Uchaguzi CUF: Prof. Lipumba ambwaga Prof. Safari

Balantanda

JF-Expert Member
Jul 13, 2008
12,476
4,754
Siku kama 2 zilizopita nilimsikia Profesa huyu akihojiwa na Idhaa ya Kiswahili ya BBC.Katika mahojiano hayo Profesa SAFARI alitangaza nia yake ya kutaka kugombea Uenyekiti wa Taifa Chama cha Wananchi(CUF)..Katika maelezo yake alisema kwamba lengo hasa la kugombe ni kutaka kurudisha uhai wa CUF ambacho(kwa mujibu wa maelezo yake) ni kama kimepoteza umaarufu na kwamba kinahitaji mabadiliko ya uongozi ngazi ya Taifa kwani uongozi wa sasa umekaa muda mrefu na haujaleta mabadiliko yoyote(alizungumzia suala la CUF kutokuwa na mbunge hata mmoja wa kuchaguliwa kutoka Tanzania bara),pia alizungumzia suala la mikutano ya CUF kutokuwa na mahudhurio ya kuridhisha kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma ambapo alisema kwamba sasa hivi mpaka wanachama waambiwe kuwa kutakuwa na Pilau ndio mahudhurio kidogo yanakuwa ya kuridhisha...Binafsi namfahamu Profesa SAFARI kama Mwanasheria maarufu na mtaalamu mahiri wa Lugha yetu adhimu ya Kiswahili...Swali,,Je kwa wanaomfahamu Profesa huyu,ana uzoefu gani katika mambo ya kisiasa???,anaweza kuvaa viatu vya Profesa Lipumba???,hivi uchaguzi mkuu wa CUF unafanyika lini???....Mkuu Mzee Mwanakijiji ninaomba kama inawezekana ufanye mahojiano na Profesa huyu na kuyaweka hapa maana kwa jinsi nilivyomsikia ana uchungu sana na jinsi CUF ilivyopoteza umaarufu(kwa mtizamo wake)..Naomba kuwasilisha wakuu...Mbarikiwe sana
 
Last edited by a moderator:
Siku kama 2 zilizopita nilimsikia Profesa huyu akihojiwa na Idhaa ya Kiswahili ya BBC.Katika mahojiano hayo Profesa SAFARI alitangaza nia yake ya kutaka kugombea Uenyekiti wa Taifa Chama cha Wananchi(CUF)[/COLOR

Kwa kweli kwa jinsi alivyokuwa anajibu yale maswali, mimi aliniacha hoi kabisa! Sijui kama mtu anaweza kumpatia uu-nyekiti mtu namna ile kwa majibu. Majibu hana tofauti na Nature, ila ya kisomi.

Halafu, huyu jamaa si ndiye mwenye scandal ya yule binti wa kutoka NIgeria pale UDSM miaka ile? Kwa wanaojua tafadhali. I was too young, lakini nakumbuka jina kama hilo......
 
Kumekuwa na wimbi la chini kwa chini miongoni mwa wanachama wa CUF kutaka apatikane mtu wa kuchukua uenyekti wa chama hicho badala ya Prof Lipumba wanayedai anaonekana kuishiwa na hoja za kukijenga chama hicho

Dr safari ameisha tangaza nia yake ya kugombea U/nyekiti CUF pia Prof Lupumba naye inasemekana ameisha chukua form.

Je Dr Safari ana nia kweli njema ya kuleta mabadiliko ndani ya CUF?

Dr anasema kuna ubabaishaji ndani ya CUF,

Je nikweli CUF imechoka na Je nikweli Prof ndio tatizo ndani ya CUF na hana dira kwa mfano kuingilia ugomvi kama ule wa wana-CCM wa kumkataa katibu mkuu wao au ule wa Mengi na Masha huku akijiegemeza moja kwa moja kwa Mengi,

Je demokrasia ya kweli imeingia CUF coz siku zote sura ni zile zile,au ndio mwisho wa CUF.
Je Dr ataweza kupambana na Lipumba? na ikitokea Prof akashindwa je atachana na CUF either kuacha kujishughulisha tena na siasa na kufanya shughuli zake binafsi,kujiunga na chama kingine au kuazisha chake?

hayo ni swali ninayojiuliza bila kupata jibu, Macho na masikio yangu Februari mwakani kwenye uchaguzi mkuu wa chama hicho.
 
Professor Lipumba ameishiwa....CUF inastahili kubadilisha mwenyekiti na mgombea rais, ama sivyo Lipumba atashika mkia 2010. Namuomba Dr.Abdallah Safari aje na hoja ya kujiunga na CHADEMA, hio itampa kura nyingi sana na itaongeza nguvu ya upinzani nchini.
 
Wote ni maprofessa....na wote wanafaa!!!...Muanzisha mada anaonesha as if kuna Mgogoro au sintofahamu ndani ya CUF...Wote wanyamwezi..ila prof Safari amekulia zaid tanga na moja wa wazazi wake nafikiri ni mtu wa tanga.....kama nimekosea mwenye nazo za usahihi aweke...

to me, Safari hawezi kumshinda lipumba..in the sense kila moja ana fani yake..na hali ya sasa ya nchi tunahitaji mtu wa style gani....Lipumba Mchumi na Safari mwanasheria..mwandishi mtunzi...so kila mmoja ana flavors zake...
 
Wote ni vichwa ila wako on the wrong side
Lipumba ni mchumi aliyebobea na binafsi huwa ninamkubali sana.Tatizo yuko kwenye chama ambacho kilishapandikizwa sera za kibaguzi na kamwe hawatakaa wafanikiwe.Kwahiyo swala la Prof.Safari kum challenge Lipumba ni zuri na kama kawaida ya waswahili na ule msemo wetu wa kimpya kinyemi basi na itokee Lipumba akashindwe halafu aje ajiunge na chama kama chadema,basi upinzani utanoga kweli.
 
Labda tungepata profile ya huyo Professor Safari kabla ya kuanza kumlinganisha na Prof Lipumba. Naamini hilo jina ni geni miongoni mwetu hasa kwenye siasa za bongo. Tupe profile yake. Profile ya Lipumba tunayo.

Isije ikawa tunalinganisha mayai viza kwa viza
.
 
Profesa Safari akichukua uenyekiti wa CUF itakuwa ni mwanzo wa kuparaganyika kwa CUF. Profesa safari ni mdini, mbaguzi na mtu wa shari. Mtu mwenye hulka kama yeye hatakiwi kuwa kiongozi wa chama kikubwa. Kwa huku bara nadhani itakuwa ndio mwisho wa CUF.
 
Profesa Safari akichukua uenyekiti wa CUF itakuwa ni mwanzo wa kuparaganyika kwa CUF. Profesa safari ni mdini, mbaguzi na mtu wa shari. Mtu mwenye hulka kama yeye hatakiwi kuwa kiongozi wa chama kikubwa. Kwa huku bara nadhani itakuwa ndio mwisho wa CUF.

Hilo neno mukulu,

Yaani you were reading my lips..
 
CUF ilikufa na James Mapalala ikawa hijacked na Seif Shariff Hamad.
 
Kauli zake tu alizotoa siku akionyesha nia yake ya kugombea zilitosha kuonyesha ni uchu tu wa madaraka umemjaa! Hata kama kuna ya kubadili humo ndani ya CUF yale maneno yalikuwa ni ya kuwakebehi hata hao watakao mpigia kura. Kwani kama mtu unataka kugombea uongozi ni lazima ukejeli waliokuwepo? si busara ndio inawezesha kutambua kiongozi bora?

Haya wana CUF tuwatakie kila la heri katika hili na busara itawale
 
Mtarajiwa,
Yaani Lipumba ashindwe CUF, ajiunge na CHADEMA ndipo upinzani unoge? Akishindwa huko CUF, CHADEMA ndiko ataweza? Kama matarajio yetu ni kunogesha upinzani kwa njia hiyo tumepotea. Nadhani CUF kuna tatizo la kimfumo ambapo mwenyekiti anakuwa na cheo kama ceremonial wakati the real power ni katibu mkuu. If this is not changed watamaliza maprofesa wote with minimal gains hasa bara.
 
Mtarajiwa,
Yaani Lipumba ashindwe CUF, ajiunge na CHADEMA ndipo upinzani unoge? Akishindwa huko CUF, CHADEMA ndiko ataweza? Kama matarajio yetu ni kunogesha upinzani kwa njia hiyo tumepotea. Nadhani CUF kuna tatizo la kimfumo ambapo mwenyekiti anakuwa na cheo kama ceremonial wakati the real power ni katibu mkuu. If this is not changed watamaliza maprofesa wote with minimal gains hasa bara.


Mkuu,Lipumba akijiunga na chadema ataongeza nguvu kule kwa sababu ni mtu makini na anakubalika Tanzania isipokuwa chama alichojiunga nacho hakikubaliki na watanzania wengi na mtazamo huu ndiyo umemkosesha Lipumba kura nyingi za watanzania wenye mawazo kuwa CUF ni chama chenye itikadi ya kibaguzi,kwani huu ubaguzi unaodhaniwa uko CUF ni mbaya kuliko hata ule wanaopakaziwa chadema.
Sasa kwanini Lipumba asiiweze chadema?Cha msingi asiende kung'ang'ania ukubwa,jukumu hili awaachie wanachama wenyewe.
 
Safari na Lipumba wote ni wasomi wazuri ila sasa Lipumba sidhani kama ana jipya linaloweza kukisaidia chama chake; nilitegemea wakati wa uchaguzi wa Tarime angeonesha leadership qualities kwa kushauri chama chake kutosimamisha mgombea na kuunga mkona Chadema hakufanya hivyo!! Safari on the other hand anaweza kufanikiwa kupata wafuasi wengi wa dini ya kiislam kwasababu ya itikadi yake; he is a hardliner oppositionist kwahiyo anaweza kukaa na Chadema wakaweka mikakati imara!!
 
Last edited:
Mods naomba hii iunganishwe na ile nyingine ya Prof.Lipumba Vs. Dr. Abdallah Safari
 
Safari na Lipumba wote ni wasomi wazuri ila sasa Lipumba sidhani kama ana jipya linaloweza kukisaidia chama chake; nilitegemea wakati wa uchaguzi wa Tarime angeonesha leadership qualities kwa kushauri chama chake kutosimamisha mgombea na kuunga mkona Chadema hakufanya hivyo!! Safari on the other hand anaweza kufanikiwa kupata wafuasi wengi wa dini ya kiislam kwasababu ya itikadi yake; he is a hardliner oppositionist kwahiyo anaweza kukaa na Chadema wakaweka mikakati imara!!

Bulesi:

Lipumba hana matatizo yote. Vilevile CHADEMA au CUF hawana matatizo. Matatizo ni kuwa kuna mikoa haijawahi kuchagua kuchagua mtu kutoka upinzani hata katika ngazi ya kijiji.

Unaweza kumpeleka punda kisimani lakini huwezi kumlazimisha kunywa maji.
 
Professor Lipumba ameishiwa....CUF inastahili kubadilisha mwenyekiti na mgombea rais, ama sivyo Lipumba atashika mkia 2010. Namuomba Dr.Abdallah Safari aje na hoja ya kujiunga na CHADEMA, hio itampa kura nyingi sana na itaongeza nguvu ya upinzani nchini.

Bwa shee!! Hilo bendela lako linafwanana na la CCM!!!!!!!!!!Your post, sound like Divide and Rule!!!!!
 
Back
Top Bottom