Michael Andrew Jr
JF-Expert Member
- Jul 1, 2020
- 219
- 665
Wakuu salute!
Jioni ya leo nikiwa maeneo ya Tegeta namanga Dsm, nilipitia pub moja at least kupoza koo kwa 'kabia kamoja' kupoza machungu ya utafutaji. Si unajua ukiumbwa mwanaume...
Kumekuwepo na tambo, mbwembwe na ubishani baina ya upinzani hususani CDM dhidi ya chama dola CCM kuelekea uchaguzi mkuu october 2020. CCM wakitamba kupeta na Upinzani ukiapa kuliangusha 'jabari' .
Binafsi naamini uchaguzi uliisha toka kipindi kile cha kukarabati daftari la kudumu la wapiga kura. Kwa wakati ule vijana wengi walisusa kujiandikisha, wengi wakisema siasa sasa basi, hasa ukizingatia wabunge walivyokua wanaunga mkono juhudi. Wengi wanakumbuka machungu jinsi walivyowapambania 2015, na jinsi usaliti waliokua wanaufanya wa kuunga mkono juhudi.
Wakati vijana wa kimapinduzi wengi wakisusa kujiandikisha, CCM walikua wakihamasisha akina mama na akina bibi kwenda kupanga foleni kujiandikisha. Ni dhahiri walikua wanajua wanachofanya hasa ukizingatia vijana kama machinga, boda boda,wavuvi nk walikiua wazito kwenda kujiandikisha. Ni kama walitengeneza tatizo makusudi, bila shaka ule ulikua ni 'mkakati' mahususi.
Tofauti na wengi tunavyodhani kua uchaguzi unaweza kuendeshwa kibabe ili kuibeba CCM. Uchaguzi wa mwaka huu unaweza kua wa haki na wazi sana kuliko chaguzi zilizopita... Ila utakua na wapiga kura wachache ambao wengi ni akina mama na wazee ambao ni wakereketwa wa CCM. Upinzani ulizubaa sana katika kuhamasisha watu, na hii ilichangiwa na 'kibano' walichopewa cha kukataza siasa na mikutano, isipokuwa kwa wabunge ndani ya majimbo yao.
Yale mambo ya upinzani kuchukua watu CCM then baadaye wanarud walipotoka yalikua yanaboa sana na kukatisha tamaa... Watu waliona siasa ni kama maigizo!
Wanasema "no research no right to speak" jaribu kuuliza kati ya vijana 10 wangapi wamejiandikisha hapo ulipo... Ni ukweli mchungu lakini lazima usemwe. Kwenye mikakati na figisu CCM they are far better, Upinzani jifunzeni.
Michael Andrew JR
Jioni ya leo nikiwa maeneo ya Tegeta namanga Dsm, nilipitia pub moja at least kupoza koo kwa 'kabia kamoja' kupoza machungu ya utafutaji. Si unajua ukiumbwa mwanaume...
Kumekuwepo na tambo, mbwembwe na ubishani baina ya upinzani hususani CDM dhidi ya chama dola CCM kuelekea uchaguzi mkuu october 2020. CCM wakitamba kupeta na Upinzani ukiapa kuliangusha 'jabari' .
Binafsi naamini uchaguzi uliisha toka kipindi kile cha kukarabati daftari la kudumu la wapiga kura. Kwa wakati ule vijana wengi walisusa kujiandikisha, wengi wakisema siasa sasa basi, hasa ukizingatia wabunge walivyokua wanaunga mkono juhudi. Wengi wanakumbuka machungu jinsi walivyowapambania 2015, na jinsi usaliti waliokua wanaufanya wa kuunga mkono juhudi.
Wakati vijana wa kimapinduzi wengi wakisusa kujiandikisha, CCM walikua wakihamasisha akina mama na akina bibi kwenda kupanga foleni kujiandikisha. Ni dhahiri walikua wanajua wanachofanya hasa ukizingatia vijana kama machinga, boda boda,wavuvi nk walikiua wazito kwenda kujiandikisha. Ni kama walitengeneza tatizo makusudi, bila shaka ule ulikua ni 'mkakati' mahususi.
Tofauti na wengi tunavyodhani kua uchaguzi unaweza kuendeshwa kibabe ili kuibeba CCM. Uchaguzi wa mwaka huu unaweza kua wa haki na wazi sana kuliko chaguzi zilizopita... Ila utakua na wapiga kura wachache ambao wengi ni akina mama na wazee ambao ni wakereketwa wa CCM. Upinzani ulizubaa sana katika kuhamasisha watu, na hii ilichangiwa na 'kibano' walichopewa cha kukataza siasa na mikutano, isipokuwa kwa wabunge ndani ya majimbo yao.
Yale mambo ya upinzani kuchukua watu CCM then baadaye wanarud walipotoka yalikua yanaboa sana na kukatisha tamaa... Watu waliona siasa ni kama maigizo!
Wanasema "no research no right to speak" jaribu kuuliza kati ya vijana 10 wangapi wamejiandikisha hapo ulipo... Ni ukweli mchungu lakini lazima usemwe. Kwenye mikakati na figisu CCM they are far better, Upinzani jifunzeni.
Michael Andrew JR