Paul Alex
JF-Expert Member
- Jul 14, 2012
- 4,239
- 9,527
Salaam!
Kuna post nyingi na kelele nyingi na kampeni nyingi za uongo kumhusu mama mitandaoni na mitaani!
Nyingi zinaendeshwa na wana CCM kindakindaki tena wengi wenye vyeo.
Unajaribu kujiuliza, kulikoni?
Kutoka kwenye, 'atake asitake tutamuongezea muda' mpaka kwenye kashfa na kejeli hizi chafu tena za uongo!!!
Jibu linakuja, 'Magufulism/ umagufuli'
Mwenda zake, nimseme kidogo japo sio kwa ubaya sanaaa maana kikwetu sio vizuri kumsema marehemu.
Mwendazake alitengeneza mapomondo ndani ya CCM... kama tu yale yanayozungukaga mtaani, 'tunauza sumu ya kunguni, utitiri, chawa, papasi, viroboto na vyombo vipo' ... Likimaliza linaanza tena... na tena ..na tena hadi betri iishe.
Watu waliazimisha akili zao, wakasifu na kuabudu na kishangilia bila kufikiri..
Sasa kibao kimegeuka kidogo, mama anataka watu wenye kufikiri na kuwajibika katika uongozi wake na hana mpango wa kusifiwa au kuabudiwa...yale mapomondo yameduwaa, hayajui yaanzie wapi.
Kidogokidogo yakaanza...'hatuchanji'...Mchungaji huyo mwenye ruti za Ulaya na Marekani kila wakati anadanganya waumini na taifa kwa ujumla ili hali anajua bila cheti cha chanjo kule haingii.
Mwingine akaanza shule ya uongozi... ambayo hajawahi kuiishi wala kuijaribu pindi alipopewa madaraka.
Watu wanamkejeli mama mpaka unadhani hawa wamesahau kama wanamkejeli rais wa nchi na mwenyekiti wa chama?
Anyway, dawa ni kumalizana nao 2022 katika uchaguzi ndani ya chama ili kuwakumbusha kiongozi ni nani!!
Kuna post nyingi na kelele nyingi na kampeni nyingi za uongo kumhusu mama mitandaoni na mitaani!
Nyingi zinaendeshwa na wana CCM kindakindaki tena wengi wenye vyeo.
Unajaribu kujiuliza, kulikoni?
Kutoka kwenye, 'atake asitake tutamuongezea muda' mpaka kwenye kashfa na kejeli hizi chafu tena za uongo!!!
Jibu linakuja, 'Magufulism/ umagufuli'
Mwenda zake, nimseme kidogo japo sio kwa ubaya sanaaa maana kikwetu sio vizuri kumsema marehemu.
Mwendazake alitengeneza mapomondo ndani ya CCM... kama tu yale yanayozungukaga mtaani, 'tunauza sumu ya kunguni, utitiri, chawa, papasi, viroboto na vyombo vipo' ... Likimaliza linaanza tena... na tena ..na tena hadi betri iishe.
Watu waliazimisha akili zao, wakasifu na kuabudu na kishangilia bila kufikiri..
Sasa kibao kimegeuka kidogo, mama anataka watu wenye kufikiri na kuwajibika katika uongozi wake na hana mpango wa kusifiwa au kuabudiwa...yale mapomondo yameduwaa, hayajui yaanzie wapi.
Kidogokidogo yakaanza...'hatuchanji'...Mchungaji huyo mwenye ruti za Ulaya na Marekani kila wakati anadanganya waumini na taifa kwa ujumla ili hali anajua bila cheti cha chanjo kule haingii.
Mwingine akaanza shule ya uongozi... ambayo hajawahi kuiishi wala kuijaribu pindi alipopewa madaraka.
Watu wanamkejeli mama mpaka unadhani hawa wamesahau kama wanamkejeli rais wa nchi na mwenyekiti wa chama?
Anyway, dawa ni kumalizana nao 2022 katika uchaguzi ndani ya chama ili kuwakumbusha kiongozi ni nani!!