walimu ili madai yao yasiwafikie waajiri.

UTAKUBALIANA NA MIMI: Ili uwe mkuu wa shule au Waratibu Elimu Kata (MEK) lazima uwe na mahusiano ya karibu na Mkurugenzi na Afisa Elimu (DEO) wakupeleka taarifa za walimu wengine, kujipendekeza(Kibaraka). Mkurugenzi anasimama kama Mwajiri, kwa Wakuu wa Shule na Waratibu Elimu Kata (MEK) mwajiri (Mkurugenzi na Afisa Elimu (DEO))wananafasi kubwa kuliko walimu.Je katika hali ya kawaida mtadhubutu kuwahoji bila kupepesa macho?

Chamilo Nicolaus nasema ili chama kirudi wenye misingi kama inavyoainishwa katika Katiba ya Chama Toleo la Sita la mwaka 2014: Sehemu ya I Wapiga kura (Walimu wawakilishi wa kila shule) kuweni makini sana na aina ya Walimu waliojitokeza kugombea, Vinginevyo tutabaki kukiona chama kisicho na muelekeo.
 
Nadhani hili umeliandika kimehemuko sana. Cwt ni chama kinachoongozwa na sheria taratibu na kanuni zilizowekwa.
Pia kile chama kina katiba na miongozo mbalimbali inayotumika.

Sasa kama hivyo vyote haviwazuii wao kuchagua au kuchaguliwa wewe ni nani mpaka uje humu kueneza upupu wako?
Huu ndio upopoma wa baadhi ya walimu, yaani hawawezi kabisa kusoma na kuzielewa taratibu mbalimbali zinazoongoza vyama au makundi ya watu.

Sasa huyu ni mwalimu tunaowategemea watufundishie watoto wetu anakuja na 'fallacy arguments' kama hizi unaweza jiuliza hivi huko darasani huwa wanafundisha nini hawa wanafunzi wetu?

Watu ambao hawaruhusiwi kugombea kwenye vyama vya wafanyakazi ni Watunga na Wasimamia Sera.
Maana yake ni DED na DEO waliobaki yaani Maafisa takwimu na taaluma, maafisa Elimu watu wazima, sayansi kimu aj elimu maalumu, Elimu watu wazima, wadhibiti ubora maafisa Elimu kata wote wanaruhusiwa na wengine wameshachaguliwa tayari jiandae kukutana nao Chamani.

Acha mikwala ya kishamba nenda kagombee ukipigwa chini tulia check number si unayo una wasiwasi gani???

Acha ujinga jikite kwenye taratibu na kanuni na sheria za Chama zisome taratibu utaelewa.
 
Kuna baadhi ya watu wanadhani ukigombea vyama vya wafanyakazi basi ni lazima uwe mtata, mgomvi, muhamasisha migomo au mtu fulani hivi mtata mtata. Hii dhana imepitwa na wakati.

Walimu wachague watu wenye busara na hekima za kutosha wakiongozwa na kanuni na sheria na taratibu zao watu wanaoweza kusimamia kile wanachokiamiani na kuboresha mazingira ya utoaji na upatikanaji wa Elimu shuleni. Hapa wote tunaamini ili hilo litokee 'the key person' ni mwalimu. Sasa Zama za utata, uharakati usio na tija ama majungu kama ya mleta uzi ndio yanakiharibu chama.

Upo mfano mzuri wa madaktari miezi kadhaa nyuma walitafuta nafasi wakapata wakaongea na Muheshimiwa Rais wakapata hata zile nafasi za ajira mpya kwa madaktari (1000) hicho ndicho kinahitajika.

Sasa huku kazi imeanza mara nani hatakiwi nani anatakiwa vitu ambavyo hata kwenye Katiba na Kanuni wala Taratibu za vyama vya wafanyakazi i.e CWT havipo sijui mleta uzi kavitoa wapi
 
Nadhani hili umeliandika kimehemuko sana. Cwt ni chama kinachoongozwa na sheria taratibu na kanuni zilizowekwa.
Pia kile chama kina katiba na miongozo mbalimbali inayotumika.

Sasa kama hivyo vyote haviwazuii wao kuchagua au kuchaguliwa wewe ni nani mpaka uje humu kueneza upupu wako?
Huu ndio upopoma wa baadhi ya walimu, yaani hawawezi kabisa kusoma na kuzielewa taratibu mbalimbali zinazoongoza vyama au makundi ya watu.

Sasa huyu ni mwalimu tunaowategemea watufundishie watoto wetu anakuja na 'fallacy arguments' kama hizi unaweza jiuliza hivi huko darasani huwa wanafundisha nini hawa wanafunzi wetu?

Watu ambao hawaruhusiwi kugombea kwenye vyama vya wafanyakazi ni Watunga na Wasimamia Sera.
Maana yake ni DED na DEO waliobaki yaani Maafisa takwimu na taaluma, maafisa Elimu watu wazima, sayansi kimu aj elimu maalumu, Elimu watu wazima, wadhibiti ubora maafisa Elimu kata wote wanaruhusiwa na wengine wameshachaguliwa tayari jiandae kukutana nao Chamani.

Acha mikwala ya kishamba nenda kagombee ukipigwa chini tulia check number si unayo una wasiwasi gani???

Acha ujinga jikite kwenye taratibu na kanuni na sheria za Chama zisome taratibu utaelewa.
jibu hoja! hata kama umeguswa tako
Hoja ni wakuu wa shule hata katika maswala madogo ya msingi hawawezi kuyajengea hoja, wanajenga fitina na chokochoko, hofu na woga kwa walimu kuwa ni walimu wakorofi na wasumbufu, na wanaanza kuwaandikia barua mbaya za kuwachafua.
Swali ni watawezaje kuwatetea walimu ambao wao wanawaita wakorofi na wasumbufu???? husilete hang over zako leta hoja bwege weee
 
jibu hoja! hata kama umeguswa tako
Hoja ni wakuu wa shule hata katika maswala madogo ya msingi hawawezi kuyajengea hoja, wanajenga fitina na chokochoko, hofu na woga kwa walimu kuwa ni walimu wakorofi na wasumbufu, na wanaanza kuwaandikia barua mbaya za kuwachafua.
Swali ni watawezaje kuwatetea walimu ambao wao wanawaita wakorofi na wasumbufu???? husilete hang over zako leta hoja bwege weee
Wanajenga fitina wanajengaje?
Hizi ni hear-says tu!! Nani akujengee fitina wewe?? Wewe una nini mpaka ujengewe fitina??? Mbona wenzako hawajengewi?? Lete ushahidi usikute ni 'inferiority complex' zako tu.

Wakuu wa shule wengi wapo smart na wakurugenzi wengi wapo smart sana hawawezi kudeal na individual issues za kijinga kama hizo. Wewe weka ushahidi wako nani kakujengea fitina au majungu. Wewe kama mtoro kazini, kiburi mjuaji au unalala na wanafunzi unataka wakuchekee??? unanyooshwa tu.

Weka ushahidi usaidiwe usilete generalisation za ajabu ajabu humu as if wanaosoma wote hawana uelewa. Pia jitahidi kutumia lugha nzuri ukitumia lugha yako chafu haikufanyi ionekane hoja yako ina mashiko.

By the way, hamna walimu wenye lugha na mwandiko mchafu kama huo wako

Be smart, wewe ni kijana kama sikosei
 
UHALISIA NI HUU: JE UNADHANI WAKUU WA SHULE NI WATETEZI WAZURI WA WALIMU????
1. Wastani wa uwiano wa mwalimu na idadi ya wanafunzi kwa darasa ni 90
2: Wastani wa idadi ya vitabu na idadi ya wanafunzi ni 1:90 kwa shule nyingi za msingi
3; baadhi ya shule haina hata mihtasari ya masomo,
ole wako mwalimu useme umeshindwa kuhudhuria kipindi kwa sababu huna mhitasari wa somo, mkuu atakushambulia kwa maneno, macho yatamtoka, sasa haki iko wapi??? JE UNADHANI WAKUU WA SHULE NI WATETEZI WAZURI WA WALIMU????
 
Wanajenga fitina wanajengaje?
Hizi ni hear-says tu!! Nani akujengee fitina wewe?? Wewe una nini mpaka ujengewe fitina??? Mbona wenzako hawajengewi?? Lete ushahidi usikute ni 'inferiority complex' zako tu.

Wakuu wa shule wengi wapo smart na wakurugenzi wengi wapo smart sana hawawezi kudeal na individual issues za kijinga kama hizo. Wewe weka ushahidi wako nani kakujengea fitina au majungu. Wewe kama mtoro kazini, kiburi mjuaji au unalala na wanafunzi unataka wakuchekee??? unanyooshwa tu.

Weka ushahidi usaidiwe usilete generalisation za ajabu ajabu humu as if wanaosoma wote hawana uelewa.

Be smart, wewe ni kijana kama sikosei
SIKIA:
1. Mwalimu yeyote mwenye akili timamu huwezi kumwambia afundishe vipindi zaidi ya 24 akakubali, mkuu wa shule atamchukia
2. mwalimu Yeyeto mwenye akili timamu huwezi kumpangia majukumu week end akayatekereza ......utamwita mbishi
3.Mwalimu yeyote mwenye akili timamu anajali muda wake.....utamwita mzembe
NB:mwalimu wa disegn hiyo wakuu wa shule hawampangi kwenye nafasi za usimamizi wa mitihani (TAIFA) ya nje ya shule, wala hawezi kumpendekeza kwa nafasi yeyote, na barua yake yoyote ya promotion ikija unaificha ili kumkomoa, kwa unafiki huuu wakuu wa shule hamfai kuwa watetezi wa walimu
 
jibu hoja! hata kama umeguswa tako
Hoja ni wakuu wa shule hata katika maswala madogo ya msingi hawawezi kuyajengea hoja, wanajenga fitina na chokochoko, hofu na woga kwa walimu kuwa ni walimu wakorofi na wasumbufu, na wanaanza kuwaandikia barua mbaya za kuwachafua.
Swali ni watawezaje kuwatetea walimu ambao wao wanawaita wakorofi na wasumbufu???? husilete hang over zako leta hoja bwege weee
Labda mkuu wako. Sisi shuleni kwetu kuanzia mkuu hadi walimu wote tunaishi kama mapacha. Hakuna siri katika mapato na matumizi, incase mmoja amepotoka basi tunakaa na kueleweshana. Tunagawana kazi kwa usawa hasa zile zenye ofa hakuna upendeleo wa kuzifanya mmoja au aadhi ya watu.
Kama kwenu kuna utata, usidhani kote kuko hivo. Pambana na hali yenu na poleni sana.
 
Labda mkuu wako. Sisi shuleni kwetu kuanzia mkuu hadi walimu wote tunaishi kama mapacha. Hakuna siri katika mapato na matumizi, incase mmoja amepotoka basi tunakaa na kueleweshana. Tunagawana kazi kwa usawa hasa zile zenye ofa hakuna upendeleo wa kuzifanya mmoja au aadhi ya watu.
Kama kwenu kuna utata, usidhani kote kuko hivo. Pambana na hali yenu na poleni sana
husijitetee kwa kuwa wewe ni mkuu, nakujua vizuri, wewe binafsi kuna walimu 2 hamsalimiani mlifikishana kwa DEO, weeeee ishia hapo hapo tusije kuhuumbuana humu ni kataja jina lako........
Kifupi hakuna mkuu wa shule hasiye na migogoro na walimu..... Wakuu wa shule njaaa, wanahitaji kubana hadi kipesa ambacho walimu wangekula mmmmmmmmmm
Vinginevyo kama nimkuu wa vishule vipya vilivyo funguliwa mwezi march 2020
 
husijitetee kwa kuwa wewe ni mkuu, nakujua vizuri, wewe binafsi kuna walimu 2 hamsalimiani mlifikishana kwa DEO, weeeee ishia hapo hapo tusije kuhuumbuana humu ni kataja jina lako........
Kifupi hakuna mkuu wa shule hasiye na migogoro na walimu..... Wakuu wa shule njaaa, wanahitaji kubana hadi kipesa ambacho walimu wangekula mmmmmmmmmm
Vinginevyo kama nimkuu wa vishule vipya vilivyo funguliwa mwezi march 2020
Fallacy assumption
 
-Wengi wao ni vibaraka wa Wakurugenzi na Maafisa Elimu (DEO);Wametumwa
--Wakuu wa shule, Waratibu Elimu Kata (MEK) hawafai kuchaguliwa


Siku na Tarehe ya kufanya uchaguzi wa kupata viongozi wa Chama Cha Walimu (CWT) utatangazwa muda wowote, hii ikiwa ni baada ya tarehe ya awali kuhairishwa kufuatia tishio la ugojwa wa CORONA. Poleni kwa usumbufu uliojitieza.

Wapiga kura (Walimu wawakilishi wa kila shule) kuweni makini sana na aina ya Walimu waliojitokeza kugombea nafasi ndani ya chama.Miongoni mwa Walimu waliojitokeza baadhi yao ni Wakuu wa shule na Waratibu Elimu Kata (MEK), na hawa wanaonekana wanahushawishi wa kifedha kwa sababu ya posho ya madaraka, hivyo elfu kumi, kumi kwao sio shida.

NIWAKUMBUSHE WALIMU: Miongoni mwa watu wanaofanya kazi ya ualimu kuwa ngumu ni wakuu wa Shule na Waratibu Elimu Kata. Hii inanipa kigugumizi , kundi hili la viongozi wanaotaka tena uongozi watawatetea vipi walimu ikiwa migogoro mingi ya walimu inatengenezwa na Wakuu wa shule na Waratibu Elimu Kata? Walimu mlioko mashuleni mnalijua hili. Walimu wengi wanaohoji masuala ya msingi kama vile mapato na matumizi ya shule, wakuu wa shule huwajengea hoja kuwa ni walimu wakorofi na wasumbufu, na wanaanza kuwaandikia barua mbaya za kuwachafua.

LAKINI: Wakuu wa shule na Waratibu Elimu Kata (MEK), kwa sababu ya posho ya madaraka huwa mnajisahau kuwa na ninyi ni walimu kama walivyo walimu wengine. Mnabadilika kuwa vibaraka wa Wakurugenzi na Maafisa Elimu (DEO). Mnadiliki muda mwingine kutoa maneno ya shombo kwa walimu wenzenu wanapotoa madai ya msingi, mara nyingine mnaficha barua za walimu ili madai yao yasiwafikie waajiri.

UTAKUBALIANA NA MIMI: Ili uwe mkuu wa shule au Waratibu Elimu Kata (MEK) lazima uwe na mahusiano ya karibu na Mkurugenzi na Afisa Elimu (DEO) wakupeleka taarifa za walimu wengine, kujipendekeza(Kibaraka). Mkurugenzi anasimama kama Mwajiri, kwa Wakuu wa Shule na Waratibu Elimu Kata (MEK) mwajiri (Mkurugenzi na Afisa Elimu (DEO))wananafasi kubwa kuliko walimu.Je katika hali ya kawaida mtadhubutu kuwahoji bila kupepesa macho?

Chamilo Nicolaus nasema ili chama kirudi wenye misingi kama inavyoainishwa katika Katiba ya Chama Toleo la Sita la mwaka 2014: Sehemu ya I Wapiga kura (Walimu wawakilishi wa kila shule) kuweni makini sana na aina ya Walimu waliojitokeza kugombea, Vinginevyo tutabaki kukiona chama kisicho na muelekeo.
Tatizo njaa,wivu na tamaa





Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijui kwanini watu wakiwa walimu wanapoteza akili zao halisi

Maana naona walimu wao kwa wao wanachukiana


Hii inapelekea walimu kuonekana ni kichaka cha watu walio feli kisa matendo na mienendo yao inaonyesha hivyo


kwa mtazamo wangu walimu wanahitaji kujitambua ila nasisi wengine tuwatambue



Sasa inaonekana hawajitambui thamana yao je tulio nje tutawatambua thaman yao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijui kwanini watu wakiwa walimu wanapoteza akili zao halisi

Maana naona walimu wao kwa wao wanachukiana


Hii inapelekea walimu kuonekana ni kichaka cha watu walio feli kisa matendo na mienendo yao inaonyesha hivyo


kwa mtazamo wangu walimu wanahitaji kujitambua ila nasisi wengine tuwatambue



Sasa inaonekana hawajitambui thamana yao je tulio nje tutawatambua thaman yao

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna ofisi isiyo na migogoro,
Umebahatika kuyajua haya ya walimu kwasababu ya wingi wao, pia masuala yao ni rahisi kujulikana mtaani kwasababu kuna uhusiano wa moja kwa moja na wanachi
Hata hivyo walim ni watu wasio na uwezo wa kuwashughulikia wambea, wachafuzi wa kazi yao kwani hawana meno hayo, mbona hamuwasemi maaskari hivyo??

When your toddler was learning to walk, you’d encourage her to get back up after she fell down,Parents should practice that approach as their children get older.
 
Hakuna ofisi isiyo na migogoro,
Umebahatika kuyajua haya ya walimu kwasababu ya wingi wao, pia masuala yao ni rahisi kujulikana mtaani kwasababu kuna uhusiano wa moja kwa moja na wanachi
Hata hivyo walim ni watu wasio na uwezo wa kuwashughulikia wambea, wachafuzi wa kazi yao kwani hawana meno hayo, mbona hamuwasemi maaskari hivyo??

When your toddler was learning to walk, you’d encourage her to get back up after she fell down,Parents should practice that approach as their children get older.
Kumbe ndivyo ilivyo mkuu


Maanake hata matatizo yao hawezi kuyamaliza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom